Waziri Bernard Membe kalipotosha Bunge kuhusu mpaka wa Tanzania na Malawi kwenye Ziwa Nyasa

Kiongozi hujaelewa mantiki. Vyote viwili vinatubana. Ramani ndio iliyopelekea mkataba ambao inaondoa ziwa nyasa lote kwenye miliki ya Tanganyika. Wote mfahamu pia kuwa huyo huyo Mwingereza ambae ni chanzo cha ramani au mkataba (as the case may be) ndie aliyetawala nchi hizi mbili (South Rhodesia -Malawi) na Tanganyika (TZ). Ndie ambae sasa anahusika na exploration kwenye ziwa Nyasa au Malawi. Tunachopaswa kuangalia ni msingi wa hoja zetu! Kwani mipaka na nchi nyingine tumenaithibitisha kwa kutumia nini kati ya Ramani au Mikataba? Kama tukienda kwa staili hii eti mipaka iliwekwa na wakoloni hatuwezi kushinda hoja kwani bila hiyo mipaka ya wakoloni hata leo sisi tusingejiita nchi huru Tanzanian na hata ile kesi yetu na wakenya kuhusu mlima kilimanjaro au ujenzi wa uwanja wa ndege wa kimataifa pale Taveta tutakosa hoja za msingi kwa nini hilo eneo lisiwe la Kenya (nini kinatulinda)?!. Kwa hili hata tukienda kidiplomasia tutaingia kwenye chaka la kutengeneza mkataba mpya kama sio kuambiwa tumilikishwe sehemu ndogo ya ziwa nyasa kwa kuwa kisheria hatuna haki ya moja kwa moja. Kuwapiga stop Malawi wasifanye utafiti kwny ziwa lote hatuwezi, wao wanatueleza wamenza kwa eneo wanalotumia sasa na wanaweza kuendelea au kuacha pindi mgogoro wa umiliki wa ziwa ukiisha. Umakini unahitajika kwa hili, wabongo siku zote tunaishi kwa kutumaini huruma za wenzetu.

Nakubaliana na hoja zako ila kuna marekebisho kidogo na ninadhani umeteleza kwa bahati mbaya na unahitaji kuelimishwa. Mipaka yote haitawaliwi na ramani iliyochorwa bali inalindwa na mkataba uliopo hata kama ilikuwa ni ile tuliyoita bogus-treaties kama ule aliosaini Sultani kuuza kisiwa cha Mafia kwa kitambaa kinachoweza kuizunguka Mafia yote.
 
Hakuna Heligoland Treaty ya Tanzania au ya Malawi. Heligoland Treaty kwa siku zote ni ileile moja na jina jingine inaitwa Anglo-German Agreement of 1890.

Hata Membe hajasema kwamba kuna mkataba mwingine zaidi ya huu (Helligoland) ama katika archive za Tanzania au za Malawi zinazoeleza ugawaji mpya wa mpaka huu uliopita kwenye kingo za ziwa {Eastern shore of Lake Malawi}.

Mkataba wenye mipaka ni huu tu. Hayo maneno au michoro mingine kama una justification nenda kai-submit kwa Membe upate award tushinde kesi hii.

Kumbe muda wote unakomaa hapa Nikupateje unatafuta tuzo?
Kwanini sasa hujampelekea membe hizi latitudes sahihi bali umezileta JF!?
 
Last edited by a moderator:
Kumbe muda wote unakomaa hapa Nikupateje unatafuta tuzo?
Kwanini sasa hujampelekea membe hizi latitudes sahihi bali umezileta JF!?

Aliyekomaa nalo ni huyu Membe na sijui kwa nini amelichukua so public kiasi hiki. Hakuwa na sababu za kulipeleka Bungeni kiasi kile halafu unafika huko kwa sababu hukujiandaa majibu yenyewe yanakuwa paragraph mbili na hizi zenye makosa wakati huohuo kuna mazungmzo yanaendelea. Wenzake wote tangu Nyerere walijua kuwa hili si rahisi kiasi hiki na kulipa public interest kama linavyomtokea puani sasa.

Yeye angefanya diplomacy ya kimyakimya kama anavyofanya kimyakimya kwenye suala la OIC na husikii kelele zinamsakama.

Lakini hata leo Membe akitaka kulikoroga la OIC basi nalo alipe publicity kama alivyofanya hili la Malawi. Nadhani hili ilmempa a sounding class.
 
Duh ama kweli!!! Ivi ni kwamba unatafuta kushinda au? Sawa inawezekana hawakupata uelewa huo kipind hicho sasa mambo ndo yameibuka, ivi kweli ndugu yangu kwa mfano ukaitwa kama shaidi huo utakua utetezi wako kweli , eti walikua wapi muda wote!!!

Sijaona popote pale alipo watetea wamalawi kinacho kushinda wewe ni uvivu wa kuelewa na kuamini hoja za Membe as if yeye awezi kukosea na kwamba eti kwakua ni waziri basi anaelewa kila kitu. Hili swala tusilifanye kiitikadi cse litatugarimu.Mleta mada ni mwenzetu na anachosema kinaeleweka sana hata huyo membe hataonekana mshamba akifuata ushauri wa huyu bwana.

Sasa hapa ndio ume comment kwa busara yako yote. Ndio nini hiki umeandika?
Hili nimeliandikia mara nyingi sana hapa, kwa sasa ni marudio kwahiyo usikurupuke!
 
Mtoa mada nina wasiwasi kama wewe ni Mtanzania. Kwanza kwa kukariri Ziwa Malawi badala jina linalojulikana na Watanzania pamoja na jumuiya ya mataifa kama Ziwa Nyasa hii imenithibitishia kuwa wewe ni Mmalawi. Pole sana, ila kumiliki ziwa lililompakani kwa asilimia 100% ni kitu ambacho hakiwezekani. Kukubali umiliki wa Msumbiji na kukataa umiliki wa Tanzania ni jambo ambalo aliingii akilini.
 
Acha ujuha, hotuba si mkataba wala statement ya mahakamani. Subiri waweke documents vizuri ambazo zina details kama hujajikuta ulicho prtesent hapa ni cha mtoto.
 
Hivi unadhani haya uliyoeleza yanamsaidia Membe atakapokaa na wamalawi hapo August 20, 2012? Mbona kakaa nao majuzi lakini akienda hewani na mwenzake wa Malawi ni kama vile Membe anafundishwa geography and history?!

tatizo lako una hamisha goli ili ufunge, sasa hiyo inaonyesha udhaifu ulio kuwa nao, unaweza kuwa una akili, lakini bado hujakuwa na uwezo wa kuitumia vizuri, ndio maana sasa hadithi zako zimekwenda kwa Membe, badala ya kuongelea suala halisi, weeakness ya membe or whoever, ni weakness ya huyo mtu na sio weakness ya Taifa au ya facts, pili unatakiwa kuelewa katika kujibu swali, msahihishaji haangali hadthi yako ndefu? bali anaangalia key points, sasa mimi ninapo kusoma si angali maelezo yako marefu ambayo baadae yanapotea muelekeo, eg issue ya lattitudes or longitudes etc , ni error ndogo ambayo haiwezi kuharibu jambo kuu? nalo ni la mpaka upo wapi? at the shore of the lake or in the middle of the lake, hivi vingine unavyo ongelea ni sawa na kuweka kachumbari au kutokuwa na kachumbari
 
Wewe Mmalawi usitake kutufanya sisi wabongo hatujuwi haya mambo, kukufahamisha ziwa Nyasa kwa juu liko latitude ya 9 degree na dakika 40 kwa longitude ya 34 degree na dakika 15 (kwenye ramani ya QDS 273/2) ambayo inaitwa Lupila.

Kusini ziwa liko kwenye longitude ya 34 degree na dakika 40 ambalo ni eneo la Lundu kwa wenyeji wa huko watakuwa wanapafaham na latitude yake ni 10 degree na dakika 45 (QDS 297-1 Lituhi).

Naomba nikukumbushe kitu kimoja unapotaja hizi point huwezi kutaja latitude pake yake bila kutaja longitude yake na kwa UTM Ssystem huwezi kutaje X- cordinate bila Y - cordinate na ARC1960 kwa WGS84 ni conversion tu ndugu yangu 300m kwa X na 200m kwa Y.
 
Wewe Mmalawi usitake kutufanya sisi wabongo hatujuwi haya mambo, kukufahamisha ziwa Nyasa kwa juu liko latitude ya 9 degree na dakika 40 kwa longitude ya 34 degree na dakika 15 (kwenye lamani ya QDS 273/2) ambayo inaitwa Lupila.
Kusini ziwa liko kwenye longitude ya 34 degree na dakika 40 ambalo ni eneo la Lundu kwa wenyeji wa huko watakuwa wanapafaham na latitude yake ni 10 degree na dakika 45 (QDS 297-1 Lituhi).
Naomba nikukumbushe kitu kimoja unapotaja hizi point huwezi kutaja latitude pake yake bila kutaja longitude yake na kwa UTM Ssystem huwezi kutaje X- cordinate bila Y - cordinate na ARC1960 kwa WGS84 ni conversion tu ndugu yangu 300m kwa X na 200m kwa Y.

Asante kwa ufafanuzi mkuu!

Huyo mmalawi wakuogopwa!
 
We gamba chama hapa tunazungumzia masuala ya kitaifa. Hizo siasa zako za mataputapu ya mabwepande ziache huko huko lumumba.

Mkuu Mwita,
Tasi hana gamba; mimi ni mzalendo halisi niashi kwa kipato halali sitegemei ajira kutoka serikali ya JMT; CCM wala sifanyi biashara na vyombo hivyo, mimi ni clean ila nina wasiwasi sana na watu wa kaliba yako wanaopiga kelele gamba la kobe ilhali wao wenyewe wamevaa magamba ya kasa; hapa nilimpongeza Yericko Nyerere kwa kuongea ukweli na kuonyesha uzalendo na utaifa, pitia posti za vijana wako wa Chadema kina matola, precise pangolin na wengine tu; badala ya kuwakemea vijana wako umekimbilia kunishutumu, mimi nilipitia JKT najua nini maana ya utaifa na unazi wa kichama, kwangu taifa mbele period!!! I trust you don`t be simple just because you want to side with some stupid and simple minded makamanda

Chama
Gongo la mboto DSM
 
MIMI NATATIZIKA SANA NA SUALA LA MIPAKA YA NCHI! kwakweli mimi sijawahi kufika mipakani, kwani hakuna visible thing to show the national boundary??

Maana tangu miaka yooote hii Mkapa,- Mwinyi hakuna mgogoro malawi, Tz wote wapo ok, isipokuwa vipindi hivi viwili Nyerere ambaye nilidhani alisolve.

kiramani kwakweli mimi naona ziwa tunalo watz
 
Nikupateje kwanza niseme tu kwamba sihitaji kukupata kama jina lako lilivyo.
Pili nikuulize unachohangaikia ni kitu gani? Ile thread yako nyingine ulipewa hoja za kutosha kukujibu hoja zako. Sasa umekuja kuanzisha nyingine yenye hoja zile zile.
Hii bidii unayofanya kujaribu kuhadaa watu na vilatitudes hapa wala haikusaidii wewe mnyasa na makuwadi wenzako wa kinyasa mliojazana hapa nchini.
Malawi hawawezi kumiliki ziwa lote, watake wasitake lazima kuna kipande chetu ndani ya ziwa nyasa.

Mkuu hebu tujikite kwenye hii mada kijografia zaidi ili tufikie lengo, tuweke mengine pembeni kwa nia ya kufikia lengo kwa logic and reasoning.
Samahani kama sijakufurahisha kaka.
 
Hebu waelez maana hata mimi nimesahau kukitaja unachokitaja. Kwamba baada ya Wordl Wara the first kwamba kuna ramani zilionyesha hivyo, na Waziri anatamka hivyo Bungeni na anapata washangiliaji huko Bungeni na huku mitandaoni. Ni uvivu wa kusoma na kutafiti kiasi kwamba inatia aibu.

Ujuha wa wamalawi na wanaowaunga mkono umelala kwenye imani ya kile wakiitacho makubaliano ya wajerumani na waingereza,wala si makubaliano wenyeji wa mwambao wa ziwa hilo,hata kama akili yako haijakomaa ni mahakama ya nguruwe pekee inayoweza toa haki kwa Malawi kumiliki ziwa lote wakati hilo ziwa linagusa ardhi ya nchi nyingine inayokaliwa na watu ambao wanayo haki ya asili kutumia maji ya ziwa hilo. Iwe Membe kakosea malatitude na malongitude au kapatia ukweli unabaki kama ulivyo kuwa ziwa ni mali ya wale wanaoapakana nalo nusu kwa nusu.
 
Nimeisoma Heligoland Treaty neno kwa neno na nimerudia mara kadhaa. Na kila nikiisoma sioni tutachomokea wapi kuhusu hili la Malawi.
Temporary treaty aimed at resolving the boundaries between British sphere of influence and German sphere of influence.
Only lake victoria was marched upon the delimiting line between them.
The rest of interterritorial waters were not, simply because there were no lands (habitable) between Tanganyika and Nyasaland.
The Lake was being treated by both as international waters. There were German and British gunboats sailing freely in those waters prior to 1914.... why do you think Britain allowed German vessels in their waters? Or vice versa?
 
Nikupateje kwanza niseme tu kwamba sihitaji kukupata kama jina lako lilivyo.
Pili nikuulize unachohangaikia ni kitu gani? Ile thread yako nyingine ulipewa hoja za kutosha kukujibu hoja zako. Sasa umekuja kuanzisha nyingine yenye hoja zile zile.
Hii bidii unayofanya kujaribu kuhadaa watu na vilatitudes hapa wala haikusaidii wewe mnyasa na makuwadi wenzako wa kinyasa mliojazana hapa nchini.
Malawi hawawezi kumiliki ziwa lote, watake wasitake lazima kuna kipande chetu ndani ya ziwa nyasa.
ni vita za 2015 ndani ya ccm mkuu... kitu gani huoni hapo??? yani unaona mkia halafu bado unauliza mku**du wa mbwa uko wapi??? nyanyua mkia utaona tundu
 
OSOKONI miaka ya 70 inamaanisha kati ya mwaka 1970 na 1980 siyo 1979! right?
By the way nafurahi kujua kuwa huyu@Nikupatejew ni Mnyasa na ndiyo maana anatokwa mishipa ya shingo kutetea Malawi kwamba inamiliki ziwa Nyasa kwa 100%!
Basi nazipuuza threads zake tangu sasa!
asante kwa masahihisho, hilo ziwa unataka kuniambia kuwa kabla ya kuja kwa wakoloni lilikuwa linatumika na upande mmoja tu yaani malawi?? halafu mbaya zaidi watershed ipo upande wetu yaani milima inayotiririsha maji ipo kwetu kwa nn tunyimwe haki ya kulitumia kisa wakoloni??
 
Mnyasa wa Maravi huyu ...:hat:
mimi naona hapa kuna hoja, hebu tuchangie badala ya kuhukumu mleta hoja kama mnyasa wa malawi au wa TZ! Kesho akichangia mmakonde utasema nae ni wa msumbiji?
natoa rai kwa wataalamu wa sheria za mikataba ya kimataifa mliomo humu jamvini mtusaidie kujibu swali hili: Je shauri hili likipelekwa mbele ya mizani ya umoja wa mataifa kuna hoja itakayotusaidia wa TZ kushinda kesi hii?
maana kama JK( rais) kadanganywa mara nyingi tu na wasaidizi wake kwa nini membe nae asipotoshwe na wasaidizi?
 
12 Reactions
Reply
Back
Top Bottom