Waziri Chami nae kalazwa India

Status
Not open for further replies.
"Haumwi kama watu wanavyodhani, ni kwamba amejiskia vibaya kama watu wengine wanavyoweza kujiskia na hivyo amekwenda hospitali kwa ajili ya uchunguzi zaidi" hii ni kauli ya Naibu Waziri Kijana wa viwanda na biashara ndg Razaro Nyarandu alipoulizwa juu ya afya ya Bosi wake Dr Chami.

Hapa ninajiuliza maswali kadhaa!
Mosi, hivi Nyarandu anaposema anajiskia kama wanaweza kujiskia watu wengine, je hao watu wengine wakijiskia nao waende India?
Pili, hapa kwetu hakuna madaktari wa kufanya uchunguzi wa mtu akijiskia kawaida?
Tatu, anataka kutuambia kodi zetu zimewafanya wajisahau namna hiyo hata kama mtu akijiskia ugonjwa wa kawaida akafanye vipimo nje ya nchi?
Nne, inamaana viongozi wa nchi hii wanajua udhaifu wa hospitali zetu na hivyo hawaamini kuzitumia hata pale wanapojiskia kuumwa kawaida tu?

Kwa mbwembwe hizi za wabunge wetu.....!!!!! Naomba wataalamu wa mahesabu wanijuze ni lini kikao cha ngapi cha Bunge la Tanganyika kitafanyika 'hospitalini' India.....!!!!!!
 
"Haumwi kama watu wanavyodhani, ni kwamba amejiskia vibaya kama watu wengine wanavyoweza kujiskia na hivyo amekwenda hospitali kwa ajili ya uchunguzi zaidi" hii ni kauli ya Naibu Waziri Kijana wa viwanda na biashara ndg Razaro Nyarandu alipoulizwa juu ya afya ya Bosi wake Dr Chami

Kama kujisikia vibaya kunamfanya aende India then, akipatikana na ugonjwa unaomfanya ajisikie vibaya anaona atapelekwa Marekani kutibiwa.. Hii ndio Tz, ukipiga mahesabu ya gharama za matibabu za mawaziri hao watatu utakuta ni zaida ya bajeti ya wizara ya Afya yenyewe


Yaani ni kweli kabisa ndugu unachokisema, sisi tuko jikoni na mpaka sasa waziri fulani ameshatumia US$ 65,000 KWA MATIBABU, hii tz jamani inahitaji mabadiliko, we really need changes jamani!!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom