rennychiwa
Member
- Oct 14, 2010
- 13
- 1
Ndugu zangu wanajamiiforum, naomba mnikaribishe rasmi kuwa mwanachama mpya. Nimeamua kujiunga nanyi katika kutoa michango ya kimawazo kwa Taifa letu. Na ninawapongeza sana wale wote walioanzisha tovuti hii.
Ni kwa muda mrefu sana tumeishi kwa upofu, bila ya kujitambua na wakati mwingine tulifanywa vipofu kwa manufaa ya wachache. CCM imetuziba macho kwa muda mrefu, huku hali ya maisha ya mtu wa chini ikiendelea kudidimia. Chama tawala kimeshindwa kujipanga katika kuinua uchumi wa Taifa letu, wamejipanga kulinda maslai yao binafsi wakasahau umoja wetu wa kitaifa. Wameua viwanda walivyoachiwa na Baba wa Taifa, Kilimo kimebaki kuwa siasa majukwaani, madini leo hii hata mtoto mdogo amegundua kwamba si ya kwetu tena, huduma za afya kwa mtu maskini imekuwa ndoto.
Leo hii watanzania waliokuwa wanaitwa wadanganyika wamekula tunda wamegundua miaka yote ya utawala wa CCM walikuwa wanatembezwa uchi sasa wanakimbilia nguo, CCM haitaki wavae nguo wanafunika nyeti zao kujisitiri na aibu. Sasa wanadai kuvalishwa nguo. Wanataka kujua nchi yao inakwenda imetoka wapi, inakwenda wapi na kwa nini?
Tunaitaji uwiano wa wabunge, tunaitaji katiba mpya tunaitaji Rais mpya mwenye fikra mbadala na tunaitaji chama kipya. Tunataka tuwe na udhubuti wa kusema HAPANA miaka yako mitano uliaidi A,B na C hujatekeleza hata moja, Nenda zako. Ndani ya miaka mitano tuwapime, ndani ya miaka mitano tuwaangushe kama hakuna walilofanya kwa maslai ya Taifa letu.
Nina kila sababu ya kukiunga mkono CHADEMA.
Tujitokeze kwa wengi, tuwapigie kura. Huu ndio wakati wetu wa kufanya maamuzi sahihi.
Kura yako ina nguvu zaidi ya Risasi.
Ni kwa muda mrefu sana tumeishi kwa upofu, bila ya kujitambua na wakati mwingine tulifanywa vipofu kwa manufaa ya wachache. CCM imetuziba macho kwa muda mrefu, huku hali ya maisha ya mtu wa chini ikiendelea kudidimia. Chama tawala kimeshindwa kujipanga katika kuinua uchumi wa Taifa letu, wamejipanga kulinda maslai yao binafsi wakasahau umoja wetu wa kitaifa. Wameua viwanda walivyoachiwa na Baba wa Taifa, Kilimo kimebaki kuwa siasa majukwaani, madini leo hii hata mtoto mdogo amegundua kwamba si ya kwetu tena, huduma za afya kwa mtu maskini imekuwa ndoto.
Leo hii watanzania waliokuwa wanaitwa wadanganyika wamekula tunda wamegundua miaka yote ya utawala wa CCM walikuwa wanatembezwa uchi sasa wanakimbilia nguo, CCM haitaki wavae nguo wanafunika nyeti zao kujisitiri na aibu. Sasa wanadai kuvalishwa nguo. Wanataka kujua nchi yao inakwenda imetoka wapi, inakwenda wapi na kwa nini?
Tunaitaji uwiano wa wabunge, tunaitaji katiba mpya tunaitaji Rais mpya mwenye fikra mbadala na tunaitaji chama kipya. Tunataka tuwe na udhubuti wa kusema HAPANA miaka yako mitano uliaidi A,B na C hujatekeleza hata moja, Nenda zako. Ndani ya miaka mitano tuwapime, ndani ya miaka mitano tuwaangushe kama hakuna walilofanya kwa maslai ya Taifa letu.
Nina kila sababu ya kukiunga mkono CHADEMA.
Tujitokeze kwa wengi, tuwapigie kura. Huu ndio wakati wetu wa kufanya maamuzi sahihi.
Kura yako ina nguvu zaidi ya Risasi.