armanisankara
JF-Expert Member
- Jul 15, 2011
- 283
- 49
Zaidi ya wananchi 100 wamekamatwa katika Operesheni iliyoanza juzi ya kuwaondoa watu waliovamia maeneo yasiyo yao, inayoendeshwa katika eneo la Nakasangwe, Kata ya Wazo, wilayani Kinondoni chini ya Kamanda Charles Kenyela ambaye pia ni Kamanda wa kipolisi wa mkoa huo, kwa makosa ya kuvamia maeneo ya watu, kulishambulia jeshi la polisi wakati likiingia kutekeleza zoezi hilo kwa kutumia silaha za jadi ambazo ni panga, shoka, upinde na mawe pamoja na kukutwa na pombe haramu ya gongo.
Aidha, zaidi ya makazi ya kudumu na siyo ya kudumu 500 yamebomolewa kufikia jana katika operesheni hiyo.
Kamanda Kenyela aliiambia NIPASHE jana kwamba operesheni hiyo haikupata upinzani wowote kwa siku ya jana.
Leo (jana) tumeingia hapa Nakasangwe tukianzia kwenye kitongoji cha Kaza Roho kwa amani, na hatukupata mtu wa kutuzuia, kuturushia chochote na kwa kweli kuko shwari kama unavyoona.Wengi wa wananchi waliopo wanatoa vifaa vyao na sisi hatuna tatizo la kumzuia mtu anayetoa mali yake, kwa kuwa lengo letu sisi kama tulivyokuwa tumewaambia toka awali, ni kuwa hatutaki watu wa kuvamia maeneo ya wenzao, alisema.
Alisema polisi jana haikurusha bomu hata moja la kutoa machozi wala risasi katika eneo hilo kwa kuwa hali ilikuwa shwari.
Kamanda Kenyela alisema wakati wa operesheni hiyo jana walifanikiwa kuvunja nyumba moja ambayo iligundulika kuwa ndiyo ilikuwa inatumiwa na wavamizi kama Ofisi ya Serikali ya Mtaa huo katika kitongoji cha Kaza Roho ambapo walikuta mihuri, nakala ya hati za mauziano ya maeneo ya watu zilizokuwa zikisimamiwa na serikali hiyo bandia, nakala ya barua feki zilizokuwa zikiwatambulisha wananchi wa maeneo hayo kama wakazi halali pamoja na ubao wa matangazo.
Aidha alisema kwamba waliweza kuvunja vile vile shina la wakereketwa wa Chama cha Mapinduzi (CCM) la Kinondo C lililokuwa limejengwa kwenye eneo la mmiliki aliyekuwa amevunjiwa nyumba yake na wavamizi, kufukuzwa na mbuzi wake 50 walichinjwa na wavamizi hao.
Alisema polisi pia wamewakamata wanawake watatu na dalali wao waliokuwa wameletwa kuonyeshwa eneo la kununua ambalo linamilikiwa na mtu mwingine.
Kamanda Kenyela aliwaasa wananchi wanaomiliki maeneo yao katika eneo hilo na maeneo mengine jijini Dar es salaam, kutoyaacha kwa muda mrefu bila kuyatembelea wala kuyaendeleza kwani yanapobaki hivyo, yanageuka kishawishi kwa baadhi ya watu kudhani hayana wenyewe na hivyo kuyavamia.
CHANZO: NIPASHE
Aidha, zaidi ya makazi ya kudumu na siyo ya kudumu 500 yamebomolewa kufikia jana katika operesheni hiyo.
Kamanda Kenyela aliiambia NIPASHE jana kwamba operesheni hiyo haikupata upinzani wowote kwa siku ya jana.
Leo (jana) tumeingia hapa Nakasangwe tukianzia kwenye kitongoji cha Kaza Roho kwa amani, na hatukupata mtu wa kutuzuia, kuturushia chochote na kwa kweli kuko shwari kama unavyoona.Wengi wa wananchi waliopo wanatoa vifaa vyao na sisi hatuna tatizo la kumzuia mtu anayetoa mali yake, kwa kuwa lengo letu sisi kama tulivyokuwa tumewaambia toka awali, ni kuwa hatutaki watu wa kuvamia maeneo ya wenzao, alisema.
Alisema polisi jana haikurusha bomu hata moja la kutoa machozi wala risasi katika eneo hilo kwa kuwa hali ilikuwa shwari.
Kamanda Kenyela alisema wakati wa operesheni hiyo jana walifanikiwa kuvunja nyumba moja ambayo iligundulika kuwa ndiyo ilikuwa inatumiwa na wavamizi kama Ofisi ya Serikali ya Mtaa huo katika kitongoji cha Kaza Roho ambapo walikuta mihuri, nakala ya hati za mauziano ya maeneo ya watu zilizokuwa zikisimamiwa na serikali hiyo bandia, nakala ya barua feki zilizokuwa zikiwatambulisha wananchi wa maeneo hayo kama wakazi halali pamoja na ubao wa matangazo.
Aidha alisema kwamba waliweza kuvunja vile vile shina la wakereketwa wa Chama cha Mapinduzi (CCM) la Kinondo C lililokuwa limejengwa kwenye eneo la mmiliki aliyekuwa amevunjiwa nyumba yake na wavamizi, kufukuzwa na mbuzi wake 50 walichinjwa na wavamizi hao.
Alisema polisi pia wamewakamata wanawake watatu na dalali wao waliokuwa wameletwa kuonyeshwa eneo la kununua ambalo linamilikiwa na mtu mwingine.
Kamanda Kenyela aliwaasa wananchi wanaomiliki maeneo yao katika eneo hilo na maeneo mengine jijini Dar es salaam, kutoyaacha kwa muda mrefu bila kuyatembelea wala kuyaendeleza kwani yanapobaki hivyo, yanageuka kishawishi kwa baadhi ya watu kudhani hayana wenyewe na hivyo kuyavamia.
CHANZO: NIPASHE