WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano), Mohammed Seif Khatib amesema hana ushahidi wa nyaraka yoyote ya Mkataba wa Muungano kati ya iliyokuwa Jamhuri ya Watu wa Zanzibar na Jamhuri ya Watu wa Tanganyika, inayoonyesha kusainiwa na Rais wa kwanza wa Zanzibar Mzee Abeid Amani Karume au kiongozi yoyote wa Baraza la Mapinduzi ambalo, liliridhia mkataba huo.
Kauli hiyo, ya Waziri Khatib imekuja wakati kukiwa na mjadala mkubwa kuhusu suala la muungano kati ya Jamhuri hizo mbili, uliosababisha kuzaliwa kwa Jamhuri moja ya Muungano wa Tanzania.
Suala la Muungano kati ya Jamhuri hizo, mbili limezua mjadala mkubwa katika siku za karibuni hasa baada ya kuzuka fununu za kuwepo kwa mafuta na gesi asilia katika visiwa vya Zanzibar na kutangazwa kuwa mali hiyo ni katika orodha ya mambo ya muungano.
Jambo hilo, lilisababisha baadhi ya viongozi na wananchi wa Zanzibar kupinga kwa nguvu zote rasilimali hiyo, kuingizwa ndani ya mambo ya muungano huku baadhi yao wakisema wako tayari hata kuvunja muungano.
Mjadala huo, pia uliibua hoja ya kwamba muungano kati ya jamhuri hizo, si halali kwa sababu hauna misingi ya kikatiba na keshiria wala ridhaa ya wazanzibari kwa kutokuwapo saini za viongozi wao katika mkataba wa muungano.
Akizungumza na Mwananchi mjini hapa juzi, Wazir Khatibu alisema hana nyaraka yoyote ya mkataba wa muungano inayoonyesha saini ya Rais wa kwanza wa Zanzibar au kiongozi yeyote wa Baraza la Mapinduzi kuridhia mkataba huo.
"Mimi nafahamu ushahidi wa aina mbili unaonyesha uhalali wa muungano kati jamhuri ya watu wa Zanzibar na watu wa Tanganyika. Moja ni picha waliyopiga Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Mzee Karume wakati wakitia saini mkataba huo.
"Lakini pia nina ushahidi wa picha ambayo viongozi hao walipiga wakati wa kukabidhiana nyaraka za mkataba huo baada ya kusainiwa na walikuwa wameshikana mikono," alisema Waziri Khatib.
Baada ya waziri Khatibu kutoa ushahidi huo, mwandishi wa habari hii alimuuliza waziri huyo ambaye pia ni mjumbe wa kamati maalum ya serikali ya kushughulikia kero za muungano kama ana nyaraka yoyote ya mkataba wa muungano, inayoonyesha saini ya Mzee Karume au kiongozi mwingine wa baraza la Mapinduzi.
"Ahh kwanza nsubiri nimalize kwanza, nyaraka ya namna hiyo, sina lakini nafahamu hizo aina mbili za ushahidi kwa maana picha waliyopiga wakati wakisaini na nyingine waliyopiga wakikabidhiana au kubadilishana nyaraka hizo baada ya kusainiwa," alisema Wazir Khatib.
Suala la kuwapo kwa picha hizo, limekuwa likipingwa na watu wengi wanaofuatilia historia ya muungano huo, wakidai kuwa picha hizo hazithibitishi kuwa kilichokuwa kikisainiwa au kukabidhiwa ni mkataba wa muungano kweli.
Mwananchi ilibahatika kupata nyaraka mbili za mkataba wa Muungano kati ya Zanzibar na Tanganyika ambapo moja ilisainiwa na aliyekuwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Pius Msekwa na nyingine ikisainiwa na baba wa taifa Mwalimu Nyerere huku katika nyaraka zote kukiwa hakuna saini ya mtu wa upande wa Zanzibar.
Licha ya kasoro hiyo, waziri Khatibu alizidi kuutetea na kuulinda muungano kati ya Zanzibar na Tanganyika kuwa ni halali.
Alisema kama kuna watu hawaridhiki na uhalali wa muungano huo, waende mahakamani kuishitaki serikali.
"Muungano kati ya zanzibar na Tanganyika ni halali, lakini kama kuna watu hawaridhiki na uhalali wa muungano huu, basi waende mahakamani na kama wakishindwa katika mahakama za binadamu waende hata katika mahakama ya Mwenyezi Mungu," alisema Wazir Khatibu.
Wakati huohuo, waziri Khatib alikataa kuzungumzia taarifa zilizosambaa visiwani hapa kwamba ana nia ya kujitupa katika kinyangâanyiro cha urais wa Zanzibar mwaka 2010, akisema muda wake bado.
"Hilo la kuhusu urais muda wake bado ukifika nitaweka wazi kama ni kweli au si kweli," alisema Waziri Khatibu.
Baadhi ya watu ambao wanasemwa kuwa wana nia ya kumrithi rais anayemaliza muda wake visiwani Zanzibar ni pamoja na Waziri Mohammed Seif Khatib, Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa na mototo wa rais mstaafu wa awamu ya pili Dk Hussein Mwinyi, Waziri Kiongozi mstaafu wa SMZ Dk Mohammed Gharib Bilal na Balozi Ally Karume.
This is very strange and funny kama hakuna mkataba au makubaliano yeyote ya muungano zaidi ya picha sasa ina maana hakuna muungano wa zanzibar na tanganyika.
Nataka kucheka huku nikilia mie nadhani wazanzibar wanakaliwa kimabavu kama hakuna kitu kama hicho sidhani kama kuna muungano wowote. Picha si kigezo cha muungano.
Kauli hiyo, ya Waziri Khatib imekuja wakati kukiwa na mjadala mkubwa kuhusu suala la muungano kati ya Jamhuri hizo mbili, uliosababisha kuzaliwa kwa Jamhuri moja ya Muungano wa Tanzania.
Suala la Muungano kati ya Jamhuri hizo, mbili limezua mjadala mkubwa katika siku za karibuni hasa baada ya kuzuka fununu za kuwepo kwa mafuta na gesi asilia katika visiwa vya Zanzibar na kutangazwa kuwa mali hiyo ni katika orodha ya mambo ya muungano.
Jambo hilo, lilisababisha baadhi ya viongozi na wananchi wa Zanzibar kupinga kwa nguvu zote rasilimali hiyo, kuingizwa ndani ya mambo ya muungano huku baadhi yao wakisema wako tayari hata kuvunja muungano.
Mjadala huo, pia uliibua hoja ya kwamba muungano kati ya jamhuri hizo, si halali kwa sababu hauna misingi ya kikatiba na keshiria wala ridhaa ya wazanzibari kwa kutokuwapo saini za viongozi wao katika mkataba wa muungano.
Akizungumza na Mwananchi mjini hapa juzi, Wazir Khatibu alisema hana nyaraka yoyote ya mkataba wa muungano inayoonyesha saini ya Rais wa kwanza wa Zanzibar au kiongozi yeyote wa Baraza la Mapinduzi kuridhia mkataba huo.
"Mimi nafahamu ushahidi wa aina mbili unaonyesha uhalali wa muungano kati jamhuri ya watu wa Zanzibar na watu wa Tanganyika. Moja ni picha waliyopiga Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Mzee Karume wakati wakitia saini mkataba huo.
"Lakini pia nina ushahidi wa picha ambayo viongozi hao walipiga wakati wa kukabidhiana nyaraka za mkataba huo baada ya kusainiwa na walikuwa wameshikana mikono," alisema Waziri Khatib.
Baada ya waziri Khatibu kutoa ushahidi huo, mwandishi wa habari hii alimuuliza waziri huyo ambaye pia ni mjumbe wa kamati maalum ya serikali ya kushughulikia kero za muungano kama ana nyaraka yoyote ya mkataba wa muungano, inayoonyesha saini ya Mzee Karume au kiongozi mwingine wa baraza la Mapinduzi.
"Ahh kwanza nsubiri nimalize kwanza, nyaraka ya namna hiyo, sina lakini nafahamu hizo aina mbili za ushahidi kwa maana picha waliyopiga wakati wakisaini na nyingine waliyopiga wakikabidhiana au kubadilishana nyaraka hizo baada ya kusainiwa," alisema Wazir Khatib.
Suala la kuwapo kwa picha hizo, limekuwa likipingwa na watu wengi wanaofuatilia historia ya muungano huo, wakidai kuwa picha hizo hazithibitishi kuwa kilichokuwa kikisainiwa au kukabidhiwa ni mkataba wa muungano kweli.
Mwananchi ilibahatika kupata nyaraka mbili za mkataba wa Muungano kati ya Zanzibar na Tanganyika ambapo moja ilisainiwa na aliyekuwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Pius Msekwa na nyingine ikisainiwa na baba wa taifa Mwalimu Nyerere huku katika nyaraka zote kukiwa hakuna saini ya mtu wa upande wa Zanzibar.
Licha ya kasoro hiyo, waziri Khatibu alizidi kuutetea na kuulinda muungano kati ya Zanzibar na Tanganyika kuwa ni halali.
Alisema kama kuna watu hawaridhiki na uhalali wa muungano huo, waende mahakamani kuishitaki serikali.
"Muungano kati ya zanzibar na Tanganyika ni halali, lakini kama kuna watu hawaridhiki na uhalali wa muungano huu, basi waende mahakamani na kama wakishindwa katika mahakama za binadamu waende hata katika mahakama ya Mwenyezi Mungu," alisema Wazir Khatibu.
Wakati huohuo, waziri Khatib alikataa kuzungumzia taarifa zilizosambaa visiwani hapa kwamba ana nia ya kujitupa katika kinyangâanyiro cha urais wa Zanzibar mwaka 2010, akisema muda wake bado.
"Hilo la kuhusu urais muda wake bado ukifika nitaweka wazi kama ni kweli au si kweli," alisema Waziri Khatibu.
Baadhi ya watu ambao wanasemwa kuwa wana nia ya kumrithi rais anayemaliza muda wake visiwani Zanzibar ni pamoja na Waziri Mohammed Seif Khatib, Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa na mototo wa rais mstaafu wa awamu ya pili Dk Hussein Mwinyi, Waziri Kiongozi mstaafu wa SMZ Dk Mohammed Gharib Bilal na Balozi Ally Karume.
This is very strange and funny kama hakuna mkataba au makubaliano yeyote ya muungano zaidi ya picha sasa ina maana hakuna muungano wa zanzibar na tanganyika.
Nataka kucheka huku nikilia mie nadhani wazanzibar wanakaliwa kimabavu kama hakuna kitu kama hicho sidhani kama kuna muungano wowote. Picha si kigezo cha muungano.