CULCULUS
JF-Expert Member
- Nov 17, 2011
- 316
- 619
Leo nikiwa nimevinjari ndani ya Ofisi za Wizara ya Afya kwa shughuli zangu binafsi niliingia Ofisi moja ambayo nilikuta Watumishi wapo katika mjadala mkali wa kulinganisha Uongozi wa Katibu Mkuu wa sasa Bi Blandina Nyoni na aliyekuwepo kabla Mzee Wilson Mukama ambae alihamishiwa Wizara ya Maji kisha kustaafu na baadae Kikwete akamteua kuwa Katibu Mkuu wa CCM Taifa hadi sasa.
Watumishi waliokuwepo ambao walikuwa takribani 12 hivi walionyoesha ni jinsi gani Wilson Mukama alivyokuwa anawajali kwa kuwalipa stahili zao haraka mfano Malipo ya likizo, uhamisho, Overtime, nk. Wanakereka na jinsi Nyoni anavyoendesha Wizara kwa kutumia watu waliowataja kuwa ni maaskari wake (Informers) wa kusikiliza huyu anasema nini na yule anasema nini dhidi ya utawala wake. Kibaya zaidi wanaghadhabika na jinsi Blandina Nyoni anavyojidai ni mlinzi wa mali za serikali wakati yeye ndiye mdokozi mkubwa wa mali hizo. Kwa haraka haraka wanaonekana ni watumishi waliochoka na kuukatia tamaa na uongozi uliopo. Mmoja wao alisema hivi nanukuu: 'Licha ya kwamba ni MwanaCCM lakini tutamkumbuka sana Wilson Mukama, ni Katibu Mkuu bomba sana, hatutakuja kumpata mtu kama yeye' Mwisho wa kunukuu..
Watumishi waliokuwepo ambao walikuwa takribani 12 hivi walionyoesha ni jinsi gani Wilson Mukama alivyokuwa anawajali kwa kuwalipa stahili zao haraka mfano Malipo ya likizo, uhamisho, Overtime, nk. Wanakereka na jinsi Nyoni anavyoendesha Wizara kwa kutumia watu waliowataja kuwa ni maaskari wake (Informers) wa kusikiliza huyu anasema nini na yule anasema nini dhidi ya utawala wake. Kibaya zaidi wanaghadhabika na jinsi Blandina Nyoni anavyojidai ni mlinzi wa mali za serikali wakati yeye ndiye mdokozi mkubwa wa mali hizo. Kwa haraka haraka wanaonekana ni watumishi waliochoka na kuukatia tamaa na uongozi uliopo. Mmoja wao alisema hivi nanukuu: 'Licha ya kwamba ni MwanaCCM lakini tutamkumbuka sana Wilson Mukama, ni Katibu Mkuu bomba sana, hatutakuja kumpata mtu kama yeye' Mwisho wa kunukuu..