Waziri Hatibu na Kampuni ya Mobitel

Kichankuli

JF-Expert Member
Dec 18, 2008
887
189
Waziri, wa Masuala ya Muungano, amejiandaa kuongea na vyombo vya habari kwaajili ya kuhimiza Taasisi na Makampuni mbalimbali kuchangia katika sherehe za Muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Cha kushangaza ni pale ombi lake la kwanza kwa makampuni ya simu linaangukia kwenye kampuni ya simu ya Mobitel ambayo haipo tena katika ulimwengu wa biashara ya simu. Lakini kibaya zaidi ni kwa Waandishi aliokuwa akiongea nao kushindwa kumsahihisha, sijui na wao hawakugundua au la, kosa hilo na kwenda kurusha habari hiyo hivyohivyo kwa wananchi.

Hapa ndipo linapojitokeza suala la kutokuwa na umakini kwa vyombo vyetu vya habari. Inakuwa ni kama wanakopi na kupesti. Tofauti na wenzetu wa nchi za magharibi, mathalani, kumbuka namna Wanahabari wa Marekali walipoujulisha umma wa Wamarekani juu ya Hilary Clinton alivyoshindwa kukumbuka jinsi alivyotembeleaBosnia; walimpa fact na kumaliza uzia.
 
Hapa tunaongeza utata au tunarekebishana.
Hatibu alisema mobitel nadhani akimaanisha 'mobile telephones'na hakuwa na maana ya kampuni moja ambayo ama ilifilisika au ilibadilisha jina.pia huenda kutokana na kampuni hiyo kuwa ya kwanza kwa huduma hiyo ili jipatia umaarufu uliyoifanya ionekane ndilo jina la huduma kama hizo.
Katika hili tulaumiane sote hasa wale walio katika nafasi nzuri ya kuelimisha jamii pana zaidi.Mfano mpaka sasa watu wengi wanajua kuwa kituo chochote cha kuuzia mafuta(petrol stations) kinaitwa "SHELL" na wachache wanajua kuwa ni "BP".Hii ni kutokana na haya ndiyo makampuni ya kwanza kuanzisha biashara hizo hapa nchini.
Tukirudi kwa bro HATIBU,hivi alitakiwa aombe michango kwa makampuni ya "SIMU" za mikononi au wasambazaji wa huduma ya masaliano kupitia simu za mikononi?HAPA KUNA MAMBO MAWILI "SIMU" na "SIM" ya pili ikiwa na maana ya SUBSCRIBER IDENTIFIER MODULE.
Hivyo kama aliomba msaada huo kwenye makampuni ya simu bado ni utata na kama ni hivyo aongee na wakala wa makampuni kama NOKIA,BLACKBERRY,SONYERRICSON,MOTOROLA na mengine yanayofanana nayo kama wakala wake yupo hapa nchini au ayaandikie huko yalipo.Lakini kama ni huduma,basi awaone ndugu zetu VODACOM,TIGO,ZAIN NA ZANTEL.
Nadhani mhesimiwa alimaanisha makampuni niliyotaja hapa mwishoni.
 
Hapa tunaongeza utata au tunarekebishana.
Hatibu alisema mobitel nadhani akimaanisha 'mobile telephones'na hakuwa na maana ya kampuni moja ambayo ama ilifilisika au ilibadilisha jina.pia huenda kutokana na kampuni hiyo kuwa ya kwanza kwa huduma hiyo ili jipatia umaarufu uliyoifanya ionekane ndilo jina la huduma kama hizo.
Katika hili tulaumiane sote hasa wale walio katika nafasi nzuri ya kuelimisha jamii pana zaidi.Mfano mpaka sasa watu wengi wanajua kuwa kituo chochote cha kuuzia mafuta(petrol stations) kinaitwa "SHELL" na wachache wanajua kuwa ni "BP".Hii ni kutokana na haya ndiyo makampuni ya kwanza kuanzisha biashara hizo hapa nchini.
Tukirudi kwa bro HATIBU,hivi alitakiwa aombe michango kwa makampuni ya "SIMU" za mikononi au wasambazaji wa huduma ya masaliano kupitia simu za mikononi?HAPA KUNA MAMBO MAWILI "SIMU" na "SIM" ya pili ikiwa na maana ya SUBSCRIBER IDENTIFIER MODULE.
Hivyo kama aliomba msaada huo kwenye makampuni ya simu bado ni utata na kama ni hivyo aongee na wakala wa makampuni kama NOKIA,BLACKBERRY,SONYERRICSON,MOTOROLA na mengine yanayofanana nayo kama wakala wake yupo hapa nchini au ayaandikie huko yalipo.Lakini kama ni huduma,basi awaone ndugu zetu VODACOM,TIGO,ZAIN NA ZANTEL.
Nadhani mhesimiwa alimaanisha makampuni niliyotaja hapa mwishoni.

we dare to be constructive! na si kukosoa kila kitu!
 
Back
Top Bottom