Natoa wito kwa watawala na polisi wa Tanzania kusoma alama za nyakati kuhusiana na mabadiliko yanayopamba moto.
kama ilivyo kawaida watu kubisha na kutokubali ukweli japo unajulikana wapo watakaobisha.
Hakuna wakati ambao kumetokea vuguvugu la mabadiliko kama ilivyo kwa Tanzania leo. Watawala wanalijua, CCM inajua na hata polisi wanalijua hilo kuthibitisha hilo ni pamoja na nguvu zinazotumika kudhibiti mabadiliko hayo, Msajili na kada wa CCM Tendwa naye analijua hilo na ndiyo maana anakimbilia kuitisha CHADEMA kuwa atakifuta.
Wito wangu naomba watawala wakubaliane na wakati vinginevyo Taifa litapelekwa pabaya kuliko kawida. Tangu polisi walipoamua kuua na ndivyo watanzania wanavyozidi kuongezeka kwenye mikutano na maandamano. Naomba watawala waache mara moja vitisho kama wanaweza wajibu hoja, watanzania wa leo sio wale wa jana.Mbinu zozote zinazopangwa na watawala Chadema wanazipata. Kabla ya tamko la tendwa kuliwekwa uzi hapa kuhusu sababu za polisi kuua katika mikutano ya chadema sababu mojawapo ni kutaka kupata sababu za kukifuta Chadema siku chache baadaye Tendwa akatoa tamko kama kupima upepo
Ushauri wangu kwa Tendwa asijaribu kufanya hivyo maana akifanya hivyo ajue kutatokea machafuko ya ajabu kwani kwa sasa Chadema ni zaidi ya CCM. CCM wanatumia mbinu zile za zamani wakati watanzania wamebadilika, Hivyo nawaomba watawala waache mbinu chafu vinginevyo haya yatakuja wahukumu. Polisi acheni kusikiliza amri haramu za CCM kwa kuua watanzania wasio na hatia damu zao zitawalilia. Kwa damu iliyomwagika ya raia haiwezi kwenda bure hivyo CCM jiandaeni kukabidhi madaraka muda ukifika.
Polisi mkiendelea kuua ni ole wenu maana mnaua na jioni mnakuwa na watanzania haohao mnawaua, watoto wenu wanasoma na watoto wa wale wale mnaowaua sasa sijui pale watanzania watakapoamua kujibu mapigo, hatupendi tufike huko. Kumbukeni madikiteta waliotangulia leo hii wako wapi, Kikwete naomba muogope Mungu na ili ujisafishe wawajibishe waliomuua mwangosi hata kama walipokea amri toka chama chako. Watanzania hatuna imani na IGP MWEMA, Waziri Nchimbi na jeshi lote la polisi. Tume ya Nchimbi inachunguza nini wakati kila kitu kipo wazi.
Wako wapi magangwe kama Id Amin, Mabutu, Ghadafi na wengine wengi tujifunze kwa hao kuwa ubabe na fahari ya dunia ni ya kitambo tu, kuua kwa makusudi inauma, Watanzania tuombee Taifa hili ili Mungu alinusuru.
kama ilivyo kawaida watu kubisha na kutokubali ukweli japo unajulikana wapo watakaobisha.
Hakuna wakati ambao kumetokea vuguvugu la mabadiliko kama ilivyo kwa Tanzania leo. Watawala wanalijua, CCM inajua na hata polisi wanalijua hilo kuthibitisha hilo ni pamoja na nguvu zinazotumika kudhibiti mabadiliko hayo, Msajili na kada wa CCM Tendwa naye analijua hilo na ndiyo maana anakimbilia kuitisha CHADEMA kuwa atakifuta.
Wito wangu naomba watawala wakubaliane na wakati vinginevyo Taifa litapelekwa pabaya kuliko kawida. Tangu polisi walipoamua kuua na ndivyo watanzania wanavyozidi kuongezeka kwenye mikutano na maandamano. Naomba watawala waache mara moja vitisho kama wanaweza wajibu hoja, watanzania wa leo sio wale wa jana.Mbinu zozote zinazopangwa na watawala Chadema wanazipata. Kabla ya tamko la tendwa kuliwekwa uzi hapa kuhusu sababu za polisi kuua katika mikutano ya chadema sababu mojawapo ni kutaka kupata sababu za kukifuta Chadema siku chache baadaye Tendwa akatoa tamko kama kupima upepo
Ushauri wangu kwa Tendwa asijaribu kufanya hivyo maana akifanya hivyo ajue kutatokea machafuko ya ajabu kwani kwa sasa Chadema ni zaidi ya CCM. CCM wanatumia mbinu zile za zamani wakati watanzania wamebadilika, Hivyo nawaomba watawala waache mbinu chafu vinginevyo haya yatakuja wahukumu. Polisi acheni kusikiliza amri haramu za CCM kwa kuua watanzania wasio na hatia damu zao zitawalilia. Kwa damu iliyomwagika ya raia haiwezi kwenda bure hivyo CCM jiandaeni kukabidhi madaraka muda ukifika.
Polisi mkiendelea kuua ni ole wenu maana mnaua na jioni mnakuwa na watanzania haohao mnawaua, watoto wenu wanasoma na watoto wa wale wale mnaowaua sasa sijui pale watanzania watakapoamua kujibu mapigo, hatupendi tufike huko. Kumbukeni madikiteta waliotangulia leo hii wako wapi, Kikwete naomba muogope Mungu na ili ujisafishe wawajibishe waliomuua mwangosi hata kama walipokea amri toka chama chako. Watanzania hatuna imani na IGP MWEMA, Waziri Nchimbi na jeshi lote la polisi. Tume ya Nchimbi inachunguza nini wakati kila kitu kipo wazi.
Wako wapi magangwe kama Id Amin, Mabutu, Ghadafi na wengine wengi tujifunze kwa hao kuwa ubabe na fahari ya dunia ni ya kitambo tu, kuua kwa makusudi inauma, Watanzania tuombee Taifa hili ili Mungu alinusuru.