Salary Slip
JF-Expert Member
- Apr 3, 2012
- 47,013
- 144,371
Wauguzi wa hospitali ya mirembe mkoani Dodoma wamegoma wakidai kuongezewa posho ya muda wa ziada wa kazi.
Wauguzi hao wanadai kiasi cha sh 3000 wanacholipwa ni kidogo ukilinganisha na kiwango wanacholipwa wengine.
Muuguzi mmoja ameiambia Nipashe kwamba wameamua kugoma baada ya kuona serikali haiwaangalii umuhimu wao.
Muuguzi huyo alisema kuwa mwezi julai walilipwa sh 10,000 lakini mwezi uliofuatia walilipwa kiwango tofauti jambo lililowashitua na kutaka kujua sababu zake.
Mganga mkuu wa hospitali hiyo Dr. Erasmusi Mndeme alikanusha kuwepo mgomo wa madaktari na kusisitiza kuwa waliogoma ni wauguzi.
Aidha alisema kuna baadhi ya madaktari na wauguzi wanaingia kazini mara mbili kwa siku kutokana na upungufu wa wafanyakazi ktk hospitali hiyo.
Dr.Mndeme alisema swala la malipo ktk hospitali hiyo liko kwenye viwango tofauti kulingana na vyeo vya watumishi hao.Alisema kuna watumishi wanalipwa sh 25,000,20,000,15,000,10,000 na kiwango cha chini cha malipo ni sh 5000 hadi sh 3000.
Alisema kulingana na viwango hivyo ndio maana wauguzi wanaona wanapunjwa bila kufahamu kuwa katika nafasi walizonazo kuna utofauti mkubwa wa malipo wanayolipwa pindi wanapofanya kwenye ziada ya masaa.
Chanzo:Nipashe la trh 06/10/2012.
Hapa ndipo tunapoona ule umuhimu na ulazima wa ule mgomo wa madaktari kwani serikali hii ni kama sikio la kufa halisikii dawa.
Wauguzi hao wanadai kiasi cha sh 3000 wanacholipwa ni kidogo ukilinganisha na kiwango wanacholipwa wengine.
Muuguzi mmoja ameiambia Nipashe kwamba wameamua kugoma baada ya kuona serikali haiwaangalii umuhimu wao.
Muuguzi huyo alisema kuwa mwezi julai walilipwa sh 10,000 lakini mwezi uliofuatia walilipwa kiwango tofauti jambo lililowashitua na kutaka kujua sababu zake.
Mganga mkuu wa hospitali hiyo Dr. Erasmusi Mndeme alikanusha kuwepo mgomo wa madaktari na kusisitiza kuwa waliogoma ni wauguzi.
Aidha alisema kuna baadhi ya madaktari na wauguzi wanaingia kazini mara mbili kwa siku kutokana na upungufu wa wafanyakazi ktk hospitali hiyo.
Dr.Mndeme alisema swala la malipo ktk hospitali hiyo liko kwenye viwango tofauti kulingana na vyeo vya watumishi hao.Alisema kuna watumishi wanalipwa sh 25,000,20,000,15,000,10,000 na kiwango cha chini cha malipo ni sh 5000 hadi sh 3000.
Alisema kulingana na viwango hivyo ndio maana wauguzi wanaona wanapunjwa bila kufahamu kuwa katika nafasi walizonazo kuna utofauti mkubwa wa malipo wanayolipwa pindi wanapofanya kwenye ziada ya masaa.
Chanzo:Nipashe la trh 06/10/2012.
Hapa ndipo tunapoona ule umuhimu na ulazima wa ule mgomo wa madaktari kwani serikali hii ni kama sikio la kufa halisikii dawa.