mpayukaji
JF-Expert Member
- Oct 31, 2010
- 940
- 349
Tanzania imegeuka shamba la bibi ambapo kila ngedere anaweza kwenda kula mahindi. Hakuna ubishi kuwa kwa sasa Tanzania ni nchi yenye huduma aghali na mbovu za simu katika Afrika. Simu zetu hazina uhakika na tunatozwa kiwango kikubwa kuliko majirani zetu. Je watanzania wameridhika na mashindano ya hovyo ya mikwanja na upuuzi mwingine na kusamehe huduma stahiki? Kuna haja ya kuwaasa wahusika watupe huduma bora badala ya mashindano ya kamari itokanayo na pesa wanayotuibia. Shinda milioni 50 hata 100. Bila huduma safi huu bado ni wizi. Je tunapumbazwa?