Researcher
Senior Member
- Dec 15, 2010
- 187
- 48
Kuna vita nzito ya kipropaganda inayoendelea baina ya hawa Jamaa wa mashariki ya mbali na wale wa magharibi. Ni ukweli usiofichika kwamba uchumi wao unakuwa kwa kasi ya ajabu na hivyo kuwa tishio kwa ulaya na marekani.. Si kusudii kujadili hilo.
Ila nimeguswa na uhusiano kati ya nchi yetu na hawa watu. Natambua kwamba nchi yetu inaheshimu haki za binadamu na vilevile ni mwanachama wa jumuiya za kibiashara za kimataifa kama WTO. Zaidi ya hivyo nchi yetu imekuwa na mahusiano ya muda mrefu kiitikadi na kiuchumi. Sote tunafahamu kwamba mwezi januari wachina waliamrishwa kufunga virago na kurudi kwao. Sijaweza kufuatilia hatma ya sakata hilo. Hata hivyo pamoja na kwamba amri ile ilikuwa na mapungufu yake, ni ishara kwamba serikali imeanza kuona kuna tatizo.
Tayari mambo kadhaa yameshajidhihirisha;
1. Kwamba kuna uwepo wa wachina wanaofanya kazi nchini bila vibali au kupitia njia zisizo halali
2. Kwamba kuna wachina wanaofanya kazi ambazo watanzania wanaweza kuzifanya na hivyo kukuza tatizo la ajira nchini
3. Kwamba kasi ya kuongezeka wachina ni kubwa na swala hili lisipowekewa mkakati itakuwa tishio kwa uchumi wa nchi yetu
Nimegundua kwamba kuna mengine ambayo yamekuwepo kama tetesi na yanahitaji utafiti kupata ushahidi;
1. Kuna idadi kubwa ya makahaba wa kichina waliosajiliwa kwa huduma za massage n.k jijini dar es salaam
2. Kampuni za kichina zimekuwa zikitumia udhaifu wa mfumo wetu wa manunuzi na tamaa ya baadhi yetu kujinyakulia zabuni kwa kukiuka taratibu
3. Nguvu ya wachina nchini inazidi kuimarika na wakati mwingine wanakuwa wababe kwa wazawa
4. Kuna viwanda vya wachina visivyotambulika na serikali nchini. havilipi kodi na ambavyo vinachochea kasi ya kuongezeka bidhaa feki
Lakini vilevile nimegundua mambo kadhaa ya mazuri kuhusiana na wachina;
1. Wachina ni watu hodari wa kufanya kazi na tunaweza kujifunza mengi katika utendaji wao. Mfano vijana waliofanya kazi kwenye gereji za wachina wakiwezeshwa wanaweza kuwa wajasiriamali wazuri sana.
2. Mazingira ya awali ya uchina ni sawa na ya kwetu ya sasa na hivyo tuna mengi ya kuiga kuhusiana na maendeleo ya viwanda toka kwao
3. Misaada ya wchina haina longolongo kama ya ulaya na ajenda kubwa kwao ni ajira kwa watu wao kwenye miradi yao.
Hata hivyo bado tunahitaji kujipanga zaidi katika swala hili;
Tunaweza kuhamisha teknolojia toka kwao kuja kwetu, mfano viwanda
Tunaweza kujifunza mbinu na namna wanavyofanya kazi kuimarisha uwezo wa ndani
Tuanze kuuhakiki mfumo wa vibali vya kazi, na mianya yake ili kulinda ajira zetu
Ikibidi tuimarishe mwenendo wa uzalendo katika manunuzi binafsi ili pesa yetu izunguke ndani isiishie nje ya nchi.
Kama kuna mengine wadau nitafurahi kupata michango yenu.
Angalizo:
Ikumbukwe kwamba nchini kwao pia kuna weusi wengi wakiwemo watanzania
Bado wachina hawajajikita (mfano madini na nishati) kwenye mikataba yenye kutuletea hasara kubwa kama wasauzi na nataifa mengine.
Binafsi siwachukii wachina ila najaribu kuona na sisi tunanufaika na uwepo wao nchini.
Ila nimeguswa na uhusiano kati ya nchi yetu na hawa watu. Natambua kwamba nchi yetu inaheshimu haki za binadamu na vilevile ni mwanachama wa jumuiya za kibiashara za kimataifa kama WTO. Zaidi ya hivyo nchi yetu imekuwa na mahusiano ya muda mrefu kiitikadi na kiuchumi. Sote tunafahamu kwamba mwezi januari wachina waliamrishwa kufunga virago na kurudi kwao. Sijaweza kufuatilia hatma ya sakata hilo. Hata hivyo pamoja na kwamba amri ile ilikuwa na mapungufu yake, ni ishara kwamba serikali imeanza kuona kuna tatizo.
Tayari mambo kadhaa yameshajidhihirisha;
1. Kwamba kuna uwepo wa wachina wanaofanya kazi nchini bila vibali au kupitia njia zisizo halali
2. Kwamba kuna wachina wanaofanya kazi ambazo watanzania wanaweza kuzifanya na hivyo kukuza tatizo la ajira nchini
3. Kwamba kasi ya kuongezeka wachina ni kubwa na swala hili lisipowekewa mkakati itakuwa tishio kwa uchumi wa nchi yetu
Nimegundua kwamba kuna mengine ambayo yamekuwepo kama tetesi na yanahitaji utafiti kupata ushahidi;
1. Kuna idadi kubwa ya makahaba wa kichina waliosajiliwa kwa huduma za massage n.k jijini dar es salaam
2. Kampuni za kichina zimekuwa zikitumia udhaifu wa mfumo wetu wa manunuzi na tamaa ya baadhi yetu kujinyakulia zabuni kwa kukiuka taratibu
3. Nguvu ya wachina nchini inazidi kuimarika na wakati mwingine wanakuwa wababe kwa wazawa
4. Kuna viwanda vya wachina visivyotambulika na serikali nchini. havilipi kodi na ambavyo vinachochea kasi ya kuongezeka bidhaa feki
Lakini vilevile nimegundua mambo kadhaa ya mazuri kuhusiana na wachina;
1. Wachina ni watu hodari wa kufanya kazi na tunaweza kujifunza mengi katika utendaji wao. Mfano vijana waliofanya kazi kwenye gereji za wachina wakiwezeshwa wanaweza kuwa wajasiriamali wazuri sana.
2. Mazingira ya awali ya uchina ni sawa na ya kwetu ya sasa na hivyo tuna mengi ya kuiga kuhusiana na maendeleo ya viwanda toka kwao
3. Misaada ya wchina haina longolongo kama ya ulaya na ajenda kubwa kwao ni ajira kwa watu wao kwenye miradi yao.
Hata hivyo bado tunahitaji kujipanga zaidi katika swala hili;
Tunaweza kuhamisha teknolojia toka kwao kuja kwetu, mfano viwanda
Tunaweza kujifunza mbinu na namna wanavyofanya kazi kuimarisha uwezo wa ndani
Tuanze kuuhakiki mfumo wa vibali vya kazi, na mianya yake ili kulinda ajira zetu
Ikibidi tuimarishe mwenendo wa uzalendo katika manunuzi binafsi ili pesa yetu izunguke ndani isiishie nje ya nchi.
Kama kuna mengine wadau nitafurahi kupata michango yenu.
Angalizo:
Ikumbukwe kwamba nchini kwao pia kuna weusi wengi wakiwemo watanzania
Bado wachina hawajajikita (mfano madini na nishati) kwenye mikataba yenye kutuletea hasara kubwa kama wasauzi na nataifa mengine.
Binafsi siwachukii wachina ila najaribu kuona na sisi tunanufaika na uwepo wao nchini.