Nyani Ngabu
Platinum Member
- May 15, 2006
- 92,227
- 113,583
Naji contradict vipi? Unafikiri ukiamua kucheat utakuwa umenikomoa mimi? Mimi siogopi matatizo ya ki ukweli. Hayo ya kuwinda mwanamke nyuma mwanaume aliyekamilika hana muda nayo. Maana utakuwa unaongozwa na hisia na si lazima kuwe na ukweli... akicheka kosa, akisalimiana na mtu kosa, akichelewa kurudi kosa. Wewe unafikiri hayo yatakuwa maisha? Najiamini kabisa natimiza wajibu wangu na sina muda wa kutafuta matatizo yasiyokuwepo. Nyinyi mnaoona hayo ndio mapenzi kila la kheri
Mwanaume wa ukweli haogopi chochote. Hata aje simba ndani ya nyumba atakuwa yuko tayari kufa kulinda familia yake seuze kulinda heshima yake dhidi ya mwanamke anayemvunjia?
Labda siku hizi fasili ya uanaume wa kweli imebadilika lakini kwangu mwanaume ambaye yuko delicate na ambaye hapendi kujua ukweli kisa anaogopa kuumizwa huyo kwangu siyo mwanaume kamili. Ni mwaname wa kuchorwa huyo.