Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,883
- 6,884
WAZIRI MAIGE AWAPIGA 'STOP' WAWEKEZAJI KUWANYIMA AJIRA WATANZANIA
WAZIRI wa maliasili na utalii Ezekiel Maige amewataka wawekezaji wa makampuni na viwanda katika wilaya ya Mufindi mkoani Iringa kuendesha viwanda hivyo kwa kuzingatia mahitaji ya nchi ikiwa ni pamoja na kutoa ajira kwa vijana nchini badala ya kutumia mashine kufanya kazi ambazo vijana wangeweza kuzifanya.
Waziri Maige ametoa kauli hiyo jana wilayani Mufindi wakati kikao chake na wawekezaji wakubwa katika msitu wa hifadhi ya Taifa wa Sao Hill Mufindi .
Amesema kuwa hatua ya wawekezaji kutumia mashine na wageni kutoka nchi kwa kazi ambazo watanzania wanaziweza ni kutowatendea haki watanzania ambao walitegemea uwekezaji huo kuwawezesha kupata ajira zaidi.