Andrew Nyerere
JF-Expert Member
- Nov 10, 2008
- 3,007
- 2,429
Mimi nadhani ingekuwa bora kama watuhumiwa wote wa EPA wangesamehewa. Siyo wasamehewe na Rais au Mahakama,ila wasamehewe na wananchi. Watanzania ni bora tujifunze kusamehe,kwa sababu Allah ni msamehevu.
Huu ni mwanzo mpya,awamu mpya,siyo kwetu sisi,lakini awamu mpya imeanza Marekani baada ya Obama kuchaguliwa. Kwa hiyo,awamu mpya zozote,zinapaswa kuanza na watu kusameheana.
Let us begin a New Dispensation. Dispensation[katika Kanisa Katoliki] ni uwezo wa kiongozi mpya kuyasamehe makosa yaliyotokea wakati wa kiongozi aliyepita. Tutambue kwamba sasa kuna madiliko ya uongozi. Viongozi wa zamani hawapo. Viongozi wapya wapewe nafasi ya kutekeleza sera zao,sera mpya.
Mtume Muhammad alisema katika hotuba yake ya mwisho,kwamba wasamehewe wale wote waiotenda makosa kabla ya Uislamu kuanza.
Kwenye Biblia imeandikwa kwamba mtu akiua kwa bahati mbaya[manslaughter],apelekwe,au akimbilie kwenye City of Refuge,na akae huko mpaka High Priest atakapokufa,halafu anaweza kurudi. Kwa hiyo Wayahudi wahalifu walikuwa wanakimbila kwenye miji hiyo,kama vile Hebron.
Siku za karibuni BBC kipindi cha World Have Your Say walifika Mwanza. Walikuwa kule St Marys School. Wakakuta vijana kule wanaunga mkono rushwa,wanaunga mkono kila uovu,inaelekea. Yule BBC reporter alishtuka sana,na mwalimu wao wale wanafunzi akaongea apologetic remarks. Lakini ukweli ni kwamba hawa ni vijana wa siku hizi ambao inaonekana wapo tayari kusamehe maovu ambayo wazazi wao walikuwa hawako tayari kuyasamehe,ili tuweze kujenga Dunia Mpya.
Tuwasamehe hawa mafisadi sasa hivi,au tuwasikilize,lakini hatimaye tuwasamehe.
Tuwe na roho hii ya kusameheana,tuwasamehe watu waliolikosea Taifa,yaani waliotukosea sisi wote;au mtu yeyote ambaye ametukosea sisi wenyewe,labda kwa mfano mtu amemuua ndugu yako.
Pia tujisamehe sisi wenyewe,makosa ambayo tumefanya. Kwa sababu inatokea,mtu hajafanya kosa lolote,lakini hata hivyo anaona kwamba ni lazima ajilaumu sana kwa mambo mengine ambayo aliruhusu yatokee,au aliyafanya,basi,anaona taabu sana kujisamehe.
barua ya jumatatu,tusameheane.
Huu ni mwanzo mpya,awamu mpya,siyo kwetu sisi,lakini awamu mpya imeanza Marekani baada ya Obama kuchaguliwa. Kwa hiyo,awamu mpya zozote,zinapaswa kuanza na watu kusameheana.
Let us begin a New Dispensation. Dispensation[katika Kanisa Katoliki] ni uwezo wa kiongozi mpya kuyasamehe makosa yaliyotokea wakati wa kiongozi aliyepita. Tutambue kwamba sasa kuna madiliko ya uongozi. Viongozi wa zamani hawapo. Viongozi wapya wapewe nafasi ya kutekeleza sera zao,sera mpya.
Mtume Muhammad alisema katika hotuba yake ya mwisho,kwamba wasamehewe wale wote waiotenda makosa kabla ya Uislamu kuanza.
Kwenye Biblia imeandikwa kwamba mtu akiua kwa bahati mbaya[manslaughter],apelekwe,au akimbilie kwenye City of Refuge,na akae huko mpaka High Priest atakapokufa,halafu anaweza kurudi. Kwa hiyo Wayahudi wahalifu walikuwa wanakimbila kwenye miji hiyo,kama vile Hebron.
Siku za karibuni BBC kipindi cha World Have Your Say walifika Mwanza. Walikuwa kule St Marys School. Wakakuta vijana kule wanaunga mkono rushwa,wanaunga mkono kila uovu,inaelekea. Yule BBC reporter alishtuka sana,na mwalimu wao wale wanafunzi akaongea apologetic remarks. Lakini ukweli ni kwamba hawa ni vijana wa siku hizi ambao inaonekana wapo tayari kusamehe maovu ambayo wazazi wao walikuwa hawako tayari kuyasamehe,ili tuweze kujenga Dunia Mpya.
Tuwasamehe hawa mafisadi sasa hivi,au tuwasikilize,lakini hatimaye tuwasamehe.
Tuwe na roho hii ya kusameheana,tuwasamehe watu waliolikosea Taifa,yaani waliotukosea sisi wote;au mtu yeyote ambaye ametukosea sisi wenyewe,labda kwa mfano mtu amemuua ndugu yako.
Pia tujisamehe sisi wenyewe,makosa ambayo tumefanya. Kwa sababu inatokea,mtu hajafanya kosa lolote,lakini hata hivyo anaona kwamba ni lazima ajilaumu sana kwa mambo mengine ambayo aliruhusu yatokee,au aliyafanya,basi,anaona taabu sana kujisamehe.
barua ya jumatatu,tusameheane.