MWEEN
JF-Expert Member
- Feb 6, 2010
- 482
- 207
Wapendwa nana JF;
Nakumbuka mwaka jana au juzi Morogoro mjini kulitokea varangati kubwa sana baina ya wazazi na walimu wa shule za msingi baada ya watoto kupewa dawa za kichocho na wengine kuzimia.
Nimepata habari kutoka kwa mzazi mmoja kuwa wamepata vikaratasi vinavyowaagiza kuwa wawalishe watoto wao vizuri kesho Ijumaa kwana watapewa dawa za kichocho.
Maana yake ni kuwa hao wanaofanya hilo zoezi hawajaelewa somo au ni kiburi. Ninahisi, japo sina uhakika kuwa labda kuna mtu anayefanya utafiti wake na anawafanya watoto wetu "guinea pigs" na kama sivyo, basi kuna ulegevu mkubwa kwenye sekta yetu ya afya.
naomba maoni kutoka kwa wataalamu wa afya.
Nakumbuka mwaka jana au juzi Morogoro mjini kulitokea varangati kubwa sana baina ya wazazi na walimu wa shule za msingi baada ya watoto kupewa dawa za kichocho na wengine kuzimia.
Nimepata habari kutoka kwa mzazi mmoja kuwa wamepata vikaratasi vinavyowaagiza kuwa wawalishe watoto wao vizuri kesho Ijumaa kwana watapewa dawa za kichocho.
Maana yake ni kuwa hao wanaofanya hilo zoezi hawajaelewa somo au ni kiburi. Ninahisi, japo sina uhakika kuwa labda kuna mtu anayefanya utafiti wake na anawafanya watoto wetu "guinea pigs" na kama sivyo, basi kuna ulegevu mkubwa kwenye sekta yetu ya afya.
naomba maoni kutoka kwa wataalamu wa afya.