Jumakidogo
R I P
- Jul 16, 2009
- 1,851
- 417
Ukiwa unafuga paka nyumbani kwako jaribu kumchunguza. Ukiona paka wako hakamati panya akiwaona anakimbia mpeleke kwa wataalamu wa tabia za wanyama. Inawezekana huyo siyo paka bali ni mnyama mwingine anaye fanana na paka. Basi! Inabidi umfukuze nyumbani kwako kwa sababu hana faida tena. Ukimuacha labda utakuwa umeamua awe paka wa urembo. Panya wanateketeza hazina ya mwenye nyumba ambaye ni paka, lakini anashindwa hata kuwatisha tu hao panya. Mpaka paka wadogo wadogo wapige kelele kule kwenye jumba lao kuu la mikutano. Aina hii ya paka hata akishikiwa panya hatamla. Maana amebadilika na kuiga tabia za paka wa kizungu. Nimejaribu kuweka fumbo ili MODS msije mkaifyekelea mbali japo ni nyepesi tu.