Waziri apokewa na mgogoro mzito TRL

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
219,463
911,172
Waziri apokewa na mgogoro mzito TRL


Na Rehema Mohamed.

WAFANYAKAZI wa Kampuni ya Reli Tanzania (TRL) wamemtaka Waziri wa Miundombinu Bw. Omary Nundu kutoa ufafanuzi kuhusu Menejimenti ya Kampuni ya RITES ya India kuendelea kufanya kazi na kukusanya mamilioni ya fedha zinazotokana
na mapato ya shirika hilo ikiwa tayari imeshavunja mkataba wake na Serikali.
Wafanyakazi hao wametaka, Bw. Nundu kwenda kuwapa ufafanuzi wa suala hilo Jumatatu ijayo na kuwaeleza hatma ya mafao yao (mkono wa kheri) kutokana na shirika hilo kubadilishwa kutoka Shirika la Reli Tanzania (TRC) na kuwa Kampuni ya Reli Tanzania (TRL).
Hoja hizo za wafanyakazi hao zilitolewa Dar es Salaam jana wakati wa kikao chao cha dharura kilichoitishwa na wafanyakazi hao na kumtaka Katibu wao wa Chama cha Wafanyakazi, Bw. Sylvester Rwegasira kutolea ufafanuzi masula hayo.
Wafanyakazi hao wakiwa na mabango yaliyoandikwa ‘Nini siri ya serikali na Wahindi?’ Kwanyakati tofauti walisema TRL sasa imekuwa kama Ivory Coast kutokana na kuongozwa na menejimenti mbili tofauti ikiwemo iliyoteuliwa na Serikali chini ya Mkurugenzi wake, Bw. Amani Kisamfu na ile ya wawekezaji kutoka nchini India.
“Tunataka kujua mmiliki wa TRL ni nani, Serikali au Watanzania? Tunashangaa kuona menejimenti ya Wahindi ikiendelea kukaa ofisini bila kazi yoyote ya msingi huku wakiendelea kukusanya fedha bure kwasababu hata mishahara inalipwa na Serikali,” ni moja ya malalamiko yaliyotolewa na baadhi ya wafanyakazi hao.
“Tunataka Jumatatu tusiwaone, Waziri akija aje na menejimenti ya waswahili, sisi Mhindi sio mwajiri wetu alipoteza uwajiri wake tangu aliposhindwa kutulipa mishahara yetu, “alilalamika mmoja wa wafanyakazi hao.
Akijibu hoja hizo, Bw. Rwegasira alisema hata yeye akiwa kama Katibu Mkuu wa TRAWU, hana taarifa yoyote kuhusu mustakabali wa Serikali kuhusu madai hayo ingawa Serikali ilitoa ahadi kuwa uongozi huo wa Wahindi ungeondoka wiki chache baada ya kuvunjika kwa mkataba.
Bw. Rwegasira alisema baada ya Serikali kuvunja mkataba na TRL Oktoba mwaka huu, nakala ya kuvunjika kwa mkataba huo ilitakiwa kufikishwa mbele ya Baraza la Mawaziri ili kuanza kufanyiwa kazi na hatimaye wahindi hao kuondoka rasmi.
Bw. Rwegasira, alisema kinyume na matarajio hadi sasa kumekuwa kimya hawana taarifa yoyote kama nakala hiyo ilifikishwa katika Baraza hilo au la!
“Mimi sina jibu, shirika ndio linakufa, tangu menejimenti ya Wahindi iamuriwe kuondoka hawana kazi ya kufanya, cha kushangaza fedha wanachukua na Serikali imekaa kimya, kwanini serikali ipo kimya?,”alihoji Bw. Rwegasira
B w. R w e g a s i r a a l i s e m a ingekuwa busara baada ya Serikali kuvunja mkataba wake na TRL, menejimenti ya Wahindi hao ingekaa pembeni na kuwachiwa wazalendo kuiongoza.
Katika hatua nyingine alisema hali ya usafirishaji wa abiria ni mbaya kutokana na shirika hilo kuwa na uwezo mdogo kiute
 
"Tunataka kujua mmiliki wa TRL ni nani, Serikali au Watanzania? Tunashangaa kuona menejimenti ya Wahindi ikiendelea kukaa ofisini bila kazi yoyote ya msingi huku wakiendelea kukusanya fedha bure kwasababu hata mishahara inalipwa na Serikali," ni moja ya malalamiko yaliyotolewa na baadhi ya wafanyakazi hao.

Hivi serikali hiki kigugumizi cha kuwaondoa hawa wahindi kinasababishwa na nini?
 
Back
Top Bottom