wawakilishi wa TANZANIA NA MALAWI kukutana MZUZU tarehe August 20 2012

Acheni porojo.tupeni data kama amendments za mipaka baada ya treaty ya mwaka 1890 kama alivyokuwa anaelezea Waziri Membe mwaka 1947...........bungeni, na maazimio ya umoja wa mataifa kuhusu mipika ya kwenye maji,milima,mito n.k.tuone kama tuna hoja vinginevyo hawa wamalawi watatuzidi kwa hoja yao.tutapoteza ziwa lote,wavuvi wetu watatozwa kodi na mengineyo,ni sawa na kuuza baraza ya nyumba yako wakati bado unaishi ndani ya nyumba.

Waafrika tunapashwa kuwa watu wa hekima , Hapa ni hekima na busara inapashwa kutawala ,tuachane na mambo ya wakoloni ambayo kwa akili ya kawaida unajua jambo hili si sahii.Kama Malawi wanasema ziwa lote upandewa Tanzania nia lao ina maana watu wanaoishi kando ya ziwa upande wa Tanzania itawalazimu wakachukue visa kwenda kuchota maji ziwa Nyasa ? Hapa ni kutumia busara wala sio sheria za kijinga jinga tunazoambiwa.
Nitoe mfano wa mto Kagera tunajua kuwa unatoka mbali na kupitia Tanzania na kwa kuwa unapita kwetu ni mali yetu tunaweza kufanya tunavyotaka hata kubadirisha maji yapite kwingine. Tukifanya hivyotutakuwa tumetangaza vita na nchi za waarabu. Sasa basi na watu waliokando ya maziwa haya yetu tuliyonayo wanayo haki ya kuyatumia na utakuwa unatangaza vita kama ukitaka kuwakataza kutumia hii zawadi waliyopewa na Muumba wao. Mipaka inawekwa kwa kutumia busara sio sheria wakati unaona jambo hili litaleta matatizo
 
Tuwachape haraka tuachane nao...mdogo akikuanza mmalize ili kutishia wakubwa wasikutafute, wamesahau ya Uganda inabidi tuwakumbushe
 
Malawi and Tanzania representatives are scheduled to meet in Mzuzu on August 20 2012 ;


Malawi wana hoja 3 za msingi.

3. Zoezi ili lilikuwepo kitambo kwanini baada ya kuchaguliwa raisi mwanamke ndo Tanzania inapeleka majeshi na si kipindi cha mihula ya viongozi wanaume?

Ha, ha, ha!!! Kwani Tanzania na Malawi wakipigana ni raisi JK na Banda ndio watazipiga ngumi? Au jeshi la Malawi nalo limekuwa la wanawake watupu?

Unanikumbusha Idd Amin alivyomwambia Nyerere wakati wa vita vya Kagera, "mimi na Nyerere tuingie ukumbi wa ngumi, na niko tayari kufungwa mkono mmoja! Atakayepigwa basi nchi yake imeshindwa vita!"
 
Waafrika tunapashwa kuwa watu wa hekima , Hapa ni hekima na busara inapashwa kutawala ,tuachane na mambo ya wakoloni ambayo kwa akili ya kawaida unajua jambo hili si sahii.Kama Malawi wanasema ziwa lote upandewa Tanzania nia lao ina maana watu wanaoishi kando ya ziwa upande wa Tanzania itawalazimu wakachukue visa kwenda kuchota maji ziwa Nyasa ? Hapa ni kutumia busara wala sio sheria za kijinga jinga tunazoambiwa.
Nitoe mfano wa mto Kagera tunajua kuwa unatoka mbali na kupitia Tanzania na kwa kuwa unapita kwetu ni mali yetu tunaweza kufanya tunavyotaka hata kubadirisha maji yapite kwingine. Tukifanya hivyotutakuwa tumetangaza vita na nchi za waarabu. Sasa basi na watu waliokando ya maziwa haya yetu tuliyonayo wanayo haki ya kuyatumia na utakuwa unatangaza vita kama ukitaka kuwakataza kutumia hii zawadi waliyopewa na Muumba wao. Mipaka inawekwa kwa kutumia busara sio sheria wakati unaona jambo hili litaleta matatizo

Hao wazungu hawakuwa na busara wakati wa kugawa bara la afrika,hiyo treaty 1890 inayozungumziwa na Malawi ni matatizo matupu walipeana milima mito ziwa fukwe kama zawadi kwa viongozi wao,hiyo treaty inagawa fukwe yote kuanzia Somalia hadi Sofala msumbiji kwa sultani wa Zanzibar hata wanaojiita Baraza la Mombasa huko Kenya wamezuka na hoja hiyo kuwa Mombasa siyo Kenya ni Zanzibar wanataka wajiunge huko, Mlima Kilimanjaro ulikuwa Kenya alipewa Malkia Elizabeth wa Uingereza kama zawadi na mipaka ikarekebishwa,Hivi Kenya wanaweza kulidai? si kuna sheria iliandikwa ili kuutoa kwa Tanganyika?

Ziwa Victoria halikadhalika ni zawadi ya Malkia Victoria wa uingerza,Rwanda,Burundi zilikuwa Tanganyika enzi hiyo chini ya mjerumani DEA baadae wakapewa koloni wabelgiji hapa ndipo ilipozaliwa Tanganyika,ziwa Nyasa alipewa zawadi malkia wa uingereza jina lake silijui wakati huo wajerumani kabla ya vita kuu ya kwanza ya dunia baada ya vita kuu ya kwanza kuna mabadiliko yaliyofikiwa ambayo watawala wa Malawi wakati huo Nyasaland hawakuyaafiki.

Ukumbuke Tanganyika haikuwa koloni la mwingereza kama ilivyokuwa Nyasaland hivyo asingeweza kubadili lolote kutupendelea,hata maji ya ziwa victoria na mto nile,Kagera walipewa Misri wanywe na kumwagilia mashamba yao kwani waingereza hawakuwa na cha kupoteza katika makoloni yao huko Uganda na Kenya,hili vuguvugu waliloanzisha Malawi ni kukumbushia machungu ya wakoloni walivyotugawa na kutuuza utumwani kama bidhaa hawakutujali kabisa kuwa na sisi ni binadamu kugawa maeneo yetu kama ilivyowapendeza wakubwa wao.

Kwa maoni yangu hizi choko choko zimeanzia mbali sikiliza wazanzibari wanavyosema hivi sasa,huko Kenya Mombasa huko Misri kuhusu maji ya victoria huko Rwanda na Burundi na sasa Malawi,nashindwa kuamini jinsi waafrika tunavyosumbuliwa na makubaliano ya wakoloni kama hawa wamalawi sasa,hivi toka mwaka 1964 baada ya uhuru wao walikuwa wapi,tena wanatumia sheria ya mwaka 1890 wakati huo hata Tanganyika haikuwepo karne zote hizo zimepita bila migogoro hadi imezaliwa Tanzania ndiyo mgogoro unaanza,wakati huo hata umoja wa mataifa haukuwepo,hivi ni halali kwa wangoni kudai Afika kusini ni nchi yao?

Eti kwa kuwa wametokea huko,hekima za kiafrika zinatakiwa zitumike zaidi kuliko kufuata mapandikizi ya wazungu yanayotusumbua hadi sasa,sera yao ya devide and rule inaonekana kushika kasi tena karne hii huko Kongo,Rwanda,Burundi hawaishi kwa amani toka enzi hizo kutokana na kugawanywa kwa mafungu ya kikabila mabwana na watwana,haya na sasa yanajirudia huko Malawi wanazungumzia jambo ambalo hata babu zao enzi hizo walikuwa hawalijui au walishakamatwa na kuuzwa utumwani.

Kwa wapendao kusoma vitabu tafuta kitabu kilichoandikwa Robert Roodney,How Europe undeveloped Africa,utajifunza mengi,mwandishi kwa wakati fulani alikuwa mhadhiri chuo kikuu cha Dar rs salaam,kabla ya kurudi kwao Jamaika na kwenda kukutana na mauti,nafikiri ni haohao walimuondoa kutokana na kuwaweka wazi siri zao nyingi.
 
Wamalawi: Wanatumia Helgoland treaty ya 1890 " Ziwa sehemu ya Tanzania ni lao"
Tanzania : Wanatumia UN convection ya 1982 " nusu ya ziwa upande wa Tanzania ni eneo la Tanzania"

haya sasa wakienda kwenye Internationa law sijui nani atashinda


Umesahau na Belin conference nao ni mkataba ulio upande wa tanzania.

Kuna hoja kwamba je, Uingereza na Ujerumani zilikuwa na mandate ya kurekebisha mkataba wakati wa "mandate territory?' kwani kipindi hicho Tanganyika haikuwa koloni halisi la Uingereza.
 
Umesahau na Belin conference nao ni mkataba ulio upande wa tanzania.

Kuna hoja kwamba je, Uingereza na Ujerumani zilikuwa na mandate ya kurekebisha mkataba wakati wa "mandate territory?' kwani kipindi hicho Tanganyika haikuwa koloni halisi la Uingereza.
Na kuna ishu kwamba nchi za africa zilikubaliana kuheshimu mipaka iliowekwa na wakoloni sikumbuki ni "makubaliana ya wapi haya"
 
nakubalia na wewe kiasi MAMA POROJO ,JK.Nyerere na banda walikuwa hawaendani kimtazamo, kiitikadi nafilosofia, but tukiwa focal kwenye hii dispute ya mpaka ,
swali linalohumiza kichwa ni kuwa, :
kwanini hawakufikia muafaka ??? whiy this dispute remained domant for all those year ??? je , unafikiri mazingira ya mwaka 2012 ni mazuri zaidi kwa kusolve hii issue diplomatically ukilinganisha na mazingira ya 1964 ???

kwa nini naisi vita ipo mlangoni:
1. viongozi wetu wa kisiasa wanaochulia hili suala kwa advantage ili kufanikisha azma yao ya kuwa successor wa JK-ilaza
2.pressure toka kwa wananchi wa malawi kwa raisi wao, kwamba yeye ni mwanamke dhaifu, ambaye ameshindwa hata kusema neno katika huu mgogoro wakati viongozi wake wa chini wakiongea nonsense
3.greed ya wawekezaji, hasa kwa upande wa malawi kwani ni vibaraka
4. kuna loop holes nyingi katika madai ya kila upande kuhusu umiliki wa ziwa. hili loop holes ndo zinafanya kila upande uamini kuwa hawa kwenye mahakama za kimataifa zitashinda
5. K.B na JK-Nyerere legacy kwa wananchi wao...ofcourse toka tupo chekechea tunajua mpaka upo katikati ya ziwa, je wamalawi wamekuwa wakifundishwa nini ? wamefundishwa mpaka upo kwenye shore of the lake....

UDHANI NI UPANDE GANI KATI YA TZ- & MALAWI utakao sacrifice madai yake kugrant WIN-WIN resolution na akaeleweka??? JK-ilaza dhaifu , mama banda dhaifu ... nguvu ya watu walio nyuma inatupeleka vitani

Hili suala halikubaki domant kama unavyotaka sisi tukuelewe labda kama lilibaki domant kwako tu.....

Baada ya kamuzu Banda alikuja Bakili Muluzi ndipo lilianza kuzungumzwa chini ya Mkapa na kIKWETE AKIWA WAZIRI WA NJE halikupata muafaka. Wakati Mazungumzo yanaendelea Malawi ikapata rais mpya Bingu wa Mutharika ambaye alikuwa muumini wa ziwa lote ni lao hakutoa ushirikiano wa kutosha na kuthibitisha hili ndiye aliyeleta makampuni ya mafuta kutafiti........ je huyo tungekaa naye meza moja?
 
Tunataka tujue timu itakayounda jopo la Tanzania. Mimi sitaki AG Werema awemo huyu ni kiazi mkubwa.

Jopo la Tanzania lipitie kwa umakini evidence ambazo Malawi wanadai zinahalalisha ziwa lote kuwa ni lao. From there Tanzania wajenge hoja zao.

Mimi nadhani tujike tuu katika vita huenda tutafanikiwa lakini maswala ya kukaa mezani wawakaili wa kibongo watatuangusha, kwa mfano unaweza ukaamini namna Serikali ilivyoshindwa katika kesi na kuamliwa kuwalipa Dowans? Hapa kuna watu tuliwatuma kutuwakilisha lakini hawawezi ku-argue
 
Na kuna ishu kwamba nchi za africa zilikubaliana kuheshimu mipaka iliowekwa na wakoloni sikumbuki ni "makubaliana ya wapi haya"

Je ishu hii haikukiuka mikataba ya kimataifa? je heligoland haikukiuka mkataba wa Belin Conference? Ni upi mkataba mama????
 
Mimi nadhani tujike tuu katika vita huenda tutafanikiwa lakini maswala ya kukaa mezani wawakaili wa kibongo watatuangusha, kwa mfano unaweza ukaamini namna Serikali ilivyoshindwa katika kesi na kuamliwa kuwalipa Dowans? Hapa kuna watu tuliwatuma kutuwakilisha lakini hawawezi ku-argue


nalo neno????
 
Je ishu hii haikukiuka mikataba ya kimataifa? je heligoland haikukiuka mkataba wa Belin Conference? Ni upi mkataba mama????
Mama Porojo haya yote yatajibiwa wakipeleka hii ishu kwenye internationa Court, other wise tukae tu kama walivyosema mwanzo "we are all brother, let them fish , swim, do whatever they like coz it's their inheritance"
 
LAKENYASA.jpg
haka karamani kameshaniharibia geografia yangu ndogo niliyokuwa naijua
 
Waafrika tunapashwa kuwa watu wa hekima , Hapa ni hekima na busara inapashwa kutawala ,tuachane na mambo ya wakoloni ambayo kwa akili ya kawaida unajua jambo hili si sahii.Kama Malawi wanasema ziwa lote upandewa Tanzania nia lao ina maana watu wanaoishi kando ya ziwa upande wa Tanzania itawalazimu wakachukue visa kwenda kuchota maji ziwa Nyasa ? Hapa ni kutumia busara wala sio sheria za kijinga jinga tunazoambiwa.
Nitoe mfano wa mto Kagera tunajua kuwa unatoka mbali na kupitia Tanzania na kwa kuwa unapita kwetu ni mali yetu tunaweza kufanya tunavyotaka hata kubadirisha maji yapite kwingine. Tukifanya hivyotutakuwa tumetangaza vita na nchi za waarabu. Sasa basi na watu waliokando ya maziwa haya yetu tuliyonayo wanayo haki ya kuyatumia na utakuwa unatangaza vita kama ukitaka kuwakataza kutumia hii zawadi waliyopewa na Muumba wao. Mipaka inawekwa kwa kutumia busara sio sheria wakati unaona jambo hili litaleta matatizo

Hata pale mkazi wa kyela atakapotaka kumwagia busitani kwa maji ya ziwa nyasa ambayo yako hatua 10 kutoka kwenye nyumba yake atakuwa anatumia maji ya Malawi ni tresspass...... hizo ndizo sheria za wazungu tunaowaona wana busara.
 
Mimi nadhani tujike tuu katika vita huenda tutafanikiwa lakini maswala ya kukaa mezani wawakaili wa kibongo watatuangusha, kwa mfano unaweza ukaamini namna Serikali ilivyoshindwa katika kesi na kuamliwa kuwalipa Dowans? Hapa kuna watu tuliwatuma kutuwakilisha lakini hawawezi ku-argue

chukua 84%
 
Kimantiki kwa mtu yoyote mwenye hekima na busara atakubaliana nami kwamba kama wazungu wa Kiingereza ndio waliweka mipaka hiyo ilikuwa kwa maslahi yao sio maslahi ya nchi zetu na wakazi wanaoishi kwenye mwambao wa Ziwa Nyasa kwa pande zote za Malawi na Tanganyika( tanzania).
 
Mama Porojo haya yote yatajibiwa wakipeleka hii ishu kwenye internationa Court, other wise tukae tu kama walivyosema mwanzo "we are all brother, let them fish , swim, do whatever they like coz it's their inheritance"

Well said. thx..... hata mimi vita sipendi mjadala ndio utanipeleka vitani lakini ukweli unabaki palepale wamalawi waache kutuambia ziwa sio letu na waondoe makampuni ya mafuta ili tuweze kurudi mezani.

Huwezi kuendelea kuzungumza na mtu ambaye tayari anaweka wawekezaji kwenye eneo la mgogoro.
 
Maji ni uhai huwezi kuwapa upande mmoja wa nchi wakati maji hayo yako mpakani...... huwezi kulinganisha na mlima kilinjaro eti na mwenyewe wangegawa katikati..... wapi na wapi.
 
Maji ni uhai huwezi kuwapa upande mmoja wa nchi wakati maji hayo yako mpakani...... huwezi kulinganisha na mlima kilimanjaro eti na mwenyewe wangegawa katikati kat ya Kenya na Tanzania..... wapi na wapi. Mlima ni lazima uwe upande mmoja.
 
Back
Top Bottom