Wazanzibari na Watanganyika wamekuwepo tangu 1964....TANZANIA SIO NCHI.

Swali: Ni kwa namna gani Serikali ya Tanganyika ndani ya Muungano itatuondolea ufisadi, umaskini, maradhi, ujinga, kutujengea shule, kutujengea zahanati/hospitali, kutupunguzia vifo vya mama wajawazito, kutulindia raslimali zetu dhidi ya wageni, kupunguza division 0 za f4, etc? Just let me know, au tunataka tuheshimu Wajerumani walioianzisha Tanganyika ambayo hata hivyo ilijumuisha Rwanda na Burundi? Only that? Kwa nini tusiheshimu kile tulichokitengeneza wenyewe? Mbona Zanzibar ya 1600s ilijumuisha mikoa ya Pwani na Morogoro? Nini "faida" ya kutengana anyway? Au watz wanataka vyeo tu, eti mimi Rais wa Tanganyika! Dhambi ya ubaguzi itauua Muungano, Tanganyika itakayozaliwa na hata Zanzibar!

Ndugu yangu Urusi uliamuwa kutowa uhuru kwa mataifa iliyoyajumuisha kwake kwa hila ili ipate nafasi ya kujiendeleza. Nayo Tanganyika ifanye hivyo iache hila na kuiachia Zanzibar ijiendeshe na kama kuna mambo ya kujumuika basi na iwe hivyo huku kila mmoja akiwa huru. Kuungana ambako viongozi wetu wanatdanganya kuwa kunafanyika duniani sio mujumuiko ya kiutawala bali kwa mambo mnayoona yana faida kwa pamoja na ndio maana tunasikia kunaJumuiya ya Ulaya.
 
Ibara gani ya Katiba inayotaja mambo ya ukoloni? Na unavyodai kushirikishwa kuko kwa aina mbili kwa Zanzibar: 1. Ndani ya Bunge la Muungano Wazanzibari wamo na pia, wanaweza kukataa kwa mujibu wa Ibara ya 98 ya Katiba ya JMT, 2. Ndani ya BLW Muswada unaweza usiridhiwe kutumika Zanzibar and it becomes the end of the story! Usiweke dhana ambayo haipo!

Wakoloni hawakuwahi kuandika katika Katiba yao kuwa wao wanatawala makoloni lakini matukio yalivyo kwa Muungano huu wa Tanganyika ni sawa na ukoloni. Wazanzibari wanawakilishwa katika Bunge la nani iwapo Wazanzibari wana Serikali yao ambayo ndiyo inayoshughulikia mambo ya Wazanzibari? Hivyo wewe huoni kizungumkuti kilichopo hapo? Hao Wabunge w Zanzibar wanawakilisha au wanahoji kitu gani wakati Serikali ya Zanzibar iko Zanzibar na ndiyo inayofanya mambo ya Zanzibar? Wanatyunga Sheria za kutumika wapi wakati Zanzigbar wana chombo cha kutunga sheria yao?
Wewe mwenyewe si umesema BLW wakikataa inakuwa basi? Sasa nani kati yetu ambaye analeta dhana isiyokuwepo?
 
Ngekewa et al, nitarudi asubuhi kujibu hoja. Sasa hivi bado nina kicheko cha Liverpool vs Manchester City.

Muungano lazima utizamwe upya. Kwa sasa hivi haupo. Upo kwenye makaratasi.
 
Huu Muungano wetu mbona bomba tu wandugu? Mbona mnapenda sana kuchonga?

Mkuu.
Ulipotelea wapi?
Nimefahamu umevua gamba tu kama CCM.
Yale masuali uliyouliza ya ufisadi na ujenzi wa barabara nilishawahi kuchangia siku zile!!!
Lakini jina Tanzania limetusaidia vipi katika kukabiliana na uliyoyataja?soma post#11.

Mkuu. B. tusipojadili kila kitu kwa uwazi ikiwemo muungano na muundo wake na kupotea kwa jina Tanganyika basi tunajidanganya tu.Tutakuwa tunakawilisha matatizo zaidi hapo baadae. Huwa natoa mfano wa Ethiopia na Eritria pia Indonesia na East Timor. Na kwa mbali Sudan na uzao wa taifa jipya la Sudan ya Kusini. Irony ni kuwa Mkapa amelishughulikia sana hili. La Indonesia na East Timor lilishughulikiwa na Jaji mkuu, Chande.

Mkuu. Kwa mtazamo wangu ni kuwa Viongozi wa Tanganyika na Zanzibar wamejificha nyuma ya pazia la Muungano aka "changa la macho" kwa muda mrefu huku wakitugawia umaskini wakati wao wakijitajirisha na familia zao. Sasa kwa kuwa na Tanganyika na taasisi zake na kwa Zanzibar kuwa taasisi zake na pia kuwa na Muungano unaoeleweka utawapa nafasi wananchi kukabiliana na "mchawi" wao moja kwa moja kwa yale madudu yanayofanyika.

Sasa hivi kila mmoja ana kisingizio cha Muungano. Viongozi wa Tanganyika wanasema Tanganyika haipo na hivyo hasira za wananchi zinaishia kwa wazanzibari...na viongozi wa Zanzibar wanasema wanabanwa na muungano na hivyo wananchi wanaishia kuuchukia muungano. Itakapopatikana mamlaka tatu, ya Tanganyika, ya zanzibar, ya Muungano na kila mamlaka ikawa na uwezo na mipaka inayotambulikana hapo wananchi watajua nani wa kumshika mashati.

Masuali yako yamenijulisha wewe ni Mkuu B. Nimefurahi kukusoma tena.
 
Swali: Ni kwa namna gani Serikali ya Tanganyika ndani ya Muungano itatuondolea ufisadi, umaskini, maradhi, ujinga, kutujengea shule, kutujengea zahanati/hospitali, kutupunguzia vifo vya mama wajawazito, kutulindia raslimali zetu dhidi ya wageni, kupunguza division 0 za f4, etc? Just let me know, au tunataka tuheshimu Wajerumani walioianzisha Tanganyika ambayo hata hivyo ilijumuisha Rwanda na Burundi? Only that? Kwa nini tusiheshimu kile tulichokitengeneza wenyewe? Mbona Zanzibar ya 1600s ilijumuisha mikoa ya Pwani na Morogoro? Nini "faida" ya kutengana anyway? Au watz wanataka vyeo tu, eti mimi Rais wa Tanganyika! Dhambi ya ubaguzi itauua Muungano, Tanganyika itakayozaliwa na hata Zanzibar!

Mkuu.
Ninaposoma michango mingi huona watu wanaweka options mbili.
ya kwanza...Muungano ujadiliwe upya ili uwe makini, wa haki na usawa. Hii ndio hoja yenye nguvu sana.

Option ya pili ni msisitizo wa hiyo ya kwanza. Inasema kama Muungano unaoeleweka, wa haki na usawa hauwezekani basi wabia wa muungano watengane. Kila nchi, taifa, watu waende kivyake.

To me these are valid, good options.

Watu, nchi zinaungana kwa sababu gani? Bila shaka kupata tija fulani. Sasa kama mwananchana au mbia hapati au anahisi hapati tija Muungano una maana gani? Ni vyema bila vita watu, nchi kutengana kwa salama kama vile walivyoungana kwa sherehe.

Halafu mkuu hakuna Muungano duniani unaoua nchi wanachama wa muungano na majina ya wanachama hao. That happens only in Tanzania. Why?

Cha kuchekesha zaidi au cha kuhuzunisha ni kuwa Wabia ,wanachama wa muungano wa Tanzania hawakuunganisha kila kitu. waliunganisha baadhi ya mambo tu. Sasa vipi Tanzania inakuwa nchi moja kwa kuunganisha baadhi ya mambo tu?
 
Kila kitu hutathminiwa kwa faida au hsara zake.

Mimi kama Mzanzibari sijui faida ya muungano huu wa Tanzania.

Wewe kama Mtanganyika umeona nchi yenu(Tanganyika) imefaidika na nini tokea kuungana ?

Jamani tujaribuni kuzitumia akili zetu tusiburuzwe tu kwamaslahi ya wajanja wachache.
 
LordJustice1

Mimi natathmini ubora wa kitu kwa faida zake lakini sio kuambiwa tu kua kitu hiki kinafaida.

Kama mzanzibari nasema muungano haujaifaidisha Zanzibar isipo kua kuiathiri kwa kiasi kikubwa.

Jibu hoja hii wewe kama Mtanganyika faida gani mulioipata tokea kuasisiwa kwa muungano huu?
 
Nonda,

Mambo ambayo si ya Muungano yanashughulikiwa na nani? Inapotokea suala ambalo si la muungano linahusu inayoitwa Tanzania Bara makamu wa Raisi ambaye ni Mzanzibari au Waziri wa Mambo ya Ndani halimuhusu? Au wakati wa Bunge wabunge kutoka Zanzibar hawachangii? Hawapigi kura? Au masuala hayo hayatokei?

Muungano wa Tanganyika na Zanzibar una matatizo. Kuutazama upya ni kwa kuuvunja na kuanza upya. Suala la faida na hasara za muungano lijadiliwe kwa mapana na mifano halisi na sio kinadharia. Tuache woga. Kila kitu kinazungumzika. Fikra za Mwenyekiti zisitugeuze watumwa. Ni haki yetu kuhoji.

Hayo mambo ya 'inviolability' na 'sanctity' ni udumazaji wa fikra chanya. Nani anaamua kuhusu hali hiyo? Haki yangu kama mtanzania kutoa maoni na kuwa na fikra huru iko wapi?
 
Tanzania, nchi mpya baada ya muungano wa nchi mbili....baadhi ya mambo!
Mkuu.
Muungano haukuzaa Tanzania.

Tanzania ni brain-child ya Mwalimu.
Mkuu hebu pitia hii doc uone kama utalikuta jina Tanzania.
Articles.znz+Tngk[1]

Vipi imekuja Tanzania, natumai utapata jibu.

Mimi msimamo wangu ni kuwa Muungano huu ulivurugwa tokea kuanzishwa kwake.

Mimi najiuliza pia kama ilikusudiwa kuwa nchi moja, kwa nini ilikubaliwa ziwepo serikali mbili? Tena ziwepo mamlaka tatu za kisheria?, Mamlaka ya Muungano, mamlaka ya Tangayika lakini ifanye kazi ndani ya mamlaka ya Muungano na mamlaka ya Zanzibar.

Halafu nchi moja inaunganisha mambo 11 tu ndio yanakuwa ya pamoja.
Mkuu. tutaendelea kushangaa sana kama Muungano huu na muundo wake hautafanyiwa over-haul!

La kushangaza ,viongozi hawataki Muungano uguswe. Je ni muungano wa wananchi au wa viongozi?

Lakini mkuu kama utaisoma hiyo doc basi majibu ya masuali yako yamo humo. Na hiyo doc ina sahihi ya Rais wa nchi yetu kabla ya Muungano.

Yeye hatunae tena, lakini Msekwa, Mtei. Warioba wapo hai. Hawa wanaweza kutusaidia sana katika kujibu masuali tuliyonayo.Hawa wamefanya kazi kwa karibu na Mwalimu na ndio walikuwa wanaratibu ama upitishaji wa sheria au uandishi wa katiba, pia ubadilishaji wa majinaya nchi na sehemu za nchi.

Muungano uliendeshwa tofauti sana na waasisi wa Muungao huu na pale baada ya muasisi mmoja alipokuwa "vaporised".
 
Nonda,

Mambo ambayo si ya Muungano yanashughulikiwa na nani? Inapotokea suala ambalo si la muungano linahusu inayoitwa Tanzania Bara makamu wa Raisi ambaye ni Mzanzibari au Waziri wa Mambo ya Ndani halimuhusu? Au wakati wa Bunge wabunge kutoka Zanzibar hawachangii? Hawapigi kura? Au masuala hayo hayatokei?

Mimi nikiviangalia vipengele hivi ndio vinaniacha hoi.

7. On the commencement of the interim Constitution of the United
Republic, the Constitution of Tanganyika shall cease to have effect
for the government of Tanganyika as a separate part of the United
Republic.

8. -(1) Subject to the provisions of this section, on and after Union
Day the existing law of Tanganyika and of Zanzibar shall continue
to be the law in the territories of Tanganyika and of Zanzibar respectively,

Na hii list ya mambo ya Muungano. Ni wazi orodha ya awali haikukidhi kuifanya Jamhuri ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar kuwa ni nchi moja. Na ndio sababu ya kuongezeka mambo ya Muungano kadiri miaka ilivyokwenda na orodha haijakamilika bado kuifanya Jamhuri ya Muungano kuwa nchi moja.

Hii ndio orodha ya mwanzo ya mambo ya muungano.

(iv) There shall reserved to the Parliament and Executive of the united
Republic the following matters-
( a ) The Constitution and Government of the united Republic.
(b) External Affairs.
(c) D efence.
(d) Police.
(e) Emergency Powers.
(f) Citizenship.
(g) Immigration.
(h) External Trade and Borrowing.
(i) The Public Service of the united Republic.
(j) Income Tax, Corporation Tax, Customs and Excise.
(k) Harbours, Civil Aviation, Posts and Telegraphs.
And the said Parliament and Executive shall have exclusive authority in such
matters throughout and for the purposes of the united Republic and in addition
exclusive authority in respect of all other matters in and for Tanganyika.

Mkuu. kwa bahati mbaya badala ya sisi kutafuta majibu kutoka kwa wanasheria wetu wa serikali na viongozi wetu juu ya utata huu wa muungano, juu ya "kutokueleweka huku" kwa Muungano huu na muundo wake, tunaelekeza masuali na ghadhabu zetu kwa watu ambao wao wenyewe wako "buffled" na Muungano huu.

Kipofu anaetaka kuelekezwa njia hawezi kumuuliza kiziwi ambaye hatasikia suali analoulizwa.

Na sisi tunafanya kosa hilo, tunataka Ngekewa au Mtu wa pwani ajibu masuali yanayohusu Tanganyika. Je hatuoni ni jambo la busara kuwauliza viongozi wa Tanganyika aka Tanzania bara ili watupe majibu sahihi?

Zamani uraia baada ya muungano mtu alisema "mimi ni raia wa jamhuri ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar".kwa vile uraia lilikuwa jambo la Muungano. Na jina Tanzania halikuwepo. Sasa hapo ndio ililazimisha dharura ya kuunda jina Tanzania. na jina hili lilianza kutumika Augus?t au October ?. Watu wa Tanganyika tukawa conditioned tusitumie tena Tanganyika. Leo tunajiita wabara au watanzania bara.

Sasa kabla ya jina jipya, nchi iliitwa kwa jina lipi? Au sehemu mbili za Jamhuri ziliitwa kwa majina yepi? Na nini kilipelekea majina hayo kubadilika baadae?
 
Zanzibar imeendelea kuwepo siku zote. Tanganyika ilikufa. Muungano utaendelea kuwa kitendawili mpaka siku ambayo tutakuwa na kiongozi mwenye nia ya dhati kuondoa mapungufu ya muungano.
 
Zanzibar ni nchi. Hamuna ushahidi wowote wa kuunganisha nchi sasa liliopo nimpango wakutuachia nchi yeetu kwa salama bila matatizo. Sisi hatuna haja ya vita wal kusumbuana. miaka 47 ya kudanganyana imekwisha. Wazanzibari walimueleza Mh. Sitta kuhusu hili na ndivyo ilivyo. Muungano basi.
 
Zanzibar ni nchi. Hamuna ushahidi wowote wa kuunganisha nchi sasa liliopo nimpango wakutuachia nchi yeetu kwa salama bila matatizo. Sisi hatuna haja ya vita wal kusumbuana. miaka 47 ya kudanganyana imekwisha. Wazanzibari walimueleza Mh. Sitta kuhusu hili na ndivyo ilivyo. Muungano basi.
Je, Zanzibar ni nchi kwa maana ya kuwa na Rais, BLW, bendera, nk? Msijipe moyo kusikokuwa na sababu yeyote! Je, Zanzibar inaweza kuingia vitani na nchi nyingine bila kuishirikisha Tanzania? Je, Zanzibar ni mwanachama wa UN? Je, kimataifa Zanzibar ina "personality" yoyote kama nchi? Kama majibu hayo ni hapana basi kisheria Zanzibar sio "a sovereign country!" Kwa lugha nyingine, kujiita NCHI sio lazima uwe NCHI! Mimi sihitaji pasipoti kuja Zanzibar wala Mzanzibari hahitaji pasipoti kuja Tanzania Bara, je, umewahi kwenda kwenye nchi nyingine bila pasipoti? All in all, mimi siamini kama Zanzibar ni nchi KISHERIA as long as wako ndani ya Muungano!
 
Mkuu.Ninaposoma michango mingi huona watu wanaweka options mbili.ya kwanza...Muungano ujadiliwe upya ili uwe makini, wa haki na usawa. Hii ndio hoja yenye nguvu sana. Option ya pili ni msisitizo wa hiyo ya kwanza. Inasema kama Muungano unaoeleweka, wa haki na usawa hauwezekani basi wabia wa muungano watengane. Kila nchi, taifa, watu waende kivyake. To me these are valid, good options. Watu, nchi zinaungana kwa sababu gani? Bila shaka kupata tija fulani. Sasa kama mwananchana au mbia hapati au anahisi hapati tija Muungano una maana gani? Ni vyema bila vita watu, nchi kutengana kwa salama kama vile walivyoungana kwa sherehe. Halafu mkuu hakuna Muungano duniani unaoua nchi wanachama wa muungano na majina ya wanachama hao. That happens only in Tanzania. Why? Cha kuchekesha zaidi au cha kuhuzunisha ni kuwa Wabia ,wanachama wa muungano wa Tanzania hawakuunganisha kila kitu. waliunganisha baadhi ya mambo tu. Sasa vipi Tanzania inakuwa nchi moja kwa kuunganisha baadhi ya mambo tu?
Nashukuru kwa mchango wako! Mimi nina wazo tofauti! Inawezekana kabisa kuunganisha nchi kwa kuziua kama ilivyo USA, zile States zina sheria zake tofauti, japokuwa Muungano wetu sio Federal kama ilivyo USA! Inategemeana na makubaliano yenu! Kwa hiyo tunaweza kuunganisha baadhi ya mambo na tukawa na nchi moja, wala si kichekesho kama unavyodai!Kuhusu tija, sidhani kama hakuna faida kabisa za Muungano, hiyo si kweli! Kwa mfano tuchukulie suala la ulinzi na usalama, ambalo ni jambo la Muungano, watu wanachukulia for granted kwamba usalama na amani vimekuwepo tuu bila kutengenezwa! Wanasahau ile methali isemayo "usione vyaelea vimeundwa!" Niliwahi kumsikia Prof Lipumba na uprofesa wake akidai kwamba Watz "HUWA" ni watu wa amani! Kama Watz "huwa" ni watu wa amani basi tuondoe vyombo vya ulinzi na usalama?
 
Mimi nikiviangalia vipengele hivi ndio vinaniacha hoi. 7. On the commencement of the interim Constitution of the United Republic, the Constitution of Tanganyika shall cease to have effect for the government of Tanganyika as a separate part of the United Republic. 8. -(1) Subject to the provisions of this section, on and after Union Day the existing law of Tanganyika and of Zanzibar shall continue to be the law in the territories of Tanganyika and of Zanzibar respectively, Na hii list ya mambo ya Muungano. Ni wazi orodha ya awali haikukidhi kuifanya Jamhuri ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar kuwa ni nchi moja. Na ndio sababu ya kuongezeka mambo ya Muungano kadiri miaka ilivyokwenda na orodha haijakamilika bado kuifanya Jamhuri ya Muungano kuwa nchi moja. Hii ndio orodha ya mwanzo ya mambo ya muungano. (iv) There shall reserved to the Parliament and Executive of the united Republic the following matters- ( a ) The Constitution and Government of the united Republic. (b) External Affairs. (c) D efence.(d) Police. (e) Emergency Powers. (f) Citizenship. (g) Immigration. (h) External Trade and Borrowing. (i) The Public Service of the united Republic.(j) Income Tax, Corporation Tax, Customs and Excise.(k) Harbours, Civil Aviation, Posts and Telegraphs. And the said Parliament and Executive shall have exclusive authority in such matters throughout and for the purposes of the united Republic and in addition exclusive authority in respect of all other matters in and for Tanganyika. Mkuu. kwa bahati mbaya badala ya sisi kutafuta majibu kutoka kwa wanasheria wetu wa serikali na viongozi wetu juu ya utata huu wa muungano, juu ya "kutokueleweka huku" kwa Muungano huu na muundo wake, tunaelekeza masuali na ghadhabu zetu kwa watu ambao wao wenyewe wako "buffled" na Muungano huu. Kipofu anaetaka kuelekezwa njia hawezi kumuuliza kiziwi ambaye hatasikia suali analoulizwa. Na sisi tunafanya kosa hilo, tunataka Ngekewa au Mtu wa pwani ajibu masuali yanayohusu Tanganyika. Je hatuoni ni jambo la busara kuwauliza viongozi wa Tanganyika aka Tanzania bara ili watupe majibu sahihi? Zamani uraia baada ya muungano mtu alisema "mimi ni raia wa jamhuri ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar".kwa vile uraia lilikuwa jambo la Muungano. Na jina Tanzania halikuwepo. Sasa hapo ndio ililazimisha dharura ya kuunda jina Tanzania. na jina hili lilianza kutumika Augus?t au October ?. Watu wa Tanganyika tukawa conditioned tusitumie tena Tanganyika. Leo tunajiita wabara au watanzania bara. Sasa kabla ya jina jipya, nchi iliitwa kwa jina lipi? Au sehemu mbili za Jamhuri ziliitwa kwa majina yepi? Na nini kilipelekea majina hayo kubadilika baadae?
Mambo ya Muungano yaliongezeka kulingana haja ya wakati husika! Mathalani baada ya kuvunjika kwa iliyokuwa EAC mambo yaliyokuwa chini ya EAC kama vile Mahakama ya Rufani ya Afrika Mashariki yalihamishiwa kwenye mambo ya Muungano kwa kuunda Mahakama ya Rufani ya Tanzania mwaka 1979! Sidhani kama kulikuwa na kipengele kilichokuwa kinakataza kuongeza mambo ya Muungano as long as Sheria zinafuatwa, ie theluthi mbili ya wabunge kwa kila upande wa Muungano! Kuhusu Jina Tanganyika kutokutumika na badala yake likatumuka Jina Tanzania Bara, sijaona dhambi iko wapi hapa au tuseme Sheria ipi imevunjwa? Hata Zanzibar iliacha kutumia jina lake la awali yaani Jamhuri ya Watu wa Zanzibar na kutumia Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) baada ya Muungano!
 
Wakoloni hawakuwahi kuandika katika Katiba yao kuwa wao wanatawala makoloni lakini matukio yalivyo kwa Muungano huu wa Tanganyika ni sawa na ukoloni. Wazanzibari wanawakilishwa katika Bunge la nani iwapo Wazanzibari wana Serikali yao ambayo ndiyo inayoshughulikia mambo ya Wazanzibari? Hivyo wewe huoni kizungumkuti kilichopo hapo? Hao Wabunge w Zanzibar wanawakilisha au wanahoji kitu gani wakati Serikali ya Zanzibar iko Zanzibar na ndiyo inayofanya mambo ya Zanzibar? Wanatyunga Sheria za kutumika wapi wakati Zanzigbar wana chombo cha kutunga sheria yao? Wewe mwenyewe si umesema BLW wakikataa inakuwa basi? Sasa nani kati yetu ambaye analeta dhana isiyokuwepo?
Hapa suluhisho ni Serikali MOJA tu, otherwise malalamiko hayataisha!
 
Naona unafikiria kinyume hakuna nchi ya Zanzibar wala Tanganyika kuna nchi ya Tanzania!!!!. Inabidi tuache kuishi kwa ndoto!

usione aibu kama wewe ni mtanganyika au umesahau kama mkataa kwao ni mtumwa...Zanzibar ipo na wenyewe manajivunia kuwa wazanzibari...
 
Swali: Ni kwa namna gani Serikali ya Tanganyika ndani ya Muungano itatuondolea ufisadi, umaskini, maradhi, ujinga, kutujengea shule, kutujengea zahanati/hospitali, kutupunguzia vifo vya mama wajawazito, kutulindia raslimali zetu dhidi ya wageni, kupunguza division 0 za f4, etc? Just let me know, au tunataka tuheshimu Wajerumani walioianzisha Tanganyika ambayo hata hivyo ilijumuisha Rwanda na Burundi? Only that? Kwa nini tusiheshimu kile tulichokitengeneza wenyewe? Mbona Zanzibar ya 1600s ilijumuisha mikoa ya Pwani na Morogoro? Nini "faida" ya kutengana anyway? Au watz wanataka vyeo tu, eti mimi Rais wa Tanganyika! Dhambi ya ubaguzi itauua Muungano, Tanganyika itakayozaliwa na hata Zanzibar!

Hiyo nchi ya tz(bara) tanganyika imewashinda sasa mnalazimisha hata zanzibar washindwe kwa kutumia neno tz... Pamoja na rasili mali zote zilizopo hapa Tanganyika bado hamjui nini mnafanya. Umasikini , rushwa, maradhi , ufisadi sasa vinaonekana vitu vya kawaida. Wazanzibar nje ya muungano wanaweza kupata nafuu. Kama ushirika hauna tija ni haki ya kila mshirika kutafuta njia nyengine.
 
Back
Top Bottom