Waziri Bernard Membe kalipotosha Bunge kuhusu mpaka wa Tanzania na Malawi kwenye Ziwa Nyasa

Haya ndio mambo ya Misri kudai kuwa ni marufuku kwa Tanzania kutumia maji ya ziwa Victoria huko Shinyanga na Mwanza - Sababu, mikataba ya wakoloni!
 
Aliyekomaa nalo ni huyu Membe na sijui kwa nini amelichukua so public kiasi hiki. Hakuwa na sababu za kulipeleka Bungeni kiasi kile halafu unafika huko kwa sababu hukujiandaa majibu yenyewe yanakuwa paragraph mbili na hizi zenye makosa wakati huohuo kuna mazungmzo yanaendelea. Wenzake wote tangu Nyerere walijua kuwa hili si rahisi kiasi hiki na kulipa public interest kama linavyomtokea puani sasa.

Yeye angefanya diplomacy ya kimyakimya kama anavyofanya kimyakimya kwenye suala la OIC na husikii kelele zinamsakama.

Lakini hata leo Membe akitaka kulikoroga la OIC basi nalo alipe publicity kama alivyofanya hili la Malawi. Nadhani hili ilmempa a sounding class.

kwenuye kauli au maandishi uliyoongea yenye tija katika hii thread ni hii kwamba Waziri wa Mambo ya Nje na Bunge letu likiongozwa na hiyo kamati ya ulinzi na usalama, kupiga kelele saana kwenye kitu ambacho kina zungumzika, labda iwe kwa sababu za kisiasa kutuzuga na vita vya Malawi , kumbe huku watu wanataka kuhairisha uchaguzi au kukomba hela.
 
mkimaliza kubisha kisiasa,ki-raman,ki-latitude...mtatuambia...ikifika muda wa kuhakikisha wakina ful kunjombe wanafua nguo zao kwa maji yale...hapo ndo patachimbika...
Kama ni la kwao mia aslmia...walibebe walipeleke ikulu yao wawe wanaliona muda wote...

Wewe kama unajijua n mnyasa...omba mungu pasichimbike...muda si mrefu nita mwaga humu majina ya attached intelligence ambao ni malawian....
 
Aliyekomaa nalo ni huyu Membe na sijui kwa nini amelichukua so public kiasi hiki. Hakuwa na sababu za kulipeleka Bungeni kiasi kile halafu unafika huko kwa sababu hukujiandaa majibu yenyewe yanakuwa paragraph mbili na hizi zenye makosa wakati huohuo kuna mazungmzo yanaendelea. Wenzake wote tangu Nyerere walijua kuwa hili si rahisi kiasi hiki na kulipa public interest kama linavyomtokea puani sasa.

Yeye angefanya diplomacy ya kimyakimya kama anavyofanya kimyakimya kwenye suala la OIC na husikii kelele zinamsakama.

Lakini hata leo Membe akitaka kulikoroga la OIC basi nalo alipe publicity kama alivyofanya hili la Malawi. Nadhani hili ilmempa a sounding class.
Nikupateje Wacha kumung'unya maneno wewe.
Umemjibu Yericko Nyerere kwamba ampelekee Membe hizo taarifa sahihi alizokuwa nazo ili apatiwe tuzo. Nami nikakushauri kwamba kwanini usimpelekee wewe hizo latitudes sahihi ili nawe upate tuzo? wala usitafute kuhamisha goal post kuelekea kwa membe kwamba ndiye anakomaa, yes hata akikomaa ni wajibu wake kama waziri wa mambo ya nje.

Ambacho wengi wetu tunajiuliza hapa wewe unakomaa kwa maslahi ya nani? tukisema una dalili za umalawi unang'aka. Kama kweli wewe ni mzalendo wa kweli na una nia thabiti ya kuisaidia nchi yako, kwanini usimpelekee waziri membe latitudes sahihi ili aweze kuwa na hoja ya msingi katika meza ya mazungumzo? na unatambua kikao kingine ni tarehe 20/08/2012 kwahiyo bado hujachelewa kupeleka findings zako ili kuisaidia Tanzania kama kweli wewe ni mtanzania.
 
Last edited by a moderator:
Nikupateje Wacha kumung'unya maneno wewe.
Umemjibu Yericko Nyerere kwamba ampelekee Membe hizo taarifa sahihi alizokuwa nazo ili apatiwe tuzo. Nami nikakushauri kwamba kwanini usimpelekee wewe hizo latitudes sahihi ili nawe upate tuzo? wala usitafute kuhamisha goal post kuelekea kwa membe kwamba ndiye anakomaa, yes hata akikomaa ni wajibu wake kama waziri wa mambo ya nje.

Ambacho wengi wetu tunajiuliza hapa wewe unakomaa kwa maslahi ya nani? tukisema una dalili za umalawi unang'aka. Kama kweli wewe ni mzalendo wa kweli na una nia thabiti ya kuisaidia nchi yako, kwanini usimpelekee waziri membe latitudes sahihi ili aweze kuwa na hoja ya msingi katika meza ya mazungumzo? na unatambua kikao kingine ni tarehe 20/08/2012 kwahiyo bado hujachelewa kupeleka findings zako ili kuisaidia Tanzania kama kweli wewe ni mtanzania.

Huyo ni kibaraka wa Malawi, na anatumia kila ushawishi kuwaaminisha watanzania uongo wake,
Ukweli haupingiki kile nilichomueleza pale ndio msimamo wa Tanzania na ndio ukweli ambao histori ya dunia inatambua na walimwengu wanatambua!

Mwacheni aendelee kupepeta uongo wake hapa!
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Mwita,
Tasi hana gamba; mimi ni mzalendo halisi niashi kwa kipato halali sitegemei ajira kutoka serikali ya JMT; CCM wala sifanyi biashara na vyombo hivyo, mimi ni clean ila nina wasiwasi sana na watu wa kaliba yako wanaopiga kelele gamba la kobe ilhali wao wenyewe wamevaa magamba ya kasa; hapa nilimpongeza Yericko Nyerere kwa kuongea ukweli na kuonyesha uzalendo na utaifa, pitia posti za vijana wako wa Chadema kina matola, precise pangolin na wengine tu; badala ya kuwakemea vijana wako umekimbilia kunishutumu, mimi nilipitia JKT najua nini maana ya utaifa na unazi wa kichama, kwangu taifa mbele period!!! I trust you don`t be simple just because you want to side with some stupid and simple minded makamanda

Chama
Gongo la mboto DSM

Mkuu chama unapozungumzia masuala ya kitaifa halafu unaanza kuchomekea vijembe hapo itakuwa vigumu kusalimika na mashambulizi ya ku-counter.
Kwahiyo ni muhimu kujiepusha na lugha yoyote yenye kuudhi ama kejeli kwa wenye itikadi tofauti na wewe tunapozungumzia masuala ya nchi yetu, mipaka ya nchi yetu. Otherwise nimekusoma, washauri na wenzako wajitahidi kujitegemea kama wewe, hii ya kutegemea huruma ya chama ndio inawafanya wageuke kuwa manamba.
 
Last edited by a moderator:
Ngoja nilale tutakutana asubuhi.
Siku mpya imeanza, ngoja sasa nizane kujibu hoja zenu ambazo ni rahisi sana kama ifuatavyo.

Wewe Mmalawi usitake kutufanya sisi wabongo hatujuwi haya mambo, kukufahamisha ziwa Nyasa kwa juu liko latitude ya 9 degree na dakika 40 kwa longitude ya 34 degree na dakika 15 (kwenye lamani ya QDS 273/2) ambayo inaitwa Lupila.

Kusini ziwa liko kwenye longitude ya 34 degree na dakika 40 ambalo ni eneo la Lundu kwa wenyeji wa huko watakuwa wanapafaham na latitude yake ni 10 degree na dakika 45 (QDS 297-1 Lituhi).
Naomba nikukumbushe kitu kimoja unapotaja hizi point huwezi kutaja latitude pake yake bila kutaja longitude yake na kwa UTM Ssystem huwezi kutaje X- cordinate bila Y - cordinate na ARC1960 kwa WGS84 ni conversion tu ndugu yangu 300m kwa X na 200m kwa Y.

Narudia tena hoja niliyoirudia na sintachoka kuirudia. naongeza tena kwamba aliyesema watanzania ni wavivu wa kusoma au kutafiti hakukosea tena ni Rais wenu wa thrid phase (Mkapa). Sasa na wewe hapa umeona umeeleza kiasi kwamba mwenzako Yeriko Nyerere naye karidhika na kukupongeza.

Asante kwa ufafanuzi mkuu! Huyo mmalawi wakuogopwa!

Hapa mwenzako Yeriko hata kama si mtaalamu hata flow ya thread haikumsaidia hata kama coordinate zako zingekuwa sahihi.

Kwa sababu hata kwa hizi coordinate zako bado hujafuta kosa la Waziri Membe kule Bungeni ambalo yeye anasema umiliki wetu wa ziwa unaanzia kwenye latitude 9 hadi 11. Wewe unasema ni latitude deg. 9 min 40 yaani unapopaita Lupila hadi lat deg. 10 min. 45 unapopaita Lituhi.

Tukiacha huo ujinga wa Yeriko sasa tuje kwenye ujinga wa hivi vipimo vyako na hiyo ramani yako. Umesema kwamba liko 9 degree na dakika 40 kwa longitude ya 34 degree na dakika 15 na hapo ukapaita Lupila.

Huu ni uongo mkavu kwa sababu hiyo coordinate iko kilomita 44.2 toka ziwani na iko kilomita 38.64 tu kutoka Njombe.
Kusini unakosema ziwa linaishia kwenye longitude ya 34 degree na dakika 40 na latitude 10 degree na dakika 45.

Hapa ni kweli ni karibu na ziwani ni kweli ni kilomita 21.8 kutoka Lithuli unapopataja. Lakini wewe ungempa Membe hizi coordinate zako basi ungekuwa umechemsha kuliko yeye maana yeye haitambui kwamba Mbamba Bay ni yetu kwa kilomita 33.7, sasa wewe hapa umeongeza kutoitambua kwani umeitupa Mbamba Bay nje ya umiliki wa tanzania kwa kilomita 63. Yaani umeongeza makosa ya kilomita 29.3 kutoka kwenye makosa ya Membe kwenye hansard.

Ndipo hapa ninapokuwa na wasiwasi kama Tanzania itaweza kushinda kesi hii kama kuna rundo la watu wanaokurupuka kama watetezi wakati hawajui wanachotetea.

Membe hakukosea kusema lile ziwa limelala kutoka kaskazini kwenda kusini, kitu ambacho mtoto wa darasa la nne anakijua. Hivyo alipotaja latitude maana yake ni kuanzia point ipi maana kidunia kaskazini unapima kwa latitude.

Mimi naweza kuamini kitendo cha kuona ziwa liko shared kule Mozambique kimewachanganya na kuwafanya muige. Kwa sababu ni kweli kule Mozambique wanaligawana ziwa na Malawi, si kote bali kuanzia latitude ya 11.57281 hadi 13.4791 na ukiangalia utaona kweli hapo kuna horizontal boundary demarcation.

Endeleeni kukurupuka tuwajibu mikurupuko yenu ili isionekane kuwa watanzania wote ni wakurupukaji na hasa ilivyoripotiwa kwenye thread moja humu kuwa hata wamalawi na mataifa mengine yanasoma JF!
 
Ujuha wa wamalawi na wanaowaunga mkono umelala kwenye imani ya kile wakiitacho makubaliano ya wajerumani na waingereza,wala si makubaliano wenyeji wa mwambao wa ziwa hilo,hata kama akili yako haijakomaa ni mahakama ya nguruwe pekee inayoweza toa haki kwa Malawi kumiliki ziwa lote wakati hilo ziwa linagusa ardhi ya nchi nyingine inayokaliwa na watu ambao wanayo haki ya asili kutumia maji ya ziwa hilo. Iwe Membe kakosea malatitude na malongitude au kapatia ukweli unabaki kama ulivyo kuwa ziwa ni mali ya wale wanaoapakana nalo nusu kwa nusu

Ujuha ulioonyesha kwamba kama mkataba wa wajerumani ulipitwa na wakati hayo makubaliano na wenyeji ambayo yamo akilini mwako yalifanyika lini wakati wenye mawazo kama wewe humu wametetea kwamba hata Nyerere hakuwahi kukaa meza moja na Banda kuhusu hili katika uhai wao.
 
Temporary treaty aimed at resolving the boundaries between British sphere of influence and German sphere of influence.
Only lake victoria was marched upon the delimiting line between them.
The rest of interterritorial waters were not, simply because there were no lands (habitable) between Tanganyika and Nyasaland.
The Lake was being treated by both as international waters. There were German and British gunboats sailing freely in those waters prior to 1914.... why do you think Britain allowed German vessels in their waters? Or vice versa?

Hakuna neno temporary ndani ya ule mkataba na hizi assumption zako ni kutokana hukujishughulisha hata kuusoma mkadhani mkija na imagination zenu zitawafurahisha wenye kupenda mawazo yenu..
 
Mwacheni aendelee kupepeta uongo wake hapa!

Mkuu Yericko Nyerere hili la kupepeta uongo hatutamuachia kamwe Nikupateje aendelee kupotosha watu.

Kama ana hoja ya msingi tutakubaliana naye, na kama kweli ni mzalendo basi awasilishe findings zake kwa waziri wa mambo ya nje ili kutia uzito katika mazungumzo. Ni jambo la ajabu kama tutakuwa na watu wanajiita wazalendo wa namna yake lakini hawatumii taaluma zao kuisaidia nchi. Hapo uzalendo ama uraia wao ni lazima utakuwa questionable!!
 
Last edited by a moderator:
Siku mpya imeanza, ngoja sasa nizane kujibu hoja zenu ambazo ni rahisi sana kama ifuatavyo.

Unajibu hoja zao akina nani?? kwamba wewe si mmoja wao? (Watanzania)

aliyesema watanzania ni wavivu wa kusoma au kutafiti hakukosea tena ni Rais wenu wa thrid phase (Mkapa).

Sawasawa ni kweli raisi wetu alisema hivyo. Kwakuwa wewe si mtanzania hiyo haikuhusu. We si mnyasa!!??

Mimi naweza kuamini kitendo cha kuona ziwa liko shared kule Mozambique kimewachanganya na kuwafanya muige.

Kweli aisee watanzania wamechanganyikiwa wakati ninyi wanyasa mkishangilia kujichukulia ushindi wa mezani.

All in all pamoja na kujaribu kujificha kwenye ngozi ya utanzania, sina sababu ya kutoamini kwamba wewe ni mnyasa na unachofanya hapa ni kujionyesha kwamba tayari wamalawi mmeshashinda hii vita ya mpaka bila kujua kwamba katika hili hamuwezi kujichukulia point za mezani.

Haya makosa yaliyofanywa na waziri membe kule bungeni yasikudanganye kwamba ndio Tanzania imeishiwa cha kuzungumza ama kutetea mpaka wake.
Kama utakuwa mkweli wa nafsi yako ukakumbuka kilichotokea baina ya Mwl Nyerere na Kamuzu Banda mwanzoni kabisa mwa miaka ya 60 ndipo utafahamu ugumu wa malawi kumiliki ziwa lote.
 
Nikupateje Wacha kumung'unya maneno wewe.
Umemjibu Yericko Nyerere kwamba ampelekee Membe hizo taarifa sahihi alizokuwa nazo ili apatiwe tuzo. Nami nikakushauri kwamba kwanini usimpelekee wewe hizo latitudes sahihi ili nawe upate tuzo? wala usitafute kuhamisha goal post kuelekea kwa membe kwamba ndiye anakomaa, yes hata akikomaa ni wajibu wake kama waziri wa mambo ya nje.

Ambacho wengi wetu tunajiuliza hapa wewe unakomaa kwa maslahi ya nani? tukisema una dalili za umalawi unang'aka. Kama kweli wewe ni mzalendo wa kweli na una nia thabiti ya kuisaidia nchi yako, kwanini usimpelekee waziri membe latitudes sahihi ili aweze kuwa na hoja ya msingi katika meza ya mazungumzo? na unatambua kikao kingine ni tarehe 20/08/2012 kwahiyo bado hujachelewa kupeleka findings zako ili kuisaidia Tanzania kama kweli wewe ni mtanzania.

Mwita,

Kama ni suala la uzalendo basi mshabiki wa Yanga ana uzalendo usiopimika siku Yanga inapocheza na Simba. lakini uzalendo huo kamwe hauwezi kugeuka na kuwa mbinu ya kuwashinda Simba kama hoja za kuiandaa yanga ni hafifu na hata kama wanaYanga watakuwa na uzalendo hadi ukiwachanja ikatoka damu ya njano kweny emishipa yao.

Kinachoongelewa ni kosa lililomo kwenye Hansard kwamba coordinate alizo-submit Waziri membe zina makosa. Membe angekuwa ameenda na projector mle bungeni ninaamini wapo wabunge ambao wangemuuliza palepale.

Kuna mbunge mmoja kwenye House of Commons aligundua kosa la Waziri wa Ulinzi alipotoa statement kwamba taarifa aliyopelekewa Tony Blair ilisema kwamba mabomu ya Sadam Hussein yalienda range ambayo likipigwa Baghdad bomu litafika London.

Range hii ilionekana nimakosa na Tony Blair aliomba masamaha kulisha uongo ule. Sasa sijui nyinyi hapa ndiyo niwaulize mnakomaa nini.

Thread zima mimi ninakomaa si kwa sababu ya madai ya Malawi kuhusu ziwa lile. bali ninakomaa na utetezi wa kitoto ambao hadi sasa sijaona thread au hata comment moja inayoonyesha kuwa tuna hata tone la matumaini ya kulipata lile ziwa.

Ungekuwa unapitia thread hii yote basi wenzako wameshaonyesha jinsi Membe ambavyo angeweza kuepuka kosa hili. Soma hapa.

Bahati nzuri Membe mwenyewe kwa kuilaumu na kuiponda JF basi ametuhakikishia kwamba yeye ni msomaji mzuri wa mtandao huu.

Hivyo, ni uamuzi wake kuchukua ama kuacha ushauri wetu.
 
Mkuu chama unapozungumzia masuala ya kitaifa halafu unaanza kuchomekea vijembe hapo itakuwa vigumu kusalimika na mashambulizi ya ku-counter.
Kwahiyo ni muhimu kujiepusha na lugha yoyote yenye kuudhi ama kejeli kwa wenye itikadi tofauti na wewe tunapozungumzia masuala ya nchi yetu, mipaka ya nchi yetu. Otherwise nimekusoma, washauri na wenzako wajitahidi kujitegemea kama wewe, hii ya kutegemea huruma ya chama ndio inawafanya wageuke kuwa manamba.

Mkuu Mwita
Hapo kwenye umenionea bure mimi nilikuwa nasisitiza utaifa tu vijana wako ndio wanatumia silaha za sumu sijui maslahi ya nani wengine naona ni vizazi vya wamalawi wanachoongea wanajua wenyewe.

Chama
Gongo la mboto DSM
 
Hata Misri walikuja na hoja kuwa Tanzania haturusiwi kutumia maji ya ziwa victoria kwa matumizi zaidi ya kunywa.Lakini leo kule shinyanga ninayo bustani kubwa kishenzi inatumia maji ya ziwa victoria.Kwa taarifa yenu aliyeukataa huo mkataba wa kishenzi ni Mh.Ngoyai Lowassa EDUARDO wakati akiwa waziri wa maji.Chezea LOWASSA WEYEEEEE MALAWIEEEH!!! Utatoka manundu
 
Nimeamua kuiweka hii kwenye separate thread kwa sababu nimeona ina extra concept kulingana na ile ya jana.

Wakati nanunua gazeti nilitumaini kabisa Membe atakuwa na hoja ya ku-convice kwani humu JF mnaongea tu kama mimi. Kwa wale waliosoma RAIA MWEMA wafungua attached paper kwenye ukurasa wa iv. Ndipo anaeleza msimamo wa Serikali kuhusu mpaka wa Ziwa Malawi.

Nakiri kwamba hata wakati naleta thread ile ya kwanza, nilitumaini Bernard Membe atakuwa ameongelea findings ambazo zingetushawishi na mimi nisingesita kuungana kwenye nia ya kukidhi madai haya ya Lake Malawi.

Lakini baada ya kusoma speech ya Membe basi matumaini yote ya kulipata Lake Malawi yamenitoka. Narudia sipingi Tanzania kupata sehemu ndogo ya Lake Malawi kama baadhi mnavyoropoka. Na hata mnavyoropoa wengine hainipi matumani ya kulipata hilo Ziwa. Lakini aliyenisikitisha zaidi ni Waziri Membe na sasa kwangu ni dhahiri kwamba tusahau kabisa kulipata Ziwa hili.

Siku moja nilifanya hesabu ubaoni nikapata jibu na baadaye nikaongeza madoido mwalimu akanikata maksi akasema "Kujitawaza kwingi mwisho unashika kinyesi". Naona ndugu yetu Waziri Membe kaingia katika mtego huu. Kwa nini nasema hivi? Ninanukuu majibu yake kama ifuatavyo:


****
Mheshimiwa Spika,
Lipo tatizo la muda mrefu kati yetu na nchi jirani ya Malawi linalohusiana na mpaka kwenye Ziwa Nyasa. Tatizo lenyewe ni kwamba Malawi wanadai kwamba ziwa lote kaskazini ya Msumbiji kuelekea Ruvuma na Mbeya ni mali yao kwa mujibu wa Mkataba wa Heligoland uliowekwa mwaka 1890.

Mheshimiwa Spika,
Tanzania kwa upande wetu tunasema kuw ampaka wa kweli kati yetu na malawi unapita katikati ya ziwa hivyo kufanya
eneo lote la Kaskazini Mashariki ya Ziwa kati Latitude digrii 9 na digrii 11 kuwa mali ya Tanzania kwa mujibu wa mkata huouo wa Heligoland wa mwaka 1890 ambao ulikubali kuwa kwa vile kuna maeneo ya mpaka ambayo hayana mantiki, pande zinazohusiana zikutane na kurekebisha. Aidha tunazo ramani ambazo waingereza wenyewe walipitisha mpaka katikati kama ulivyo mpaka kati ya Msumbiji na Malawi.
****

Nimemalizia hapa kwa sababu mengine yanayofuata ni diplomatic process. Sasa hapa tuchambue hotuba hii ya Membe. Binafsi nimeusoma mkataba wote wa Heligoland na wala si alichokisema Membe. Kama membe anataka kuikomboa Tanzania walau tupate sehemu ya Ziwa basi washauri wake wamempotosha kutumia mkataba ule ambao hautetei hoja yake hata kidogo.

Lakini pia Membe ni mmoja wa wanaodhani watanzania wa sasa hawajui kufukua mambo na ndiyo maana kwenye thread yangu nimesema tutumie usomi wetu. Membe ametaja kwamba sehemu ya ziwa kati ya Latitude digrii 9 na digrii 11 ni mali ya Tanzania.

Hapa ndipo Membe ameumbuka umbuko ambalo hatalisahau. Kwa nini nasema kaumbuka. Kaumbuka kwa sababu geography ya Tanzania wote tunaijua. Ncha ya juu kabisa ya Lake Malawi iko kwenye coordinate { S9.49214 E34.03563} ambapo ni only 7.0km kutoka kijiji kiitwcho Matema kilichopo kwenye coordinate { S9.49601 E33.97215}.

Ukiangalia coordinate hizi maana yake ni kwamba Ziwa Malawi linaishia kwenye Latitude 9.49214. Sasa hapa Membe anasema eti ni kuanzia Latitude 9. Kwa maana hii ya Membe kama Ziwa ni letu kuanzia latitude 9 maana yake ni kwambaMmembe kafanya makosa kwa kulirefusha ziwa hili kwa umbali wa 54.4km kuelekea kaskazini!

Watu mnaotoka kusini hasa Mbeya mnafahamu sehemu iitwayo Matamba. Hapa coordinate zake ni { S9.01171 E34.09959}. Kwa mujibu wa Membe, hii Matamba ingekuwa imeguswa na Ziwa hili!

Hakika waliomletea Membe hizi data wamemvuruga kuliko kulietengeneza suala hili. Ziwa Malawi au Nyasa linaishia kwenye Latitude 9.49214 kama nilivyosema hapo juu. Hapa membe kadanganya Bunge na kadanganya watanzania kasi kwamba sijui sasa ni nani mwenye nguvu ya kulitetea hili.

Tuje sasa kwa upade wa kusini yaani unaotambuliwa na membe kama sehemu yaetu ya Ziwa. Membe anasema sisi mali yetu ni mpaka kwenye latitude 11. Sijui wangapi mmeona kosa hili la mwaka. Unaposema kwamba unaishia hapa kwenye Latitude 11, je mnaotetea hoja hii mnaelewa madhara yake? Kama hamyajui basi mimi nayasema hapa.

Kama Membe kasema Bungeni kwamba tunaishia kwenye Latitude 11 basi maana yake pale ni kaskazini ya sehemu iitwayo Liuli ambayo iko { S11.05023 E34.63908}. Kumbe, Mwanakijiji wa Liuli haruhusiwi kuvua samaki kwenye ziwa lile kwa sababu ni sehemu ya Malawi, kwa mujibu wa Waziri Bernard Membe!

Yaani mwanakijiji huyu wa Liuli, anakuwa amekiuka mpaka kwa kilomita 6.6 kwa mujibu wa Serikali anayoshiriki membe wala si kwa mujibu wa Serikali ya Malawi!

Nimeanza na mfano huo wa Liuli ambao najua wengine hampaju ahapo. Sasa tuje kwenye mfano ambao wengi mnaujua na mmeutumia kunipinga humu na kuniita mimi ni mmalawi.

Mfano wenyewe ni wa Mbamba Bay. Ndiyo maana nimesema kajipangeni hii kesi tutajikuta tunasambaratika tukidhani tunatetea huku tunajiangamiza. Narudia kusema kwa mujibu wa hotuba ya Waziri Membe ni kwamba umiliki wetu wa Ziwa hili unaishia kwenye latitude 11. Mbamba Bay iko kwenye coordinate { S11.30519 E34.80449}.

Hii maana yake ni nini? Maana yake ni kwamba Mbamba Bay haiko katika eneo linalotambuliwa na Waziri Membe kwa latitude degree 0.30519!

Uki-convert hizi latitude kwenda kwenye kilomita basi maana yake Membe haitambui Mbamba Bay kwani iko 33.7km nje ya eneo ambalo Tanzania tunamiliki ziwa!

Waziri membe pia inaelekea kuwa hajui mpaka unavyopita pale Msumbiji. yeye anasema kule ni nunu kwa nusu lakini wote fungueni ramani muone kama hilo nalo lina ukweli. Mpaka wa Msumbiji ni nusu kwa nusu kuanzia kwenye latitude 11 had 13 lakini kuanzia hapo kueleka kule chini kusini ziwa lote liko sehemu ya Malawi na linaishia kwenye coordinate {S14.44635 E35.23539} ambako ni latitude 14.44635.

Hivyo, tujenge hoja zinazojikita kwenye ukweli na tusishabikie mambo kama vile Simba na Yanga. Hapa hatufanyi ushabiki. Hapa tunasaidia kujenga na kupima hoja kama kweli tunaweza kuisaidia nchi yetu kupata sehemu ya ziwa hili.

Ninasubiri kwa hamu kuona mtakuja na hoja gani kuhusu hizi findings zinazochambua hotuba ya Membe na matokeo yake niliyoeleza humu.

Wanyasa mpo wengi sana humu, mnaongea mpaka povu linawatoka lakini hiyo haitawasaidia na ushoga wenu, hapa ni kichapo kwa kwenda mbele then ndo mtakuja kwenye mazungumzo mkiwa na p.o.p na ngeu kibao. hujui liwalo na liwe kijana. Sie muda wa kuwabembeleza mashoga hatuna
 
Hata Misri walikuja na hoja kuwa Tanzania haturusiwi kutumia maji ya ziwa victoria kwa matumizi zaidi ya kunywa.Lakini leo kule shinyanga ninayo bustani kubwa kishenzi inatumia maji ya ziwa victoria.Kwa taarifa yenu aliyeukataa huo mkataba wa kishenzi ni Mh.Ngoyai Lowassa EDUARDO wakati akiwa waziri wa maji.Chezea LOWASSA WEYEEEEE MALAWIEEEH!!! Utatoka manundu

Afadhali hata Lowasa yeye hakutaka tangu mwanzo kusikia neno mkataba na akauita mkataba wa zamani. Tulimjua hivyo Lowasa na tulimuunga mkno kwa sababu hoja yake ilijitosheleza kwamba hatutaki kusikia mkataba wa mwaka 1920.

Tatizo hata hapa si mkataba au la. tatizo kwangu hapa ni maafisa wa serikali wanavyotumia kauli zao kutetea hoja zao. Wakati Lowasa hakutaka hata kuutja mkataba, juzi Bungeni Membe kautetea mkataba wa Heligoland akisema kwamba ndani ya mkataba huo (Heligoland) sisi Tanzania tumegawana nusu kwa nusu lile ziwa.

Hapa ndipo alipochemka Membe na ndipo panaponifanya nipige kelele zote hizi kwani wanaonipinga humu JF hawajui wanalilitetea maana mimi nimeusoma mkataba ule neno kwa neno.

Kama Membe ataendelea kung'ang'ania kwamba kwa mujibu wa mkataba na sisi tuna haki basi kamwe siwezi kunyamaza. Lakini kama atakuwa kama Lowasa akasema sisi Tanzania hatuuhitaji mkataba wa Heligoland, ninaweza kuunga mkono kwa sababu akifanya hivyo walau nitakuwa na matumaini kwamba hatutaaibika.

Lakini mwache aendelee kuwadanganya ambao hawakuusoma mkataba ule na ambao hawaksuoma speech yake Bungeni halafu uone aibu itakayowapata kama hawatafikia hatua ya kutaka thread za Malawi ziwe-blocked.
 
Back
Top Bottom