Watoto wa vigogo na upendeleo wa ajira nyeti serikalini

"Set your course by the stars, not by the lights of every passing ship" - Omar Bradley
 
Some inspiration for the desparate and despairing seafarer with low expectations from a battle proven five star general of "The Class The Stars Fell On".WYKAT.

Two wrongs do not make a right.To do wrong because another does so is worse than to do wrong.The focus is on excellence at BOT, justifying nepotism because of some other nepotism in my opinion exhibits cowardice nature, low self esteem changing the subject and shifting goals and focus.
 
The best y'all can do is whine behind the backdrop of the internet. Waafrika Ndivyo Tulivyo.
Jamani tuwe makini, this is INFORMATION AGE. Kama ilivyokuwa wakati wa INDUSTRIAL AGE, kwa sasa information is power. Kama kuna malalamiko tujifunze kusikiliza na kufanya linalowezekana kuondoa shaka iliyoanza kujengeka miongoni mwa wanajamii.

Haya malalamiko yameanza muda mrefu hivyo ingekuwa bora kama wahusika wangetoa majibu kuwaridhisha wenye kunung'unika (au wapika majungu kama ambavyo wengine tunawaona). Tukiendelea kupuuza na kutoa majibu yasiyomridhisha huyu mwenye 'doubt' basi ujue tunaanza kupandikiza mbegu chafu taratibu. Kenya ndivyo walivyoanza!!
======================
 
Sasa hoja hii ina zaidi ya mwezi, mwanzishaji kimyaa. Anasubiri ijifie? Anasubiri iingie kwenye archive kisha aseme "Imefutwa kabisa"? Ni bora uendelee, none is moving this thread to anywhere. Be fair, kuandika kuwa utaamishwa kuwa-protect watoto wa wakubwa ni kutukosea tu moderators. Ni vema uendeleze mjadala. Mchangiaji akitukana basi ndipo hoja yake hufutwa, ama mwanzishaji akibadili mtizamo na kushauri hoja ifungwe itafungwa. Ama vinginevyo hoja ikijaa udaku bila data zaidi na kuwa mada ya salaam n.k basi hakika itahamishiwa kuleee...

Lete data, hakuna asiyeongeleka. Ila tuwe fair katika hoja. Kila mtanzania ana haki ya kuheshimiwa utu wake. Haijalishi kazaliwa na Mkapa, Nyerere, Malecela, Mbowe n.k. Ili mradi tusiwatukane na kuwachafulia majina kwa makusudi. Ukitoa hoja tarajia kupingwa ama kuungwa mkono, ni two way traffic.

Karibu GT :)


INVISIBLE
Hoja hivi hapa zimeletwa pamoja na picha kazi nu merge tuu hizi threads:
http://www.jamboforums.com/showthread.php?t=8593
 
Hivi ktk nchi zilizoendelea hakuna upendeleo kweli?
Kwa uzoefu wangu mimi nimeuona upendeleo kila nchi niliyoishi na kila sehemu niliyofanyia kazi.....

So? kwani hii ndio inahalalisha upendeleo (uhalifu)? Kwani siku hizi makosa mawili yanatengeneza kweli?
 
So? kwani hii ndio inahalalisha upendeleo (uhalifu)? Kwani siku hizi makosa mawili yanatengeneza kweli?

No! Haihalalishi upendeleo hata kidogo. Mimi binafsi naupinga upendeleo wa aina yoyote ile na kwa nguvu zangu zote alizonijalia Mnyazi Mungu. Pointi niliyokuwa natengeneza ni kwamba upendeleo ni moja ya hulka/ silka za binadamu, upo tokea enzi na enzi na utaendelea kuwepo no matter what. Pundit aka Mjuzi wa mambo alisema kwamba upendeleo ktk nchi zetu hizi za Kiafrika ndio unasababisha sisi Waafrika tuwe na hali tuliyonayo sasa. Ndio na mimi nikasema mbona hata kwenye nchi zilizoendelea upo lakini na bado wameendelea? Kuwepo kwa upendeleo kila sehemu ya dunia ni kithibitisho tosha kuwa hiyo ni asili yetu (sisi binadamu). Nimeeleweka?
 
No! Haihalalishi upendeleo hata kidogo. Mimi binafsi naupinga upendeleo wa aina yoyote ile na kwa nguvu zangu zote alizonijalia Mnyazi Mungu. Pointi niliyokuwa natengeneza ni kwamba upendeleo ni moja ya hulka/ silka za binadamu, upo tokea enzi na enzi na utaendelea kuwepo no matter what. Pundit aka Mjuzi wa mambo alisema kwamba upendeleo ktk nchi zetu hizi za Kiafrika ndio unasababisha sisi Waafrika tuwe na hali tuliyonayo sasa. Ndio na mimi nikasema mbona hata kwenye nchi zilizoendelea upo lakini na bado wameendelea? Kuwepo kwa upendeleo kila sehemu ya dunia ni kithibitisho tosha kuwa hiyo ni asili yetu (sisi binadamu). Nimeeleweka?


Bado hujaeleweka kabisa, tupe mifano
 
Kwa mfano wapi (be specific) kuna upendeleo wa aina hii??

Kule Marekani kuna yule dada anayeongoza idara ya uhamiaji...somebody Myers...ni niece (sijui kiswahili chake) wa aliyekuwa Chairman of the joint chiefs of staff. Inavyosemeka hana sifa zinazohitajika kuongoza hiyo idara lakini aliteuliwa na raisi Bush kushika hiyo na nafasi ingawa kwa muda tu akisubiri confirmation ya congress. Bush na Myers inavyosemekana ni washikaji. Mifano iko mingi mno.
 
Standards, even if plagued by the Selassian dilemma to be "pursued but never attained" must be set and adhered to.

Nepotism is bad for good governance and eventually for the economy, even if just from the image it potrays.Regardless of whether there is nepotism in developed countries, we can hardly say we can afford "kuiga tembo kunya".Hata kama kuna nepotism kwao (which is debatable, one person is not the same as the army given here), we need to run while others are walking, walishatuacha nyuma zamani sana!

For example, the negative effects of USA being blacklisted by "Transparency International" are not the same as the same effects on Tanzania.So even if you take moral issues aside and remain "pragmatic", if you are reasonable you can see that we cannot afford nepotism, it is a luxury that the rich may afford if they want to toss away their principles.

Another issue ni kwamba huyu Myers yuko na nani mwingine hapo immigration? Hii level yetu ambayo unakuta watu lukuki wa "familia nzito" kwenye ofisi moja ni sawa na huyo Myers mmoja?

Halafu tulivyo-despair tunaenda kuchukua mfano wa the cronyism ya the Bush administration na kuufanya kuwa role model!
 
Sidhani kama tatizo ni ndugu au jamaa kushika nafasi za juu katika sehemu mbalimbali. Rais Bush alikuwa Rais wa Marekani wakati mdogo wake Jeb Bush alikuwa Gavana wa Florida. Itakuwa ni kichekesho kusema kuwa hapo kuna "undugu" katika nafasi hizo.

Hivyo hoja kuwa watu wa familia moja au ndugu wa damu kushika nafasi mbalimbali za juu siyo tatizo kimsingi; ndiyo maana tumekuwa na Karume (Zanzibar) na mdogo wake Balozi wetu Ujerumani n.k

Kinachosumbua watu wengi ni jinsi gani walipata nafasi hizo na kwanini walizipata wao na si wengine.

Endapo mtoto wa Kigogo X amefuata njia zote za kawaida za kupata ajira, na akapandishwa vyeo kama wengine bila upendeleo maalum na matokeo yake akafikia mahali akashika nafasi ya juu kama ndugu yake wa kitengo kingine, hakuna Mtanzania atakayekuwa na tatizo na hilo.

Ndiyo maana tulipokuwa na Aden Mwamunyange kule Polisi na sasa hivi kaka yake ni Mkuu wa Jeshi ni rahisi mtu kukimbilia kusema kuwa kuna undugu hapo. Lakini hawa wawili walifuata nyazo za baba yao kwa namna tofauti na pole pole wakapanda ngazi taratibu hadi wakati huu.

Tatizo la Benki Kuu ni kuwa ni wazazi gani waliofanya kazi kwenye taasisi za fedha hadi watoto waanze kulundikana huko? Daktari ana uwezekano wa baadhi ya watoto wake kuwa madaktari, au Mzazi Polisi watoto wake kuwa Polisi n.k wakifuata nyayo.

Hata hivyo unapokuja Benki Kuu hauoni hilo zaidi ya kuona majina ya watoto ambao wazazi wao ni viongozi wa kisiasa na wenye nafasi kubwa za maamuzi katika serikali na ushawishi mkubwa. Unapoangalia majina hayo na kujiuliza ilikuwaje inakuwa vigumu kuelewa ilikuwaje hawa wote wakalundikana BoT?

Kuna hoja ambayo imetolewa kuwa ati "wamesoma sana" na walipata nafasi nyingi. Hilo tunaweza kulikubali; lakini kwanini wote waende BoT? kwanini wasiingie kwenye sekta binafsi au makampuni binafsi au kuanzisha makampuni yao wao wenyewe?

Watoto hawa wangepata heshima kubwa kama tungesikia wameanzisha makampuni yao na wakachakarika kama vijana wengine wanaomaliza elimu ya juu na kujianzishia biashara zao wao wenyewe.

Hata hivyo hilo wao hawaliwezi kwani linahitaji roho ya kuchangamka na kujishughulisha bila kutegemea jina lako.

Hawa watoto wote wako kwenye vitengo gani maana hapo ndipo tunaweza kupata majibu kidogo na kuelewa nini kinaendelea.
 
Mfano wako wa Bush sio mzuri kwa sababu Ugavana wa Jeb kule Florida ni wa kuchaguliwa na wananchi wa Florida. Tena alichaguliwa kuwa gavana wakati kaka yake (Raisi Bush) akiwa gavana wa Texas......
 
nafikiri ni mfano sahihi kwa sababu anayeweza kuona magavana wawili ambao ni ndugu anaweza kufikiria walipeana. Hivyo kama kuna Lowassa mwingine anachaguliwa kwenye kiti kingine cha Ubunge kama ilivyo kwa Kawawa na Malima hakuna anayeweza kupiga kelele. Au kama alivyo mdogo wake Mkapa ambaye naye ni Mbunge..
 
nafikiri ni mfano sahihi kwa sababu anayeweza kuona magavana wawili ambao ni ndugu anaweza kufikiria walipeana. Hivyo kama kuna Lowassa mwingine anachaguliwa kwenye kiti kingine cha Ubunge kama ilivyo kwa Kawawa na Malima hakuna anayeweza kupiga kelele. Au kama alivyo mdogo wake Mkapa ambaye naye ni Mbunge..

We Mwanakijiji unaianza vibaya 2008!! Mweee!! Narudia tena mfano wako si sahihi. Huyo mtu anayeweza kufikiria kuwa walipeana ni mtu gani huyo? Najua kabisa unajua taratibu za uchaguzi hapa Marekani lakini umeamua kuniyeyusha tu. Happy New Year bwana and stay warm....maana hiyo theluji iliyoanguka huko kijijini si mchezo.
 
Sioni tatizo kwa watoto wa wakubwa kupata ajira, lakini ni wa ngapi ambao umesikia wako wanafanya kazi namanyele! Karibu walio wengi wanafanya kazi kati maofisi ambayo yanaonekana kama ndio bora ki malipo, ulaji na mazingira ya kazi. Is it a coincidence? Wanapita kwenye chekecheke tunalopitia wengine?
 
Middle,
1. Unamaanisha kuwa Watz wengi wanaopata nafasi kusoma na wapo JF kwa UK, US na kwingineko ni watoto wa wakubwa?

2. Tanzania kutafuta Mchawi bwana- hawa watoto wa vigogo wao sii Watz? Waishi na kufanya kazi wapi? Mbinguni? Ni % ya Civil Service ni watoto wa vigogo? Isije onekana kama ni ubaguzi!

Tatizo sio wakafanye kazi mbinguni, swali ni kwanini BOT??? au kwenye ulaji mzuri? kama ni civil services ziko kibao ambazo zinalipa mshahara wa kawaida mbona hatusikii huko kuna hayo majina ya wakubwa??? kama ni kusoma hata sisi watoto wa maskini tumesoma na tungependa kupata hizo kazi zenye neema. Hakuna haja ya kuogopa kumjadili yeyote katika hii forums "its time to call a snake a snake and a lizard a lizard,ok" na anayeona anasimangwa asikae kimya, afungue mdomo tupambane kwa data; i.e vyeti,uzoefu n.k! Aluta continua weka mambo hadharani... we are ready.
 
Ninajaribu kuuelewa vizuri huu mjadala lakini ninashindwa kuelewa, Freeman kama mtoto wa Marehemu Mhasisi wa TANU, na mkwe wa Mwenyekiti muanzilishi wa Chadema, kwa baadhi ya hoja ninazoziona hapa kwenye hii topic, ilikuwa ni lazima awe yeye tu mwenyekiti wa Chadema? Kwa nini sio sisi watoto wa masikini ili na sisi tule nchi?

Let me understand this, mimi ni bin-adam kama wengine wote duniani, ninaongozwa na selfish motives kama wengine wote ndio maana nimetoka umasikini mpaka kufanikiwa kimaisha, leo nimefanikiwa kimaisha na nina nafasi katika jamii, eti ninataka watoto wangu wasifanye kazi walizo na ujuzi nazo na ambazo zinawalipa mafao mazuri kulingana na uwezo wao kielimu? Eti kuwa politically correct ni lazima niwatafutie kazi za mshahara mdogo? Hivi hawa viongozi wetu walizaliwa kwenye mali au utajiri? Si walipigana na maisha na sasa wanachuma jasho lao? Off course siku zote kuna isolated cases za abusiveness, za kujaribu kuajiri watoto wasiokuwa na qualifications kwenye sehemu wasizoziweza, basi wasemwe badala ya kuzunguka bila mwisho wa safari, I mean topic ndefu lakini hakuna juice hiyo sio kumkoma nyani, mambo yawekwe hadaharani kama kuna dataz!

Wakuu Azimio La Arusha halipo tena, usishangae kuwa siku hizi watoto wengi wako kwenye makampuni ambayo baba zao ni wawekezaji, regardless ya nafsi zao serikalini! Watoto wa viongozi ambao inaeleweka kuwa wamepewa nafasi za ulaji ambazo hawana qualifications nazo wasemwe hapa, lakini hatuwezi kuwa-generalize wote, kwa sababu kuna ambao wamesota sehemu walipo mpaka kufikia kwenye nafasi za juu, Freeman amesoma Ihungo, amefanya kazi BOT, amesota mpaka kufkia alipo leo, sasa kwa hii hoja iatkuwaje kuwa amepewa tu kwa sababu ya baba yake na mkwe wake?

I mean labda nina-miss something, kwa sababu so far sioni the juice au dataz!
 
Je twaweza kuona connection ya matatizo na kashfa benki kuu na uwepo wa watoto wengi wa vigogo kwenye taasisi hiyo nyeti? Binafsi hadi hivi sasa najaribu kujiambia kuwa hayo majina ni ya kutunga tu na watu hao hawapo Benki Kuu. Najaribu kujilazimisha kuamini kuwa hakuna watoto au ndugu wa kina Lowassa Benki Kuu.

Kama wapo binafsi ningependa kujua wako vitengo gani na wana position gani ili kujua kama maamuzi yao yanaweza kwa namna fulani kutiwa kiza na nafasi za wazazi au ndugu zao serikalini.

Hadi hivi sasa jina ambalo linaweza kunishtua sana ni la Lowassa, Sumaye, na Mkapa. Tunaposikia kashfa Benki Kuu na upotevu wa mabilioni ya shilingi hatuna budi kujiuliza kama hawa "ndugu zetu" waliona jambo lolote na walifanya nini kuliumbua na kuhakikisha linakomeshwa?

Hofu yangu ni kuwa kama ni kweli hawa wapo na wengine ambao hawatumii majina ya ubini wa familia zao basi uwezekano kuwa hawakujua mambo ya Tangold, Meremeta, Deep Green na makampuni mengine kama 40 hivi yaliyoanzishwa ili kuchota fedha za Umma itakuwa ni nasibu ya mwaka!

Binafsi naamini kwa moyo wangu wote Watanzania tumeshindwa kuisimamia Benki Kuu na short of firing the senior management hatuwezi kufika mahali popote pale.

Na wakishawatimua wote hao, serikali lazima iwahamishe na kupangua nafasi zote za makao makuu ya benki kuu na ikibidi walete watu toka nje kuja kuiendesha Benki Kuu kwa Mkataba maana sisi wenyewe tumeshindwa!

Mwanakijiji,

Hivi ni lini hizo nafasi za kazi hapo BOT zilitangazwa japo magazetini ili watanzania wote wazione au ndiyo kupachikana tu ati kwa sababu baba ni waziri?.
Hivi kuna mtu anaweza kutuletea titles za hawa watoto hapo BOT ili tulinganishe education,experience zao na hizo position? maana kama ni wafagiaji au ni majanitors nafikiri wanaweza kuwa wanaqualify.
Halafu kuna huyu mtoto wa Makama anaitwa January Makamba ambaye mara tu baada ya kumaliza shule kapata kazi IKULU sasa sijui kuna utaratibu gani unatumika kuwaajili hawa watoto ili tujue kuwa qualifications ni kuwa mtoto wa mkubwa tu!! au la?

-Wembe
 
Mimi ningependa kijua hushusan kazi za hao so called watoto wa wakubwa ambao kwanza wengine madingi zao walishavuta muda mrefu. Maana hapa sasa baadhi ya watu hata kama mtu ni karani ili mradi ni mtoto wa mkubwa watu watalalamika...
 
Back
Top Bottom