Waziri kivuli (Afya - CHADEMA) fanyia kazi hili katika M4C LINDI...

mchaichai

JF-Expert Member
Nov 5, 2011
648
76
WAziri KIVULI, CHADEMA, WAZIRI WA AFYA, TAKUKURU shirikianeni kutusaidia sisi wanyonge wa Mkoa wa LIndi, juzi 23/05/2012 katika kijiji cha RUtamba alikufa mama mjamzito kwa gari ya wagonjwa kuishiwa mafuta njiani, katika dodosa gari hiyo ya dharura ilikuwa na mafuta kigodo sana. hii inatokana na uzembe a idara ya Afya makao makuu, ili hali serikali inatenga fedha za kutosha katika budget ili kuokoa maisha ya mama na mtoto na pia ni MDG 4 & 5. ni tatizo na kufanya kazi kwa mazoea MWAZIRI NA TAKUKURU huu ndiyo wakati wa kuwawajibisha wahusika wa sakati hili....kuna fununu kwamba zinafanyika kila jitihada kumwangushia dereva mzigo huu tunaomba haki itendeke si haki hata kidogo!
 
Weka details kamili hapa, jina la hospitali, If possible hata namba za hiyo gari ya wagonjwa na picha ili tulivalie njuga hadi wahusika wajute kuwa mafisadi!
 
Weka details kamili hapa, jina la hospitali, If possible hata namba za hiyo gari ya wagonjwa na picha ili tulivalie njuga hadi wahusika wajute kuwa mafisadi!

namba za gari siwezi kuzikumbuka kwa sasa lakini....ni gari ya kituo cha Afya Rutamba na gari ya kituo husika maana ilikuwa inasomeka ubavuni...maana mimi nilikuwa natoka maeneo ya huku vijijini katika shughuli zetu za miradi kupitia organization yetu na sikuwa nimejiangaa sana kuchukua picha, maana hata wakati nafika mambo yalikuwa yameharibika..mgonjwa alikuwa amekwisha fariki tayari...njiani nilikutana na gari nyingine ambulance iliyosomeka Rondo Hospital inaelekea barabara hiyo kutoka mjini sasa sijui ndiyo ilikuwa inakwenda eneo la tukio au la...maana hospital ya Rondo iko katika halmashauri ya Wilaya Lindi ambayo ndiyo inamkasa huu. nawasilisha
 
Back
Top Bottom