Nyati
JF-Expert Member
- Mar 6, 2009
- 2,489
- 1,814
Wadau,
Leo nimeshuhudia watoto wakishiriki ktk maadhimisho ya Siku ya Mwl. Nyerere na kuhitimisha mbio za mwenge katika kile kilichoitwa harahiki kule Kigoma. Mimi sipingi hizi harahiki bali watoto wale wamechoshwa sana katika mazingira magumu ya vumbi wakati ni watoto wadogo.
Wamekaa juani karibia masaa matano bila sababu yeyote ile ya msingi. Kwanza kabla ya Raisi hajafika wamekaa pale karibia masaa matatu. Wakati huu tayari wengine walishaanza kusinzia sinzia na kuamshwa kwa makwenzi. Baada ya Rais ya kufika mambo mengine yakaendelea na baadaye wakaanza hiyo harahiki ambayo nayo imechukua muda mrefu wakipiga kwata bila kupumzishwa kama masaa mawili hivi bila kupumzika.
Hivi Wizara ya akina mama na watoto inatoa mwongozo gani juu ya jambo hili??. Kweli ni haki kwa watoto kupigishwa kwata kwa muda wote huo tena katika vumbi??
Je Mwl. angekuwepo angefurahia hali hii? Ni wakati muhafaka wa kufuata haki za watoto badala ya kuwatumia isivyohalali kama ilivyofanyika leo. Kwa wale mlioshuhudia mtakubaliana nami katika hili kwani hakukuwa na haja ya kuwaweka katikati ya uwanja katika vumbi muda wote huo. Wangewekwa jukwaani kama washiriki wengine na wakaitwa uwanjani wakati wa harahiki hiyo na vile vile wafanye kwa muda mfupi siyo kama leo.
Huu ni mtizamo wangu
Leo nimeshuhudia watoto wakishiriki ktk maadhimisho ya Siku ya Mwl. Nyerere na kuhitimisha mbio za mwenge katika kile kilichoitwa harahiki kule Kigoma. Mimi sipingi hizi harahiki bali watoto wale wamechoshwa sana katika mazingira magumu ya vumbi wakati ni watoto wadogo.
Wamekaa juani karibia masaa matano bila sababu yeyote ile ya msingi. Kwanza kabla ya Raisi hajafika wamekaa pale karibia masaa matatu. Wakati huu tayari wengine walishaanza kusinzia sinzia na kuamshwa kwa makwenzi. Baada ya Rais ya kufika mambo mengine yakaendelea na baadaye wakaanza hiyo harahiki ambayo nayo imechukua muda mrefu wakipiga kwata bila kupumzishwa kama masaa mawili hivi bila kupumzika.
Hivi Wizara ya akina mama na watoto inatoa mwongozo gani juu ya jambo hili??. Kweli ni haki kwa watoto kupigishwa kwata kwa muda wote huo tena katika vumbi??
Je Mwl. angekuwepo angefurahia hali hii? Ni wakati muhafaka wa kufuata haki za watoto badala ya kuwatumia isivyohalali kama ilivyofanyika leo. Kwa wale mlioshuhudia mtakubaliana nami katika hili kwani hakukuwa na haja ya kuwaweka katikati ya uwanja katika vumbi muda wote huo. Wangewekwa jukwaani kama washiriki wengine na wakaitwa uwanjani wakati wa harahiki hiyo na vile vile wafanye kwa muda mfupi siyo kama leo.
Huu ni mtizamo wangu