Wazanzibari kufungua kesi katika Mahakama za Kimataifa Uingereza

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,299
33,082
Magufuli.jpg


WAZANZIBARI KUFUNGUA KESI KATIKA MAHAKAMA ZA KIMATAIFA (UINGEREZA) DHIDI YA SERIKALI YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WAKIDAI UKIUKWAJI WA KATIBA.

Habari za kiuchunguzi zinadai kuwa wazanzibari kwa umoja wao bila kujali itikadi zao sasa kufungua kesi katika mahakama ya kimataifa Uingereza dhidi ya serikali ya jamhuri ya Muungano wa Tanzania kushinikiza ukiukwaji wa katiba ya Zanzibar na kuwanyima wazanzibar haki ya msingi ya kuchagua kiongozi wanayemtaka.

Taarifa zinasema wazanzibari watadai mahakani kwamba Serikali ya Dk Magufuli inatumia nguvu za dola kukandamiza haki yao ya msingi na ya kikatiba ya kuchagua kiongozi wanayemtaka, hatua hiyo imekuja baada ya CUF chama kikuu cha upinzani Zanzibar kutokuwa na imani na mahakama za Zanzibar juu ya uvunjwaji wa katiba ya Zanzibar na sheria ya uchaguzi.

Wachunguzi wa mambo ya kisiasa wameeleza kuwa hatua hiyo itaukuza mgogoro wa kikatiba wa Zanzibar na kuwa mgogoro wa kimataifa huku baadhi ya mataifa ya magharibi yakiotoa wataalamu waelekezi (consultants) kuwaelekeza kundi hilo la wazanzibari jinsi ya kufungua na kuendesha keshi hiyo kwa umahiri mkubwa.

Endapo wazanzibari hao watashinda madai yao na Serikali ya Tanzania ikashindwa kutekeleza madai amri ya mahakama ya kimataifa Tanzania itakabiliwa na vikwazo vya kimataifa hali ambayo itapelekea uchumi wa Tanzania kuporomoka na hali ya maisha ya watu wa kawaida kuwa ngumu zaidi (maarufu kama tutaisoma namba). Kutokana na hali hiyo baadhi ya wanasiasa wakongwe nchi wameshauri haki itendeke Zanzibar ili kuepusha Tanzania na aibu zaidi.


Chanzo: Mwandishi wetu
 
Sometimes you will never know the value of your ignorance and stupidity, until it becomes open secret!

Ndio yale yale ya UKAWA na International Court of Justice (ICJ) na baadhi ya wananchi wakaamini kama kauli ya Jaji Lubuva kuhusu ushindi wa Dkt. Magufuli itabadilishwa kisheria.

By the way, huko duniani Zanzibar haitambuliki kama ni nchi pamoja na kwamba Wazanzibari walivunja Katiba ya JMT kwa kujiita nchi. Kwa maana nyingine, chaguzi zao za Rais zinatambulika kimataifa ni kama chaguzi za mwakilishi ndani ya Tanzania!

Kama utaweza kupeleka kesi ya kupinga matokeo ya wawakilishi kama madiwani au wabunge kwenye mahakama za kimataifa. Good on you!

Ama kweli wajinga ndio waliwao!
 
Things starting being very serious now. Itafikia wakati itabidi uamuzi utakaotolewa utekelezwe au tukubali wananchi wateseke kwa vikwazo. Kupanga ni kuchagua. Ikifikia hapo hakuna kukaa kimya tena.
 
Hivi vijamaa vinachosha kuvisikiliza. Ndio maana walipelekwa kuwa watumwa utumwani. Historia inasema walikusanywa hapo Zanzibar sokoni. Soko la watumwa. Na wao bado hawajabadilika ingawa wamefanya mapinduzi, kumbe hawajapindua fikra za utumwa bali ni yale yale. Nitamaa ya wengi kuona sasa hawa jamaa wabadili fikira za kitumwa. Bora kujikita katika kuiboresha Zanzibar, zanzibar yenye historia nzuri na ya kupendeza.
 
Cuf wanadhan wapo nje ya zanzibar? Mbona wanatesa watu kwa tamaa za madaraka? Wel upo mwisho ya haya yote. Ninachojuwa taifa lipo tayar kula majan kuliko kutengua muungano.
 
Bado napata ukakasi naomba wanasheria wanijuze kuwa...kesi ya katiba ya zanzibar ambayo ni sehemu ya jamhuri ya muungano wa Tanzania inasikilizwaje na kutolewa maamuzi nchini uingereza....nadhani haya ni masuala ya ndani ya nchi usika na bila shaka kuna vyombo vya haki ndani ya nchi husika vinavyoweza kushughulika na hilo.....
Wajuzi wa sheria watujuze katika hili kuwa je wanachokifanya CUF ni sahihi kwa mujibu wa sheria za kimataifa katika kesi za kikatiba.....???

Isijekuwa kama ya CHADEMA na ICJ....
 
View attachment 324107

WAZANZIBARI KUFUNGUA KESI KATIKA MAHAKAMA ZA KIMATAIFA (UINGEREZA) DHIDI YA SERIKALI YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WAKIDAI UKIUKWAJI WA KATIBA.

Habari za kiuchunguzi zinadai kuwa wazanzibari kwa umoja wao bila kujali itikadi zao sasa kufungua kesi katika mahakama ya kimataifa Uingereza dhidi ya serikali ya jamhuri ya Muungano wa Tanzania kushinikiza ukiukwaji wa katiba ya Zanzibar na kuwanyima wazanzibar haki ya msingi ya kuchagua kiongozi wanayemtaka.

Taarifa zinasema wazanzibari watadai mahakani kwamba Serikali ya Dk Magufuli inatumia nguvu za dola kukandamiza haki yao ya msingi na ya kikatiba ya kuchagua kiongozi wanayemtaka, hatua hiyo imekuja baada ya CUF chama kikuu cha upinzani Zanzibar kutokuwa na imani na mahakama za Zanzibar juu ya uvunjwaji wa katiba ya Zanzibar na sheria ya uchaguzi.

Wachunguzi wa mambo ya kisiasa wameeleza kuwa hatua hiyo itaukuza mgogoro wa kikatiba wa Zanzibar na kuwa mgogoro wa kimataifa huku baadhi ya mataifa ya magharibi yakiotoa wataalamu waelekezi (consultants) kuwaelekeza kundi hilo la wazanzibari jinsi ya kufungua na kuendesha keshi hiyo kwa umahiri mkubwa.

Endapo wazanzibari hao watashinda madai yao na Serikali ya Tanzania ikashindwa kutekeleza madai amri ya mahakama ya kimataifa Tanzania itakabiliwa na vikwazo vya kimataifa hali ambayo itapelekea uchumi wa Tanzania kuporomoka na hali ya maisha ya watu wa kawaida kuwa ngumu zaidi (maarufu kama tutaisoma namba). Kutokana na hali hiyo baadhi ya wanasiasa wakongwe nchi wameshauri haki itendeke Zanzibar ili kuepusha Tanzania na aibu zaidi.


Chanzo: Mwandishi wetu
“In order to be credible, electoral processes must be inclusive and representative. Under the current circumstances, the provision of international electoral observation would be difficult to consider.
“We urge President Magufuli to exercise leadership in this political impasse, and to pursue his previous calls for a negotiated solution between parties, so as to ensure a peaceful outcome, but also one that ensures the integrity of the electoral process.
 
Unanyimwa haki ya kuchagua…!! Kwan nani amewaambia wajitoe kwenye uchaguzi?
 
Kisiwa cha Scotland kilichopo Uingereza nacho kije kufungua kesi katika mahakama za kimataifa ya Tanzania kuwa Uingereza inawanyanyasa kwa kuto wapa uhuru wa kuchagua watakacho… nakumbuka mwaka juzi kulikuwa na kura ya maoni pale wakitaka kujitenga ila ikashindikana
 
Kisiwa cha Scotland kilichopo Uingereza nacho kije kufungua kesi katika mahakama za kimataifa ya Tanzania kuwa Uingereza inawanyanyasa kwa kuto wapa uhuru wa kuchagua watakacho… nakumbuka mwaka juzi kulikuwa na kura ya maoni pale wakitaka kujitenga ila ikashindikana
Ilishindikana nini maana kura ilipigwana wengi hawakuafiki kujitenga na sio kwmba ilishindikana
 
Wa Tanzania tunashangaza sana.
Kila siku kuwa tusi hao wazungu .

Mashoga hatuwataki, blahh blahh.

Haya yakitushinda kitu cha Kwanzaa utasikia
Tunaenda kuwa tafuta hao wazungu watutatulue
Matatizo yetu.

Kazi tu nayo.
 
Back
Top Bottom