Watu Muhimu katika Historia ya Nchi yetu

alisema nini shiekh takadir?

Hujui aliyowatahadharisha wana TANU kuhusu alivyoanza kumuona Nyerere akiwaondoa Waislam mmoja baada ya mwingine kwa majungu. Shehe Takadir akalizungumza hilo bayana, Nyerere akalia katika mkutano na kusema Takadiri ni MTAKA DINI.

Tangu siku hiyo akatengwa kabisa, manake ilionekana ukiwa karibu na Shehe Takadiri ni msaliti. Na kuna siku kundi lilitoka na kuelekea kwa Takadir lililopangwa na Nyerere likaenda mpaka nyumbani kwa huyu Marhum, likaanza kumzomea, kumkejeli, kumtusi kwa kila lugha mbaya. Akatoka ndani kwake na kuwaambia waliokuwepo (wengi Waislam), MTANIKUMBUKA.

Kweli aliyosema yalitokea, UDINI ulioonyeshwa na Nyerere ndio huo aliusema Takadir, hivyo kweli alisema Marhum Shehe Takadir.
 
Nina hakika Mkandara kauliza maswali kwa nia njema sana. Lakini naona mada imeshatekwa na wadini akina Mtimti, Mfumwa na GT. Takadir was on the wrong side of history. Soma kitabu cha Mohammed Said cha uamuzi wa busara. Na hao wengine wametajwa katika kitabu cha Judith Listowell, The Making of Tanganyika. Hakuna mahali ambapo Nyerere ameandika historia na kuwafuta wenzake walioshiriki katika harakati za ukombozi.
 
Hakuna cha Nyerere wala Kawawa. Mtu muhimu kwa Tanganyika ni Karl Peter tu. Mtake msitake.
 
watu muhimu walikuwa waswahili waliomvalisha Nyerere kaptula na siku uhuru waliachwa chini huku kule juu aliwachukua akina Kambona na wagala wenzie the rest is history

sasa mnaona woga gani kulisema hilo?

Yep..i knew hii thread ndipo ilipokuwa inalenga huku!

Wazee wa mashuzi a.k.a gret sinkaz woyee!
 
Tanzania tunaogopa "udini" mpaka inatisha.....
hivi kama dini kweli ndio zilizosaidia kuleta uhuru ....tubadilishe historia, tuache kuzitaja kwa kuwa tu tunaogopa udini? historia haiwezi kubadilika kwa kile tu hatutaki kukijua.

kwa nafsi yangu hii kwangu ni shule .....kwa kuwa historia siijui, ila kama dini ya kiislam ndio ilosaidia kuleta uhuru ( kama shule za makanisa zilivyosaidia elimu kwa miaka ya zamani), ningependa kujifunza.
 
Mchungaji Paulo Mashambo, Rashidi Kadio, Masudi Kivandiko,Yohana Mcharo, Rafaeli Kanyampwe, Mbwana Mronga, Selemani Mavura,Elieza Mkonda, Mbura Mkhande, Mbonea Singo, Luka Kasha, Mchungaji Tuvako, na maelfu ya wananchi walioshiriki mgomo wa Mbiru.

wakinamama wa Usangi wanaokadiriwa kufikia 500 waliomtia msukosuku DC Muingereza 'bwana Pringo', Chifu Kibacha Singo wa Same, na Chifu Sabuni wa Usangi, wakidai maelezo kuhusu mgomo wa waume zao uliokuwa ukiendelea Same kwa takriban miezi miwili. ilibidi askari wa Muingereza watumie virungu na vitako vya bunduki kuwatawanya kinamama wasiokuwa na silaha ambao walizingira makazi ya Chifu Sabuni.

mgomo wa Mbiru ulianza 6/1/1945 na maandamo ya kinamama yalifanyika 22/2/1945. wakinababa toka kila pembe ya wilaya za sasa za Same na Mwanga waliandamana kwenda Same mjini wakidai kufutwa kwa kodi ya Mbiru. kinababa hao walipiga umbali mfupi toka ofisi ya DC. kila siku ya kazi kwa kipindi cha miezi miwili wananchi hao walikuwa wakiandamana kwa amani (NON VIOLENCE) kwenda ofisini kwa DC kutaka majibu ya petition yao ya kufutwa kwa kodi ya mbiru.

mgomo wa pili wa mbiru ulifanyika Julai 1946 na safari hiyo serikali ilisalimu amri kwa madai ya wananchi na kufuta kodi ya Mbiru. wananchi wa Upare tunakumbuka sana matukio haya ya kishujaa na kihistoria. pia tunakumbuka kuanzishwa kwa chama cha Pare Union 4/1/1946.
 
GT,

Mbona unapenda kupotosha ukweli, kama kusema kambona alipata post siku ya uhuru, wakati yeye alikuwa katibu wa tanu kabla ya uhuru.

Pili historia gani ya nchi hii inayoandikwa kwenye msikiti wa manyema huoni hiyo histori inaweza kuwa biased.

Tatu mbona Rashid Mfaume Kawawa aliachiwa uwaziri mkuu? Je, sio kutambua mchango wake au waislamu katika mchango wao wa kuleta uhuru wa nchi hii? Je, kupewa jina uwanja wa Sheikh Amri Abeid huko Arusha sio kutambua huo mchango wake?

Je, Sykes kuwa balozi mpaka alipostaafu sio kutambua mchango wake? Huyo Kitwana Kondo from 'taxi driver' mpaka kupata kile alicho nacho sio kutambua mchango wake, au ulitaka mpaka apewe uraisi wa nchi ndio utambue hilo? Au ulitaka baraza lote la mawaziri liwe la hapo msikiti wa Manyema ndio uone kwamba huo mchango wao umetambulika?

Na huyo Nyerere alijichagua mwenyewe? Si walimchagua wao wenyewe kwa kuuona busara au akili zake au kipaji au uwezo wake wa kuongoza?

Vugu vugu la ukombozi Tanzania lililetwa na watu wengi kwa njia tofauti, na si kwa dhana unayotaka kuileta, kuna Abdul Mtemvu alikuwa na TLP, na kuna wengine wengi, kutegemeana na huyo mtu yupo wapi, kama ni Kilimanjaro, Mwanza, Tabora, Dar es Salaam, Arusha, Kigoma, na kwa mtu mwenye akili ratio ya watu fulani inategemea upo wapi e.g Dsm - kwa wakati huo wakazi wake wengi walikuwa wanaishi hapo Livingstone, Shule ya Uhuru mpaka hiyo Magomeni Mikumi, na kwa sababu vugu vugu kubwa ilikuwa makao makuu ya serikali i.e Dsm, basi yanaweza kuonyesha, hiyo picha unayotaka wewe.

Lakini ukiwa unataka ukweli uchambuzi wako au mchango wako usijikite hapo Manyema, maana vyama vilivyokuwa na nguvu wakati huo vilikuwa vingi na ni watu wengi ndio waliotoa mchango wa nchii hii kupata uhuru. Ilikuwepo Nyanza Co-op Union na akina Bomani, KNCU na akina Marealle, na kuna watu wengine ambao hawakuwa upande wa Nyerere, ambao bahati mbaya historia haijawaandika au walielezwa tofauti kama ilivyokuwa kwa Abel Muzorewa Zimbabwe au kwa kuwa muda umepita saana vitu vingine hatuvikumbuki.

Au ulitaka nchi igawanyike kwenye kila kanda ili ujuwe michango ya watu wengine?

Kuna watu kama Chifu Lukumbuzia (kama jina nima andika vizuri), kuna Jaji Ruhumbika etc je hao wote walikuwa hawajui kuvaa Suruali mpaka wakaja kufundishwa kuvaa hizo suruali hapo Manyema? Au ndio akutukanae hakuchagulii tusi?
 
na katiika hao waliomvalisha kaptula walikuwa ni akina Sheikh Hassan bin Amir, Sheikh Said Omari Abdallah, Tewa Said Tewa, Katibu wa EAMWS enzi hizio Abdul-Aziz Khaki na mzee wa TANU Mzee Mwinjuma Mwinyikambi; Makisi Mbwana, Issa Mtambo, Omari Muhaji na Saleh Masasi

unless bwana Mkandara aataka listi nyingine tofauti

Sasa mtoto wa mjini hapo nani? Nani aliyewaingiza mjini wenzie? Mie naona Nyerere ni kiboko, mmemvalisha kaptula akawaacha kwenye mataa! Ahhhh! Akatawala miaka 24 mlikuwa hamtaji hizo kaptula. Kafa mnaanza umbeya.

Mbona huwa hamsemi vile vile mlikuwa mnauza watumwa!!

Lakini kule kwetu Shujaa wa Tanzania tunayemkumbuka ni Mkwawa!! Hata ukipita barabarani pale Lugalo Iringa unaona lile "mass grave" la nyundo!
 
Wataanzia wapi wanabaki Hi! he! nafikiri kwanza wanalinganisha mtindi ulioutowa hapo juu na ule waliopewa na baba wa taifa kama unalingana, na bado waambiew vizuri kuwa hiyo TANU anayojivunia Nyerere kuiasisi ilikuwapo tokea yeye ananyonya,
hivi watu wengine mnavyo andika kitu mnakuwa mmekunywa au kuvuta au ndio hivyo tena kuandika ili uonekane umeandika. kama unajua historia tanu ilianzishwa na kuasisiwa nyerere akiwa tayari katika harakati za kuleta uhuru, sasa hiyo ya kusema ilikuwepo tokea akiwa ana nyonya si ni kujidanganya wewe mwenyewe? au ndio huko kutokujua historia go back to you history books uone tanu ilianzishwa lini. au ndio hivyo shule less halafu unataka kupewa uongozi, na ukishindwa unasema una hujumiwa.
 
Sasa mtoto wa mjini hapo nani? Nani aliyewaingiza mjini wenzie? Mie naona Nyerere ni kiboko, mmemvalisha kaptula akawaacha kwenye mataa! Ahhhh! Akatawala miaka 24 mlikuwa hamtaji hizo kaptula. Kafa mnaanza umbeya.

Mbona huwa hamsemi vile vile mlikuwa mnauza watumwa!!

Lakini kule kwetu Shujaa wa Tanzania tunayemkumbuka ni Mkwawa!! Hata ukipita barabarani pale Lugalo Iringa unaona lile "mass grave" la nyundo!

Kwani Hujui Mkwawa alikuwa Mswahili?
 
Kwani Hujui Mkwawa alikuwa Mswahili?
Kwani hapa tunaangalia Shujaa Mswahili au Shujaa Mtanzania?? Kule huwa hatujali Mswahili, mpagani au nani, kavaa lubega, kaptula au suruali wote twende tu!

Kwa Taarifa fupi tu Mkwawa hakuwa Mswahili; ila Mwana wake aitwaye Sapi ndiyo alianza Uswahili!
 
hivi watu wengine mnavyo andika kitu mnakuwa mmekunywa au kuvuta au ndio hivyo tena kuandika ili uonekane umeandika. kama unajua historia tanu ilianzishwa na kuasisiwa nyerere akiwa tayari katika harakati za kuleta uhuru, sasa hiyo ya kusema ilikuwepo tokea akiwa ana nyonya si ni kujidanganya wewe mwenyewe? au ndio huko kutokujua historia go back to you history books uone tanu ilianzishwa lini. au ndio hivyo shule less halafu unataka kupewa uongozi, na ukishindwa unasema una hujumiwa.
Halafu inaelekea kweli hatufikiri. Nyie huyu Nyerere kasoma lini? Halafu Nyie mmemvika hiyo suruali au sijui, nani wa kuvikwa suruali? Nyerere kasoma kabla hata hamjaanza kudai Uhuru; au kwa sababu kafa ndiyo mnaanza uongo? Wakati ule Elimu yake tu ilibidi kuwa yeye awe kafunguka zaidi ya hao mnaowasema. Hivi hao wazee wote na ile population ya Dar wkati ule ilmshindwa mtu mmjoa aitwaye Nyerere? La, huyu jamaa alikuwa intelligent kuwazidi wengi wakati huo, na mie naamini kwa wakati ule Wengi walimwona wa maana.

Unajua tena always kuna wale BIG FISH wanaotaka kuwa BIG FISH kwenye "SMALL POND" ndiyo wanajitokeza sasa kuongea hayo! At that time Nyerere was a BIG FISH IN A BIG POND na akaendelea hadi kafariki.

Historia hapo ishakwisha, mngesimama wakati anaishi mie ningewaona ni BIG FISH! tena Mapapa au Nyangumi!!
 
Honestly blame it to Baba wa taifa ambaye alijali umaarufu wake tu wengine a a a!!![/QUOTE] [/B]

Mwacheni Mtumishi wa Mungu apumzike kwa amani. Tukishamlaum baba wa Taifa so what! Lets stop the blame game jamani! Mwalimu alikiri mara kadhaa kwamba kamwe hakuwa malaika kuna aliyoharibu na aliyojitahidi. Wajibu wetu ni kuendeleza mazuri na kuyaacha ya kijinga. kwa kuwa unajua udhaifu wa mchonga, anzia hapo kurekebisha.
 
Wakuu zangu,
Kusema kweli nimeileta mada hii kwa mtazamo wazi kabisa na sio ule unaoitwa NDIVYO TULIVYO kwani mara nyingi tunajaribu kuvuta hoja za kidini ktk WATU washuhuri ambao waliweza kubadilisha historia ya nchi yetu..Tuklumbuke tu utukufu wa mtu ni kwa yale alofanya na sio kwa majina au dini zao..Hivi kweli Mkandara hapa ningekuwa sina dini ningekuwa na mtazamo tofauti wa viongozi wetu?..Ningemsifia Lowassa na Mkapa kwa sababu wao ni Wakristu na kutupilia mbali madai yote ya Ufisadi! I don't think so.....

Sisi sote hapa ni matunda ya nguvu za hawa wazee, iwe, isiwe kwani navyoelewa mimi hiyo Magomeni Mikumi ndiko chanzo cha nguvu zote za uhuru na walikaa watu wa kila dini na makabila.
Ndiko alikokuwa akikaa Kawawa, Kambona, Saadan Kandoro, Nyerere na wengine wengi tu ambao kwa njiaq moja ama nyingine walichangia sana ktk Uhuru wetu... Jamani hatujafika hata miaka hamsini, watu hawaoni umuhimu wa watu wale isipokuwa wale waliopanda mlima Kilimanjaro na kutembea kwa miguu kuunga Azimio la Arusha..mbona hao hamwatambui kwa dini zao?..

Tuwe makini sana ktk maswala haya wakuu zangu tafadhalini kwani JK leo anayafanya anayoyafanya sii kwa sababu ni Muislaam wala Lowassa kwa sababu ni Mkristu. hawa watu hata kama wasngekuwa karibu na Mungu kiasi gani bado wangeyafanya waloyafanya kwa sababu ndio upeo wa AKLI zao ktk Ufahamu walizopewa...

Kuna majina mengine ambayo yamepewa ward za Wagonjwa Muhimbili kina ambao pia walikuwa muhimu sana isipokuwa leo hii tunabakia na majina bila kuelewa vizuri mchango wao..
Waswahili wanasema usipojua ulikotoka ni vigumu sana kwenda mbele... na hakika sababu zote za kushindwa kwetu kuendelea zinachangiwa na kutofahamu tulikotoka, hivyo tunapuyanga tu bila Malengo.. Kila mtu akianza safari huwa na fikra ya wapi anakwenda na mara zote hufuata njia ambayo itamfikisha ktk safari yake...Sasa sisi kama tunaenda mbila dira hatujui tumetoka wapi tumerukia bandwagon katikati ya safari maadam linasafiri inawezekana kabisa kuwa tunarudishwa nyuma..Na ndio maana Wadanganyika wengi hawakubaliani na data za maendeleo yetu hata kidogo...kwani hatujui tulikotoka.
Hawa watu tunaowazungumza humu ni muhimu sana na hakika ningependa sana kuelewa maisha na michango yao ktk nchi yetu..
Mkandara,
umeleta hoja watu wanakupa majibu na list uliyotaka, sasa umeamnza kuingiwa na woga kisa umeona kuna kaudini kameanza kuingia kwenye hoja hii.
kwa taarifa yako, huwezi kuongelea historia ya Tanganyika au Uhuru wetu bila kuhusa dini kwani wkati ule kitu ambacho hata nyerere alikiri kwenye hotuba zake, watu waliokuwa wameendelea na waliomsaidia sana katika kudai Uhuru ni waislamu, ndio walimzamini na kumtuma, unakumbuka mwalimu alisema kuna siku ilibidi nae afunge kama ibada ya maombi na waislamu...lakini baada ya uhuru sijui imekuwaje, inavyosemekana mwalimu aliwatosa wale wote waliomsaidia na kufukuza wengine nchni na kuwauwa wengine...
labda hii hoja tuijadili kwa mtazamo mwingine, kutafuta historia za wazalendo na mashujaa wetu, historia yetu imejaa propaganda sana, vitu vingi vimepindishwa, ni sawa na kuambiwa Iddi Amini alikuw anakula nyama za watu, wakati baadhi wa waganda waliwahi kusema Iddi Amini was the best leader...suala lilikuwa udini ambao Amini alionekana kuupa nafasi uislamu.....
kuna haja ya kuweka historia upya.......
 
this thread is 90% crap,just because so and so were alwatans in those days recognition is a neccesity-just because our written history is suspect we are making heroes of nobodies.some of us are trying to learn a bit of history here,but some of the names being mercilessly thrown at our faces,smell of history being falsely rewritten
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom