ChescoMatunda
JF-Expert Member
- Jan 7, 2009
- 1,232
- 442
Nasikitika kuwa jamii ya burudani ya music hasa bongo fleva hapa tanzania haiwezi kukua wala kusonga mbele kwakuwa ina watu wajanja wajanja wapenda pesa za burudani bila kupenda maendeleo ya musiki wenyewe hebu fikiria wasanii wanalalamika kila siku kuwa musiki haujawalipa vya kutosha na sababu kubwa ni baadhi ya wadau waliopo kwenye fani hiyo hasa wasambazaji na mapromota wa matamasha, hivyo baadhi ya wasanii wakaungana na kuanza kile walichokiita vita dhidi ya watu wanaowarudisha nyuma kimusiki hasa wakimlenga ruge na kampuni anazosimamia yeye, kimsingi hapo ndio vita yao ilipoanzia sasa ushindani wa matangazo utoaji wa matamasha vyote vilipelekea mashabiki kujua vita hiyo ya wasanii hasa baada ya tamasha kubwa la tarehe 26 kufanyika kwa pamoja ambapo pande mojawapo ilikosa wingi wa mashabiki hasa upande wa ruge na makampuni yao pamoja na matangazo yao yote kuhamasisha radioni na kwenye tv bado ilionekana ni mafanikio kwa vinega. Niseme hapo ndipo kulizuka mwafaka feki kati yao nasema feki coz ruge kakutana na sugu wamekubaliana baadhi ya mambo kama kuongeza maslahi kwa wasanii na kupunguza upendeleo lakini kwangu mimi naona hayo yalikuwa feki sababu tangu mwafaka ufanyike kuna vitu vimejitokeza mojawapo ni mdau mmoja kujitoa kwenye kuutangaza muziki na katangaza kuanza kuangalia michezo hasa mpira wa miguu wiki moja tuu tangu kutiana saini ya makubaliano kaingia mkataba na yanga halafu ikafuata simba na kuna uwezekano na nyingine ziko kwenye mazungumzo pia wakati msemaji wa prime time promotions akieleza waandishi kuhusu makubaliano ya kampuni ya prime time promotions kutiana mkataba na yanga alieleza wazi kuwa mpango wao sasa wanaangalia michezo hasa mpira wa miguu kuanzia sasa mpaka mwaka 2015. Mimi nilidhani baada ya makubaliano yale wangefanya show moja kati ya vinega na upande wa pili kuonyesha kuwa mambo yako safi na wameanza kuendeleza fani sasa kwa mipango yao ya baadae hawana nia na muziki makubaliano yalikuwa ya nini hasa???????? Je hapo ndipo wasanii watanufaika na nini kwa hali hiyoo??? Nahisi ni chenga ya mwili na akili za watu wadau great thinker tujadili hili vipi?