MAMMAMIA
JF-Expert Member
- Feb 26, 2008
- 3,811
- 1,603
Ama kweli huyu jamaa ni juha sana. Kwa nini akataka liondoshwe neno Tanzania liwekwe Zanzibar, bila ya kuzingatia kuondoa neno Wageni/ Watu kutoka nje ya Zanzibar?Jussa alisema kwamba kifungu cha 23 (3) cha sheria kinachosema ajira katika sekta ya utalii lazima awe Mtanzania neno Mtanzania lifutwe na kuweka lazima awe Mzanzibari kwa malengo ya kulinda na kuongeza ajira kwa Wazanzibari.
Kwa kweli tunapoelekwa siko kabisa, Hili suala la ubaguzi linalofanywa na wanzanzibari limezidi kushamiri sasa, tunalipatiaje ufumbuzi?
Kwa sababu ambazo nimeshazisema kabla, suluhisho la ajira Zanzibar halitapatikana kwa kuondosha neno Tanzania bali kusomesha vijana wao.