Waziri akiri Slaa noma!

MwanaFalsafa1

JF-Expert Member
Feb 26, 2008
5,565
836
Na Ramadhan Mbwaduke

Waziri wa Maji na Umwagiliaji Profesa Mark Mwandosya, amesema Bungeni kuwa, hakustushwa na bomu la tuhuma za ufisadi katika mradi wa maji mkoani Shinyanga lililolipuliwa na Dk.Wilbroad Slaa, kutokana na ukweli kwamba anamfahamu mbunge huyo hizo ndiyo zake na kila wanapomuona na kabrasha, wanajua amebeba taarifa nyeti.

Profesa Mwandosya alisema hayo jana jioni wakati akihitimisha mjadala wa makadirio ya bajeti ya wizara yake kwa mwaka wa fedha 2009/2010.

Pamoja na ufafanuzi wa hoja za wabunge wengine kadhaa, pia alikuwa na kazi ya ziada ya kujibu kombora la tuhuma za ufisadi lililolipuliwa na Mbunge huyo wa Karatu ambaye pia ni Katibu Mkuu wa chama cha Demokrasia na Maendeleo.

Prof. Mwandosya alisema licha ya ukweli kuwa Wizara imebaini taratibu hazikufuatwa katika kumsimamisha Mkurugenzi wa Fedha wa Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Shinyanga, (SHUWASA), Bw. Charles Mwibula, ambaye Slaa alisema amesimamishwa kinyume cha utaratibu kwa sababu tu alikataa kushiriki 'dili' hilo, lakini kamwe wao hawakushtushwa na hoja zilizoibuliwa na Dk. Slaa kwa vile wanamjua kuwa kila anapokuwa na kabrasha, huwa ndani yake amebeba siri za Serikali.

"Kama Slaa atakuwa na nyaraka zaidi ya hizi anazosema, nitafurahi akinionyesha... kwa sababu lengo letu ni moja ambalo ni kuhakikisha kuwa wananchi wanapata maji," akasema Prof. Mwandosya.

Kuhusiana na kusimamishwa kwa Mkurugenzi wa Fedha, Prof. Mwandosya akasema: "Tunakiri kuwa taratibu hazikufuatwa... tumeelekeza aitwe tena, taratibu zifuatwe," akasema.

Sakata lenyewe lililoibuliwa na Dk. Slaa jana wakati akichangia bajeti ya Wizara hiyo, ni juu ya tuhuma za ufisadi, ambapo anadai zilitokana na kukiukwa kwa sheria za manunuzi ya umma katika mradi wa Maji Shinyanga uliotajwa kuwa na thamani ya Shilingi Bilioni 2.1.

Alidai kuwa vigogo katika Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Shinyanga (SHUWASA) ndio waliokiuka sheria kuhusiana na mradi huo wa usambazaji maji na kusababaisha Mkurugenzi wa Fedha wa SHUWASA, Charles Mwibula, asimamishwe kazi na wakubwa wake hao baada ya kukataa kushiriki mradi huo.

Kwa mujibu wa Dk. Slaa, SHUWASA waliomba Sh. bilioni 2.1 kinyume cha utaratibu, ambapo licha ya kasoro kadhaa zilizopo, bado kuna maofisa wa Wizara ya Maji na Umwagiliaji walipeleka Sh. Milioni 700.

Akadai kuwa jambo hilo linaonyesha wazi kuwa maofisa wengine wizarani wanashirikiana na wale wa SHUWASA kufanyia ufisadi fedha za mradi huo.

Alidai kuwa kinacholalamikiwa hapo ni kuwa taratibu za tenda zilikiukwa na kiwango cha fedha kilikiukwa kwani kilipaswa kupata kibali kutoka kwenye bodi ambayo kwa bahati mbaya, haikuhusishwa na pia kuna nyaraka za kugushi zilitumika.Hata hivyo, katika ufafanuzi wake kuhusiana na sakata hilo, Profesa Mwandosya alisema kwa mujibu wa taarifa alizo nazo, hakuna ubaya wowote uliofanyika kuhusiana na mchakato wa mradi huo.Katika hatua nyingine, Prof. Mwandosya alieleza kuwa awali, makampuni mawili yalipewa tenda ya kusambaza maji, moja ikiwa kwa wateja wa Kahama na kampuni nyingine kwa wateja wa Shinyanga.Hata hivyo, Profesa Mwandosya akasema kuwa kampuni iliyopewa tenda ya Shinyanga ilionekana kushindwa kazi, kwani hadi kufikia Februari mwaka huu, ilikuwa imeweza kuunganishia maji wateja 200 pekee na kuibua shaka ya wazi kuwa hawataweza kufikia lengo la kuwasambazia maji wateja 5,000 kufikia mwezi Machi mwaka huu.

Source: ALASIRI
 
Sasa Huyu Mh.Mwandosya ndio kapangua hoja au ndio nini kusema:- Tunamjua Dr. Slaa hizo ndiyo zake na kila wanapomuona na kabrasha, wanajua amebeba taarifa nyeti.
 
Sasa Huyu Mh.Mwandosya ndio kapangua hoja au ndio nini kusema:- Tunamjua Dr. Slaa hizo ndiyo zake na kila wanapomuona na kabrasha, wanajua amebeba taarifa nyeti.

Mkandara,

Hayo maneno ya "ndio zake" sio ya Mwandosya, ni mleta mada au muandika gazeti ndio wameyatunga, usiyaweke mdomoni mwa huyu waziri mahiri. Tuzingatie tofauti ya reported speech na direct speech.

Tungekuwa tunachagua viongozi kwa kuangalia nani anastahili, merit, badala ya mwenye sura nzuri na mcheshi, Mwandosya angekuwa rais sasa hivi.

Sijawahi kusikia waziri anampa credit Dr. Slaa bungeni, yani Mwandosya is too big kupingana na ukweli just because unasemwa na mpinzani. In fact, amesema kama Dr. Slaa ana la zaidi alileta, maana lao moja, kuleta maji kwa wananchi. Very classy, extremely gentlemanly. Na, amekiri makosa yaliyofanyika kwa huyo afisa aliyekataa dili. That is unheard of. Jamaa ni mstaarabu hakuna mfano.
 
Last edited:
Mkuu pengine mimi sielewi kiswahili lakini yaliyoandikwa hapo juu hayasemi ni mawazo ya mwandishi ila alichokisema Mh. Mwadosya..imeandikwa hivi:-
- Waziri wa Maji na Umwagiliaji Profesa Mark Mwandosya, amesema Bungeni kuwa, hakustushwa na bomu la tuhuma za ufisadi katika mradi wa maji mkoani Shinyanga lililolipuliwa na Dk.Wilbroad Slaa, kutokana na ukweli kwamba anamfahamu mbunge huyo hizo ndiyo zake na kila wanapomuona na kabrasha, wanajua amebeba taarifa nyeti.
Profesa Mwandosya alisema hayo jana jioni wakati akihitimisha mjadala wa makadirio ya bajeti ya wizara yake kwa mwaka wa fedha 2009/2010.
 
mkandara ndio tunapokuwa tunakosa kuamini habari nyengine kwa sababu muandishi hakutuwekea direcct quote.
angelikuwa kamnukuu moja kwa moja, tungekuwa na uhakika na maneno aliyoyasema waziri, lakini leo tunasoma habari kisha tuanze kupima maneno yanamuelekea au hayamuelekei ndio tuamini!
its a shame kwa kazi ya uandishi..................hawaoni kuwa angalau sehemu nyengine watuwekee maneno yake mwenyewe mtu na sio kumjazia maneno kinywani?
 
Nachoshindwa uelewa kwamba;Yale mazuri kayasema Mwandosa wala hamna lawama kwa mwandishi bt linavyokuja jambo baya..................haaaaaaaa
 
papokwapapo,
Mkuu ndicho nachojaribu kuelewa hapa... yaani huyu Mwadosya kakwepa hoja au ndio ktk kujisafisha kwake.. maanake hoja ilihusu Ufisadi ndani ya wizara yake na ukisoma kwa makini kila kitu kimeandikwa vizuri kabisa.. Mwadosya anadai apelekewe nyaraka nyingine zaidi.. haya sii ndio ya JK jamani?
Jibu swali, hoja hujibiwa kwa hoja kulingana na info ulokuwa nayo. pinga madai ya Dr. Slaa kwa kutumia nyaraka zako..
Yeye kenda kuzungumzia habari za mtu kufukuzwa kazi, haya hizo Contract jamaa bado wanatesa pamoja na kwamba wizara yake inajua fika kuwa jamaa wameshindwa..Ushahidi gani zaidi unataka zaidi ya kuona kwamba wananchi wako bado hawana maji kinyume cha mkataba! After all, Dr.Slaa katoa hint tu ni kazi yake yeye kama waziri kufuatilia ili apate uhakika wa madai ya Dr.Slaa akitumia nyaraka zake yeye (hizo za siri) zinasema nini.
 
Sasa Huyu Mh.Mwandosya ndio kapangua hoja au ndio nini kusema:- Tunamjua Dr. Slaa hizo ndiyo zake na kila wanapomuona na kabrasha, wanajua amebeba taarifa nyeti.

__________________
na yeye ana jiami JIMBONI JAMANI;KWANI APENDI KURUDI??BUNGENI ASHAJUA MWENZAKE SILAA ASHASHIKA BUNGE MIAKAA 15 IJAYO KWA MAMBO YA AJABU ALIYOWAFANYIA SI WANA.....BALI WATANZANIA KWA UJUMLA....MWANGA WA ULINZI WA MILLELLE UMUMMLIKE KILA AENDAKO
 
Bora Prof Mwandosya umesema kweli. Tunataka Wabunge kama Dr Slaa bungeni ili nchi iendelee
 
Mh. mwandosya ni mtu mahiri na makini sana katika utendaji wake.

lengo huduma za jamii zipatikana kama kuna itirafu basi taratibu stahiki zifuatwe kuondoa hizo itirafu.

hivi kazi ya wapinzani ni kukosoa tu na kutafuta mabomu?!
 
Nilisikia habari za kukanushwa na viongozi TUGHE kuhusu taratibu za kufukuzwa kwa huyo Mkuru wa fedha na wakadai kuwa slaa amepotosha ukweli...vipi na hawa viongozi wa vyama vya wafanyakazi si ndo wanapaswa kutetea au na wao wamo kwenye dili la ufisadi?
 
Kwa kifupi anakiri kwamba Dr. Slaa ni Moto wa kuotea mbali na hali kama hii ni udhaifu mkubwa sana
 
Mkandara,

Hayo maneno ya “ndio zake” sio ya Mwandosya, ni mleta mada au muandika gazeti ndio wameyatunga, usiyaweke mdomoni mwa huyu waziri mahiri. Tuzingatie tofauti ya reported speech na direct speech.

Tungekuwa tunachagua viongozi kwa kuangalia nani anastahili, merit, badala ya mwenye sura nzuri na mcheshi, Mwandosya angekuwa rais sasa hivi.

Sijawahi kusikia waziri anampa credit Dr. Slaa bungeni, yani Mwandosya is too big kupingana na ukweli just because unasemwa na mpinzani. In fact, amesema kama Dr. Slaa ana la zaidi alileta, maana lao moja, kuleta maji kwa wananchi. Very classy, extremely gentlemanly. Na, amekiri makosa yaliyofanyika kwa huyo afisa aliyekataa dili. That is unheard of. Jamaa ni mstaarabu hakuna mfano.


Mwandosya is too big kwa kuwa naye ni mwizi mkubwa na fisadi in kind wote tunajua habari zake ama ? Prof huyu sijui hata inakuwaje lakini anyaway hata nakosa la kusema.Mwandosya ni fisadi mkubwa tu na mkabila mno .
 
Mh. mwandosya ni mtu mahiri na makini sana katika utendaji wake.

lengo huduma za jamii zipatikana kama kuna itirafu basi taratibu stahiki zifuatwe kuondoa hizo itirafu.

hivi kazi ya wapinzani ni kukosoa tu na kutafuta mabomu?!
Think before you post you comments here..
 
Mkandara,

Hayo maneno ya "ndio zake" sio ya Mwandosya, ni mleta mada au muandika gazeti ndio wameyatunga, usiyaweke mdomoni mwa huyu waziri mahiri. Tuzingatie tofauti ya reported speech na direct speech.

Tungekuwa tunachagua viongozi kwa kuangalia nani anastahili, merit, badala ya mwenye sura nzuri na mcheshi, Mwandosya angekuwa rais sasa hivi.

Sijawahi kusikia waziri anampa credit Dr. Slaa bungeni, yani Mwandosya is too big kupingana na ukweli just because unasemwa na mpinzani. In fact, amesema kama Dr. Slaa ana la zaidi alileta, maana lao moja, kuleta maji kwa wananchi. Very classy, extremely gentlemanly. Na, amekiri makosa yaliyofanyika kwa huyo afisa aliyekataa dili. That is unheard of. Jamaa ni mstaarabu hakuna mfano. QUOTE]

GIVE ME A BREAK!!!!!!!!!
 
Mh. mwandosya ni mtu mahiri na makini sana katika utendaji wake.

lengo huduma za jamii zipatikana kama kuna itirafu basi taratibu stahiki zifuatwe kuondoa hizo itirafu.

hivi kazi ya wapinzani ni kukosoa tu na kutafuta mabomu?!

Something must be wrong somewhere!
 
Mkandara,

Hayo maneno ya “ndio zake” sio ya Mwandosya, ni mleta mada au muandika gazeti ndio wameyatunga, usiyaweke mdomoni mwa huyu waziri mahiri. Tuzingatie tofauti ya reported speech na direct speech.

Tungekuwa tunachagua viongozi kwa kuangalia nani anastahili, merit, badala ya mwenye sura nzuri na mcheshi, Mwandosya angekuwa rais sasa hivi.

Sijawahi kusikia waziri anampa credit Dr. Slaa bungeni, yani Mwandosya is too big kupingana na ukweli just because unasemwa na mpinzani. In fact, amesema kama Dr. Slaa ana la zaidi alileta, maana lao moja, kuleta maji kwa wananchi. Very classy, extremely gentlemanly. Na, amekiri makosa yaliyofanyika kwa huyo afisa aliyekataa dili. That is unheard of. Jamaa ni mstaarabu hakuna mfano.

Dilunga,
Tanzania hii haihitaji Rais 'classy & extremly gentleman'! Ukiwafanyia ugentleman wahalifu waliojaa kwenye safu ya juu nchini hatufiki mbali! Tunahitaji Rais rough na agressive, ustaarabu hauwezi kupambana na ufisadi uliokithiri nchini.

Dr. Slaaa k.k. ameibua ufisadi mwingine ambao umekwamisha maendeleo nchini. Wala Dr. Slaa si mwendawazimu wa kukurupuka na makabrasha yasiyo na sababu. Inasikitisha sana mtu kama Prof. Mwandosya ambaye watu kama Dilunga wanamtegemea kuwa Rais mzuri anaweza kuwa sacarstic katika kujibu hoja muhimu ya mustakabali wa tatizo sugu la ufisadi. Nilitarajia angetumia u'gentleman' wake kuona uzito wa hoja na kutoa maelezo aliyoyatoa ya ufafanuzi wa shauri lenyewe bila kuwa sacarstic na bila kujaribu kuwakingia kifua waliotenda makosa ambayo amekiri yalifanyika.
 
Sasa umakini wa Mwandosya hapo nini?kujua kuwa Slaa ni hatari kwa mabomu au??tunataka ajibu hizo hoja nzito za ufisadi mkubwa zaidi hata ya EPA sawa na Rich.......asitupe wasifu wa Slaa....
 
Slaa kweli noma anapolipua bomu ni la kweli hivyo uvisadi huo wa Wizara ya Maji ufanyiwe kazi.
 
Back
Top Bottom