Watanzania wanauongeleaje wizi wa makampuni ya simu nchini?

mpayukaji

JF-Expert Member
Oct 31, 2010
940
349
Tanzania imegeuka shamba la bibi ambapo kila ngedere anaweza kwenda kula mahindi. Hakuna ubishi kuwa kwa sasa Tanzania ni nchi yenye huduma aghali na mbovu za simu katika Afrika. Simu zetu hazina uhakika na tunatozwa kiwango kikubwa kuliko majirani zetu. Je watanzania wameridhika na mashindano ya hovyo ya mikwanja na upuuzi mwingine na kusamehe huduma stahiki? Kuna haja ya kuwaasa wahusika watupe huduma bora badala ya mashindano ya kamari itokanayo na pesa wanayotuibia. Shinda milioni 50 hata 100. Bila huduma safi huu bado ni wizi. Je tunapumbazwa?
 
Hakuna ubishi kuwa kwa sasa Tanzania ni nchi yenye huduma aghali na mbovu za simu katika Afrika. Simu zetu hazina uhakika na tunatozwa kiwango kikubwa kuliko majirani zetu.

Una ushahidi wowote kuhusu hoja yako hapo juu?
 
Una ushahidi wowote kuhusu hoja yako hapo juu?
Kwa suala la wizi hata mimi nimeibiwa mara kadhaa na inaniuma sana. Kuna tatizo la TCU wanaopokea maalamiko bila kuuyafanyia kazi. Tatizo la serikali inayowajibika kwa mwenye nacho na siyo kwa mwananchi. Nadhani iko haja kuwajibisha makampuni kisheria na kuyadai fifia kubwa mahakamani bila vyombo kama TCU na Ewura kuingilia kati na kuleta porojo zao. Hawa jamaa hawajaingia kwenye anga za akina Mtikila bado!
 
Ndjabu Da Dude unataka ushahidi upi? Nakupa mfano mdogo tu. Ukipiga simu kutoka nje unatozwa senti 27 za dola wakati Kenya wanatoza senti 5. Muda wa kuongea Kenya ni mara tano ya muda wa kuongea Tanzania. Imefikia mahali watu wanapiga simu kupitia Kenya na Uganda kuepuka kulanguliwa. Kama haitoshi, ukipiga simu wanakata ili kuzidi kuchaji pesa ya kuunganisha. Wakati mwingine unapiga simu unaambiwa uongeze salio au namba unayopiga siyo wakati ni ubabaishaji mtupu. Wanaopenda kubisha bisha wanakuwa kama hawaishi duniani. Kaulize bei za vitu Tanzania ulinganishe na majirani zetu utajua ninachomaanisha. Tunalanguliwa umeme kuliko hata Kenya isiyozalisha umeme.
 
Ndjabu Da Dude unataka ushahidi upi? Nakupa mfano mdogo tu. Ukipiga simu kutoka nje unatozwa senti 27 za dola wakati Kenya wanatoza senti 5. Muda wa kuongea Kenya ni mara tano ya muda wa kuongea Tanzania. Imefikia mahali watu wanapiga simu kupitia Kenya na Uganda kuepuka kulanguliwa. Kama haitoshi, ukipiga simu wanakata ili kuzidi kuchaji pesa ya kuunganisha. Wakati mwingine unapiga simu unaambiwa uongeze salio au namba unayopiga siyo wakati ni ubabaishaji mtupu. Wanaopenda kubisha bisha wanakuwa kama hawaishi duniani. Kaulize bei za vitu Tanzania ulinganishe na majirani zetu utajua ninachomaanisha. Tunalanguliwa umeme kuliko hata Kenya isiyozalisha umeme.

Hayo bado yanabakia kuwa ni maoni yako tu, mkuu. Tupatie independently verifiable sources to back-up your contentions. Thank you.
 
I am a human being. Do you need independently corroboration to support my assertion? Try to understand simple things. Not every assertion does need verification or corroboration my dear. I am the one who is making the said calls to Tanzania. So who else do you want me to avail to corroborate my assertion? After all, you are but an exception to the general rule so to speak.
 
Back
Top Bottom