kavulata
JF-Expert Member
- Aug 2, 2012
- 12,233
- 12,508
Mbwa huwa wanatabia ya kubweka. Mwenye mbwa anafurahi akisikia mbwa wake anabweka sana sana nyakati za usiku akiwa amelela kwakua anapata ishara ya watu, vicheche na vitu vingine vinavyoikaribia nyumba yake. Mwenye mbwa huwa hadharau mbweko wa mbwa wake hasa usiku, mara nyingi atataka kujua kwanini mbwa anabweka. Atatoka nje ama atachungulia dirishani ili kuona sababu ya mbwa kubweka. Bahati mbaya wako mbwa waoga ambao wanabwekea hata vivuli vyao wenyewe na vile vya miti, hivyo kusababisha mashaka yasiyo ya lazima kwa watu waliolala na kufurahia usingizi wao.
Miaka 46 ya muungano wetu imesababisha mambo mengi na makubwa, miongoni mambo haya ni pamoja na
1. Watu wa pande mbili za muungano kuoana na kuzaa watoto
2. Wanzanzibar wengi wamehamia Bara na kufanya biashara, kujenga, kusoma na kufanya kazi hata kwenye taasisi zisizo za muungano bila masharti.
3. Wazanzibari wanatoa mahitaji mbalimbali toka bara kwenda visiwani bila usumbufu wowote
4. Wazanzibar wako 1 mil lakini kwenye bunge la muungano wanawakilishwa na wabunge wasiopungua 40 na kushiriki katika kupitisha sheria na bajeti za taasisi ambazo sio za muungano wakati kwao hakuna mbara hata mmoja kwenye baraza lao la wawakilishi.
5. ....... endelea kutaja! ha, ha,
Pamoja na mafanikio haya mazuri kwa wazanzibari juu ya muungano wako wazanzibari wanaobweka eti muungano uvunjwe. Binafsi watu wanaotaka muungano uvunjwe ninawafananisha na mbwa wanaobwekea vivuli vyao, hawako serious na makini wa wanachobwekea, wanatupigia kelele tu za kubweka. Kama kweli wako serious wanataka muungano huu ufe basi yafuatayo yatimizwe kwanza:
1. waanze kwa kuwarudisha visiwani wazanzibari wao wote walioko bara (shaurimoyo, msasani, chumbageni, maofisini, mashuleni, vyuoni, hospitalini, n.k) kwa shughuli mbalimbali kuonyesha msisitizo
2. Viongozi na wastaafu wao wote wahame bara wakaishi visiwani (kwao), waache kulala bara
3. Wasuse kuchukua umeme, nyama, mazao toka bara
4. Wawashawishi wabunge na mawaziri wao walioko bara wajiuzulu mara moja
5. .... endelea kutaja mi nakohoa na kupiga chafya kwanza, teh
Kusema tu tufunje muungano bila ya kuanza na mambo haya Maalim Seif na wenzake (Uamsho) wanabwekea vivuli vyao tu, waache kuwasumbua watu waliolala, hiyo ni danganya toto na wala tusipoteze muda wetu kuwasikiliza. Hiyo ni danganya toto. Tunajua hawawezi kuvunja muungano asilani, wajaribu tuone. Wao ndio wanaobunya matunda ya muungano bwana! Wasitutishie ngongoti wala wasitingishe kiberiti chenye njiti kibao
Miaka 46 ya muungano wetu imesababisha mambo mengi na makubwa, miongoni mambo haya ni pamoja na
1. Watu wa pande mbili za muungano kuoana na kuzaa watoto
2. Wanzanzibar wengi wamehamia Bara na kufanya biashara, kujenga, kusoma na kufanya kazi hata kwenye taasisi zisizo za muungano bila masharti.
3. Wazanzibari wanatoa mahitaji mbalimbali toka bara kwenda visiwani bila usumbufu wowote
4. Wazanzibar wako 1 mil lakini kwenye bunge la muungano wanawakilishwa na wabunge wasiopungua 40 na kushiriki katika kupitisha sheria na bajeti za taasisi ambazo sio za muungano wakati kwao hakuna mbara hata mmoja kwenye baraza lao la wawakilishi.
5. ....... endelea kutaja! ha, ha,
Pamoja na mafanikio haya mazuri kwa wazanzibari juu ya muungano wako wazanzibari wanaobweka eti muungano uvunjwe. Binafsi watu wanaotaka muungano uvunjwe ninawafananisha na mbwa wanaobwekea vivuli vyao, hawako serious na makini wa wanachobwekea, wanatupigia kelele tu za kubweka. Kama kweli wako serious wanataka muungano huu ufe basi yafuatayo yatimizwe kwanza:
1. waanze kwa kuwarudisha visiwani wazanzibari wao wote walioko bara (shaurimoyo, msasani, chumbageni, maofisini, mashuleni, vyuoni, hospitalini, n.k) kwa shughuli mbalimbali kuonyesha msisitizo
2. Viongozi na wastaafu wao wote wahame bara wakaishi visiwani (kwao), waache kulala bara
3. Wasuse kuchukua umeme, nyama, mazao toka bara
4. Wawashawishi wabunge na mawaziri wao walioko bara wajiuzulu mara moja
5. .... endelea kutaja mi nakohoa na kupiga chafya kwanza, teh
Kusema tu tufunje muungano bila ya kuanza na mambo haya Maalim Seif na wenzake (Uamsho) wanabwekea vivuli vyao tu, waache kuwasumbua watu waliolala, hiyo ni danganya toto na wala tusipoteze muda wetu kuwasikiliza. Hiyo ni danganya toto. Tunajua hawawezi kuvunja muungano asilani, wajaribu tuone. Wao ndio wanaobunya matunda ya muungano bwana! Wasitutishie ngongoti wala wasitingishe kiberiti chenye njiti kibao