Watu wapora hela na kuzitupa jijini Mwanza

Jodoki Kalimilo

JF-Expert Member
Feb 12, 2012
12,013
10,170
Leo majira ya mchana kuna jamaa wamepora begi la hela na kuanza kukimbia nalo katikati ya jiji la Mwanza huku wakikimbia kwenda kugawana wakati wananchi wengine wakifukuzia mchongo jamaa wakatumia mbinu ya kuchua mabunda kadhaa na kuyarusha hivyo wananchi wengine wakabaki wanagombea hela jamaa wakasepa. Nimeiweka kwenye tetesi kwa kuwa sijathibitisha kwa undani japokuwa nilikuta tukio limefanyika dakika kadhaa zilizopita huku wananchi wakijadili hili tukio, labda wenye habari kamili watujuze maana sijaiona hii habari hasa kwa Star tv
 
Mwanza kubwa mtaa gani duka gani wamekimbilia maeneo gani.
 
DUUUUUUUUUUUUU, e bibieee!

Mjanga unadhani!
Yani mtu kakuletea habari nawe ni hiari yako,uisome na kuichangia au uisome na kuipotezea.
Lakini utakuta jitu kwa makusudi linatoka huko na kumkatisha tamaa mleta mada kwa kubandika utumbo wake.
Inakera sana hii mijamaa.
 
Last edited by a moderator:
Mwanza kubwa mtaa gani duka gani wamekimbilia maeneo gani.

Maeneo ya Liberty (maeneo ya duka la Semira kuvuka kadaraja ka kuelekea ofisi za Akamba) mitaa hiyo ndio nilikuta watu wamejaa wanazungumzia hilo tatizo ila kwa kuwa sikuwa na detailed information nika-post kama tetesi ili wenye full mkanda watiririke kwani ni kweli watu walikuwa kwende makundi wakijadili kwa mshangao (ila inasemekana ziliibiwa duka moja wakala wa Airtel Money hapo hapo mtaa wa Liberty)
 
hii ingefaa iitwe umbea! lisema ulikuta tayar, basi huu ni umbea

Sikufanya conclusion ndio maana nikasema kama mtu ana information za ziada atujuze maana kukuta watu wamekaa kwenye vikundi vikundi sio justification ya tukio limetokea kweli ndio maana nikaweka tetesi. Iliwahi tokea Dar miaka mingi iliyopita story za MTU JOKA na kila ukipita unakuta watu wanasema amepita mtaa ule wakati hakuwepo. Ningekuwa na full data nisingeweka tetesi kwa kuwa vyanzo vya habari vilivyokuwepo vilikuwa katika simulizi ya tukio lililopita ambalo sikulishuhudia
 
Ndiyo jukwa! muda mwingine tunalazimisha uvumilivu!

Mjanga unadhani!
Yani mtu kakuletea habari nawe ni hiari yako,uisome na kuichangia au uisome na kuipotezea.
Lakini utakuta jitu kwa makusudi linatoka huko na kumkatisha tamaa mleta mada kwa kubandika utumbo wake.
Inakera sana hii mijamaa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom