Watanzania wana kiu kikubwa cha kuitoa CCM, Je tatizo ni nini?

Tatizo si wananchi, tatizo ni mfumo wa uchaguzi hautoi mwanya kwa wananchi kufanya maamuzi. Hii ni hatari sana kama wananchi wanakosa imani na system nzima ya uchaguzi. Tungekuwa na chaguzi huru na haki watu wengi wangeshiriki. Lakini tatizo lingine linalofanywa na Tume ya uchaguzi ya CCM ni voters supression. Ku-scramble majina ya wale wanaoonekana kutowaunga mkono ni moja ya njia pekee iliyobaki ya kupunguza hamasa ya wapiga kura. Mtu hawezi kuwa anahamishwa vituo uchaguzi baada ya uchaguzi bila ridhaa yake. Tume inabandika majina siku moja kabla mtu anatoka kwake na kufika kituoa alichopigia kura uchaguzi uliopita bila mafanikio. Hii ni demotivation factor kubwa sana ya ushiriki wake uchaguzi ujao.

2015 inaweza kuwa worse zaidi.

Ndio maana wasomi wanalilia katiba mpya ambayo rais atakuwa na madaraka machache na bunge kupewa madaraka mengi. Ila vile vile katiba mpya inayorohusu kila mmoja wetu afaidi keki ya nchi yetu. Na sio wachache ndio wanakula nchi hii lakini wengi wanabakia mafukara. Binafsi naunga mkono katiba mpya ila SIO KWA MTAJI WA KISIASA. Katiba mpya isimamiwe na wasomi ambapo taaluma itumike katika kuitunga. Vyenginevyo tutapata KATIBA MBOVU BADALA YA KATIBA MPYA.
 
Mdondoaji,

..lakini JK na Pinda ni matajiri wakubwa kuliko Mbowe.

..kitu cha kushangaza ni kwamba hawana deni ktk taasisi yoyote ile ya fedha hapa nchini.

..kwa madudu waliyofanya CCM, kwa kweli mtu yeyote yule naona anafaa kuongoza nchi hii.

..YES, they have lowered the standards/bar that low.
 
Mdondoaji,

..lakini JK na Pinda ni matajiri wakubwa kuliko Mbowe.

..kitu cha kushangaza ni kwamba hawana deni ktk taasisi yoyote ile ya fedha hapa nchini.

..kwa madudu waliyofanya CCM, kwa kweli mtu yeyote yule naona anafaa kuongoza nchi hii.

..YES, they have lowered the standards/bar that low.
Shukran mkuu wangu yaani Wadanganyika kusema kweli sijui tuko kundi gani la binadamu... Nchi za Ulaya tajiri kama JK au Pinda na hana madeni angefuatiliwa zaidi ya Mbowe ambaye anadaiwa na Utajiri wake unaonyesha wapi kapata mtaji wa utajiri wake. lakini kwetu kinyume kabisa kutokana na mila na desturi za mtu kuiba halali kama hatakamatwa..

Matajiri wengi Tanzania ni wezi na wameupata utajiri huo kwa dhulma lakini maadam hatuna kesi mahakamani hawa ni wasafi isipokuwa yule anayedaiwa na inajulikana anadaiwa ndiye mbaya. Kesho Mbowe akiondoka duniani (mwenyezi Mungu apitishie mbali) tutaweza kukamata mali zake kurudisha deni letu lakini hao waloiba na kuhalalisha mali za wizi tutawakamata vipi??

Aaaaah turudi kwenye mjadala nawasoma kisha nitakuja changia mada inapopaswa..
 
Mdondoaji,

..lakini JK na Pinda ni matajiri wakubwa kuliko Mbowe.

..kitu cha kushangaza ni kwamba hawana deni ktk taasisi yoyote ile ya fedha hapa nchini.

..kwa madudu waliyofanya CCM, kwa kweli mtu yeyote yule naona anafaa kuongoza nchi hii.

..YES, they have lowered the standards/bar that low.

Joka kuu,

Ndio maana nasema Tanzania is full of corrupt bureaucrat hata hao unaosema wanamadeni ni kwamba hawajapata mwanya kushika funguo za mirija. Wakifunguliwa tutalia kuliko tunavyolia na CCM.

Mie naona hakuna bado chama cha kuongoza taifa hili kwani wote waliopo ni bunch of political opportunist. Hebu niambie kwanini tuwape nchi Chadema au CUF?
 
Joka kuu,

Ndio maana nasema Tanzania is full of corrupt bureaucrat hata hao unaosema wanamadeni ni kwamba hawajapata mwanya kushika funguo za mirija. Wakifunguliwa tutalia kuliko tunavyolia na CCM.

Mie naona hakuna bado chama cha kuongoza taifa hili kwani wote waliopo ni bunch of political opportunist. Hebu niambie kwanini tuwape nchi Chadema au CUF?
Hawataweza ikiwa tutaipata Katiba tuitakayo.. wewe na mimi tutakuja na mawazo kuziba miaya hiyo...Kwa hiyo kabla ya CCM au CDM kuchukua utawala wa mwaka 2015 tunatakiwa tuijenge katiba ambayo inajali maslahi yetu kwanza na sii ya vyama au viongozi. Tukisha pata katiba mpya, imani ya watu itarudi..Inanishangaza kuona wengi wenu mnafikiri vyama vinaweza kurudisha imani za watu... Laa hasha, imani imepotea pale mwongozo unapopotosha.

Mtu yeyote ataacha kuwa Muislaam au Mkristu kwa sababu ameona makosa ama mapungufu ktk vitabu vya imani hiyo na sio kwa sababu kanisa, msikiti au Sheikh na Padre wana mapungufu. Hii dhana ya kuamini CCM au CDM na wanasiasa wao ni makosa makubwa ikiwa mnashindwa kuyaona makosa ktk sheria mama.
 
Ndio maana wasomi wanalilia katiba mpya ambayo rais atakuwa na madaraka machache na bunge kupewa madaraka mengi. Ila vile vile katiba mpya inayorohusu kila mmoja wetu afaidi keki ya nchi yetu. Na sio wachache ndio wanakula nchi hii lakini wengi wanabakia mafukara. Binafsi naunga mkono katiba mpya ila SIO KWA MTAJI WA KISIASA. Katiba mpya isimamiwe na wasomi ambapo taaluma itumike katika kuitunga. Vyenginevyo tutapata KATIBA MBOVU BADALA YA KATIBA MPYA.

Mkuu,

Ni wasomi wa wapi hawa unaowazungumzia?
 
Hawataweza ikiwa tutaipata Katiba tuitakayo.. wewe na mimi tutakuja na mawazo kuziba miaya hiyo...Kwa hiyo kabla ya CCM au CDM kuchukua utawala wa mwaka 2015 tunatakiwa tuijenge katiba ambayo inajali maslahi yetu kwanza na sii ya vyama au viongozi. Tukisha pata katiba mpya, imani ya watu itarudi..Inanishangaza kuona wengi wenu mnafikiri vyama vinaweza kurudisha imani za watu... Laa hasha, imani imepotea pale mwongozo unapopotosha.

Mtu yeyote ataacha kuwa Muislaam au Mkristu kwa sababu ameona makosa ama mapungufu ktk vitabu vya imani hiyo na sio kwa sababu kanisa, msikiti au Sheikh na Padre wana mapungufu. Hii dhana ya kuamini CCM au CDM na wanasiasa wao ni makosa makubwa ikiwa mnashindwa kuyaona makosa ktk sheria mama.

Je Mkandara unadhani haya madai tunayodai ya katiba hayana mapendekezo ya vyama vyenyewe husika? Unajua mkuu wangu haya madai ya katiba yanahitaji majadiliano ya wananchi wote na sio mapendekezo yatakayowasaidia CCM au Chadema kiuongozi. Tunahitaji katiba iliyo makini ili tuweze kuwabana hawa corrupt bureaucrats.

Kama katiba ikiwalinda watawala sisi hatutaweza hata kuziba mianya itakayojitokeza. Kama unavyoona wabunge wa CCM wanavyoishadidia mapendekezo yao ya katiba yanayompa nguvu nyingi Rais kwani wanajua wakishinda urais they will have power to do whatever they want. Sasa katiba inabidi iwakilishe mawazo yetu kama wananchi na not otherwise.
 
Mkuu,

Ni wasomi wa wapi hawa unaowazungumzia?

Mkuu.

Nawazungumzia wasomi waliosoma na kuelimika na sio wasomi wa kujaza makaratasi na mavyeti. Waliosoma vyeti wapo wengi ndio hawa mafisadi waliotuzunguka ila wasomi walioelimika ndio wanaodai mabadiliko haya.
 
Ndio maana wasomi wanalilia katiba mpya ambayo rais atakuwa na madaraka machache na bunge kupewa madaraka mengi. Ila vile vile katiba mpya inayorohusu kila mmoja wetu afaidi keki ya nchi yetu. Na sio wachache ndio wanakula nchi hii lakini wengi wanabakia mafukara. Binafsi naunga mkono katiba mpya ila SIO KWA MTAJI WA KISIASA. Katiba mpya isimamiwe na wasomi ambapo taaluma itumike katika kuitunga. Vyenginevyo tutapata KATIBA MBOVU BADALA YA KATIBA MPYA.
Kama wabunge wanafikiria hivyo nao wana makosa... tena makubwa sana. Wananchi hatuwezi kuwap[a ridhaa hiyo kwa sababu tunataka kuondoa mambo mengi ndani ya bunge letu. Kwa uchache tu utamaduni wa TAKRIMA iwe haramu, Posho za sitting Allowance ziwe marufuku. Mbunge ajulikane analipwa kiasi gani kwa mwaka na walipe kodi, Mbunge haruhusiwi kuwa waziri, mashangingi na fedha za mafuta na kadhalika hivyo tume tuitakayo sisi wananchi ni kuhakikisha wabunge pia wanabanwa.

Tume itaundwa sawa na mapendekezo ya rais au waziri wa sheria isipokuwa madaraka ya rais yatapungua tu mwanzo wa uratibu na mchakato wake lakini maamuzi ya kupitisha katiba hii ndipo wao na Marais wa pande mbili watakaa kusoma na kujadili vipengele vyote hasa ktk maswala ya Muungano. Lakini fikra za kusema rais au Wabunge ndio wachague tume wakati tunajua fika watalinda maslahi na nafasi zao halitakubalika...

Acha CDM waurudishe muswada Bungeni wakituwakilisha sisi leo hii, kisha sisi tuuchambue muswada tena naweza kabisa kutoa mawazo yangu hapa hapa JF kwa kuupitia muswada kama raia na mzalendo...
 
Watanzania wana uchu mkubwa wa kuiona CCM inahama IKULU, na kukipisha chama kingine kuingia Ikulu. Haya ni majibu ya utafiti wa kile kikundi chetu binafsi "SONGAMBELE" amabacho kina wanachama na wataalam wake toka vyuo vikuu mbali mbali Tanzania.

Aidha katika taarifa hiyo imeonyesha kuwa 70% kati ya watanzania walioshiriki katika utafiti huo ( 1 milioni) wanahitaji chama kingine zaidi ya CCM Kuingia Ikulu. Lakini walipoulizwa ni chama gani kati ya vyama pinzani walipenda kukiona kinaingia Ikulu, 65% walijibu "hakuna". Hii inaonyesha wazi jinsi vyama vya upinzani vilivyowakatisha tamaa watanzania toka katika ndoto yao ya kukiona chama cha upinzani kuingia ikulu.

Nilipomhoji Prof Safari kuhusu matokeo hayo alisema yafuatayo "Sishangazwi wala kushitushwa na taarifa hiyo, angalia kampeni zao ni za kubabaisha tu, hakuna chama kinachokidhi matakwa ya wananchi. Hakuna chama cha upinzani katika vyama vikuu kilichoweza kuonyesha kuliweka wazi swala la umoja wa kitaifa. Vyama hivi aidha vimelaumiwa kwa kuendekeza ukabila au udini, na wameshindwa kujibu tuhuma hizo kwa kiwango ambacho watanzania watawaelewa. Kuwa na viongozi wa vyama ambao walishiriki au wanashiriki katika nyadhifa za taasisi za kidini ni kosa kubwa kwa kipindi hiki, watanzania hawako tayari kwa hilo japokuwa kisheria inakubalika."

Katika utafiti huo CHADEMA iliongoza kati ya vyama pinzani kuingia IKULU kwa kuwa na 16% ikifuatiwa na CUF 14%. Cha kushangaza hata maeneo yale ambayo huhesabika kama ngome yaCHADEMA, ilifanya vibaya. Kwa mfano Arusha ni 35% na Moshi 40% tu ndio waliohitaji kuiona CHADEMA yaingia IKULU. Kwa Arusha wengi walikatishwa tamaa na viongozi wao hasa kwa tukio la hivi karibuni la kuwapeleka wanachama kuandamana bila mipango maalum.

Mh Slaa nilipompigia simu alikataa kusema lolote na kukata simu. Mh Zitto Kabwe, alicheka na kusema "sina uhakika kama hizo namba zinawakilisha hali halisi. Hata hivyo kuwaeleza watu mpaka wakuelewe inachukua muda, chama hakina haraka. Tunachojua sisi ni kuwa tukilinganisha na tulikotoka tunajivuna kuwa chama kinapiga hatua"

Nilipomhoji Julius Mtatiro alisema yafuatayo: "Watanzania wanapenda propaganda, chama chetu hatukujiandaa kwa hilo na wala hatuamini hilo. Namba si tatizo kwa chama chetu, tutaendelea kuwaambia ukweli watanzania na tuna program nzuri inayokwenda hatua kwa hatua. Tumetatua mgogoro wa Zanzibar kwa amani, sasa nguvu yote tunaielekeza Tanzania bara. Utajionea mwenyewe matokeo ya uchaguzi ujao."

Hali ya vyama vya upinzani ni mbaya, kwani kama haitasikiliza matakwa ya watanzania kuna hatari kwa vyama hivyo kufa. Wakati ni huu, asiyesikia la mkuu huvunjika guu.

Crappppppppppppppppppppppppppppppppp.....................................Utafiti kufikirika. Ignore.
 
Niliwahi kusema zamani kuwa 54% ya watanzania mwaka 2010 hawakupiga kura. From 46% ya wapiga kura only 62% ya wapiga kura walikuwa wameipigia kura CCM na Chadema kilipata asilimia 27% huku CUF ikiwa ya tatu kikipata 8.3%.

Kama kuna chama kitaweza kutambua matatizo ya asilimia 54% ya watanzania ambao hawakupiga kura basi chama hicho kitaweza kuwaangusha CCM, Chadema, na CUF. Kwasababu hawa 54% wangelikuwa chama cha siasa basi sasa hivi tungelikuwa na serikali mbadala ya CCM.

Tafakari!!!


MDDJ

Swala liko wazi, sisi si wa kwanza kukumbwa na tatizo hili la watu kutopiga kura, after wota geti scandal USA lilitokea tatizo hili..sababu ni hizi

1. Machungu na majeraha ya raia wengi juu ya matatizo kama vile ufisadi kutochukuliwa hatua madhubuti, vidonda vyao vinakosa kuponywa

2. Vyama vya siasa (upinzani) kutofanya au kuishi yale wanayoyahubiri au kukemea

mwisho wa siku raia wanaona bora wasipige kura!!

hutapata sababu zingine..this is researched information
 
Kama wabunge wanafikiria hivyo nao wana makosa... tena makubwa sana. Wananchi hatuwezi kuwap[a ridhaa hiyo kwa sababu tunataka kuondoa mambo mengi ndani ya bunge letu. Kwa uchache tu utamaduni wa TAKRIMA iwe haramu, Posho za sitting Allowance ziwe marufuku. Mbunge ajulikane analipwa kiasi gani kwa mwaka na walipe kodi, Mbunge haruhusiwi kuwa waziri, mashangingi na fedha za mafuta na kadhalika hivyo tume tuitakayo sisi wananchi ni kuhakikisha wabunge pia wanabanwa.

Tume itaundwa sawa na mapendekezo ya rais au waziri wa sheria isipokuwa madaraka ya rais yatapungua tu mwanzo wa uratibu na mchakato wake lakini maamuzi ya kupitisha katiba hii ndipo wao na Marais wa pande mbili watakaa kusoma na kujadili vipengele vyote hasa ktk maswala ya Muungano. Lakini fikra za kusema rais au Wabunge ndio wachague tume wakati tunajua fika watalinda maslahi na nafasi zao halitakubalika...

Acha CDM waurudishe muswada Bungeni wakituwakilisha sisi leo hii, kisha sisi tuuchambue muswada tena naweza kabisa kutoa mawazo yangu hapa hapa JF kwa kuupitia muswada kama raia na mzalendo...

Nitakuwa pamoja na wewe hapa JF kujadili kuhusu katiba mungu akipenda, but mie nafikiri hakuna cha rais kukaa na kujadili mamlaka ya rais wala mamlaka ya bunge.

Ni jukumu la sote tulijadili kwa pamoja ili tukishakamilisha katiba tuwe na katiba inayokidhi mahitaji yote. Kuna msemo unasema umoja ni nguvu utengano udhaifu penye wengi hakuharibiki jambo. Marais wakikaa peke yao na kujadili mamlaka ya rais mie sikubaliani nalo kwani kama marais wote wakiwa mafisadi unafikiri watakubali bunge liwe na mamlaka ya kumng'oa rais madarakani? Nafikiri tujadili wananchi wote muswada huu ili tupate kitu kinachokidhi mahitaji kama wenzetu wakenya.
 
It is just a matter of time, all things will be in good order. Let us wait and see. Every body will enjoy the remain part of fruits of our country instead of being angry with their own county.
 
Nitakuwa pamoja na wewe hapa JF kujadili kuhusu katiba mungu akipenda, but mie nafikiri hakuna cha rais kukaa na kujadili mamlaka ya rais wala mamlaka ya bunge.

Ni jukumu la sote tulijadili kwa pamoja ili tukishakamilisha katiba tuwe na katiba inayokidhi mahitaji yote. Kuna msemo unasema umoja ni nguvu utengano udhaifu penye wengi hakuharibiki jambo. Marais wakikaa peke yao na kujadili mamlaka ya rais mie sikubaliani nalo kwani kama marais wote wakiwa mafisadi unafikiri watakubali bunge liwe na mamlaka ya kumng'oa rais madarakani? Nafikiri tujadili wananchi wote muswada huu ili tupate kitu kinachokidhi mahitaji kama wenzetu wakenya.
Inshaallah lakini kumbuka tu tukiwaachia wao wachague TUME tumekwisha..mamlaka yote yaliorodheshwa na waziri sehemu ya tatu hayana maslahi yako wewe wala mimi wala Mzanzibar na kama umesoma vizuri sharti la tume kutojadili RAIS na BARAZA KUU LA MAPINDUZI lina impact kubwa sana ktk wigo la kukusanya mawazo ya wananchi ktk ujenzi wa katiba mpya ambayo ndio mwongozo wa Utaifa wetu. Katiba siku zote inaanza kujadiliwa from top - bottom sasa kama hatuwezi gusa huko juu kweli tutakuwa tunajenga Uzalendo ama Udikteta. Matatizo yetu yote yanaanzia sehemu hizo mbili halafu ndio yanafuata maswala ya kiutawala.

Na nakuhakikishia ukiusoma muswada kwa makini JK kalinda sana nafasi ya urais na baraza la Mapinduzi ambalo ni CCM hata kabla ya kuchaguliwa tume.. WHY?
 
Mdondoaji said:
Mie naona hakuna bado chama cha kuongoza taifa hili kwani wote waliopo ni bunch of political opportunist. Hebu niambie kwanini tuwape nchi Chadema au CUF?

Mdondoaji,

..nadhani sasa hivi tunaumia kwasababu CCM wameshika serikali pamoja na bunge.

..sasa kama unadhani CDM au CUF r unworthy of ur trust kuongoza nchi hii, basi walau tungepunguza wingi wa wabunge wa CCM.

..tungekuwa na ahueni kubwa sana kama CCM wangekuwa na slim majority ndani ya bunge kuliko ilivyo sasa.

NB:

..kwa mtizamo wangu kuwa effective ndani ya bunge siyo lazima uwe na wasomi na lukuki.

..kinachotakiwa na "vichwa" vichache vizuri ambavyo vitaongoza wenzao, wengine ni kujazilia kura.
 
Zawadi Ngoda,
Nakusikitikia sana na utafiti wako usiokuwa na macho. Taznzania haijawahi kuwa na uchaguzi ulio huru na wa haki kwa sababu Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi ni mteuliwa wa Rais, wasimamizi wa uchaguzi ni Wakurugenzi wa Halmashauri ambao ni wateuliwa wa Rais! Wewe unategemea nini kwenye mazingira haya?
Hilo la udini na ukabila ni matunda yaliyotokana na mbegu mbaya inayoenezwa na CCM! Hakuna chama chochote cha upinzani kinachopanda mbegu mbaya ya udini na ukabila, ni CCM tu ndio kinara! Wewe kwa akili yako finyu kwa nini hujiulizi Msajili wa Vyama vya Siasa havifuti "vyama vya udini na ukabila" kwa mujibu wa Sheria ya Vyama vya Siasa, 1992? Ni CCM tu ndio yenye "macho" ya kuona udini na ukabila uliopo kwenye vyama vya upinzani? Hizo propaganda haziendelezi nchi yetu hata hiyo CCM unayoifagilia haitafika mbali kwa mtaji huo!

Yawezekana hakujakuwepo na uchaguzi huru na wa haki, lakini katika chaguzi zote ule wa mwaka 2010 ulisifiwa na mataifa mengi pamoja na taasisi. Hata wenyewe tulishuhudia kwa wagombea wote kupewa nafasi sawa katika vyombo vya habari ikiwepo pamoja na TV na magazeti. Hii ilikuwa tosha kwa vyama hivyo kueleza kwa kina kwa nini wao ni bora kuliko CCM. Hawakufanikiwa kuwashawishi watanzania kutokana na udhaifu mkubwa wa Vyama hivyo.

Kusajiliwa kwa chama ni rahisi zaidi kuliko kuaminiwa kwa chama na wananchi. Hapa ni muhimu unifahamu vizuri sana.
Ili usajiliwe wahitaji maandishi tu ya katiba yako tu yatayoendana na masharti ya uundaji wa vyama vya siasa. Unapofika kwa watanzania swali ni kubwa sana. Private life ya mgombea tu, au personality yake inaweza kumpandisha au kumuangusha. Ni nini alijishughulisha mgombea kabla ya kuingia siasa, inaweza kuwa ni suala kubwa sana kwa mpiga kura. Au hata Elimu yako. Kifupi kumshawishi mpiga kura akuamini ni ngumu zaidi kuliko kumshawishi Tendwa akusajili.

Kwa mfano, uchaguzi wa 2010 kuna vyama vilishutumiwa hadharani kuhusika na udini na wala haikuwa siri. Kwa mpiga kura si muhimu kwake sheria ya usajili wa vyama kuwa kisiwe cha kidini, la msingi kwa mpiga kura ni jinsi utavyomueleza kuwa ushahidi uliotolewa kuwa chama chako ni cha kidini ni uongo. Hapo ndio vyama vingi vimeshindwa.

Unajua, ukimuweka Sheikh PONDA kuwa kiongozi wa chama cha siasa, ni rahisi sana kwa mtu yeyote akatia sumu kuwa chama chako kinanukia udini na watanzania wataamini hayo kutokana na uhusiano wa Sheikh Ponda na msimamo wake katika dini. Nafikiri utanielewa.
 
Watanzania wana uchu mkubwa wa kuiona CCM inahama IKULU, na kukipisha chama kingine kuingia Ikulu. Haya ni majibu ya utafiti wa kile kikundi chetu binafsi "SONGAMBELE" amabacho kina wanachama na wataalam wake toka vyuo vikuu mbali mbali Tanzania.

Aidha katika taarifa hiyo imeonyesha kuwa 70% kati ya watanzania walioshiriki katika utafiti huo ( 1 milioni) wanahitaji chama kingine zaidi ya CCM Kuingia Ikulu. Lakini walipoulizwa ni chama gani kati ya vyama pinzani walipenda kukiona kinaingia Ikulu, 65% walijibu "hakuna". Hii inaonyesha wazi jinsi vyama vya upinzani vilivyowakatisha tamaa watanzania toka katika ndoto yao ya kukiona chama cha upinzani kuingia ikulu.

Nilipomhoji Prof Safari kuhusu matokeo hayo alisema yafuatayo "Sishangazwi wala kushitushwa na taarifa hiyo, angalia kampeni zao ni za kubabaisha tu, hakuna chama kinachokidhi matakwa ya wananchi. Hakuna chama cha upinzani katika vyama vikuu kilichoweza kuonyesha kuliweka wazi swala la umoja wa kitaifa. Vyama hivi aidha vimelaumiwa kwa kuendekeza ukabila au udini, na wameshindwa kujibu tuhuma hizo kwa kiwango ambacho watanzania watawaelewa. Kuwa na viongozi wa vyama ambao walishiriki au wanashiriki katika nyadhifa za taasisi za kidini ni kosa kubwa kwa kipindi hiki, watanzania hawako tayari kwa hilo japokuwa kisheria inakubalika."

Katika utafiti huo CHADEMA iliongoza kati ya vyama pinzani kuingia IKULU kwa kuwa na 16% ikifuatiwa na CUF 14%. Cha kushangaza hata maeneo yale ambayo huhesabika kama ngome yaCHADEMA, ilifanya vibaya. Kwa mfano Arusha ni 35% na Moshi 40% tu ndio waliohitaji kuiona CHADEMA yaingia IKULU. Kwa Arusha wengi walikatishwa tamaa na viongozi wao hasa kwa tukio la hivi karibuni la kuwapeleka wanachama kuandamana bila mipango maalum.

Mh Slaa nilipompigia simu alikataa kusema lolote na kukata simu. Mh Zitto Kabwe, alicheka na kusema "sina uhakika kama hizo namba zinawakilisha hali halisi. Hata hivyo kuwaeleza watu mpaka wakuelewe inachukua muda, chama hakina haraka. Tunachojua sisi ni kuwa tukilinganisha na tulikotoka tunajivuna kuwa chama kinapiga hatua"

Nilipomhoji Julius Mtatiro alisema yafuatayo: "Watanzania wanapenda propaganda, chama chetu hatukujiandaa kwa hilo na wala hatuamini hilo. Namba si tatizo kwa chama chetu, tutaendelea kuwaambia ukweli watanzania na tuna program nzuri inayokwenda hatua kwa hatua. Tumetatua mgogoro wa Zanzibar kwa amani, sasa nguvu yote tunaielekeza Tanzania bara. Utajionea mwenyewe matokeo ya uchaguzi ujao."

Hali ya vyama vya upinzani ni mbaya, kwani kama haitasikiliza matakwa ya watanzania kuna hatari kwa vyama hivyo kufa. Wakati ni huu, asiyesikia la mkuu huvunjika guu.
Takwimu hizi zilikusanywa kwa muda gani na katika mikoa ipi ya Tanzania na idadi ya walioshiriki katika research hii ni ipi. Pia usisahau kwamba Kikwete alishindwa katika uchaguzi wa 2010 lakini Magamba ikabidi wachakachue uchaguzi kwa kutumia tume ya uchaguzi wa magamba na vyombo vya dola. Halafu hizi takwimu ni bomu kabisa eti CHADEMA wanakubalika kwa 16% na CUF wanakubalika kwa 14%!!!! Kipande yetu ya Tanganyika, CUF hata siku moja haiwezi kula sahani moja na CHADEMA na hiyo siyo siri.

:peace::peace::peace::peace::peace:
 
Just imagine kuwa kuna chama kimekaa kikao na kumpendekeza Freeman Aikaeli Mbowe awe rais wa Tanzania ......... are you serious? Kwa lipi ambalo litamfanya mtanzania yeyote amchague yeye kuwa rais? hata jimboni kwake kashinda kwa asilimia chache sana.
Upinzani umedoda!!
 
Takwimu hizi zilikusanywa kwa muda gani na katika mikoa ipi ya Tanzania na idadi ya walioshiriki katika research hii ni ipi. Pia usisahau kwamba Kikwete alishindwa katika uchaguzi wa 2010 lakini Magamba ikabidi wachakachue uchaguzi kwa kutumia tume ya uchaguzi wa magamba na vyombo vya dola. Halafu hizi takwimu ni bomu kabisa eti CHADEMA wanakubalika kwa 16% na CUF wanakubalika kwa 14%!!!! Kipande yetu ya Tanganyika, CUF hata siku moja haiwezi kula sahani moja na CHADEMA na hiyo siyo siri.

:peace::peace::peace::peace::peace:
Na sisi tunataka ushahidi hapo kwenye nyekundu. Kama huna ushahidi ..... you know the rest!
 
Shukran mkuu wangu yaani Wadanganyika kusema kweli sijui tuko kundi gani la binadamu... Nchi za Ulaya tajiri kama JK au Pinda na hana madeni angefuatiliwa zaidi ya Mbowe ambaye anadaiwa na Utajiri wake unaonyesha wapi kapata mtaji wa utajiri wake. lakini kwetu kinyume kabisa kutokana na mila na desturi za mtu kuiba halali kama hatakamatwa..

Matajiri wengi Tanzania ni wezi na wameupata utajiri huo kwa dhulma lakini maadam hatuna kesi mahakamani hawa ni wasafi isipokuwa yule anayedaiwa na inajulikana anadaiwa ndiye mbaya. Kesho Mbowe akiondoka duniani (mwenyezi Mungu apitishie mbali) tutaweza kukamata mali zake kurudisha deni letu lakini hao waloiba na kuhalalisha mali za wizi tutawakamata vipi??

Aaaaah turudi kwenye mjadala nawasoma kisha nitakuja changia mada inapopaswa..

Jamani tuacheni dhana kuwa kama JK ana makosa basi makosa ya MBOWE nayo ni halali. Matamko haya nayasikia mara nyingi sana hapa JF, huwa nasikitishwa sana. Na ndio hapo kwenye tatizo, kwa sababu kwa mtanzania haoni sababu kwa nini amtoe mwizi na kumuweka mwizi, si ni bora kumuachia mwizi huyu niliyemzoea aendelee.

Kifupi hayo ndiyo mawazo ya mtanzani kama methali isemavyo "Zimwi likujualo halikuli likakwisha". Mtanzania matakwa yake ni kupata chama safi, chenye viongozi safi na chenye kudumisha amani ikiwa pamoja na umoja wa kitaifa. Hivyo vyama vya uupinzani vya kisiasa ni lazima viqwe safi.
 
Back
Top Bottom