Wawakilishi wataka wazanzibari wapewe uhuru wakuchagua juu ya muungano

GHIBUU

JF-Expert Member
Jan 13, 2011
4,432
3,006
Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi kutoka CUF na CCM leo hawakutafuna maneno na waliungana pamoja kueleza waziwazi kuwa Mswada wa Sheria ya Mapitio ya Katiba unapaswa kuwapa fursa wananchi kujadili mambo yote likiwemo Muungano na kwamba iwapo wanaona hauna maslahi nao na wakataka usiwepo, basi maoni hayo yaheshimiwe maana mamlaka ya nchi yanatoka na yanaamuliwa na wananchi wenyewe. Samwel Sitta aliondoka na ujumbe huo.
 
Mi naona ni vzr wapewe nafasi ya kupiga kura wanaotaka muungano waseme ndiooo na wasiotaka waseme siooo.kwani wananchi ndio wenye maamuzi juu ya nchi yao na serikari yao!
 
Huu upuuzi sasa. Kama zanzibar ni nchi basi ukerewe nayo nchi, au pemba nayo nchi, au dsm nayo nchi maana dsm ina watu milioni 4, wakati zanzbar ina milioni 1 na ina rais, wakati dsm inaongozwa na mkuu wa mkoa.
 
Huu upuuzi sasa. Kama zanzibar ni nchi basi ukerewe nayo nchi, au pemba nayo nchi, au dsm nayo nchi maana dsm ina watu milioni 4, wakati zanzbar ina milioni 1 na ina rais, wakati dsm inaongozwa na mkuu wa mkoa.

@kinenekejo: rudi shule, hujui unaongea nn? nailaumu ccm kukunyima elimu
 
Back
Top Bottom