Wazir anasema katiba mpya ndio itakayotoa ufafanuzi ni muungano upi wananchi wanautaka, wakati rais yeye anawatisha watu wasiujadili kabisa kwenye katiba mpya.
Wazir anasema katiba mpya ndio itakayotoa ufafanuzi ni muungano upi wananchi wanautaka, wakati rais yeye anawatisha watu wasiujadili kabisa kwenye katiba mpya.
JK be fair! Let Zanzibaris and tanganyikans decide what type of union they want. Viongozi hampo hapa kuwachagulia wananchi ni muungano gani wanaupenda even to say the least if at all there should be muungano. Watu waamue. Usiwatishe kama muungano unaupenda sana wewe, convince them waone umuhimu wa muungano, watakuja kwako na wataupitisha muungano. Jenga hoja, hawa watu ni waelewa. Mimi binafsi naupenda maana USA imesimama kwa nguvu za umoja wao!! Europe wanatafuta kuungana etc
Ni upuuzi kusema watu wasiujadili muungano, bila kuujadili hakuna maana ya katiba mpya, muungano sio baina ya viongozi na familia zao bali ni wa wananchi. Tukiacha kuujadili sasa tuendako sio salama kabisa., muhimu ni kuwasikiliza ni muungano gani tunaoutaka. Lakini kwa hali ilivyo tubakoelekea muungano utakufa na kuzaliwa shirikisho la tanganyika na zanzibar.
Kumbukeni kwamba huyu JK anayetaka Muungano usijadiliwe, ndiye huyu huyu anayepelekewa maoni yaliyokusanywa na Kamati ili ayafanyie kazi kabla na baada ya kwenda kwenye Bunge la Katiba. Sasa katika utaratibu huu, kuna jambo au mjadala utakaokuwa umehusisha Muungano utakaopita hapo! Tafakari, Chukua hatua Mapema!
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.