Watetezi. . .

Dr Lizzy

Platinum Member
May 25, 2009
30,806
59,285
Hivi umewahi kuona mtu anatetea sana kitu japo kwa nje anaweza akaonekana yeye ndie anaeonewa/kosewa?

Wakati mwingine watu hua wanawatetea wenzao sio kwasababu wanapenda bali kwasababu nafsi zao zinawasuta. Yani kile wanachotetea na wao hua wanafanya sema tu hawajulikani. [Mf. Mzuri ni wadada wa kazi na ndugu wengine au hata marafiki. . . unakuta pesa imepotea ndani na tayari yupo mtoto ambae anajulikana ndio mdokozi. All of the sudden anaibuka mtu na kuanza kumtetea yule mtoto kuwa "hakukusudia, pengine hatorudia tena, pengine watoto wenzake walimlazimisha/ mponza"] ili asiadhibiwe kwasababu yeye ndie aliechukua hiyo pesa hivyo kwasababu hawezi kukiri ili aadhibiwe yeye anatafuta namna ya kumtetea yule anayetuhumiwa ili asiadhibiwe bure.

Anyway, nimejikuta nafikiria haya kwasababu nashawishika kufanananisha 'BAADHI' ya watu wanaotetea waume/wake/wapenzi wao wanapocheat na kuishia kutoa visingizio vingi vya kwanini wenzi wao wamecheat ili waonekane hawana hatia.
Inawezekana 'baadhi' ya hawa watu na ni cheaters kwa namna yao wenyewe (kuflirt na co-worker/marafiki, kuwa na mpenzi wa kwenye mtandao, kuwa na mtu ambae wanafantasize juu yake, kuwa na mtu wanaemtamani na kumuota kila walalapo) hivyo wanashindwa kuwahukumu wenzi wao moja kwa moja na kukataa kuonewa kwasababu hata wao wana yao. Hususan wale wanaotetea sana privacy ya simu na account za mitandaoni, inawezekana wanafanya hivyo kwasababu huko ndipo wao wanapofanya yale yanayowapa wao nafuu na hawataki wenzi wao wajue.
Mimi nadhani huo ndio uhalisia, na haijalishi mara ngapi nasikia watu wakisema 'privacy muhimu' bado sijashawishika kwamba mtu ambae unakula nae, unalala nae, unamwita ubavu wako wa pili , unazaa nae anatakiwa apewe mipaka kwenye vitu ambavyo sio muhimu ikiwa havifichi siri yoyote. Ningefurahi kweli kama watu wasiweza kutulia kwenye mahusiano ya watu wawili tu wasingekubali kuao ama kuolewa, labda ndoa ingerudi kuwa kitu cha heshima tofauti na sasa ilovyogeuzwa kuwa "cover" ya maovu.
 
Duh, its complictaed.

Partly yes, partly no kwenye cheating

wakati mwingine unatetea sababu nafsi inakusuta.
Wakati mwingine unatetea sababu huamini kama cheating ni sabau tosha ya kuvunja mahusiano.

Siamini usiri baina ya wanandoa iwe ya simu, pesa, biashara au kitu chochote.
 
Duh, its complictaed.

Partly yes, partly no kwenye cheating

wakati mwingine unatetea sababu nafsi inakusuta.
Wakati mwingine unatetea sababu huamini kama cheating ni sabau tosha ya kuvunja mahusiano.

Siamini usiri baina ya wanandoa iwe ya simu, pesa, biashara au kitu chochote.

Ndio maana nikasema baadhi.

Kwahiyo wewe kama wewe upo tayari kuwa muwazi kwa mwenzako linapokuja swala la mawasiliano? Je yeye akiwa anaamini kinyume na hapo. . . mtaelewana?
 
Mimi nimesema BAADHI hivyo sielewi kwanini umeuliza kuhusu WOTE.
Ok sawa naona unanza kukwepa kidogo dogo hapo, haya turidi kwenye swalii tena....Wewe unauhakika gani kama badhi ya hao wanao watetea wenzao, huwa nafsi zao zinawasuta?

Na umezipiata wapi hizo infomation na study tips??

Nani aliye zi study??
 
sasa Lizzy Luu..
unataka asitetewe mtu au wasifiche mambo?

Well kama hawana ya kuficha wawe wawazi, na wakiwatete wenzao wasitake kuonekana kwamba wao ni wavumilivu/wana huruma sana wakati nao ni wale wale.
 
Ok sawa naona unanza kukwepa kidogo dogo hapo, haya turidi kwenye swalii tena....Wewe unauhakika gani kama badhi ya hao wanao watetea wenzao, huwa nafsi zao zinawasuta?

Na umezipiata wapi hizo infomation na study tips??

Nani aliye zi study??

Ningependa urudie kusoma tena alafu ukishaelewa kila nilichoandika tuendelee kujadiliana.

KEY WORDS: Nadhani, Nashawishika, Baadhi, Inawezekana. YAZINGATIE SANA.
 
Lizzy
kuna kitu Kongosho anakueleza sidhani kama unakielewa...

labda nikuulize umewahi kukutana na kitu kinaitwa
'the power of subconscious'???????/
 
Well kama hawana ya kuficha wawe wawazi, na wakiwatete wenzao wasitake kuonekana kwamba wao ni wavumilivu/wana huruma sana wakati nao ni wale wale.

na vipi kama ni mapenzi haswa..
huyo Bi dada kaamua kuwa mvumilivu, huruma
kumtunza mumewe mpaka kifo kiwatenganishe ..

Je hapo huyu Bi dada anahaki ya kumtetea mumeo kwa lolote.?
kumbuka kuna ila ya kupenda upande mmoja pia..
 
na vipi kama ni mapenzi haswa..
huyo Bi dada kaamua kuwa mvumilivu, huruma
kumtunza mumewe mpaka kifo kiwatenganishe ..

Je hapo huyu Bi dada anahaki ya kumtetea mumeo kwa lolote.?
kumbuka kuna ila ya kupenda upande mmoja pia..
Kurwa hao wanaowatetea huku wenyewe wakiwa faithful kwa kila namna sio nnaowaongelea.
 
Ningependa urudie kusoma tena alafu ukishaelewa kila nilichoandika tuendelee kujadiliana.

KEY WORDS: Nadhani, Nashawishika, Baadhi, Inawezekana. YAZINGATIE SANA.
Aisay nimerudia kama mara mbili naona ni vile vile...hizo study zako umezipata wapi, au umezistudy vipi mpaa ukamake sure ziko sawa...Au ni akili yako tu imekutuma vile.

Hebu chukua mfano mdogo sana....Leta wizi wawili hapo ufanye kama joke, uwaulize nani kaiba pesa zako uone wanavyo jiishitaki...kila mmoja atamsonta mwenzie ndio kaiba, Kwa sababu kila mmoja wao anaona kaharibiwa deal yake.
 
Care to point out what i'm missing?

ok ni hivi
kuna vitu tunaviamini ndani kabisa ya mioyo yetu
ambavyo vinasababisha viwe 'maamuzi' makuu wakati wa crisis....

viko ndani ya subcouncious yetu kwa sababu tumevipokea kwa miaka miingi sometimes bila kujua....

mfano binti alielelewa na mama anaepigwa na mumewe na kusamehe.......hata akisema mdomoni
sitasamehe nikipigwa.....ndani ya subconscious yake anaamini ni jambo linalosameheka....

sasa likimkuta na akipata sababu tu 'anasamehe'.....

kwa hiyo misimamo yetu sanasana iko deep mno

hao watetezi sio wanatetea kwa sababu na wao wapo hivyo
but ndani ya subcouncious haaoni kuwa ni dhambi kubwa kihivyo

wengine wamelelewa kuamini ni jambo lakusameheka atasamehe na kutetea hata kama yeye hafanyi
 
ok ni hivi
kuna vitu tunaviamini ndani kabisa ya mioyo yetu
ambavyo vinasababisha viwe 'maamuzi' makuu wakati wa crisis....

viko ndani ya subcouncious yetu kwa sababu tumevipokea kwa miaka miingi sometimes bila kujua....

mfano binti alielelewa na mama anaepigwa na mumewe na kusamehe.......hata akisema mdomoni
sitasamehe nikipigwa.....ndani ya subconscious yake anaamini ni jambo linalosameheka....

sasa likimkuta na akipata sababu tu 'anasamehe'.....

kwa hiyo misimamo yetu sanasana iko deep mno

hao watetezi sio wanatetea kwa sababu na wao wapo hivyo
but ndani ya subcouncious haaoni kuwa ni dhambi kubwa kihivyo

wengine wamelelewa kuamini ni jambo lakusameheka atasamehe na kutetea hata kama yeye hafanyi

Sasa mbona ulichonieleza ndicho nilichoelewa na kujibu kule mwanzo Boss? Kwamba nafahamu wapo wanaosamehe kwa sababu nyingine na ndio maana nikatumia neno BAADHI kuwakilisha ninaowaongelea.
Nwy tuendelee mbele. . . .
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom