Waziri Dr. Milton Makongoro Mahanga na PhD FEKI

Hili swala la viongozi wenye Shahada za kusuka liliwahi kujadiliwa hadi bungeni; Kama sikosei mheshimiwa Shelukindo ndiye aliyeanzisha mjadala huo na waziri Msola akaahidi kulishuhulikia lakini mpaka leo kimya!! Inaelekea wanamtandao ndio wengi wenye vyeti feki ndio maana hatua hazichukuliwi ipasavyo ukianzia na Nchimbi, Lukuvi, Makongoro. David Mattayo, Mzindakaya , Masaburi , Nangale etc. Jambo la kusikitisha ni kwamba usanii wetu tumeupeleka mpaka kwenye E.A. legislative assembly ambako wabunge wa wenzetu ni wasomi kweli kweli na ndio maana wanasema ukihiyo wetu ndio unatufanya tuogope soko la ajira Afrika Mashariki lisiwe huru !! Hii ni aibu, ni vizuri vyeti vya waomba uongozi mwaka 2010 vikahakikiwa na competent authority kabla ya kuruhusiwa kugombea ili tuondokane na aibu hii.

Lukivi wakati fulani alialikwa mahala fulani na watu fulani(watasha) alijikanyaga kutoa just speech ya vote of thanks. Akanirushia wakati huo mie nikiwa undergraduate pale mlimani Dr Huyo.
 
Karume from form 6 leaver straight to PhD holder,tehe tehe tehe!
Huyu nae amefanya nini la maana mpaka apewe PhD?

Kupata Uraisi wa nchi mara mbili kwa kuiba kura wewe unafikiria mchezo???? Tena naona wamempunja... anatakiwa apewe Uprofesa....
 
Lukivi wakati fulani alialikwa mahala fulani na watu fulani(watasha) alijikanyaga kutoa just speech ya vote of thanks. Akanirushia wakati huo mie nikiwa undergraduate pale mlimani Dr Huyo.

Watu wengine hawapendi kuongea mbela ya watu wengi... kuna hata "genuine" wasomi wenye udhaifu huu.. Wakati mwingine huwezi kupima usomi wa mtu kwa kuangalia umahiri wake wa kuongea mbele za watu...
 
Kupata Uraisi wa nchi mara mbili kwa kuiba kura wewe unafikiria mchezo???? Tena naona wamempunja... anatakiwa apewe Uprofesa....


Hahahahaha!Kama ni hivyo kweli anastahili kwa kuwadhibiti ngangari.Lakini mbona Komandoo hawajampa au kwavile anayo tayari???
 
Watu wengine hawapendi kuongea mbela ya watu wengi... kuna hata "genuine" wasomi wenye udhaifu huu.. Wakati mwingine huwezi kupima usomi wa mtu kwa kuangalia umahiri wake wa kuongea mbele za watu...

Elimu ya Lukuvi siijui na ndiyo kwanza nasikia naye ana PhD la kufoji.Kuhusu umahili wa kuongea jukwaani ni kweli kabisa siyo kipimo cha usomi na ndiyo mana watu wa darasa la nne kama kina Makamba wana uwezo mkubwa wa kulimiliki jukwaa,je nao tuwaite wasomi?
 
Kama kuna mtu alistahili kupata PhD hata hiyo ya hisani kama ya JK basi si mwingine bali Mwaibula. Huyu jamaa hata kama alikwenda kudesa sehemu juu ya namna ya kuboresha utaratibu wa usafiri wa daladala Jijini DSM, lakini naamini kazi yake aliyoifanya wengi mtaikubali. Mimi ningekuwa kibosile wa chuo fulani watu wa aina hii wenye impact kwenye jamii ndiyo wanastahili kutunukiwa PhD zinazoitwa za hisani, siyo wanaokwenda kubariki wizi wa kura
 
Kuhusu umahili wa kuongea jukwaani ni kweli kabisa siyo kipimo cha usomi na ndiyo mana watu wa darasa la nne kama kina Makamba wana uwezo mkubwa wa kulimiliki jukwaa,je nao tuwaite wasomi?

Umesema vema. Uwezo wa kumiliki jukwaa. Yaani "art of public speech". Tatizio ni kuwa anamiliki jukwaa kwa kutoa point ya maana 1 na matusi 50. Baada ya hotuba yake ameikwaza jamii zaidi badala ya kuielimisha.
 
Niko na wewe ndugu yangu.No wonder serikali yetu ina ubabaishaji wa kutisha.Inaelekea vichwa vilivyopo serikalini katika ngazi za maamuzi vyote ni fake,ndio maana hakuna hatua yeyote inayochukuliwa.Swala hili tumelipigia kelele kwa muda mrefu sana sasa,lakini the issue has fallen on deaf ears.Ni rahisi,katika sehemu zote za kazi watu walete vyeti vyao for re-assessment.Ni fake unafungwa kwanza kwa kuliibia taifa,na ukitoka jela unapata viboko ukamwambie mkeo,halafu mikakati inaandaliwa ya kulipa fedha ulizoiba.It's as easy as that.

Swala la mawaziri na wabunge kuwa na vyeti feki ni vipi? Milton Makongoro Mahanga na baadhi ya wabunge wana PhD's na masters feki je ni nini inafnywa kurekebisha tatizo?

Makongoro Mahnga alipta phD yake toka "Washington international" university isiyo na campus yoyote isipokuwa ofisi ya mtu mmoja Maryland ambayo inatumika kama campus na head office. Unaweza kupata hiyo Degree kwa wiki tatu je ni haki hawa kuhachwa kuendelea kuwa mawaziri na wabunge?

Jamani leteni mahoni
 
Swala la watu kutumia questionable academic credentials hapa kwetu ni kubwa mno., na linaendelea kukua kwa vile linaonekana kuwa na manufaa kwa vile watu wanaweza kuukwaa uwaziri kwa kutumia credentials za kununua.

Ingawa tumeshalipigia kelele tatzio hili kwa muda mrefu, nadhani serikali yetu haioni haja ya kulichukulia hatua kwa kuwa inazidi kuwapandisha vyeo watu tuliowaongelea kuwa digirr feki, na kuwafnya mawaziri kamili. Mawaziri, wabunge na viongozi wengine wenye kutumia questionable academic credentials walishadiliwa sana kwenye thread hii hapa. Vile vile wahadhiri wa vyo vikuu wenye digrii feki pia walishajadiliwa kwenye thread hii hapa.
 
Huyo Dr. Mathayo ninavyofahamu mimi ni Doctor wa mifugo from SUA (BVM)sasa kama ana-claim ana PhD hiyo ni kiboko
 
Hii nimeipenda sana ila jamaa ana PhD ya SUA kwa inavyosemekana

Umeshajibiwa na post #30 uk.3 na mkuu mujuni2 kuwa Mathayo ni bwana mifugo - dokta wa mifugo. PhD kaipata wapi tena? Anajua hata kuandika thesis huyo Mathayo?
 
Lukivi wakati fulani alialikwa mahala fulani na watu fulani(watasha) alijikanyaga kutoa just speech ya vote of thanks. Akanirushia wakati huo mie nikiwa undergraduate pale mlimani Dr Huyo.

Wana JF naona mjadala sasa unataka kuharibika kwa dataz za kudhania vile. Naomba ieleweke kuwa kuna makundi mawili hapa tunayoyaongelea: La kwanza ni kundi la akina Mzindakaya, JK, Karume, Rwakatare n.k. Hawa wana shahada za heshima tu (honoris causa) siyo za kusomea! Chuo chochote kinaweza mtunukia mtu shahada hiyo ya heshima kwa kutambua mchango wake katika jambo fulani. Siku za nyuma hata baba wa Taifa Mwalimu Nyerere, Spika Adam Sapi, Salim Ahmed Salim, Kaunda na Obote walipewa heshima hiyo na vyuo mbalimbali duniani.

Kundi lenye matatizo ni lile lenye shahada feki na linadai kuzisomea shahada hizo! Kundi hili ni hatari sana maana linaharibu kabisa heshima, sifa na viwango vya elimu nchini. Wafuatao wana vyeti feki vinavyoitia aibu Serikali na nchi kwa ujumla:

(1) Salmin Amour - Ph.D yake ni feki, ya kisiasa. Aliipata Ujerumani Mashariki enzi hizo kwa miezi mitatu tu huku akiwa na cheti cha form four tu!
(2) Pius Ng'wandu - Ph.D yake ni feki. Chuo anachodai kusoma cha Stanford, Marekani hakina kumbukumbu zake. Aliosoma nao huko Marekani, akina Prof. Baregu, wanajua kuwa ana Masters tu!
(3) Mary Nagu - Ph.D yaje ni ya kununua kwenye mtandao.
(4) Emmanuel Nchimbi - Ph.D yake ya uchumi ni ya kununua. Hana uelewa wowote wa economics kichwani mwake.
(5) Makongoro Mahanga - Ph.D yake ya ugavi ni ya kununua kama Nchimbi.
(6) Didas Masaburi - Ph.D yake ilinunuliwa pamoja na ya kaka yake Makongoro.
(7) Norman Sigallah - Ph.D yake ni ya kununua kwenye mtandao.
(8) Mafwenga - Ph.D yake sawa na ya Sigallah
(9) Nangale - Ph.D yake ni kutoka chuo kimoja bomu cha chini ya viwango, London.
(10) Mathayo David - Ph.D ya kujipachika.
(11) Mutamwega - Ph.D yake ni feki, ya kununua. Mhusika hawezi kuandika hata sentensi moja sahihi ya Kiingereza.
(12) Lukuvi - Masters yake ni feki. Kaipata akiwa na sifa za elimu ya darasa la saba na cheti cha ualimu, class C.
(13) Samuel Chitalilo - Vyeti vyake vya elimu ya juu toka Uganda vyote ni feki. Ana kesi ya kujibu mahakamani!

Nimepata taarifa mbalimbali kuhusu vyeti vya Wabunge wafuatao: Sigonda, Capt.Komba, Omari Mzeru na Savelina Mwijage. Nazifanyia kazi. Nitazianika hapa muda muafaka!

Ijabu
 
Wana JF naona mjadala sasa unataka kuharibika kwa dataz za kudhania vile. Naomba ieleweke kuwa kuna makundi mawili hapa tunayoyaongelea: La kwanza ni kundi la akina Mzindakaya, JK, Karume, Rwakatare n.k. Hawa wana shahada za heshima tu (honoris causa) siyo za kusomea! Chuo chochote kinaweza mtunukia mtu shahada hiyo ya heshima kwa kutambua mchango wake katika jambo fulani. Siku za nyuma hata baba wa Taifa Mwalimu Nyerere, Spika Adam Sapi, Salim Ahmed Salim, Kaunda na Obote walipewa heshima hiyo na vyuo mbalimbali duniani.

Kundi lenye matatizo ni lile lenye shahada feki na linadai kuzisomea shahada hizo! Kundi hili ni hatari sana maana linaharibu kabisa heshima, sifa na viwango vya elimu nchini.

Wafuatao wana vyeti feki vinavyoitia aibu Serikali na nchi kwa ujumla:

(1) Salmin Amour - Ph.D yake ni feki, ya kisiasa. Aliipata Ujerumani Mashariki enzi hizo kwa miezi mitatu tu huku akiwa na cheti cha form four tu!
(2) Pius Ng'wandu - Ph.D yake ni feki. Chuo anachodai kusoma cha Stanford, Marekani hakina kumbukumbu zake. Aliosoma nao huko Marekani, akina Prof. Baregu, wanajua kuwa ana Masters tu!
(3) Mary Nagu - Ph.D yaje ni ya kununua kwenye mtandao.
(4) Emmanuel Nchimbi - Ph.D yake ya uchumi ni ya kununua. Hana uelewa wowote wa economics kichwani mwake.
(5) Makongoro Mahanga - Ph.D yake ya ugavi ni ya kununua kama Nchimbi.
(6) Didas Masaburi - Ph.D yake ilinunuliwa pamoja na ya kaka yake Makongoro.
(7) Norman Sigallah - Ph.D yake ni ya kununua kwenye mtandao.
(8) Mafwenga - Ph.D yake sawa na ya Sigallah
(9) Nangale - Ph.D yake ni kutoka chuo kimoja bomu cha chini ya viwango, London.
(10) Mathayo David - Ph.D ya kujipachika.
(11) Mutamwega - Ph.D yake ni feki, ya kununua. Mhusika hawezi kuandika hata sentensi moja sahihi ya Kiingereza.
(12) Lukuvi - Masters yake ni feki. Kaipata akiwa na sifa za elimu ya darasa la saba na cheti cha ualimu, class C.
(13) Samuel Chitalilo - Vyeti vyake vya elimu ya juu toka Uganda vyote ni feki. Ana kesi ya kujibu mahakamani!

Nimepata taarifa mbalimbali kuhusu vyeti vya Wabunge wafuatao: Sigonda, Capt.Komba, Omari Mzeru na Savelina Mwijage. Nazifanyia kazi. Nitazianika hapa muda muafaka!

Ijabu


Dr.Salmin ana thread yake jukwa la siasa na nilikuwa on the way kuuliza udaktari wake.Shukrani kwa kunijuza mkuu.Kumbe hawa wote kina Dr.Salim wana PhD za heshima?Nilidhani mzee alijipinda kwenye mambo ya kimataifa na diplomasia kumbe yaleyale ya kina JK,duh!
Hata Ngw'andu nae?Yani watu hata aibu hawana,wanajitangaza madoctor kumbe ni form 4 leavers tu wakati wenzetu wana ma PhD yenyewe ya msuli lakini hata hawana mpango wa kujulikana.Waafrika kweli misifa ya kijinga inatumaliza!
 
Wana JF naona mjadala sasa unataka kuharibika kwa dataz za kudhania vile. Naomba ieleweke kuwa kuna makundi mawili hapa tunayoyaongelea: La kwanza ni kundi la akina Mzindakaya, JK, Karume, Rwakatare n.k. Hawa wana shahada za heshima tu (honoris causa) siyo za kusomea! Chuo chochote kinaweza mtunukia mtu shahada hiyo ya heshima kwa kutambua mchango wake katika jambo fulani. Siku za nyuma hata baba wa Taifa Mwalimu Nyerere, Spika Adam Sapi, Salim Ahmed Salim, Kaunda na Obote walipewa heshima hiyo na vyuo mbalimbali duniani.

Kundi lenye matatizo ni lile lenye shahada feki na linadai kuzisomea shahada hizo! Kundi hili ni hatari sana maana linaharibu kabisa heshima, sifa na viwango vya elimu nchini. Wafuatao wana vyeti feki vinavyoitia aibu Serikali na nchi kwa ujumla:

(1) Salmin Amour - Ph.D yake ni feki, ya kisiasa. Aliipata Ujerumani Mashariki enzi hizo kwa miezi mitatu tu huku akiwa na cheti cha form four tu!
(2) Pius Ng'wandu - Ph.D yake ni feki. Chuo anachodai kusoma cha Stanford, Marekani hakina kumbukumbu zake. Aliosoma nao huko Marekani, akina Prof. Baregu, wanajua kuwa ana Masters tu!
(3) Mary Nagu - Ph.D yaje ni ya kununua kwenye mtandao.
(4) Emmanuel Nchimbi - Ph.D yake ya uchumi ni ya kununua. Hana uelewa wowote wa economics kichwani mwake.
(5) Makongoro Mahanga - Ph.D yake ya ugavi ni ya kununua kama Nchimbi.
(6) Didas Masaburi - Ph.D yake ilinunuliwa pamoja na ya kaka yake Makongoro.
(7) Norman Sigallah - Ph.D yake ni ya kununua kwenye mtandao.
(8) Mafwenga - Ph.D yake sawa na ya Sigallah
(9) Nangale - Ph.D yake ni kutoka chuo kimoja bomu cha chini ya viwango, London.
(10) Mathayo David - Ph.D ya kujipachika.
(11) Mutamwega - Ph.D yake ni feki, ya kununua. Mhusika hawezi kuandika hata sentensi moja sahihi ya Kiingereza.
(12) Lukuvi - Masters yake ni feki. Kaipata akiwa na sifa za elimu ya darasa la saba na cheti cha ualimu, class C.
(13) Samuel Chitalilo - Vyeti vyake vya elimu ya juu toka Uganda vyote ni feki. Ana kesi ya kujibu mahakamani!

Nimepata taarifa mbalimbali kuhusu vyeti vya Wabunge wafuatao: Sigonda, Capt.Komba, Omari Mzeru na Savelina Mwijage. Nazifanyia kazi. Nitazianika hapa muda muafaka!

Ijabu

Mkuu Ijabu, heshima yako. Asante sana kwa data hizi. Umenikuna kwelikweli maana uliyoyaandika ndiyo ninayoyafahamu. Sikupingi mkuu. Shida yangu ni orodha hiyo uliyotuwekea ambayo ni ya kweli. Anayebisha au kupinga alete data, nasi tutamwaga mtandaoni kila kitu. Orodha hii ina mawaziri, Rais mstaaafu, wakuu wa mikoa, nk. Wote hawa ni watu wazito serikalini tunaotarajia watoe uamuzi mzito kwa masuala kadhaa ya kitaifa. Wenyewe ni vihiyo wanastahili kusimama kizimbani kujibu tuhuma za wazi zinazowakabili. Sikiliza tu hotuba na mangámuzi yao, unatamani kutapika maana ni pumba tupu. Zaidi sana wana kashfa za ngono kibao. Huyo Lukuvi huko Dodoma ndiye kitombi wa mkoa. Sasa, wanalipeleka wapi taifa? Nadhani tunahitaji kiongozi kichaa fulani atupilie mbali uozo huu na kuwafikisha wahuni hawa mahakamani. Nchi inayumba kwa kuongozwa na wahuni. Jitu linataaluma feki na linapata uwaziri, ukuu wa mkoa?!! Taifa gani hili? Lipo kwenye ramani ipi ya dunia? Litaendelea kwa mtaji upi? Kilichobaki ni uanamtandao ili kuishi kiujanjaujanja. Utashaangaa vipi ukiona mawaziri wa design hii wanafanya vikao vya siri kwa kodi ya wananchi ili kumfilisi mzalendo utajiri wake eti kwa sababu anatumia vyombo vyake vya habari kupinga ufisadi!! Tanzania Commission of Universities (TCU) pamoja na wizara ya elimu ipo wapi? Hatuna chombo cha kudhibiti shahada hizi feki? Hivyo TZ ipo kweli kwenye karne ya sayansi na tekelinalokujia chini ya uongozi wa vihiyo hawa? Nimechoka.
 
Mkuu Ijabu, heshima yako. Asante sana kwa data hizi. Umenikuna kwelikweli maana uliyoyaandika ndiyo ninayoyafahamu. Sikupingi mkuu. Shida yangu ni orodha hiyo uliyotuwekea ambayo ni ya kweli. Anayebisha au kupinga alete data, nasi tutamwaga mtandaoni kila kitu. Orodha hii ina mawaziri, Rais mstaaafu, wakuu wa mikoa, nk. Wote hawa ni watu wazito serikalini tunaotarajia watoe uamuzi mzito kwa masuala kadhaa ya kitaifa. Wenyewe ni vihiyo wanastahili kusimama kizimbani kujibu tuhuma za wazi zinazowakabili. Sikiliza tu hotuba na mangámuzi yao, unatamani kutapika maana ni pumba tupu. Zaidi sana wana kashfa za ngono kibao. Huyo Lukuvi huko Dodoma ndiye kitombi wa mkoa. Sasa, wanalipeleka wapi taifa? Nadhani tunahitaji kiongozi kichaa fulani atupilie mbali uozo huu na kuwafikisha wahuni hawa mahakamani. Nchi inayumba kwa kuongozwa na wahuni. Jitu linataaluma feki na linapata uwaziri, ukuu wa mkoa?!! Taifa gani hili? Lipo kwenye ramani ipi ya dunia? Litaendelea kwa mtaji upi? Kilichobaki ni uanamtandao ili kuishi kiujanjaujanja. Utashaangaa vipi ukiona mawaziri wa design hii wanafanya vikao vya siri kwa kodi ya wananchi ili kumfilisi mzalendo utajiri wake eti kwa sababu anatumia vyombo vyake vya habari kupinga ufisadi!! Tanzania Commission of Universities (TCU) pamoja na wizara ya elimu ipo wapi? Hatuna chombo cha kudhibiti shahada hizi feki? Hivyo TZ ipo kweli kwenye karne ya sayansi na tekelinalokujia chini ya uongozi wa vihiyo hawa? Nimechoka.


Mkuu una maana kuna Rais mstaafu Tanzania ana shahada feki?Mwaga dataz mkuu ni nani huyo na ni shahada gani?
Binafsi sioni ulazima wa mtu mwenye bachelor kwa mfano kuhangaika na ma PhD feki ili imuongezee CV ya uongozi.Bachelor inatosha sana kwa mtu kuwa waziri ama hata Rais ilimradi tu awe na upeo na uwezo wa kutosha wa kiuongozi,mchapakazi na uchungu wa kweli kwa umasikini wa watanzania.
Kama mnaitaka hiyo status quo si muende mkakate misuli basi?Mary Nagu kuona Migiro anaheshimika na PhD yake nae akaamua kuichonga fasta!!
 
Hahahahaha!Kama ni hivyo kweli anastahili kwa kuwadhibiti ngangari.Lakini mbona Komandoo hawajampa au kwavile anayo tayari???

Tatizo halikuwa aibu No. Iweje mbunge, waziri, mkuu wa mkoa aone aibu? aliombaje kura? Tatizo lilikuwa Ung'eng'e. Sasa kama ingekuwa ni kichina ama kiarabu au kihabeshi ningeelewa. Lakini Dr halafu Goodmorning Maimuna. Hapana.
 
Tatizo halikuwa aibu No. Iweje mbunge, waziri, mkuu wa mkoa aone aibu? aliombaje kura? Tatizo lilikuwa Ung'eng'e. Sasa kama ingekuwa ni kichina ama kiarabu au kihabeshi ningeelewa. Lakini Dr halafu Goodmorning Maimuna. Hapana.

Ijabu kanipa hamasa sana juu ya suala hili. Wote aliowaeleza kweli wana vyeti feki na hata ukiongea nao, ni vihiyo vihiyo wa kutupwa! Naomba niongeze majina mengine kwenye listi la Mhe. Diodorus Buberwa Kamala, Mbunge wa Mkenge na Waziri wa A. Mashariki. Huyu bwana kasoma Mzumbe kama Nchimbi ambako mtandao wa vyeti feki ulianzia na Mkuu wa Chuo hicho Bw. Warioba. Ph.D yake ni feki, ni ya kununua kama hizo za wenzake aliowataja Ijabu. Hata kwenye Bunge la A. Mashariki tunaambiwa anapwaya ile mbaya. Naibu wake, Mohamed Aboud, yeye ndo balaa maana ni form four failure na CV yake inasema uongo kuwa ana diploma ya Uingereza! Wote ni Ze Komedi mbele ya Wakenya, Waganda, Warwanda na Warundi!

Yupo huyu mama wa Kibaha, Zaibab Gama. Anajiita Dk. wakati ana diploma ya radiology tu! Kuhusu Mbunge Savelina Mwijage (Viti Maalum, Kagera), huyu ana matatizo makubwa maana anatumia jina la marehemu. Taarifa zote zilitoka gazetini, lakini analindwa. Hawezi hata kuandika jina lake, lakini ni Mbunge. Anayebisha aje na ushahidi maana huyu mama namfahamu miaka mingi akiwa mfanyakazi wa ndani wa Mhindi Bukoba.

Namfahamu sana Mbunge Sigonda. Ni mtu wa usalama wa Taifa aliyeishia darasa la nane. Leo naambiwa ni Dk.! Hebu tupe dataz Ijabu na wana JF wengine. Capt. Komba yeye ni msanii na mwizi asiyestahili kujadiliwa hapa maana anawaibia hata wasanii wenzake dani ya TOT. Mzeru wa Morogoro yeye ni mafix moja kwa moja. Hana udaktari wowote! Alijipachika udaktari kuombea ubunge na unaibu waziri kwa JK!
 
Hili la vyeti feki halijaanza leo. Kwenye miaka ya '80 kuna viongozi wa juu sana kitaifa ambao hawakuwa hata na digrii ya kwanza walikwenda Ujerumaini (ya Mashariki -ya kikomunisti -wakati huo) kwa miezi michache wakarudi wameishakuwa madaktari. Kuna wengi walihoji kuhusu udaktari wao lakini nyakati hizo ilikuwa ni hatari kuhoji sana mambo ya watu kama wale. Mpaka hii leo kila mtu anendelea kuwapa hizo heshima za udaktari, hata wale ambao tunajua ukweli wa mambo. Kama wao walikubalika kwa nini na wengine wasiige? Ni tatizo la kimfumo na litatugharimu sana. Madaktari tunao wengi sana lakini tuna uhaba mkubwa wa maandiko au vitabu vya kitaaluma. Ni ajabu!!!! Hivi tuna sababu ya kushangaa kwa nini mambo yetu mengi hayana mwelekeo? Ni matokea ya digrii feki, vyeti feki, mitihani kuvuja, ajira nyeti kwa wasiostahili, ........ unaweza kuendelea. Haya mambo yakiendelea muda mrefu unakuwa utamaduni wa taifa unaorithishwa kutoka kizazi kimoja kwenda kingine.
 
Kasheshe, tufanyeje wana JF???????????????????? haya mambo sishwari ni hatari.
 
Back
Top Bottom