Wazee waitabiria kifo CCM: Anguko la CCM laja?

... WaTanzania sote TUMESHAAMUA kwamba mambo yote ni kwa CHADEMA, je ni nani tena wa kutuzuia?????????????

Wazee maarufu ndani ya Chama cha Mapinduzi, Dr Hassy Kitine,Mzee Ibrahim Kaduma na Mzee Joseph Butiku wametoa ya mwaka walipokuwa wakihojiwa katika luninga Channel 10, jumamosi.
Habari hii imejirudia katika gazeti la Mwananchi leo(Machi ,26, 2012) ikisema:

"Na Elias Msuya,

Makada watatu wakongwe wa Chama cha Mapinduzi( CCM), Ibrahim Kaduma,Dk Hassy Kitine na Joseph Butiku wameibuka na kukutabiria anguko chama hicho tawala kwa kile walichosema, kwenda kinyume na misingi ya kuasisiwa kwake.

Kauili za makada hao maarufu, zinakuja kipindi ambacho upepo wa kisiasa umekuwa ukivuma vibaya ndani ya chama hicho kikongwe nchini na barani Afrika, kutokana na vita ya makundi kati ya watuhumiwa wa ufisadi na wale wanaojipambanua kwamba ni wazalendo na wapinga."


Maoni Yangu:
Asiyesikia la mkuu huvunjika guu!
 
Subirini Nape na Mkama waanze kutoa mapovu mdomoni wakisema wameongea nje ya vikao halali vya chama...

Nape ninamheshimu sana. Dogo anajitahidi. Na kwa maoni yangu ni kwamba yeye ndiyo angalau ameiongezea uhai chama yake hiyo. Ingekuwa mahututi mpaka leo. Angalau watu wanaweza kumtegea masikio lakini si wenzake walobaki huko chamani kwao.
 
Hayumkiniki si shari tena or no longer at aese,Tanzania nchi ya amani tuliyorithishwa na Mungu mwenye enzi yote,katika kudhihirisha amani yetu tukabahatika kupata jiji la Dar Es Salaam lenye maana ya amani ambayo imesababisha nchi hii kuitwa bahari ya amani.Amani tuliyoachiwa na waasisi wetu,huku tukijivunia na kutembea kifua mbele duniani kote kuitangaza amani yetu kiasi cha kusahau kuutangaza utalii wa nchi yetu.Amani hii imetubwetesha kiasi cha wananchi kusahau haki zao za msingi katika maisha yao ya kila siku.Amani tuliyoaminishwa na waasisi wetu ili pelekea kila mmoja wetu kuamini rasilimali za nchi ni zetu sote,kila mmoja ana haki sawa na ana stahili kuheshimiwa utu wake.

Tunda hili la amani ambalo tumekuwa tukilinadi kimataifa limesababisha wananchi kubweteka na kuchipuka kikundi cha walaji wa chache ndani yetu na kujiona wao ndiyo wenye haki katika kuitafuna keki hii ya taifa.Ulegelege huu umeibua makundi ya ufisadi na makundi ya wanyonge walipumbazwa na amani bandia.Ulafi wa madaraka ulio gubika nchi yetu umesababisha matabaka ya watumwa na watwana ndani nchi inayojinasibu ina fuata utawala wa sheria kwa wanyonge na kuwaneemesha wachache waliobahatika kupata dhamana ya uongozi wa taifa hili.Hali ya nchi inasikitisha nchi iko likizo hakuna rais wa vitendo wala waziri mkuu wa vitendo,kila mmoja yupo kwenye shamba la bibi ana chuma mapera(mali) kwa faida yake binafsi.Tumesahau vile viapo tulivyoaminishwa toka enzi za TANU kuwa cheo ni dhamana,sinto tumia cheo changu wala cha mtu mwingine kwa faida yangu binafsi.Serikali imekuwa ya ukoo wa kambare,kila mmoja ana sharubu hakuna wa kumkemea mwenzake.

Vunjiko kubwa la amani ya nchi hii tuliyojivunia imeshika kasi kwa kuchochewa na ulevi wa madaraka uliokithiri katika awamu hii kuliko wakati mwingine wowote ule.Ulevi huu wa madaraka umepelekea uvunjifu wa sheria na kupokwa madaraka ya wananchi kwa mwingiliano wa mihimili ya dola katika kuendesha nchi hii.Serikali imekuwa kaidi kiasi cha kupelekea kudharau mihimili mingine na kutotimiza wajibu wake ipasavyo.Kila mhimili wa dola una jitegemea katika kazi zake kisheria bila kuingiliwa au kupata shinikizo toka upande wowote.Lakini ukitaka kuamini anguko kubwa la demokrasia katika nchi zetu,jaribu kuchunguza kwa makini utagundua kuna mwingiliano usiyo wa lazima katika kutekeleza majukumu ambayo yanapelekea haki za msingi za raia kupokwa kwa maslahi ya wachache wenye meno makali.Hali kama hii ikikithiri lazima izaliwe rushwa na uwizi wa mali ya umma kwa kuwa tu mihimili imekubaliana kuzipokonya haki za raia wake.

Nilipata wakati mgumu sana kutafakari athari ya mhimili mkuu wa mahakama kuingiliwa na mhimili mwingine ambao ni serikali wakati bunge linapitisha sheria ya kusimamia chombo cha maadili katika mahakama,chombo ambacho tuliamini ndiyo mhimili pekee ambao unaweza kumkomboa mlalahoi huyu.Kitendo cha wanasiasa kuingia ndani ya chombo hiki kilidhirisha jinsi serikali ilipoamua kwa makusudi kwa kuwategemea wawakilishi wanaotokana na chama chake kupitisha maamuzi ya kumkandamiza na kupora mwananchi huyu haki zake kisheria.Leo hatuna hata mwaka,tumeona matokeo ya mhimili moja kungilia mhimili mwingine katika kuto kumtendea haki mtuhumiwa.Kuna haja gani basi kuwa na mhimili mitatu ya dola ikiwa maamuzi yote yapo chini ya serikali iliyoko madarakani.Kuna haja gani ya kuwa na mahakama ikiwa serikali inaweza kuitafsiri sheria kuliko kutumia mabilioni ya kodi za walalahoi kuwalipa watendaji wa mihimili mingine walio kaa kama rubber stamp.

Athari za mwingiliano huu zinasababisha uzalendo ndani ya nchi yetu kupotea na maadili kuvunjika.Matokeo ya athari hizi ni nchi kupoteza rasilimali zake na uchumi wa nchi kufa kwa waatalamu kuingiliwa wajibu wao ili kufanikisha matakwa ya walafi wachache.Kama kweli maamuzi ya kesi ya kupinga ubunge yana shinikizo toka Ikulu,kinachofanywa na serikali hii ni kuchochea kuni kwenye moto wa petrol kwsa kuwalazimisha wananchi kufanya maamuzi magumu kuitafuta demokrasia kwa maandamano makubwa yatakayo tuletea Tanzatunisi.Kilchojiri pale Tunisia ni uroho na ulafi wa madaraka.Kitakachotokea hapa kwetu itakuwa ni historia isiyofutika na doa kubwa ndanio ya bahari ya amani.

Goliath alpokosa uvumilivu kwa ubabe wake alipambanishwa na mfalme mdogo Daudi,lakinio Daudi alishinda vita vile kwakuwa nguvu ya umma ilikuwa nyuma yake.Imefika wakati bila kujali mwongozo wa wanaharakati na vyama vya upinzani,bali wananchi kujipanga na kukataa ukandamizaji huu wa haki zetu za msingi.Serikali hakuna inachokijua zaidi ya kukandamiza watu wake waliyoipa dhamana ya kuwaonyesha njia.Gharama za demokrasia ni kubwa hazikwepeki,lakini tuangalie gharama hizo zisiwe za kishabikina kupelekea nchi yetu kufanya uchaguzi kwa kipindi chote cha miaka mitano na kuacha shughuli za maendeleo.Kuna shule mkoa mpya wa Simiyu haina madawati ndani ya miaka hamsini ya mafanikio ya uhuru wetu,lakini tunafanya uchaguzi wa kimizengwe bila kujali changamoto zinatukabili.

Anguko la Gadaffi,pamoja na uzalendo kwa nchi yake,ilichangiwa na miingiliano ya dola kiasi cha wananchi kukosa haki zao za kutawaliwa pamoja na kupatiwa kila walicho kihitaji sembuse sisi tusio na hili wala lile.Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni.Kwa kitendo cha mihimili kushindwa kusimama yenyewe na kukubali kupokea mashinikizo toka sehemu nyingine ni udhaifu mkubwa ambao haustahili kupokewa kwa mikono miwili na wananchi waliochoshwa na umangimeza huu.Yanayofanyika katika mahakama zetu kamwe yatakubalika hatupendi tuwe mahakimu kuwahukumu watendaji wa mahakama,ila kama hawatatenda haki tutawahukumu kwa ile tourati yetu.

Sifa za kijinga zinatuboa sana sisi wananchi,tumechoshwa na kamwe hatutokubali kufanya mbuzi wa kafara ili kutunisha mitumbo ya wanafiki na wazandiki ndani ya nchi yetu.Hatuna muda wa kupoteza kuwapa muda wa kujisafisha kama slogani ya JK inavyotaka,tukiingia barabarani silaha yetu ni moja mshikamano na tutaichukua nchi yetu kama walivyofanya wenzetu wa Misri na kwingineko walikoichukia batili.Angukola serikali dhalimu limefika sasa kinachofuta ni maamuzi magumu dhidi ya walafi.:focus:
 
Wakuu hii habari nimeitoa kwenye thread ya member mwenzetu Majimoto

  • Kwenye jukwaa la Biashara na Uchumi, Ukurasa wa Sita post namba 103
    Naomba tuijadili kwa kirefu na mapana maana imenigusa sana hasa kutokana na mambo yanayofanywa na serikali yetu ya Chama Cha Mapinduzi

    Watawala wa Taifa la Tanzania, kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2010, walifanya kila aina ya mbinu chafu za kuimarisha utawala wao, ili waweze tena kuongoza taifa la Tanzania.

    Nimesema walifanya mbinu chafu zenye makufuru makubwa, na katika ulimwengu usiooneka walionekana waziwazi waliyokuwa wakiyafanya.

    Moja ya kufuru walilofanya ni kuwekwa ndani ya majeneza na kushushwa makaburini, ambako walilala huko usiku mzima, huku wachawi wa nchi wakicheza uchi wa nyama juu ya makaburi hayo. Kisha waliapishwa na majini.

    Lakini kibao kiligeuzwa ghafula katika ulimwengu usiooneka baada ya kuingiliwa na kundi kubwa la wanadamu waliokuwa wanamlilia Mwenyenzi Mungu juu ya hatima ya baadaye ya taifa la Tanzania.

    Katika ulimwengu usioonekana, utawala uliokuwa ukioonekana kama mlima Kilimanjaro, uligeuzwa kichwa chini miguu juu, ulisagwasagwa, ukasambaratishwa kutoka jiwe la mlima hadi kuwa mavumbi matupu.

    Kimsingi utawala wa taifa la Tanzania ulioliongoza taifa hili kutoka mwaka 1961 ulikoma rasmi mwezi Septemba 2010 katika ulimwengu usioonekana.

    Kazi inayoendelea sasa ni kufanya yale yaliyotendeka katika ulimwengu usioonekana, yadhihirike katika ulimwengu unaooneka. Kawaida nguvu ya mtu au ya taifa ipo katika ulimwengu usioonekana, na matokeo yake hujitokeza taratibu kwenye ulimwengu unaoonekana.

    Kwa sababu taifa la Tanzania kwa sasa hivi halipo kabisa katika ulimwengu usioonekana, yapo mambo kadhaa ambayo ni lazima yajitokeze katika ulimwengu unaoonekana.

    a) Watawala walioondolewa katika ulimwengu usioonekana, kila jambo watakalojaribu kulifanya au kutenda katika ulimwengu unaoonekana wataishia kwenye aibu ya kukata na shoka.

    b) Mambo hayo ya aibu yatakuwa yanafuta hati yao batili ya utawala polepole kwenye utawala unaoonekana.

    c) Mwenyenzi Mungu hawezi kusimamisha utawala mpya kwenye utawala uliofanya makufuru makubwa kiasi hicho hadi, utawala huo ufutike kabisa katika ulimwengu unaooneka kama ulivyogeuzwa mavumbi katika ulimwengu usioonekana.

    d) Njaa italiandama taifa, kwa sababu Mungu amegeuka, uso wake haupo tena juu ya taifa hili hadi makufuru yaliyofanyika yafutike.

    e) Waliofanya makufuru hayo wajitayarishe kwa hasira kali ya Mwenyenzi Mungu.

    Hili jambo ni hakika na kweli, na litatimia kwa asilimia 100%
 
Kwa hali inavyoendelea hapa nchini, na kwa hali jinsi iliyo pale bungeni tangu kuanza kwa vikao vya bunge. ninaona ni jinsi gani sasa CCM wameshanyoosha mikono juu kuashiria kushindwa rasmi kwao.
namuona ndugu pinda anavyojibu maswali bila kujiamini, nam,uona pia ndugu lukuvi anavyojitutumua bila kutumia akili.
kwa wanavyofanywa serikali na wabunge wa CCM na CHADEMA ni sawa na timu mbili zinazochuana kati ya moja yenye mazoezi na nyingine waliookotana barabarani.
kila la heri wapinzani.
kila la heri MBOWE
Kila la heri ZITTO.
 
Kwa hali inavyoendelea hapa nchini, na kwa hali jinsi iliyo pale bungeni tangu kuanza kwa vikao vya bunge. ninaona ni jinsi gani sasa CCM wameshanyoosha mikono juu kuashiria kushindwa rasmi kwao.
namuona ndugu pinda anavyojibu maswali bila kujiamini, nam,uona pia ndugu lukuvi anavyojitutumua bila kutumia akili.
kwa wanavyofanywa serikali na wabunge wa CCM na CHADEMA ni sawa na timu mbili zinazochuana kati ya moja yenye mazoezi na nyingine waliookotana barabarani.
kila la heri wapinzani.
kila la heri MBOWE
Kila la heri ZITTO.

CCM wameshashindwa.
namshauri ZITTO ajiandae tu kuiongoza hii nchi.
 
Kwa hali inavyoendelea hapa nchini, na kwa hali jinsi iliyo pale bungeni tangu kuanza kwa vikao vya bunge. ninaona ni jinsi gani sasa CCM wameshanyoosha mikono juu kuashiria kushindwa rasmi kwao.
namuona ndugu pinda anavyojibu maswali bila kujiamini, nam,uona pia ndugu lukuvi anavyojitutumua bila kutumia akili.
kwa wanavyofanywa serikali na wabunge wa CCM na CHADEMA ni sawa na timu mbili zinazochuana kati ya moja yenye mazoezi na nyingine waliookotana barabarani.
kila la heri wapinzani.
kila la heri MBOWE
Kila la heri ZITTO.

I always support CHADEMA.asante sana Mungu kwa kutuumbia hivi vichwa vya CHADEMA.
 
CCM na anguko lao wamejitakia wenyewe,( mlimbua inchi ni mwanainchi wenyewe) kusimamia uweledi ni jukumu lao viongozi. Kuna kamati kuu, haslimashauri kuu, mkutano mkuu mwisho wanachama. Nyakati Fulani mwanachama wa kawaida husaidiwa kujitambua na hasa kufikia maamuzi sahihi. Enzi za mwalimu chombo kama kamati kuu kilikuwa na uwezo wa kuwashauri wanachama wao kwamba chaguo lao kwenye kura ya mapendekezo siyo sahihi hivyo jina halitarudi. Msamiati wa kama jina halitarudi jimbo litapotelea kwa wapinzani enzi hizo ilikuwa ni potelea mbali jimbo wacha lipotee heshima ya chama ibaki.

Sasa kuna faida gani mtu kama Rostram Aziz, Aden Rage, Mohammed Dewji, Murji, Shabib, Abood, na wengine kama hao wabaki kwenye chama halafu wanachama wengine wote wahamie kwenye vyama vya upinzani,wao hawawezi kuhama kwa sababu wao CCM ndio mavuno yao wengine wakifa potelea mbali, Oneni sasa Arusha CCM itabaki na Mery Chatanda tu wanachama wote watahama chama.

Ni nani hajui kwamba wote hao enzi za mwalimu majina yao yalikuwa hayarudi walikuwa wanakatwa juu kwa juu? Wao kuwa CCM ni mavuno , thread ilipita jana eti nani anajitolea kama mbunge huyu (Mohamed Dewji) eti ametolea jimbo lake Billion 6. Mimi nawasaidia watu wenye kuamini amelitolea jimbo kwamba hawapo sahihi kwa sababu tuhuma zinazomkabili Waziri Mustafa Mkullo ni pamoja na kumwuzia huyo ambae pia anajulikana kama Mohammed Enterprise viwanja kwa bei ya kutupa, sasa swali ardhi na pesa kipi chenye thamani? Wewe upate pesa hizo billion 6 yeye achukue ardhi naomba mnipe jibu, wenzetu walisema _ There is no free lunch under the sun. Mtu kama Murji alianza kuwahonga wanainchi wa Mtwara mjini miaka miwili kabla ya uchaguzi, mala basi kwenye mazishi, mala kahawa ya bure kwenye vijiwe vya kahawa, mala sanda na rambirambi kwa wafiwa, kuja kura za maoni wamakonde walikuwa wanafukuzwa kama mbwa mhindi akaonekana kama lulu

CCM BADO MNA NAFASI YA KUJISAHIHISHA mkirejea enzi za mwalimu.
 
380620_316763818396527_100001887358724_761981_407995052_n.jpg
NI HATARI KULIKO MAELEZO, IMEBAKI 32% KWA MUJIBU WA WACHAMBUZI WA MASUALA YA SIASA.
 
Yaani unaota mchana tena ukiwa macho, hivi chama cha kuanguka ni chama cha wananchi wote(CCM), au chama cha kanda moja tu(CDM)?.
.
"WASIOSOMA NI CHAKULA CHA WASOMI".
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom