Mwanamutapa
JF-Expert Member
- Dec 5, 2011
- 513
- 489
Hayo ni majungu yanakusumbua mbona Bush baba na Bush mtoto wote waliitawala USA? Sasa kuna ubaya gani kwa watoto wa wana siasa kugombea uongozi
Bush mtoto au John Queens Adams ambaye ni mtoto wa Rais John Adams walitawala baada ya wazazi wao kuwa walishatoka madarakani na vyama vya mababa zao havikuwa madarakani bali vilikuwa vyama vya upinzani wakati wao wanaingia kwenye siasa. Alitakiwa Ridhiwan agombee NEC wakati baba yake alishatoka madarakani sio anagombea wakati baba yake ni Rais hiyo ni nepotism. Acheni kuwa mnatumia mfano wa Marekani kuhalalisha upumbavu wenu Bushi kaanza siasa mwaka 1992 kwa kuwa gavana wa Texas wakati baba yake alishashindwa uchaguzi na Bill Clinton kwa maana nyingine Republican walikuwa wapinzani vivyo hivyo kwa John Adams na mwane John Queens Adams ambaye aliingia kwenye siasa baba yake alishakufa zamani na chama chake kilikuwa upinzani
Ujinga huo wa CCM watu wanaona na wajiandae kutoka madarakani kwa kura au kwa nguvu kama Misri, Tunisia, Libya na sasa Syria Ridhwan hana tofauti na Saif Islam mwana wa Ghadhaffi au Kamal mwana wa Mubaraka ambao walikuwa na nguvu sana na walitakiwa kuwarithi baba zao lakini kwa sasa hata udiwani hawawezi kushinda. Nilifika Cairo wakati fulani billboards zilijaa picha za Kamal wakati kwa sasa yuko gerezani na anatia huruma mbali na billboards hata magazeti hayako interested kuchapa picha zake tena. Nawe Ridhwan siku zako zinakuja ndio maana unapigana sana Membe ashinde urais ili uwe na usalama kwa taarifa chadema wanaenda ikulu utatuambia hizo mali umezipata wapi kwa ghafla hivyo?