Dr Lizzy
Platinum Member
- May 25, 2009
- 30,770
- 59,118
Umewahi kuwa na mtoto mdogo <---5 sehemu ya public, akawa analia alafu watu kibao wanaopita au waliopo karibu wakaanza kukwambia anachohitaji huyo mtoto (kulala, kula, kubebwa, kucheza) bila kujua kwamba pengine ndio kaamka, kamaliza kula, alianza kulia akiwa mgongoni. .mabegani au mapajani, alikua anacheza n.k?
Je watu wanaofanya hivyo ("jamani mbebe. . Mpakate alale huyo atakua na usingizi tu. . .huyo ni njaa huyoo ndo inayomsumbua" nk ) ndo wanakua wanajali sana watoto? Wanaona watoto wanaonewa? Wanajisikia kumwambia mtu fanya hivi au vile au inakuwaje?
Nimeona sana hii kitu lately sema sijaweza tu kuwauliza wahusika. Yani unaweza ona mtu anainuka kabisa alipokua amekaa akamfuata mtu mwingine aliyeko na mtoto akaanza kumwambia huyo mtoto anachohitaji.
Au yaweza kuwa hata gia ya kutongozea? Maana kuna dada last week alitoka alipokaa (kwenye kijiwe fulani hivi) akamfuata kaka aliyekua amemaliza kula sehemu hiyo na tayari yuko nje anaondoka kumwambia au sijui niseme "KUMUOMBA"(maana alikua anabembeleza) ambebe mtoto aliyekua nae wakati hata hakua analia au anasumbua abebwe.
Je watu wanaofanya hivyo ("jamani mbebe. . Mpakate alale huyo atakua na usingizi tu. . .huyo ni njaa huyoo ndo inayomsumbua" nk ) ndo wanakua wanajali sana watoto? Wanaona watoto wanaonewa? Wanajisikia kumwambia mtu fanya hivi au vile au inakuwaje?
Nimeona sana hii kitu lately sema sijaweza tu kuwauliza wahusika. Yani unaweza ona mtu anainuka kabisa alipokua amekaa akamfuata mtu mwingine aliyeko na mtoto akaanza kumwambia huyo mtoto anachohitaji.
Au yaweza kuwa hata gia ya kutongozea? Maana kuna dada last week alitoka alipokaa (kwenye kijiwe fulani hivi) akamfuata kaka aliyekua amemaliza kula sehemu hiyo na tayari yuko nje anaondoka kumwambia au sijui niseme "KUMUOMBA"(maana alikua anabembeleza) ambebe mtoto aliyekua nae wakati hata hakua analia au anasumbua abebwe.