Watanzania na Ubaguzi Wa Ujinga!

Cha kushangaza ni pale kila unapozunguka mbuyu unarudi kuainisha kuwa tuna Ubaguzi wa Ujinga. Kwanini iwe Mwaarabu au Mzungu au Mhindi? au yeyote yule? kwanini isiwe Mwaafrika? iwe kwa jina lolote liwalo, kama ni kigezo tu cha kujuwana kuwa huyu ni Zomba yule ni Mkandara. Kwanini iwe hivyo?

Kwanini siwasikii wasomi waliosomeshwa hizo shule za kujazwa ujinga zikifundisha kuwa Mwaafrika (au jina lolote alilokuwa nalo kabla ya kupachikwa huo Uafriti) ndio alikuwa mtawala wa mwanzo huko bara la Asia? kama ni hivyo, ni wapi niliposoma mimi kuwa Mwaafrika aliitawala Asia? or is it Arabia? siamini kama kulikuwa kuna nchi inaitwa au inajiita Arabia kabla ya mwaka 1932. Jee, wewe hujui kuwa kuna Mwaafrika alitawala Asia kabla ya Waalimu wako kukufundisha kuwa Waarabu na Wazungu walikutawala? Jee, hao Waalimu wako walipokufundisha ujio wa Vasco Da Gama walikufundisha walikuta utawala upi pale Kilwa na Sofala? Jee, kuna uhusiano wowote na Utawala wa Kiafrika uliotawala mpaka Asia?

Raptha iko wapi?

Jiulize kisha ujaribu kueleza Ubaguzi wa Ujinga. Umeugusia mwisho mwisho wa makala yako, Jee, hiyo ndio elimu tuliyopewa? ya kujazwa ujinga? hatukufundushwa nidhamu? nataka kuamini hivyo ndivyo ilivyo lakini sikubali kuwa ni ujinga wa kuwa ni wajinga naamini ni Ubaguzi wa Ujinga.
Mkuu wangu hata kwa kujumuisha Muhindi, mwarabu na mzungu huo sio UBAGUZI ila zote hizi ni karama za mwenyezi Mungu ktk kutuwezesha sisi kutambuana toka ktk tafauti hizi..Hatukuumbwa kwa tofauti zetu isipokuwa kwa sababu ya kutuwezesha sisi kutambuana, kutofautisha baina ya Zomba na Mkandara, Zomba huyu na Zomba Mwarabu, mhindi au mzungu mana leo tuko billioni ngapi?. Kama sisi sote tungekuwa sura moja, rangi moja kama Wachina nani angeweza kukutofautisha Zomba wangu na Mkandara?.

Pili, Swala Africa sielewi wewe umelipata wapi lakini nijuavyo miye majina hata ya nchi hatakuanza juzi bali karne na karne wala sii kutoka sehemu moja. Mkuu wangu hakuna watu walostaarabika na kuwa kutangulia ELIMU kama Wamisri. Historia zote za Biblia na Quran zinatuonyesha ustaarabu wa Wamisri toka karne na karne.. na pengine wao ndio watu wa kwanza kujua kuandika.Na kwa lugha yao neno MOTHERLAND linatamkwa AFRI-UKA, hiki sii kiarabu bali Kimisri, na ndio asili na jina la bara letu, kama unabisha google. Na unaweza kurudi nyuma zaid hata ktk hadith za mitume utamkuta malikia Sheba alokwenda Uyahudi na kuolewa na Suleiman alijulikana kama Queen of Ophiria hiyo tunazungumzia mwaka 950 BC.. Sasa haya ya AFRIT hata sielewi yametokana wapi ikiwa hao waarabu (badui) wenyewe Ustaarabu wameletewa na Mtume..

Hakuna watu walokuwa nyuma na washenzi kama waarabu na sijui kama unaelewa kwa nini waliitwa Badui, na hata mtume kuteremshwa kwao Mwenyezi Mungu alikuwa na sababu kubwa sana maana ktk watu waloshushiwa mitume wao na Wayahudi ni kama vile walokuwa wamelaaniwa, tazama Sodoma na Gomola, hawa watu waliwatongoza hata malaika,sasa leo huwezi nambia huu ni ubaguzi ilihali hulka zao ndizo zilowatambulisha wao kuwa walivyo.

Halafu haya maswala ya Sofala na Kilwa sielewi yanahusu nini? hawa wote kina Vasco dagama, Speke, Livingston, Carl Steve na Masultan wote walikuwa explorer walokuwa wakisaka utajiri kutokana na historia ama hadithi za vitabu..Walikuja Afrika wakitaka kutafuta machimbo ya mfalme Suleiman na hivyo haituhusu sisi wanapoweka majina ya miji yetu ama ramani kwa sababu hayo majina ilikuwa ni ktk kumsaidia yeye kuzitambua nchi zetu kwa mipaka na ramani yake ili kesho akija mtu mwingine atajua pa kafika wapi na anaelekea wapi..

Mkuu wangu si unaelewa wazi ya kwamba Chrstopher Columbus alipofika ghuba ya Marekani, yeye katika fikra zake alifikiri amefika India? na akaiita nchi hiyo Amerika wakati yuko upande mwingine kabisaa wadunia. Hivyo yasikupe homa wewe haya majina swala kubwa ni wewe unajitambua vipi na uko wapi. Hivyo ikiwa wewe mwenyewe hujitambui upo wapi, umetoka wapi na unakwenda wapi, then You got a problem! lakini haya wanayotusema ama kutuita majina hayana maana yoyote na tuyapuuze...

Nachosema tu ni kwamba sisi tumepewa elimu ili tuendelee kuwa wajinga, na ndio maana tunarudi sana kutaka kujua Historia ya kina Vasco dagama kiuhusu Kilwa na Sofala badala ya kujifunza kuhusu nchi iloitwa Azania kiina Abushir, Mkwawa, Mirambo na wafalme wetu ambao leo walitakiwa kuwa sehemu ya makumbusho yetu badala ya wapanda milima ya Kilimanjaro..I mean sikuelewi na nitaendelea kuuliza haswa nini lengo la mada hii ikiwa sisi wote wajinga na wenye ubaguzi wa kijinga kutokana na Ujinga tulokuwa nao kama haitakuwa muendelezo wa Ujinga ule ule.
 
zomba mwarabu si lugha ndugu yangu mwarabu ni aina ya watu huko iraq kuna watu weusi wanaongea kiswahili mbona hawaitwi waarabu basi au hata waarabu weusi mbona hawaruhusiwi hadi leo kuoa binti za kiarabu mbona wanatengwa wanasemwa wao siyo waarabu sasa uarabu wako wewe wa kuwa mweusi wa tangu lini??huko qatar ukienda hata ukiongea kiarabu na rangi yako hiyo nyeusi utaitwa mwafrika tu. sasa kama waarabu wenyewe wanaweza kukubagua na kukusema kuwa wewe siyo mwenzao we utajilazimishaje kuwa wao.jua kabisa niwa hawezi kuruka katika kundi la kunguru hata akiwa mweusi namna gani. elewa mdogo wangu.
Unapoteza muda wako bure, hata kama unampenda saaaana huyu unayemwita "mdogo wako", ZOMBA ukifikiri unaweza kumwelimisha, ni vyema ujihurumia na kutunza hizo nguvu zako ukazitumie kwingine watakako kushukuru ukifanya hivyo. Ukiisha kuona mtu, katika dunia ya leo, ambaye anatumia muda kukuonesha kuwa yeye ni bora kitabaka kwakuwa tu ana uhusiana wa namna fulani (uwe wa kweli au wa kulazimisha) na mtu au watu wa tabaka au dini fulani, na wala si kwa uwezo wake unaoonekana waziwazi kamba vile mchango wake katika maendeleo ya kitekinologia au kisayansi, au jambo lolote linalowezesha dunia kuwa mahali bora zaidi pa kuishi, mtu huyo ni wa kumuepuka kabisaaa. Utamgundua kwa njia moja RAHISI SANA. Atatumia historia ya namna gani huyo bwana wake anayemsujudia aliwahi kuwa na uwezo gani hapo zamani. Hajishughulishi hata kidogo kutambua kwamba, laiti huyo bwana wake angelikuwa kweli na akili au nguvu, yeye asingelikuwa hana maendeleo. Haelewi kuwa watu wenye nguvu hawatetewi, kwani hakuna haja hiyo.
 
Asante ndugu zomba kwa maelezo yako. Mi nadhani hapo kwenye ishu Africa uwa hakuna mjadala hata kwa kutazama nakuelewa historia ya kawaida tu utaona Africa haibebi hasa maana halisi ya majority ya wakaazi wa Bara hili la pili kwa ukubwa duniani.
Ebu tuone, kwa uelewa wangu neno Afrika lina derive kutoka neno Afrit japo ukueleza maana yake sasa mimi "ujinga" niliojazwa ni kuwa Afri ni jina la Kilatini lililotumika kutambulisha Carthaginians (watu wenye chimbuko/asili Afrika Kaskazini ambako kwenye eneo ambalo sasa linatambulika kama Tunisia. Hili jina Afri lina uhusiano na Phoenician (lugha ya pwani ya Mediterrania katika sehemu iliyojulikana nyakati hizo kama Kaanani) Sasa kwa lugha hiyo ya Phoenician neno Afri lilimaanisha vumbi (dirt) lakini hypothesis ya mwaka 1981 ili assert ya kwamba hili neno Afri lina sterm kutoka neno la lugha ya kiberber (lugha ya Morroco/North Africa) Ifri au Ifran lenye maana ya mapango ikiwa ni reference ya watu wa mapangoni.
Chini ya Utawala wa Roma Carthage ikaja kuwa Capital ya jimbo la Afrika ambayo pia ilijumuisha pwani ya eneo linalojulikana sasa kama Libya.
Suffix ya Kilatini "ica" wakati mwingine inaweza kutumika kuashiria ardhi mfano Celtica kutoka Celtes. Kwahiyo utaona jinsi neno Africa lilivyokuja na ilikuwa inarefer watu gani.
Ufalme wa Kiislamu wa Ifriqiya (kwa sasa Tunisia) uliendeleza kutunza form ya jina hilo.
Sasa question is, ubaguzi wa ujinga according to you unamweka wapi Mwarabu na Mzungu katika Bara hili la "Waafrika" weusi?
Pia asante Elizabeth kwa kujibu vizuri unaonyesha uelewa mzuri hayo uliyosema hebu tuyaunganishe na haya Africa lilitokana na maneno mawili yaani "Phoenician words: AFAR, meaning "Dust" and RAYK, meaning "empty," the words were tied to form the word AFAR-RAYK-A. later a Latin suffix was added to form the word AFRICA.... The Phoenicians established outposts in what is now Tunisia, formerly Carthage, where the inhabitants spoke the Punic language, a derivative of Phoenician.http://wiki.answers.com
 
Pia asante Elizabeth kwa kujibu vizuri unaonyesha uelewa mzuri hayo uliyosema hebu tuyaunganishe na haya Africa lilitokana na maneno mawili yaani "Phoenician words: AFAR, meaning "Dust" and RAYK, meaning "empty," the words were tied to form the word AFAR-RAYK-A. later a Latin suffix was added to form the word AFRICA.... The Phoenicians established outposts in what is now Tunisia, formerly Carthage, where the inhabitants spoke the Punic language, a derivative of Phoenician.http://wiki.answers.com
Eliza na wengine, kwa mtindo huu wa mzamifu na Zombakutumia Answer.com!!! sina haja ya kuona mtoa mada, aki google, answer.com, anaona ndo ukweli......tahadhari kubwa inatakiwa kwenye mambo haya ya kihistoria jamani. kama huo ndo ujinga wetu waTz, mimi niwe wa kwanza au mwisho nafasi nipe wewe!!! mu kichwa wewe ndo JINGA langu.
Note... Kuna wachangiaji wamesema wewe hata kama vinywele vyako vya ki Farid bado ukienda huko.... utakuwa si wao!!!!
Haya matatizo ya google, na answer.com!!! huna vyanzo vingine?????
 
Naamini na nnadiriki kuandika kuwa Watanzania ni wabaguzi, ubaguzi wao si wa kidini au wa kijinsia au wa kikabila au wa rangi. Hizo ndio njia kuu zijulikanazo za ubaguzi duniani.

Watanzania, wengi wao, hawana kabisa ubaguzi huo. Ubaguzi wa Watanzania ni wakijinga au wa ujinga. Naamini kabisa kuwa ubaguzi wa Watanzania ni wa ujinga zaidi ya wakijinga. Ujinga hawana ila wana ubaguzi wa ujinga.

Ikiwa Watanzania hawana ujinga, huu ubaguzi wa ujinga wameutowa wapi? nna uhakika kuwa huu ubaguzi wamepachikwa na Waalimu wao na Waalimu wao walipachikwa na Waalimu wao na hao Waalimu wao walipachikwa huu ujinga walipojengewa mashule na kusomeshwa na kufundishwa cha kuja kuwafundisha hao waliotarajiwa kuwa ndio watakuja kufundisha, matokeo wamewajaza Watanzania ubaguzi wa ujinga.

Mara kadhaa humu JF nimekuwa nikitumia sentensi "uneducated fool from an uneducated school", nna uhakika wanaonisoma humu JF wameshaisoma sentensi hiyo, si mara moja wala mbili, wako walioielewa wakakaa kimya na wako walioielewa wakashindwa kuielewa na wakaanza kung'aka kuwa hilo si neno la kueleweka. Sina haja ya kulielewesha kwani, muelewa huelewa haeleweshwi. Asiyeelewa hutaka kuelewa na huuliza ili aelewe wala hataharuki na kujifanya anajuwa asichokijuwa, moja ya ubaguzi wa ujinga.

Ubaguzi mwengine wa ujinga tuliokuwa nao na uliojazwa vichwani mwa wengi ni kuwa Vasco Da Gama ndio kaivumbuwa hii Tanzania au Tanganyika wakati ukweli ni kuwa wakati wa Vasco Da Gama jina Tanzania halikuwepo wala Tanganyika halikuwepo. Kuna anaelipinga hili? Anza.

Isitoshe, Vasco Da Gama hajawahi kuikanyaga ardhi ya nchi hii, ambayo leo inaitwa Tanzania (jina aliloipa Muhindi wa Tanga). Vasco Da Gama aliishia baharini alipotia nanga manuwari zake, hajashuka wala kuigusa hii ardhi ambayo wengi wanajazwa ujinga wa kusema kuwa Vasco Da Gama ndio mvumbuzi. Swali la kujiuliza, Jee, Vasco Da Gama alivumbuwa kipi? alimkuta nani hapo Kilwa? (Naomba wajuzi wanipe maana ya neno "Kilwa") labda hilo ni neno la Kireno? kwa kuwa umeaminishwa kuwa Vasco Da Gama kapavumbuwa? au maana ya jina (au neno) Sofala, zilipotuwa kwanza manowari zake, ambako alipewa nahodha kipofu akamuongoza hadi Kilwa. Ndio kipofu. Ni ajabu lakini kweli.

Jee, hayo mmeyasoma huko mnakojazwa ujinga? Ni wangapi leo hii wanaojuwa kuwa hapa katika Ardhi hii kulikuwa kuna mji, kama si nchi, inayoitwa Raptha? Hii Raptha iko wapi? ilianza lini na nani walikuwa Watawala? na imeshia wapi? Maweee!

Nani leo hii anaejuwa kuwa Majimaji ilikuwa ni vita isiyokubalika na wengi leo hii?

Nani anaejuwa kuwa Mkwawa alikuwa anaandika Kiarabu, japo kuandikiwa?

Nani leo hii anaekiri kuwa nchi hii ina mbegu na si shina au tawi tu la Uarabu, la hasha, si nchi hii, Kontinenti hili? Nakuhakikishia hakuna. Kwanini hakuna? ni Ubaguzi wa ujinga.

"Afrika" ni lugha gani, au neno? tuseme jina hilo? vyovyote, iwavyo na iwe, limetokana na lugha gani uijuwayo wewe? zaidi ya neno au jina "Afrit"? kama huna zaidi ya hapo basi ujuwe umejazwa ujinga.

Dar Es Salaam. ni lugha ipi na neno hilo linatoka wapi? anaekuambia ni "Bandari Salama" basi huyo kakujaza ujinga kwani si maana yake ya ukweli.

Arusha, unajuwa maana yake? na neno hilo limetoka wapi? hali kadhalika Tanga? Tabora? Morogoro? Ruaha? Mbeya? Shinyanga? Zanzibar?

Kama huyajui yote hayo basi ujuwe umejazwa ujinga wa ubaguzi wa ujinga. Hakuna zaidi.

Tujadiliane.

Mkuu Zomba, heshima yako mkuu.

Sasa nimeangalia mada yako nimegundua masuala kadhaa ambayo inabidi niyajibu.

Kwanza, umesema kwamba Watanzania ni wabaguzi lakini umeshindwa kusema kwamba wanambagua nani mbali ya kukiri kwamba sisi si wabaguzi wa kidini , kikabila, kijinsia na hata rangi. Hii ni sifa tuliyo nayo na itaendelea kuwa hiyvo kwa miaka nenda rudi.

Pili, umesema kwamba watanzania wana ubaguzi wa kijinga au wa ujinga nafikiri ukimaanisha kwamba tunapenda kumbagua mtu bila sababu maalum na huenda hujatoa mfano lakini naweza kukufikiri tu kwamba unamaanisha labda watu wasio watanzania wanabaguliwa kwa masimango au kejeli au tu kwa kusemwasemwa.

Tatu, unasema kwamba watanzania wamejazwa ujinga kwamba Vasco Da Gama ndie alieivumbua Tanzania! Hili ni jambo la kuangalia kwasababu hakuna mahali inasemwa katika historia kwamba huyu jamaa alivumbua Tanzania.

Isipokuwa Watanzania tumefahamishwa katika historia inayosema kwamba Vasco Da Gama alipita Tanzania sehemu ya Kilwa katika safari yake ya kutafuta biashara katika pwani ya Afrika Mashariki akiwa anaelekea pwani ya India sehemu ya Calcuta.

Alipofika Kilwa aliwakuta watu wanafanya biashara zao hasa waarabu ambao walikuwa wakiendelea na biashara yao ya watumwa na pembe za ndovu. Pia historia inasema alieanzisha jina la Tanganyika ni wakoloni wa kijerumani. Na pia kwa kuongezea wakti huo biashara kwenye pwani za Tanganyika ya leo zilikuwa zimeshamiri katika miji mingine kama Bagamoyo na Kilwa yenyewe. Kilwa nayo ilikuwa na sehemu tatu Kilwa Kivinje, Kilwa Kisimani na Kilwa Masoko.

Halafu pia umeomba wanachama wenzako kama kuna anaefahamu historia ya Kilwa aeleze sasa unakuwa unafanya nini kutuita wenzako wajinga?

Kilwa ilikuwepo kwa miaka nenda rudi sehemu hiyo ilikuwa chini ya himaya ya mwarabu mmoja wa Oman aitwaye Ali bin Hasan ambae alikuwa ni mtoto wa mfalme wa Ushirazi. Huyu jamaa alioa mtoto wa chifu wa kitanganyika na kwa sababu hiyo ikabidi awepo mahala hapo akitawala na sehemu hiyo ikawa ufalme wa kisultani wa Kilwa au "Kilwa Sultanate".

Hii yote mkuu ni historia tuliyofundishwa na walimu wa kitanzania na kuchanganya na upembuzi zaidi wa historia kwa wale wanaopenda kujifunza.

Kilwa ulikuwa ni mji mashuhuri kwa biashara na hata huyo Vasco Da Gama alipokuja kwenye karne ya 16 alikuta hali hiyo kwahiyo si yeye alevumbua mji huo na wala si yeye alieita sehemu hiyo Kilwa.

Mwisho ni nani asiekubali kwamba kulikuwepo vita vya MajiMaji? na ni nani asiefahamu kwamba Chifu Mkwawa alikuwa akiandika kiarabu?maana yeye alikutana mara kwa mara na waarabu alipokuwa akiwauzia waafrika wenzie kwa kwa hao waarabu hivyo kuweza hata kuandika kiarabu?

Hayo yote ya asiejua kuhusu neno Afrika, au Daresalaam, mara Tabora au Ruaha au Mbeya na mengine si ni wewe wa kuja na mada inayohusu uchambuzi wako na ukatuelimisha kuhusu majina hayo badala ya kuandika mambo ambayo hayaeleweki?

Sasa utuambie ni nani asiefahamu historia kiasi cha kuwabagua wale anaowaona leo ambao hafahamu historia ya ujio wao katika Tanzania ya leo?
 
Eliza na wengine, kwa mtindo huu wa mzamifu na Zombakutumia Answer.com!!! sina haja ya kuona mtoa mada, aki google, answer.com, anaona ndo ukweli......tahadhari kubwa inatakiwa kwenye mambo haya ya kihistoria jamani. kama huo ndo ujinga wetu waTz, mimi niwe wa kwanza au mwisho nafasi nipe wewe!!! mu kichwa wewe ndo JINGA langu.
Note... Kuna wachangiaji wamesema wewe hata kama vinywele vyako vya ki Farid bado ukienda huko.... utakuwa si wao!!!!
Haya matatizo ya google, na answer.com!!! huna vyanzo vingine?????
mkuu vipo vyanzo vingi tu:m vitabu, encyclopaedia n.k nieona tu nitumie hii ya mtandao ili mtu akitaka kuingia aingie. wanaosoma historia chuo wamekutana na hii maana pia. sio kitu kigeni sana
 
Hakuna aliyedharauliwa, ni wapi umeiona dharau? au wewe ni katika mazao ya wale wenye Ubaguzi wa Ujinga? mimi nikikubaguwa wewe kwa dini yako au wewe ukinibaguwa mimi kwa dini yanagu kama si Ubaguzi wa Ujinga ni nini huo?
Mkuu kubali challenge, lengo ni kutaka ueleze zaidi usishtuke bwana huku kuna mawazo gongana sio lugha gongana. neno ujiga (Ignorance) wewe huoni kuwa watu wataona kuwa wamedharauliwa? unachotalkiwa ni kuzidi kufafanua usichoke!
 
Huyu ni wa kuua tu, sio kurudisha nyumbani akafunzwe upya. Kumrudisha huyu kufunzwa upya ni kutumia resources vibaya. Kiwango hiki cha ujinga alichonacho strictly speaking ni cha kumkatia tamaa na siyo kufikiri kumrudisha darasani. Muda na nguvu utakazotumia kumfunza huyu, bila kuwa na uhakika kuwa ataelimika au hapana, ni bora ukazitumia kukusanya na kuwafunza watoto wa mitaani some vocational skill na Mungu atakubariki.

Bandiko lako hili limedhihirisha usemi wangu. Jee, unajuwa kuwa wapo mitaani hata Waalimu wanaofundisha wengine hizo skills? licha ya watoto ambao wewe huna uwezo wa kuwalinda wala kuwafundisha isipokuwa Ubaguzi wako wa Ujinga unakufanya ujione kuwa unaweza, nakuhakikishia huna unachokiweza zaidi ya Ujinga.
 
Asante ndugu zomba kwa maelezo yako. Mi nadhani hapo kwenye ishu Africa uwa hakuna mjadala hata kwa kutazama nakuelewa historia ya kawaida tu utaona Africa haibebi hasa maana halisi ya majority ya wakaazi wa Bara hili la pili kwa ukubwa duniani.
Ebu tuone, kwa uelewa wangu neno Afrika lina derive kutoka neno Afrit japo ukueleza maana yake sasa mimi "ujinga" niliojazwa ni kuwa Afri ni jina la Kilatini lililotumika kutambulisha Carthaginians (watu wenye chimbuko/asili Afrika Kaskazini ambako kwenye eneo ambalo sasa linatambulika kama Tunisia. Hili jina Afri lina uhusiano na Phoenician (lugha ya pwani ya Mediterrania katika sehemu iliyojulikana nyakati hizo kama Kaanani) Sasa kwa lugha hiyo ya Phoenician neno Afri lilimaanisha vumbi (dirt) lakini hypothesis ya mwaka 1981 ili assert ya kwamba hili neno Afri lina sterm kutoka neno la lugha ya kiberber (lugha ya Morroco/North Africa) Ifri au Ifran lenye maana ya mapango ikiwa ni reference ya watu wa mapangoni.
Chini ya Utawala wa Roma Carthage ikaja kuwa Capital ya jimbo la Afrika ambayo pia ilijumuisha pwani ya eneo linalojulikana sasa kama Libya.
Suffix ya Kilatini "ica" wakati mwingine inaweza kutumika kuashiria ardhi mfano Celtica kutoka Celtes. Kwahiyo utaona jinsi neno Africa lilivyokuja na ilikuwa inarefer watu gani.
Ufalme wa Kiislamu wa Ifriqiya (kwa sasa Tunisia) uliendeleza kutunza form ya jina hilo.
Sasa question is, ubaguzi wa ujinga according to you unamweka wapi Mwarabu na Mzungu katika Bara hili la "Waafrika" weusi?

Hapo nilipokuwekea rangi nyekundu, inaonesha kabisa nawe ni katika zao za wale Waalimu niliowataja kwenye post namba moja.

Hivi Africa ina maana ya inaowabeba katika hili bara? funguka zaidi kidogo ili uepuke kuwa miongoni mwa tunaobandikwa udhalili iwe na maana ya "wamapangoni" au "waafiriti", lipi bora katika hayo? Usinikumbushe hotuba ya Alli Hassan Mwinyi ya "Mikuki Miwili".
 
Msemo wako Mkuu Zomba "uneducated fool from an uneducated school"
huu msemo wako naomba ufafanuliwe na wana linguistics hasa hapo "uneducated school " school is inanimate so it can't take an action/adjective commonly used with animate especially human beings. mfano animates can eat things that are edible. mfano huwezi kusema the boy ate the spoon hapo spoon inakorofisha kwa vile si edible.
ni vizuri zaidi kutoa hoja kuliko kuponda. kama kuna kitu unadhani ungependa watu wakijue basi andika kama makala watu watajifunza na kukushukuru

Hata samaki wana school.

Katika Wabaguzi wa Ujinga unaweza ukaandika nakala mpaka ukaota sugu za vidole kwa kubofya keyboard na mwishowe watakubaguwa kwa ujinga tu.
 
Hapa nikujichanganya kama nilivyokueleza kwenye maelezo yangu ya awali utaona kuwa awa Carthaginians ni watu wa asili ya "North Africa" na neno Afri ni neno la kilatini lililotumika kuwatambulisha mabwana hawa, utakuja ona pia baadaye katika utawala wa Roma Carthage (Afri) ilikuwa Capital ya North Africa Province na baadae Ufalme wa Kiislamu uliposhika hatamu waliendeleza matumizi ya jina hilo Ifriqiya na nikaeleza kuhusu suffix ya kilatini ya "ica" ilivyokuja kuunda neno la Africa
Whatever the meaning of Africa is, it got nothing to do with Blacks.........jaribu kuona ninachostress hapa, labda sisi Wamatumbi tulitokea tu kuwa ndani ya pande moja na Waarabu but as far as ethnicity is concerned we got nothing to do with them

Elizabeth, nimekuwekea rangi nyekundu kupenda uelewe Kilatini cha science hutumia maneno mengi yenye asili ya hapo palipo au aliyevumbuwa na kuyaandika hayo kama ni Kilatini. Ukweli utabaki kuwa ukweli iwe hao wa Carthage au isiwe wa Carthage, neno Africa halina asili ya Kilatino hata kidogo, inaweza ikawa Kilatini lakini si ki latino. Nikimaanisha halijatokana na Walatino.

Iwe isiwe, neno "Afrika" halina connotation ya utukufu kama vile "mzungu", huoni kuwa Afrit ni the nearest hata katika matamshi?

Humo ndimo kwenye vichochezi vya Ubaguzi wa Ujinga tuliojazwa nao. Havikuanza leo nakuhakikishia, kwanini kina Suleiman (Solomon) na kina Ibrahim na Yesu wasiwe katika hawa wa North Afrika? wawe wazungu? tazama picha unayojazwa nao ujinga leo hii ya Yesu, kuna M-semitic wa aina hiyo ambae hana asili ya kizungu? halafu nenda katazame picha ya Afrit leo hii uone kama hata moja itakuwa ina uzungu ndani yake! Ubaguzi wa Ujinga haukuanza leo na Watanzania na Ubaguzi wa Ujinga ni miongoni mwa wengi wa Kontinenti hili tuliojazwa nao vichwani mwetu na Waalimu wetu (soma post namba moja) para inayoongelea Waalimu.
 
Naamini na nnadiriki kuandika kuwa Watanzania ni wabaguzi, ubaguzi wao si wa kidini au wa kijinsia au wa kikabila au wa rangi. Hizo ndio njia kuu zijulikanazo za ubaguzi duniani.

Watanzania, wengi wao, hawana kabisa ubaguzi huo. Ubaguzi wa Watanzania ni wakijinga au wa ujinga. Naamini kabisa kuwa ubaguzi wa Watanzania ni wa ujinga zaidi ya wakijinga. Ujinga hawana ila wana ubaguzi wa ujinga.

Ikiwa Watanzania hawana ujinga, huu ubaguzi wa ujinga wameutowa wapi? nna uhakika kuwa huu ubaguzi wamepachikwa na Waalimu wao na Waalimu wao walipachikwa na Waalimu wao na hao Waalimu wao walipachikwa huu ujinga walipojengewa mashule na kusomeshwa na kufundishwa cha kuja kuwafundisha hao waliotarajiwa kuwa ndio watakuja kufundisha, matokeo wamewajaza Watanzania ubaguzi wa ujinga.

Mara kadhaa humu JF nimekuwa nikitumia sentensi "uneducated fool from an uneducated school", nna uhakika wanaonisoma humu JF wameshaisoma sentensi hiyo, si mara moja wala mbili, wako walioielewa wakakaa kimya na wako walioielewa wakashindwa kuielewa na wakaanza kung'aka kuwa hilo si neno la kueleweka. Sina haja ya kulielewesha kwani, muelewa huelewa haeleweshwi. Asiyeelewa hutaka kuelewa na huuliza ili aelewe wala hataharuki na kujifanya anajuwa asichokijuwa, moja ya ubaguzi wa ujinga.

Ubaguzi mwengine wa ujinga tuliokuwa nao na uliojazwa vichwani mwa wengi ni kuwa Vasco Da Gama ndio kaivumbuwa hii Tanzania au Tanganyika wakati ukweli ni kuwa wakati wa Vasco Da Gama jina Tanzania halikuwepo wala Tanganyika halikuwepo. Kuna anaelipinga hili? Anza.

Isitoshe, Vasco Da Gama hajawahi kuikanyaga ardhi ya nchi hii, ambayo leo inaitwa Tanzania (jina aliloipa Muhindi wa Tanga). Vasco Da Gama aliishia baharini alipotia nanga manuwari zake, hajashuka wala kuigusa hii ardhi ambayo wengi wanajazwa ujinga wa kusema kuwa Vasco Da Gama ndio mvumbuzi. Swali la kujiuliza, Jee, Vasco Da Gama alivumbuwa kipi? alimkuta nani hapo Kilwa? (Naomba wajuzi wanipe maana ya neno "Kilwa") labda hilo ni neno la Kireno? kwa kuwa umeaminishwa kuwa Vasco Da Gama kapavumbuwa? au maana ya jina (au neno) Sofala, zilipotuwa kwanza manowari zake, ambako alipewa nahodha kipofu akamuongoza hadi Kilwa. Ndio kipofu. Ni ajabu lakini kweli.

Jee, hayo mmeyasoma huko mnakojazwa ujinga? Ni wangapi leo hii wanaojuwa kuwa hapa katika Ardhi hii kulikuwa kuna mji, kama si nchi, inayoitwa Raptha? Hii Raptha iko wapi? ilianza lini na nani walikuwa Watawala? na imeshia wapi? Maweee!

Nani leo hii anaejuwa kuwa Majimaji ilikuwa ni vita isiyokubalika na wengi leo hii?

Nani anaejuwa kuwa Mkwawa alikuwa anaandika Kiarabu, japo kuandikiwa?

Nani leo hii anaekiri kuwa nchi hii ina mbegu na si shina au tawi tu la Uarabu, la hasha, si nchi hii, Kontinenti hili? Nakuhakikishia hakuna. Kwanini hakuna? ni Ubaguzi wa ujinga.

"Afrika" ni lugha gani, au neno? tuseme jina hilo? vyovyote, iwavyo na iwe, limetokana na lugha gani uijuwayo wewe? zaidi ya neno au jina "Afrit"? kama huna zaidi ya hapo basi ujuwe umejazwa ujinga.

Dar Es Salaam. ni lugha ipi na neno hilo linatoka wapi? anaekuambia ni "Bandari Salama" basi huyo kakujaza ujinga kwani si maana yake ya ukweli.

Arusha, unajuwa maana yake? na neno hilo limetoka wapi? hali kadhalika Tanga? Tabora? Morogoro? Ruaha? Mbeya? Shinyanga? Zanzibar?

Kama huyajui yote hayo basi ujuwe umejazwa ujinga wa ubaguzi wa ujinga. Hakuna zaidi.

Tujadiliane.

Mkuu Zomba , hapa sana sana umeandika abstract ambayo katika mizania ni relative in nature.
Kila kitu, and I mean it , kila kitu cha kudhania ni relative to what one knows.
 
zomba,
Mkuu wangu hata sikuelewi, kwanza naomba nikuombe radhi kwa hili maana kusema kweli Ujinga ule ule ulozungumzia ndio ujinga huo huo unaojaribu kuusambaza, kwa sababu kwa kila ulichoandika hapa ni kutokana na jinsi ulivyofundishwa na mwalimu ambaye simjui na engine nitamwita Mjinga mwingine vile vile. Usichokijua mkuu wangu yule mwalimu na shule yake ni Mjanja ktk Wanjanja maana kakuuzia mbuzi (elimu) ndani ya gunia..

Nitakwambia kwa nini -
Nchi hii ilikuwepo hata kabla mgeni yeyote kuwepo na hatuwezi kuujua mwanzo wake isipokuwa jina la nchi ni utambulisho tu kaa vile wewe unavyotumia jina la Zomba hapa jkijiweni. Sasa itakuwa ajabu sana miye nianze kubishana juu ya ujio wa jina hili maana haubadilisha who you are!. Jina linaweka tu utambulisho wa kutofaitisha watu ama vitu, iwe hiyo CCM iloanza na AA ikawa TANU na leo tuna CCM haina maana yoyote zaidi ya utambulisho.

Sasa mkuu wangu, ikiwa Waarabu, Maburush, na Washihir ndio walokuwa wageni wa kwanza kushuka coast ya nchi hii wewe ulitegemea majina ya miji yetu yangetoka wapi ilhai sisi wenyeji ndio wajinga?.. Na iweje watu mchukue nafasi kubwa kuwasifia waarabu kwa lugha yetu ya kiswahili wakati ukisoma maandishi yako yote uloandika hapo juu utapata maneno machache sana wala hayajai mkkononi ya hao wageni iwe waarabu au Wareno?. Iweje tusiwasifie wabantu kwa lugha hii isipokuwa wageni na tunafikia hata kubishana nani mbora zaidi ya mwingine na sii sisi wenyewe kuwa wabora zaidi yao?.. Bila shaka ni hiyo elimu ya Ujinga tulofundishwa na hao unaowaita Wajinga kwa fikra za wajinga..Hata Kifaransa chenyewe kuna maneno mengi tu ya Kiingereza pamoja na lugha nyinginezo acha mbali Kiswahili chetu, maana lugha ni nyenzo tu ya watu kuwasiliana.

Na wala sikubaliani ulipotumia maneno haya ya kiingereza "Uneducated fool from an uneducated school". Kwa sababu hizo shule tulosomeshwa ama kwenda kuipata elimu wao walijua wanatuuzia nini? Wao sii wajinga bali tunafundishwa Ujinga unaotufaa sisi kubakia wajinga.

Sii Mwarabu wala Mzungu wote hawa walitupa elimu ili kutuingiza ktk ujinga zaidi maana ni wao wanaosema ya kwamba Education is a vital key to success, lakini sisi pamoja na kupewa elimu kwa miaka zaidi ya 200 bado maskini ina maana kuna tatizo ktk elimu tunayopewa. Siku zote binadamu huvuna kile alichopanda. Iweje sisi tumeenda shule na kukabisdhiwa huo ufunguoo wa mafanikio lakini bado maskini? something is very wrong na hiyo mbegu dume tulopewa (education)

Labda nikufahamishe mtazamo wangu ktk hulka za Watanzania. Ni kwamba sisi hatuna UBAGUZI isipokuwa WABINAFSI na hii imetokana na watu kuanza kuthaminisha MALI mbele ya UTU wakati sisi ni MASIKINI. Maana tajiri wa HALI ama UTU atathamini mali inayomhusu yeye na mila nna desturi zake hata kama mali hiyo haina thamani dukani. atawathamini ukoo wake,ndugu zake, watoto wake na watu wote waliokaribu naye kwa sababu ndio mtaji wake ktk maisha ya umaskini, kwa maana fupi maskini huthamini UTU wake maana ndio mtaji pekee alokuwa nao. Na unapouthamini UTU unakuwa tajiri wa HALI na sio MALI. Iwe yule Mmasai mwenye ng'ombe 3 au mzungu anayefuga mbwa ama paka nyumbani kwake. Na tajiri wa Mali huyu huthaminisha MALI yake kutokana na mahitaji ya watu wengine na sii yake yeye..

Hivyo elimu ya Ujinga tulofundishwa ni ile inayotuondosha ktk kile tulichokuwa nacho na kuanza kuthaminisha tusichokuwa nacho - Utajiri wa MALI. Na ktk mkondo wa fikra hizi tukaibuka na UBINAFSI maana tuna elimu ya Kijinga kwa wajinga tulofundisha. Na maadam Elimu ndio msingi wa maendeleo ya mwanadamu, hiyo elimu ya kijinga imetuwezesha kufanikiwa ktk Ujinga zaidi wa kupoteza utajiri wa Hali, hivyo success yetu ni Ujinga zaidi, tunaendelea ku create opportunities za ujinga na maendeleo ya Wajinga maana usipokuwa na utajiri wa hali ina maana unapoteza NIDHAMU ambayo ndio sifa kubwa ya UTU. Na siku zote wajinga waloendelea wasipokuwa na nidhamu basi hata maendeleo yao huwa hayawezekani hata kama kuna sheria (rule of law).

Itazame nchi yetu ambayo tunaisifia kila siku kwamba tunaendelea..Mji unajengwa pasipo kuwa na sewerege system, Itazame Kariakoo ilivyo leo halafu sikia sifa zake, nenda Mbweni ausehemu yoyote ilojenwa nymba nzuri na za fahari utakuta wachimo ya visima vya maji pembeni na visima vya kinyesi pembeni yake..Haya nenda Sinza, Kigogo, Kitunda, Manseze na vitongoji vyote vya Mji wa Dar - es Salaam vilivyojengwa baada na wajinga. Na kifupi itazame miji yetu yote ya Afrika utagundua kw ahakika hizi ni nchi za Wajinga hakuna yenye unafuu na kama upo basi jua hakuwepo mjinga kama sisi.

Nyumba zimejengwa kwanza kabla ya zinapimwa hivyo barabara zitajengwa kufuata nyumba hakuna kitomgoji hata kimoja kina ramani kama Ilala, Upanga au Magomeni. Tazama magari yanavyopishana mabarabarani, nenda Vituo vya mabus uone kama watu wanaweza kupanga msitari wakaingia mmoja baada ya mwingine, nenda benki au ofisini utakuta mstari lakini kuna watu watakao pita pembeni na kuhudumiwa. Rushwa imekuwa rushwa kila mtu anatafuta kutoka ktk umaskini wa mali kumbe bado yupo kt umaskini wa hali..

Na yote haya niloandika hayakutokea kwa bahati mbaya wala sii kwamba hatuna sheria! sheria zipo sana tu lakini sii kwa watu wasiokuwa na NIDHAMU..Na ili kuirejesha nidhamu inatakiwa tubadilishe mfumo wetu wa ELIMU tufundishwe kubadilika na kuanza kuuthamini UTU wetu kwanza badala ya watu ku behave kama wanyama ama ndege maana hawa wana afadhali...

Aaah hili darasa kubwa sana yaani naweza andika kitabu kizima lakini hapa kijiweni maneno mengi huwakinaisha wasomaji.

Umesema vizuri Mkandara. Naona tatizo tulilonalo ni kutaka wote tuiangalie dunia jinsi mtu fulani anavyoiona hata kama anakosea.
 
Bandiko lako hili limedhihirisha usemi wangu. Jee, unajuwa kuwa wapo mitaani hata Waalimu wanaofundisha wengine hizo skills? licha ya watoto ambao wewe huna uwezo wa kuwalinda wala kuwafundisha isipokuwa Ubaguzi wako wa Ujinga unakufanya ujione kuwa unaweza, nakuhakikishia huna unachokiweza zaidi ya Ujinga.
ZOMBA... nijibu swali hili straight forward; ni shughuli gani uliyowahi kufanya, ama unayofanya kwa sasa, ambayo inaweza kuisaidia kuifanya dunia kuwa mahali bora pa kuishi, kwa jamii inayokuzunguka, kwa sasa na baadaye. Toa mfano halisi wa kitu kinachoonekana ulichokifanya wewe mwenyewe au kwa namna fulani kusababisha kitokee. Kwa kifupi, kujigamba kwako huku kuwa wengine ni wajinga na wewe unaakili, akili zako zinasaidia nini. Na kwanini kuwepo kwako wewe "mtu mwerevu" hakubadilishi jamii inayokuzunguka. Maana hata sasa unasema watanzania ni wajinga, na wamekuzunguka wewe mwerevu. Labda unaweza kunisaidia kuelewa hapo kidogo. Tafadhal...Zomba...
 
ZOMBA... nijibu swali hili straight forward; ni shughuli gani uliyowahi kufanya, ama unayofanya kwa sasa, ambayo inaweza kuisaidia kuifanya dunia kuwa mahali bora pa kuishi, kwa jamii inayokuzunguka, kwa sasa na baadaye. Toa mfano halisi wa kitu kinachoonekana ulichokifanya wewe mwenyewe au kwa namna fulani kusababisha kitokee. Kwa kifupi, kujigamba kwako huku kuwa wengine ni wajinga na wewe unaakili, akili zako zinasaidia nini. Na kwanini kuwepo kwako wewe "mtu mwerevu" hakubadilishi jamii inayokuzunguka. Maana hata sasa unasema watanzania ni wajinga, na wamekuzunguka wewe mwerevu. Labda unaweza kunisaidia kuelewa hapo kidogo. Tafadhal...Zomba...

Unaweza kuonesha nilipoyaandika yote hayo? Kama hutoweza, ujuwe kuwa tatizo lako ni kubwa kuliko Ubaguzi wa Ujinga.
 
Mkuu Zomba, heshima yako mkuu.

Sasa nimeangalia mada yako nimegundua masuala kadhaa ambayo inabidi niyajibu.

Kwanza, umesema kwamba Watanzania ni wabaguzi lakini umeshindwa kusema kwamba wanambagua nani mbali ya kukiri kwamba sisi si wabaguzi wa kidini , kikabila, kijinsia na hata rangi. Hii ni sifa tuliyo nayo na itaendelea kuwa hiyvo kwa miaka nenda rudi.

Hunitendei haki unaponi-quote "out-of-context". Niliandika Hivi;

Naamini na nnadiriki kuandika kuwa Watanzania ni wabaguzi, ubaguzi wao si wa kidini au wa kijinsia au wa kikabila au wa rangi. Hizo ndio njia kuu zijulikanazo za ubaguzi duniani.
 
Ni rahisi sana kuwadanganya watu, lakin ni vigumu sana kuwaeleza watu kuwa mumedanganywa.

Kwa maana hiyo watu hao wanabaki kuwa waDanganyika.

Poleni sana.
 
Mkuu wangu hata kwa kujumuisha Muhindi, mwarabu na mzungu huo sio UBAGUZI ila zote hizi ni karama za mwenyezi Mungu ktk kutuwezesha sisi kutambuana toka ktk tafauti hizi..Hatukuumbwa kwa tofauti zetu isipokuwa kwa sababu ya kutuwezesha sisi kutambuana, kutofautisha baina ya Zomba na Mkandara, Zomba huyu na Zomba Mwarabu, mhindi au mzungu mana leo tuko billioni ngapi?. Kama sisi sote tungekuwa sura moja, rangi moja kama Wachina nani angeweza kukutofautisha Zomba wangu na Mkandara?.

Jee, hukunisoma sawa?

Naamini na nnadiriki kuandika kuwa Watanzania ni wabaguzi, ubaguzi wao si wa kidini au wa kijinsia au wa kikabila au wa rangi. Hizo ndio njia kuu zijulikanazo za ubaguzi duniani.

Watanzania, wengi wao, hawana kabisa ubaguzi huo. Ubaguzi wa Watanzania ni wakijinga au wa ujinga. Naamini kabisa kuwa ubaguzi wa Watanzania ni wa ujinga zaidi ya wakijinga. Ujinga hawana ila wana ubaguzi wa ujinga.
 
Nimerudi, kuna mwenye kuendeleza mada, au mmeridhika na ufafanuzi wangu katika hiyo post kabla ya hii?
 
Back
Top Bottom