Wazanzibar na Uamsho wa Kuchoma Makanisa

Chechetuka

JF-Expert Member
May 28, 2009
549
44
Baada ya Uchaguzi Mkuu wa Vyama Vingi kumalizika Tanzania Bara na Visiwani mwaka 2010, Dunia ilishuhudia zoezi la kihistoria la kupiga kura ya maoni iliyopelekea mabadiriko ya Katiba yaliyotoa ridhaa ya Serikali ya Mseto ktk visiwa vya Zanzibar. Tukio hili la Kihistoria lilitokea baada ya wananchi ktk visiwa hivyo kukaa kwa muda mrefu wakisubiri kwa hamu kushirikishwa kwa vyama vyote hasimu ktk ujenzi wa Taifa lao.

Kukamilika kwa zoezi hili kulitoa matumaini makubwa sana ya amani ktk visiwa vya Zanzibar, kwani Serikali iliyopo sasa inaundwa na vyama vikuu viwili, yaani CCM na CUF. Vyama hivi vimekuwa ktk ushindani mkubwa wa kutawala Dola toka mfumo wa vyama vingi ulipoanzishwa rasmi mwaka 1992 na kuingia ktk uchaguzi Mkuu wa kwanza Mwaka 1995.

Hivi karibuni tulisikia kuwa visiwani Zanzibar kuna kikundi kimenzishwa chenye malengo ya kuwafikishia watu habari njema za dini ya Kiislamu. Kikundi hicho si kingine bali ni, Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara. Viongozi wote wa kikundi hiki ni wanachama wa CUF.

Wana Uamsho hao waliomba kibali cha kufanya maandamano ya kupinga zoezi la mchakato wa uundwaji wa Katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Wakati jeshi la Polisi likijadili kwa kina maombi hayo ambayo yameombwa na Jumuiya ya KIDINI, Ijumaa iliyopita (25 May 2012) kikundi hiki kilifanya "KAFARA" ktk eneo la Maruhubi mjini Unguja. "Inasemekana" ktk "KAFARA" hiyo Maalim Seif alihudhuria.

Katika "KAFARA" hiyo, Jumuiya hiyo iliamua kufanya maandamano siku ya Jumamosi hata kama kibali walichoomba hakijatoka. Waliazimia kuandamana kwa malengo mawili makubwa:

1. Kupinga mchakato unaoendelea wa kuunda Katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
2. Kupinga Muungano uliofanywa mwaka 1964 kati ya Tanganyika na Zanzibar

Ikumbukwe kuwa, siku zote vyama vya Siasa vinaposhindwa katika chaguzi mbali mbali vimekuwa vikilalamika kuwa Katiba ya Nchi HAIFAI. Leo hii Rais Jakaya Kikwete AMEAMUA KUWAPA WATANZANIA KATIBA MPYA kwa kuwashirikisha WATANZANIA wote. Hivi ni kweli tunahitaji kumpinga ktk hili au kumpongeza?

Baada ya Jeshi la Polisi kumkamata kiongozi wa Jumuiya hiyo, wanachama wake walianzisha vurugu mitaani na kusababisha kutoweka kwa amani ktk visiwa hivyo. Kama hilo halikutosha, wanachama hao walihamasishwa kuchoma Magari, maskani za CCM na Makanisa.

Zanzibar ni moja kati ya sehemu nne duniani ambazo zilichaguliwa kuwa vituo vya kufundishia DINI ya Kiislamu karne nyingi zilizopita, ukitoa kile cha Jeddah-Saudi Arabia na Cairo-Misri. Kituo hiki kipo maeneo ya KIKUTANI mjini Unguja, hapa ndipo walipokuwa wanafundishwa MASHEIKH toka sehemu mbali mbali duniani, ambapo karibu yake kuna Msikiti wa Jibril. Kutoka ktk kituo hicho mpaka MKUNAZINI lilipo Kanisa la Kianglikani lililojengwa miaka ya 1860 ni mita zinazokisiwa kuwa kati ya 200 na 300.

Nimejaribu kuchimba historia ya DINI ktk visiwa hivyo, wallah sijapata kusoma sehemu inayoonesha kuwa kuna siku Waislamu waligombana na Wakristo ktk visiwa hivyo.

Baada ya hapo nilianza kujiuliza maswali yafuatayo:

- Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara ni kikundi cha kueneza DINI au SIASA?
- Kuna Uhusiano gani kati ya shughuli zao za kidini na Chama Cha Siasa cha CCM?
- Kuna Uhusiano gani kati Makanisa na Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ulioizaa Tanzania?
- Kuna Uhusiano gani kati ya Makanisa na Katiba ya Mpya?

Wana Jamii Forum, tunahitaji kulijadili suala hili kwa kina ili tusije kusomeka vibaya ktk historia ya nchi hii.
 
Waachiwe wajitenge uone watatakavyo chapana wenyewe kwa wenyewe.
 
Baada ya Uchaguzi Mkuu wa Vyama Vingi kumalizika Tanzania Bara na Visiwani mwaka 2010, Dunia ilishuhudia zoezi la kihistoria la kupiga kura ya maoni iliyopelekea mabadiriko ya Katiba yaliyotoa ridhaa ya Serikali ya Mseto ktk visiwa vya Zanzibar. Tukio hili la Kihistoria lilitokea baada ya wananchi ktk visiwa hivyo kukaa kwa muda mrefu wakisubiri kwa hamu kushirikishwa kwa vyama vyote hasimu ktk ujenzi wa Taifa lao.

Kukamilika kwa zoezi hili kulitoa matumaini makubwa sana ya amani ktk visiwa vya Zanzibar, kwani Serikali iliyopo sasa inaundwa na vyama vikuu viwili, yaani CCM na CUF. Vyama hivi vimekuwa ktk ushindani mkubwa wa kutawala Dola toka mfumo wa vyama vingi ulipoanzishwa rasmi mwaka 1992 na kuingia ktk uchaguzi Mkuu wa kwanza Mwaka 1995.

Hivi karibuni tulisikia kuwa visiwani Zanzibar kuna kikundi kimenzishwa chenye malengo ya kuwafikishia watu habari njema za dini ya Kiislamu. Kikundi hicho si kingine bali ni, Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara. Viongozi wote wa kikundi hiki ni wanachama wa CUF.

Wana Uamsho hao waliomba kibali cha kufanya maandamano ya kupinga zoezi la mchakato wa uundwaji wa Katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Wakati jeshi la Polisi likijadili kwa kina maombi hayo ambayo yameombwa na Jumuiya ya KIDINI, Ijumaa iliyopita (25 May 2012) kikundi hiki kilifanya "KAFARA" ktk eneo la Maruhubi mjini Unguja. "Inasemekana" ktk "KAFARA" hiyo Maalim Seif alihudhuria.

Katika "KAFARA" hiyo, Jumuiya hiyo iliamua kufanya maandamano siku ya Jumamosi hata kama kibali walichoomba hakijatoka. Waliazimia kuandamana kwa malengo mawili makubwa:

1. Kupinga mchakato unaoendelea wa kuunda Katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
2. Kupinga Muungano uliofanywa mwaka 1964 kati ya Tanganyika na Zanzibar

Ikumbukwe kuwa, siku zote vyama vya Siasa vinaposhindwa katika chaguzi mbali mbali vimekuwa vikilalamika kuwa Katiba ya Nchi HAIFAI. Leo hii Rais Jakaya Kikwete AMEAMUA KUWAPA WATANZANIA KATIBA MPYA kwa kuwashirikisha WATANZANIA wote. Hivi ni kweli tunahitaji kumpinga ktk hili au kumpongeza?

Baada ya Jeshi la Polisi kumkamata kiongozi wa Jumuiya hiyo, wanachama wake walianzisha vurugu mitaani na kusababisha kutoweka kwa amani ktk visiwa hivyo. Kama hilo halikutosha, wanachama hao walihamasishwa kuchoma Magari, maskani za CCM na Makanisa.

Zanzibar ni moja kati ya sehemu nne duniani ambazo zilichaguliwa kuwa vituo vya kufundishia DINI ya Kiislamu karne nyingi zilizopita, ukitoa kile cha Jeddah-Saudi Arabia na Cairo-Misri. Kituo hiki kipo maeneo ya KIKUTANI mjini Unguja, hapa ndipo walipokuwa wanafundishwa MASHEIKH toka sehemu mbali mbali duniani, ambapo karibu yake kuna Msikiti wa Jibril. Kutoka ktk kituo hicho mpaka MKUNAZINI lilipo Kanisa la Kianglikani lililojengwa miaka ya 1860 ni mita zinazokisiwa kuwa kati ya 200 na 300.

Nimejaribu kuchimba historia ya DINI ktk visiwa hivyo, wallah sijapata kusoma sehemu inayoonesha kuwa kuna siku Waislamu waligombana na Wakristo ktk visiwa hivyo.

Baada ya hapo nilianza kujiuliza maswali yafuatayo:

- Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara ni kikundi cha kueneza DINI au SIASA?
- Kuna Uhusiano gani kati ya shughuli zao za kidini na Chama Cha Siasa cha CCM?
- Kuna Uhusiano gani kati Makanisa na Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ulioizaa Tanzania?
- Kuna Uhusiano gani kati ya Makanisa na Katiba ya Mpya?

Wana Jamii Forum, tunahitaji kulijadili suala hili kwa kina ili tusije kusomeka vibaya ktk historia ya nchi hii.

hivi mbona kila thread kanis kanisa kanisa tu?
 
Hao ndio wazanzibar uwa wanatenda sio wapiga longolongo...!hawadanganyiki kwa vijisent
 
Iwapo wazanzibari hawautaki muungano mbona dawa ni ndogo tu!!! Hivi ndio kusema Wanzanzibari hawana habari kwamba kati ya vyama vyote vya siasa ni Chadema tu ndio walio na sera za kutaka wazanzibari wenyewe wajadili aina ya muungano wanaoutaka?? Hivi hawa ndugu zetu waislamu wanaliona hilo? Mbona hata punguani anajua muungano ni wa ccm na cuf kwa maslahi ya wachache? Kazi ndogo sana hapo!! Vurugu za nini? Ipeni kura Chadema kupambazuke!!
 
Mtoa Mada,
wewe ni muongo mutlaq,viongoz wa uamsho c wafuac wa cuf,iyo uamsho ina wafuac wa vyama vyote,
tatzo nyiny wanyamwez vinganganizi,
lkn zenj itawatokeeni puani,mana nyiny hamtaendelea na ce ha2toendelea,2meanza zenj yanafutia kwen bara,au mu2achie nchi ye2,
nyie wenyewe hamuoni miaka 50 mumekua maskini,kisa nguvu zenu mumezielekeza zanzibar
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom