Zawadi Ngoda
JF-Expert Member
- Aug 13, 2009
- 3,796
- 1,849
Watanzania wana uchu mkubwa wa kuiona CCM inahama IKULU, na kukipisha chama kingine kuingia Ikulu. Haya ni majibu ya utafiti wa kile kikundi chetu binafsi "SONGAMBELE" amabacho kina wanachama na wataalam wake toka vyuo vikuu mbali mbali Tanzania.
Aidha katika taarifa hiyo imeonyesha kuwa 70% kati ya watanzania walioshiriki katika utafiti huo ( 1 milioni) wanahitaji chama kingine zaidi ya CCM Kuingia Ikulu. Lakini walipoulizwa ni chama gani kati ya vyama pinzani walipenda kukiona kinaingia Ikulu, 65% walijibu "hakuna". Hii inaonyesha wazi jinsi vyama vya upinzani vilivyowakatisha tamaa watanzania toka katika ndoto yao ya kukiona chama cha upinzani kuingia ikulu.
Nilipomhoji Prof Safari kuhusu matokeo hayo alisema yafuatayo "Sishangazwi wala kushitushwa na taarifa hiyo, angalia kampeni zao ni za kubabaisha tu, hakuna chama kinachokidhi matakwa ya wananchi. Hakuna chama cha upinzani katika vyama vikuu kilichoweza kuonyesha kuliweka wazi swala la umoja wa kitaifa. Vyama hivi aidha vimelaumiwa kwa kuendekeza ukabila au udini, na wameshindwa kujibu tuhuma hizo kwa kiwango ambacho watanzania watawaelewa. Kuwa na viongozi wa vyama ambao walishiriki au wanashiriki katika nyadhifa za taasisi za kidini ni kosa kubwa kwa kipindi hiki, watanzania hawako tayari kwa hilo japokuwa kisheria inakubalika."
Katika utafiti huo CHADEMA iliongoza kati ya vyama pinzani kuingia IKULU kwa kuwa na 16% ikifuatiwa na CUF 14%. Cha kushangaza hata maeneo yale ambayo huhesabika kama ngome yaCHADEMA, ilifanya vibaya. Kwa mfano Arusha ni 35% na Moshi 40% tu ndio waliohitaji kuiona CHADEMA yaingia IKULU. Kwa Arusha wengi walikatishwa tamaa na viongozi wao hasa kwa tukio la hivi karibuni la kuwapeleka wanachama kuandamana bila mipango maalum.
Mh Slaa nilipompigia simu alikataa kusema lolote na kukata simu. Mh Zitto Kabwe, alicheka na kusema "sina uhakika kama hizo namba zinawakilisha hali halisi. Hata hivyo kuwaeleza watu mpaka wakuelewe inachukua muda, chama hakina haraka. Tunachojua sisi ni kuwa tukilinganisha na tulikotoka tunajivuna kuwa chama kinapiga hatua"
Nilipomhoji Julius Mtatiro alisema yafuatayo: "Watanzania wanapenda propaganda, chama chetu hatukujiandaa kwa hilo na wala hatuamini hilo. Namba si tatizo kwa chama chetu, tutaendelea kuwaambia ukweli watanzania na tuna program nzuri inayokwenda hatua kwa hatua. Tumetatua mgogoro wa Zanzibar kwa amani, sasa nguvu yote tunaielekeza Tanzania bara. Utajionea mwenyewe matokeo ya uchaguzi ujao."
Hali ya vyama vya upinzani ni mbaya, kwani kama haitasikiliza matakwa ya watanzania kuna hatari kwa vyama hivyo kufa. Wakati ni huu, asiyesikia la mkuu huvunjika guu.
Aidha katika taarifa hiyo imeonyesha kuwa 70% kati ya watanzania walioshiriki katika utafiti huo ( 1 milioni) wanahitaji chama kingine zaidi ya CCM Kuingia Ikulu. Lakini walipoulizwa ni chama gani kati ya vyama pinzani walipenda kukiona kinaingia Ikulu, 65% walijibu "hakuna". Hii inaonyesha wazi jinsi vyama vya upinzani vilivyowakatisha tamaa watanzania toka katika ndoto yao ya kukiona chama cha upinzani kuingia ikulu.
Nilipomhoji Prof Safari kuhusu matokeo hayo alisema yafuatayo "Sishangazwi wala kushitushwa na taarifa hiyo, angalia kampeni zao ni za kubabaisha tu, hakuna chama kinachokidhi matakwa ya wananchi. Hakuna chama cha upinzani katika vyama vikuu kilichoweza kuonyesha kuliweka wazi swala la umoja wa kitaifa. Vyama hivi aidha vimelaumiwa kwa kuendekeza ukabila au udini, na wameshindwa kujibu tuhuma hizo kwa kiwango ambacho watanzania watawaelewa. Kuwa na viongozi wa vyama ambao walishiriki au wanashiriki katika nyadhifa za taasisi za kidini ni kosa kubwa kwa kipindi hiki, watanzania hawako tayari kwa hilo japokuwa kisheria inakubalika."
Katika utafiti huo CHADEMA iliongoza kati ya vyama pinzani kuingia IKULU kwa kuwa na 16% ikifuatiwa na CUF 14%. Cha kushangaza hata maeneo yale ambayo huhesabika kama ngome yaCHADEMA, ilifanya vibaya. Kwa mfano Arusha ni 35% na Moshi 40% tu ndio waliohitaji kuiona CHADEMA yaingia IKULU. Kwa Arusha wengi walikatishwa tamaa na viongozi wao hasa kwa tukio la hivi karibuni la kuwapeleka wanachama kuandamana bila mipango maalum.
Mh Slaa nilipompigia simu alikataa kusema lolote na kukata simu. Mh Zitto Kabwe, alicheka na kusema "sina uhakika kama hizo namba zinawakilisha hali halisi. Hata hivyo kuwaeleza watu mpaka wakuelewe inachukua muda, chama hakina haraka. Tunachojua sisi ni kuwa tukilinganisha na tulikotoka tunajivuna kuwa chama kinapiga hatua"
Nilipomhoji Julius Mtatiro alisema yafuatayo: "Watanzania wanapenda propaganda, chama chetu hatukujiandaa kwa hilo na wala hatuamini hilo. Namba si tatizo kwa chama chetu, tutaendelea kuwaambia ukweli watanzania na tuna program nzuri inayokwenda hatua kwa hatua. Tumetatua mgogoro wa Zanzibar kwa amani, sasa nguvu yote tunaielekeza Tanzania bara. Utajionea mwenyewe matokeo ya uchaguzi ujao."
Hali ya vyama vya upinzani ni mbaya, kwani kama haitasikiliza matakwa ya watanzania kuna hatari kwa vyama hivyo kufa. Wakati ni huu, asiyesikia la mkuu huvunjika guu.