Watanzania na Ubaguzi Wa Ujinga!

Na huu ubaguzi wa kijinga naona wengi wanaufagilia...teh teh teh! Mimi si mbaguzi wala sina mpango wa kuufuatilia ubaguzi. Utaninyima maisha na kula kwangu mjini bila sababu ya msingi

Hutaki hata kujuwa maana ya Iraqw? Asili na fasili ya Katibu Mkuu wa CHADEMA? basi hata maana ya jina "Jakaya" Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania?

Naomba basi japo tumia Google uje na maana ya SLAA.

Hatari kubwa sana.
 
nimeshindwa kuelewa unataka kulenga kitu gani ila kwa juu tu unamaanisha unausifia utamaduni wa kiarabu!!kuhusu Mkwawa hiyo ni kweli alikuwa ni muislam na alikuwa anaitwa Chief Abdalllah Mkwawa,na kisa hasa cha kugombana na wajerumani ni kwa sababu wajerumani waliwafukuza wafanyabiashara wa kiarabu ambao alikuwa akiwauzia watumwa na yeye anapewa bunduki ndio kisa kilianzia hapo akawawekea bifu,si yeye tu hata Bushiri aliwekeana bifu na wajerumani baada ya kupiga marufuku biashara ya utumwa.ila wote wa shenzi tu mwafrika peke yake ndio kama malaika.

Nasikitika sana kuona kuwa hata nawe uliyejitahidi kuliko wote, kujibu japo la Mkwawa, umerudia makosa yale yale ya kusomeshwa na Waalimu waliopachikwa ujinga na kuja kuwajaza ujinga ili muone kuwa mnajuwa kumbe mmejazwa Ubaguzi wa Ujinga.

Fikiria ulichokiandika halafu kwanini isiwe kinyume chake?
 
Zoba sorry Zomba utalaumu kila mtu kuanzia baba yako mama yako bibi yako hadi Mungu wako so to speak. Kuna kipindi ugonjwa na kujiona unajua waweza kuwa ugonjwa. Hali kama hiyo inaweza hata uwe psychopathic. Sioni ajabu kutotegemea kitu toka kwako. Ila kwa ujuzi wangu utokanao na madarasa na uzoefu, naweza kuwa mweledi kuliko ambavyo utakuwa katika maisha yako kama uwezo wako wa kujifunza ni huu. Tusibishane sana tell it the birds kuwa kila mtanzania ni mbaguzi. Kwa hitimisho lako ni kwamba nawe ni mbaguzi mjinga kama unavyoita wenzio. Simple.
 
Zoba sorry Zomba utalaumu kila mtu kuanzia baba yako mama yako bibi yako hadi Mungu wako so to speak. Kuna kipindi ugonjwa na kujiona unajua waweza kuwa ugonjwa. Hali kama hiyo inaweza hata uwe psychopathic. Sioni ajabu kutotegemea kitu toka kwako. Ila kwa ujuzi wangu utokanao na madarasa na uzoefu, naweza kuwa mweledi kuliko ambavyo utakuwa katika maisha yako kama uwezo wako wa kujifunza ni huu. Tusibishane sana tell it the birds kuwa kila mtanzania ni mbaguzi. Kwa hitimisho lako ni kwamba nawe ni mbaguzi mjinga kama unavyoita wenzio. Simple.

Jee, hicho sicho hiki?

Ikiwa Watanzania hawana ujinga, huu ubaguzi wa ujinga wameutowa wapi? nna uhakika kuwa huu ubaguzi wamepachikwa na Waalimu wao na Waalimu wao walipachikwa na Waalimu wao na hao Waalimu wao walipachikwa huu ujinga walipojengewa mashule na kusomeshwa na kufundishwa cha kuja kuwafundisha hao waliotarajiwa kuwa ndio watakuja kufundisha, matokeo wamewajaza Watanzania ubaguzi wa ujinga.
 
Nakubaliana na zomba, uzi wake una ukweli mwingi ngoja tuendelee kujifunza kufuta ujinga.
 
Last edited by a moderator:
...habari za jpili waheshimiwa??
Salama mkuu, ndo tuko kanisani tunasomewa agizo la kufunga na kuomba kuwasamehe wapuuzi waliochoma kanisa mbagala, tunasomewa pia tamko la Malasusa. Ukisikiliza hizo barua 2 za agizo la kufunga na barua ya Malasusa lazima ukiri kuwa hakika Ukristo ni chemchem ya busara
 
Salama mkuu, ndo tuko kanisani tunasomewa agizo la kufunga na kuomba kuwasamehe wapuuzi waliochoma kanisa mbagala, tunasomewa pia tamko la Malasusa. Ukisikiliza hizo barua 2 za agizo la kufunga na barua ya Malasusa lazima ukiri kuwa hakika Ukristo ni chemchem ya busara

Sina shaka kuwa kuna wengi wenye busara wanaoamini kuwa ni Wakristo. Labda nikukumbushe kuwa katika Historia tunasoma kuwa "immigrants" wa mwanzo alipojitangaza utume Mtume Muhammad (SAW) walikuwa ni kundi la waliomuamini na wao wakaamuwa kuwa ni Waislaam. Aliwashauri waondoke mji wa Makkah, kuhofia maisha yao kutokana na wakazi wa Makkah ambao wengi wao wakati huo walikuwa hawajaamini Uislaam na walikuwa wakitishia usalama wa walioamini, waende alipo mfalme wa "Kikristo" wa Uhabashi na wampe barua aliyowapa, cha kushangaza na ambacho hakiongelewi na wengi leo hii, Mfalme huyo aliwapokea na kuwapa ulinzi na kuwakaribisha bila kuwabaguwa na baada ya kuwasikiliza na ujumbe waliouleta akasema, kwa hakika huyo ni Mtume.

Jee, huyu Mfalme wa Uhabashi alitawala wapi? Jee, hao wahamiaji (muhajirun) wa mwanzo wa Kiislaam walikwendaje huko kwa Mfalme wa Uhabashi? mipaka ya uhabashi ilianzia na kuishia wapi? Jee, kuna uhusiano wowote na kaburi lililopo Kilwa linaloonyesha tarehe za aliozikwa hapo ni miaka 11 tu tangu (tarehe za uhamiaji wa pili wa Waislaam kutokea Makkah kuelekea Madinah na Mtume Muhammad akiwa minogoni mwao), na hao muhajirun wa mwanzo? Jee, Kilwa ikitawaliwa na Mfalme wa Kihabashi?

Umeshawahi kuyasoma hayo? Jee, hayana impact yoyote kwako?

Naamini kuwa, kuna wanaojiita Wakristo ambao ni waumini na wana imani ya kweli kwa Mwenyeezi Mungu muumba wa vyote. Na nnaamini miongoni mwao wapo wenye hekima na busara kama unavyohadithia na mfano mzuri ni huo niliokuandikia kuwa hata Mfalme Mkristo wa Uhabashi alikubalika na Mtume Muhammad na aliamuwa kuwapeleka muhajirun wa mwanzo kwake.

Huyu Mfalme ni nani? kisa chake kinaanzia na kuishia hapo kwa hawa Muhajirun tu? Jee, kama katika bara hili Ukristo ulikuwepo miaka zaidi ya 1400 nyuma, kwanini wengi waamini kuwa Ukristo umeletwa na wazungu? Waislaam tunaamini Ukristo ulikuwepo bara hili kabla ya ujio wa wazungu na hicho ni kisa tosha cha kukukinaisha kuwa tujuavyo ni hivyo. Kama ni hivyo, Utawala huo wa Kikristo ulianzia na uliishia wapi, hata tuamini kuwa Ukristo uliletwa na wazungu?

Ubaguzi wa Ujinga?
 
zomba,
Mkuu wangu hata sikuelewi, kwanza naomba nikuombe radhi kwa hili maana kusema kweli Ujinga ule ule ulozungumzia ndio ujinga huo huo unaojaribu kuusambaza, kwa sababu kwa kila ulichoandika hapa ni kutokana na jinsi ulivyofundishwa na mwalimu ambaye simjui na engine nitamwita Mjinga mwingine vile vile. Usichokijua mkuu wangu yule mwalimu na shule yake ni Mjanja ktk Wanjanja maana kakuuzia mbuzi (elimu) ndani ya gunia..

Nitakwambia kwa nini -
Nchi hii ilikuwepo hata kabla mgeni yeyote kuwepo na hatuwezi kuujua mwanzo wake isipokuwa jina la nchi ni utambulisho tu kaa vile wewe unavyotumia jina la Zomba hapa jkijiweni. Sasa itakuwa ajabu sana miye nianze kubishana juu ya ujio wa jina hili maana haubadilisha who you are!. Jina linaweka tu utambulisho wa kutofaitisha watu ama vitu, iwe hiyo CCM iloanza na AA ikawa TANU na leo tuna CCM haina maana yoyote zaidi ya utambulisho.

Sasa mkuu wangu, ikiwa Waarabu, Maburush, na Washihir ndio walokuwa wageni wa kwanza kushuka coast ya nchi hii wewe ulitegemea majina ya miji yetu yangetoka wapi ilhai sisi wenyeji ndio wajinga?.. Na iweje watu mchukue nafasi kubwa kuwasifia waarabu kwa lugha yetu ya kiswahili wakati ukisoma maandishi yako yote uloandika hapo juu utapata maneno machache sana wala hayajai mkkononi ya hao wageni iwe waarabu au Wareno?. Iweje tusiwasifie wabantu kwa lugha hii isipokuwa wageni na tunafikia hata kubishana nani mbora zaidi ya mwingine na sii sisi wenyewe kuwa wabora zaidi yao?.. Bila shaka ni hiyo elimu ya Ujinga tulofundishwa na hao unaowaita Wajinga kwa fikra za wajinga..Hata Kifaransa chenyewe kuna maneno mengi tu ya Kiingereza pamoja na lugha nyinginezo acha mbali Kiswahili chetu, maana lugha ni nyenzo tu ya watu kuwasiliana.

Na wala sikubaliani ulipotumia maneno haya ya kiingereza "Uneducated fool from an uneducated school". Kwa sababu hizo shule tulosomeshwa ama kwenda kuipata elimu wao walijua wanatuuzia nini? Wao sii wajinga bali tunafundishwa Ujinga unaotufaa sisi kubakia wajinga.

Sii Mwarabu wala Mzungu wote hawa walitupa elimu ili kutuingiza ktk ujinga zaidi maana ni wao wanaosema ya kwamba Education is a vital key to success, lakini sisi pamoja na kupewa elimu kwa miaka zaidi ya 200 bado maskini ina maana kuna tatizo ktk elimu tunayopewa. Siku zote binadamu huvuna kile alichopanda. Iweje sisi tumeenda shule na kukabisdhiwa huo ufunguoo wa mafanikio lakini bado maskini? something is very wrong na hiyo mbegu dume tulopewa (education)

Labda nikufahamishe mtazamo wangu ktk hulka za Watanzania. Ni kwamba sisi hatuna UBAGUZI isipokuwa WABINAFSI na hii imetokana na watu kuanza kuthaminisha MALI mbele ya UTU wakati sisi ni MASIKINI. Maana tajiri wa HALI ama UTU atathamini mali inayomhusu yeye na mila nna desturi zake hata kama mali hiyo haina thamani dukani. atawathamini ukoo wake,ndugu zake, watoto wake na watu wote waliokaribu naye kwa sababu ndio mtaji wake ktk maisha ya umaskini, kwa maana fupi maskini huthamini UTU wake maana ndio mtaji pekee alokuwa nao. Na unapouthamini UTU unakuwa tajiri wa HALI na sio MALI. Iwe yule Mmasai mwenye ng'ombe 3 au mzungu anayefuga mbwa ama paka nyumbani kwake. Na tajiri wa Mali huyu huthaminisha MALI yake kutokana na mahitaji ya watu wengine na sii yake yeye..

Hivyo elimu ya Ujinga tulofundishwa ni ile inayotuondosha ktk kile tulichokuwa nacho na kuanza kuthaminisha tusichokuwa nacho - Utajiri wa MALI. Na ktk mkondo wa fikra hizi tukaibuka na UBINAFSI maana tuna elimu ya Kijinga kwa wajinga tulofundisha. Na maadam Elimu ndio msingi wa maendeleo ya mwanadamu, hiyo elimu ya kijinga imetuwezesha kufanikiwa ktk Ujinga zaidi wa kupoteza utajiri wa Hali, hivyo success yetu ni Ujinga zaidi, tunaendelea ku create opportunities za ujinga na maendeleo ya Wajinga maana usipokuwa na utajiri wa hali ina maana unapoteza NIDHAMU ambayo ndio sifa kubwa ya UTU. Na siku zote wajinga waloendelea wasipokuwa na nidhamu basi hata maendeleo yao huwa hayawezekani hata kama kuna sheria (rule of law).

Itazame nchi yetu ambayo tunaisifia kila siku kwamba tunaendelea..Mji unajengwa pasipo kuwa na sewerege system, Itazame Kariakoo ilivyo leo halafu sikia sifa zake, nenda Mbweni ausehemu yoyote ilojenwa nymba nzuri na za fahari utakuta wachimo ya visima vya maji pembeni na visima vya kinyesi pembeni yake..Haya nenda Sinza, Kigogo, Kitunda, Manseze na vitongoji vyote vya Mji wa Dar - es Salaam vilivyojengwa baada na wajinga. Na kifupi itazame miji yetu yote ya Afrika utagundua kw ahakika hizi ni nchi za Wajinga hakuna yenye unafuu na kama upo basi jua hakuwepo mjinga kama sisi.

Nyumba zimejengwa kwanza kabla ya zinapimwa hivyo barabara zitajengwa kufuata nyumba hakuna kitomgoji hata kimoja kina ramani kama Ilala, Upanga au Magomeni. Tazama magari yanavyopishana mabarabarani, nenda Vituo vya mabus uone kama watu wanaweza kupanga msitari wakaingia mmoja baada ya mwingine, nenda benki au ofisini utakuta mstari lakini kuna watu watakao pita pembeni na kuhudumiwa. Rushwa imekuwa rushwa kila mtu anatafuta kutoka ktk umaskini wa mali kumbe bado yupo kt umaskini wa hali..

Na yote haya niloandika hayakutokea kwa bahati mbaya wala sii kwamba hatuna sheria! sheria zipo sana tu lakini sii kwa watu wasiokuwa na NIDHAMU..Na ili kuirejesha nidhamu inatakiwa tubadilishe mfumo wetu wa ELIMU tufundishwe kubadilika na kuanza kuuthamini UTU wetu kwanza badala ya watu ku behave kama wanyama ama ndege maana hawa wana afadhali...

Aaah hili darasa kubwa sana yaani naweza andika kitabu kizima lakini hapa kijiweni maneno mengi huwakinaisha wasomaji.
 
zomba,
Mkuu wangu hata sikuelewi, kwanza naomba nikuombe radhi kwa hili maana kusema kweli Ujinga ule ule ulozungumzia ndio ujinga huo huo unaojaribu kuusambaza, kwa sababu kwa kila ulichoandika hapa ni kutokana na jinsi ulivyofundishwa na mwalimu ambaye simjui na engine nitamwita Mjinga mwingine vile vile. Usichokijua mkuu wangu yule mwalimu na shule yake ni Mjanja ktk Wanjanja maana kakuuzia mbuzi (elimu) ndani ya gunia..

Nitakwambia kwa nini?..Nchi hii ilikuwepo hata kabla mgeni yeyote kuwepo na hatuwezi kuujua mwanzo wake isipokuwa jina la nchi ni utambulisho tu kaa vile wewe unavyotumia jina la Zomba hapa jkijiweni. Sasa itakuwa ajabu sana miye nianze kubishana juu ya ujio wa jina hili maana haubadilisha who you are!. Jina linaweka tu utambulisho wa kutofaitisha watu ama vitu, iwe hiyo CCM iloanza na AA ikawa TANU na leo tuna CCM haina maana yoyote zaidi ya utambulisho.

Sasa mkuu wangu, ikiwa Waarabu, Mabrushi, na Washihir ndio walokuwa wageni wa kwanza kushuka coast ya nchi hii wewe ulitegemea majina ya miji yetu yangeitwa nini?.. Na iweje watu mchukue nafasi kubwa kuwasifia waarabu kwa lugha yetu ya kiswahili wakati ukisoma maandishi yako yote uloandika hapo juu utapata maneno machache sana ya wageni iwe waarabu au Wareno. Iweje usiwasifie wabantu kwa lugha hii isipokuwa wageni?.. Bila shaka ni hiyo elimu ya Ujinga tulofundishwa a Wajinga..Hata Kifaransa chenyewe kuna maneno ya Kiingereza na mengine ya Kijarumani acha mbali Kiswahili..

Na wala sikubaliani ulipotumia maneno haya ya kiingereza "Uneducated fool from an uneducated school". Kwa sababu hizo shule tulosomeshwa ama kwenda kuipata elimu wao walijua wanatuuzia nini? Wao sii wajinga bali tunafundishwa Ujinga unaotufaa sisi kubakia wajinga.

Sii Mwarabu wala Mzungu wote hawa walitupa elimu ili kutuingiza ktk ujinga zaidi maana ni wao wanaosema ya kwamba Education is a vital key to success, lakini sisi pamoja na kupewa elimu kwa miaka zaidi ya 200 bado maskini ina maana kuna tatizo ktk elimu tunayopewa. Siku zote binadamu huvuna kile alichopanda. Iweje sisi tumeenda shule na kukabisdhiwa huo ufunguoo wa mafanikio lakini bado maskini? something is very wrong na hiyo mbegu dume tulopewa (education)

Labda nikufahamishe mtazamo wangu ktk hulka za Watanzania. Ni kwamba sisi hatuna UBAGUZI isipokuwa WABINAFSI na hii imetokana na watu kuanza kuthaminisha MALI mbele ya UTU wakati sisi ni MASIKINI. Maana tajiri wa HALI ama UTU atathamini mali inayomhusu yeye na mila nna desturi zake hata kama mali hiyo haina thamani dukani. atawathamini ukoo wake,ndugu zake, watoto wake na watu wote waliokaribu naye kwa sababu ndio mtaji wake ktk maisha ya umaskini, kwa maana fupi maskini huthamini UTU wake maana ndio mtaji pekee alokuwa nao. Na unapouthamini UTU unakuwa tajiri wa HALI na sio MALI. Iwe yule Mmasai mwenye ng'ombe 3 au mzungu anayefuga mbwa ama paka nyumbani kwake. Na tajiri wa Mali huyu huthaminisha MALI yake kutokana na mahitaji ya watu wengine na sii yake yeye..

Hivyo elimu ya Ujinga tulofundishwa ni ile inayotuondosha ktk kile tulichokuwa nacho na kuanza kuthaminisha tusichokuwa nacho - Utajiri wa MALI. Na ktk mkondo wa fikra hizi tukaibuka na UBINAFSI maana tuna elimu ya Kijinga kwa wajinga tulofundisha. Na maadam Elimu ndio msingi wa maendeleo ya mwanadamu, hiyo elimu ya kijinga imetuwezesha kufanikiwa ktk Ujinga zaidi wa kupoteza utajiri wa Hali, hivyo success yetu ni Ujinga zaidi, tunaendelea ku create opportunities za ujinga na maendeleo ya Wajinga maana usipokuwa na utajiri wa hali ina maana unapoteza NIDHAMU ambayo ndio sifa kubwa ya UTU. Na siku zote wajinga waloendelea wasipokuwa na nidhamu basi hata maendeleo yao huwa hayawezekani hata kama kuna sheria (rule of law).

Itazame nchi yetu ambayo tunaisifia kila siku kwamba tunaendelea..Mji unajengwa pasipo kuwa na sewerege system, Itazame Kariakoo ilivyo leo halafu sikia sifa zake, nenda Mbweni ausehemu yoyote ilojenwa nymba nzuri na za fahari utakuta wachimo ya visima vya maji pembeni na visima vya kinyesi pembeni yake..Haya nenda Sinza, Kigogo, Kitunda, Manseze na vitongoji vyote vya Mji wa Dar - es Salaam vilivyojengwa baada na wajinga. Na kifupi itazame miji yetu yote ya Afrika utagundua kw ahakika hizi ni nchi za Wajinga hakuna yenye unafuu na kama upo basi jua hakuwepo mjinga kama sisi.

Nyumba zimejengwa kwanza kabla ya zinapimwa hivyo barabara zitajengwa kufuata nyumba hakuna kitomgoji hata kimoja kina ramani kama Ilala, Upanga au Magomeni. Tazama magari yanavyopishana mabarabarani, nenda Vituo vya mabus uone kama watu wanaweza kupanga msitari wakaingia mmoja baada ya mwingine, nenda benki au ofisini utakuta mstari lakini kuna watu watakao pita pembeni na kuhudumiwa. Rushwa imekuwa rushwa kila mtu anatafuta kutoka ktk umaskini wa mali kumbe bado yupo kt umaskini wa hali..

Na yote haya niloandika hayakutokea kwa bahati mbaya wala sii kwamba hatuna sheria! sheria zipo sana tu lakini sii kwa watu wasiokuwa na NIDHAMU..Na ili kuirejesha nidhamu inatakiwa tubadilishe mfumo wetu wa ELIMU tufundishwe kubadilika na kuanza kuuthamini UTU wetu kwanza badala ya watu ku behave kama wanyama ama ndege maana hawa wana afadhali...

Aaah hili darasa kubwa sana yaani naweza andika kitabu kizima lakini hapa kijiweni maneno mengi huwakinaisha wasomaji.

Cha kushangaza ni pale kila unapozunguka mbuyu unarudi kuainisha kuwa tuna Ubaguzi wa Ujinga. Kwanini iwe Mwaarabu au Mzungu au Mhindi? au yeyote yule? kwanini isiwe Mwaafrika? iwe kwa jina lolote liwalo, kama ni kigezo tu cha kujuwana kuwa huyu ni Zomba yule ni Mkandara. Kwanini iwe hivyo?

Kwanini siwasikii wasomi waliosomeshwa hizo shule za kujazwa ujinga zikifundisha kuwa Mwaafrika (au jina lolote alilokuwa nalo kabla ya kupachikwa huo Uafriti) ndio alikuwa mtawala wa mwanzo huko bara la Asia? kama ni hivyo, ni wapi niliposoma mimi kuwa Mwaafrika aliitawala Asia? or is it Arabia? siamini kama kulikuwa kuna nchi inaitwa au inajiita Arabia kabla ya mwaka 1932. Jee, wewe hujui kuwa kuna Mwaafrika alitawala Asia kabla ya Waalimu wako kukufundisha kuwa Waarabu na Wazungu walikutawala? Jee, hao Waalimu wako walipokufundisha ujio wa Vasco Da Gama walikufundisha walikuta utawala upi pale Kilwa na Sofala? Jee, kuna uhusiano wowote na Utawala wa Kiafrika uliotawala mpaka Asia?

Raptha iko wapi?

Jiulize kisha ujaribu kueleza Ubaguzi wa Ujinga. Umeugusia mwisho mwisho wa makala yako, Jee, hiyo ndio elimu tuliyopewa? ya kujazwa ujinga? hatukufundushwa nidhamu? nataka kuamini hivyo ndivyo ilivyo lakini sikubali kuwa ni ujinga wa kuwa ni wajinga naamini ni Ubaguzi wa Ujinga.
 
Mi nadhani utakuwa na matatizo ya akili wewe yaani point zako zote ni kutaka kuhalalisha uarabu na kutaka kujifanya na wewe kuwa mtukufu!!! mfalme najesh alipotawala panajulikana ya kilwa yameanzia wapi wanuka shombo wa samaki hao??
Kwani mbantu hawezi kuendelea bila maendeleo hayo kuhusishwa na wageni wachache?? ndiyo tatizo la waswahili kila mtu anataka kuwa mwarabu mpaka mnapoteza maana sasa.kaburi la mfalme najesh lipo ethiopia hadi leo hadi barua alizoziacha zipo kwenye makaburi ya wafalme sasa kilwa wapi na wapi???
 
Mi nadhani utakuwa na matatizo ya akili wewe yaani point zako zote ni kutaka kuhalalisha uarabu na kutaka kujifanya na wewe kuwa mtukufu!!! mfalme najesh alipotawala panajulikana ya kilwa yameanzia wapi wanuka shombo wa samaki hao??
Kwani mbantu hawezi kuendelea bila maendeleo hayo kuhusishwa na wageni wachache?? ndiyo tatizo la waswahili kila mtu anataka kuwa mwarabu mpaka mnapoteza maana sasa.kaburi la mfalme najesh lipo ethiopia hadi leo hadi barua alizoziacha zipo kwenye makaburi ya wafalme sasa kilwa wapi na wapi???

Tatizo lako ni lilelile Ubaguzi wa Ujinga. Hata Kilwa huelewi kuwa ilikuwa ina sarafu za dhahabu kabla Ulaya hawajajua sarafu za dhahabu ni nini. Huelewi kuwa Kilwa ilikuwa na nyumba za ghorofa na zina rangi kabla hata ya Ulaya kujuwa rangi ni nini? huelewi kuwa Kilwa kulikuwa kunatumika Hariri na Kauri za Uchina kabla hata ya kujulikana hariri huko Ulaya wala kauri.

Unazidi kunihakikishia kuwa wengi wetu tuna Ubaguzi wa Ujinga. Sijui Uarabu umekujaje hapo?
 
Naamini na nnadiriki kuandika kuwa Watanzania ni wabaguzi, ubaguzi wao si wa kidini au wa kijinsia au wa kikabila au wa rangi. Hizo ndio njia kuu zijulikanazo za ubaguzi duniani.

Watanzania, wengi wao, hawana kabisa ubaguzi huo. Ubaguzi wa Watanzania ni wakijinga au wa ujinga. Naamini kabisa kuwa ubaguzi wa Watanzania ni wa ujinga zaidi ya wakijinga. Ujinga hawana ila wana ubaguzi wa ujinga.

Ikiwa Watanzania hawana ujinga, huu ubaguzi wa ujinga wameutowa wapi? nna uhakika kuwa huu ubaguzi wamepachikwa na Waalimu wao na Waalimu wao walipachikwa na Waalimu wao na hao Waalimu wao walipachikwa huu ujinga walipojengewa mashule na kusomeshwa na kufundishwa cha kuja kuwafundisha hao waliotarajiwa kuwa ndio watakuja kufundisha, matokeo wamewajaza Watanzania ubaguzi wa ujinga.

Mara kadhaa humu JF nimekuwa nikitumia sentensi "uneducated fool from an uneducated school", nna uhakika wanaonisoma humu JF wameshaisoma sentensi hiyo, si mara moja wala mbili, wako walioielewa wakakaa kimya na wako walioielewa wakashindwa kuielewa na wakaanza kung'aka kuwa hilo si neno la kueleweka. Sina haja ya kulielewesha kwani, muelewa huelewa haeleweshwi. Asiyeelewa hutaka kuelewa na huuliza ili aelewe wala hataharuki na kujifanya anajuwa asichokijuwa, moja ya ubaguzi wa ujinga.

Ubaguzi mwengine wa ujinga tuliokuwa nao na uliojazwa vichwani mwa wengi ni kuwa Vasco Da Gama ndio kaivumbuwa hii Tanzania au Tanganyika wakati ukweli ni kuwa wakati wa Vasco Da Gama jina Tanzania halikuwepo wala Tanganyika halikuwepo. Kuna anaelipinga hili? Anza.

Isitoshe, Vasco Da Gama hajawahi kuikanyaga ardhi ya nchi hii, ambayo leo inaitwa Tanzania (jina aliloipa Muhindi wa Tanga). Vasco Da Gama aliishia baharini alipotia nanga manuwari zake, hajashuka wala kuigusa hii ardhi ambayo wengi wanajazwa ujinga wa kusema kuwa Vasco Da Gama ndio mvumbuzi. Swali la kujiuliza, Jee, Vasco Da Gama alivumbuwa kipi? alimkuta nani hapo Kilwa? (Naomba wajuzi wanipe maana ya neno "Kilwa") labda hilo ni neno la Kireno? kwa kuwa umeaminishwa kuwa Vasco Da Gama kapavumbuwa? au maana ya jina (au neno) Sofala, zilipotuwa kwanza manowari zake, ambako alipewa nahodha kipofu akamuongoza hadi Kilwa. Ndio kipofu. Ni ajabu lakini kweli.

Jee, hayo mmeyasoma huko mnakojazwa ujinga? Ni wangapi leo hii wanaojuwa kuwa hapa katika Ardhi hii kulikuwa kuna mji, kama si nchi, inayoitwa Raptha? Hii Raptha iko wapi? ilianza lini na nani walikuwa Watawala? na imeshia wapi? Maweee!

Nani leo hii anaejuwa kuwa Majimaji ilikuwa ni vita isiyokubalika na wengi leo hii?

Nani anaejuwa kuwa Mkwawa alikuwa anaandika Kiarabu, japo kuandikiwa?

Nani leo hii anaekiri kuwa nchi hii ina mbegu na si shina au tawi tu la Uarabu, la hasha, si nchi hii, Kontinenti hili? Nakuhakikishia hakuna. Kwanini hakuna? ni Ubaguzi wa ujinga.

"Afrika" ni lugha gani, au neno? tuseme jina hilo? vyovyote, iwavyo na iwe, limetokana na lugha gani uijuwayo wewe? zaidi ya neno au jina "Afrit"? kama huna zaidi ya hapo basi ujuwe umejazwa ujinga.

Dar Es Salaam. ni lugha ipi na neno hilo linatoka wapi? anaekuambia ni "Bandari Salama" basi huyo kakujaza ujinga kwani si maana yake ya ukweli.

Arusha, unajuwa maana yake? na neno hilo limetoka wapi? hali kadhalika Tanga? Tabora? Morogoro? Ruaha? Mbeya? Shinyanga? Zanzibar?

Kama huyajui yote hayo basi ujuwe umejazwa ujinga wa ubaguzi wa ujinga. Hakuna zaidi.

Tujadiliane.

Zomba umewahi kuwa mwandishi wa mashairi? Umenikumbusha enzi zileeee za mashairi ya Andanenga. Kiukweli unakotaka kutupeleka siko maana naona unaelekea kule waliko Bhoko Haramu wanaopinga Elimu ya Kimagharibi eti ni ya kishenzi. Hawataki watoto wao waende shule eti watafundishwa ujinga.

Kwakufanya hivyo wajinga wengi wataendelea kuwa mitaani na hivyo kufanya maisha yawe ya mashakamashaka. Watu wote wanaopiga kelele za tunaonewa, hatutaki Muungano, MOU nk na hata kuiba na kuzichoma nyumba za ibada ni wapinzani sana wa Elimu Magharibi. Naomba tusifike huko unakotaka tufike.
 
Zomba umewahi kuwa mwandishi wa mashairi? Umenikumbusha enzi zileeee za mashairi ya Andanenga. Kiukweli unakotaka kutupeleka siko maana naona unaelekea kule waliko Bhoko Haramu wanaopinga Elimu ya Kimagharibi eti ni ya kishenzi. Hawataki watoto wao waende shule eti watafundishwa ujinga.

Kwakufanya hivyo wajinga wengi wataendelea kuwa mitaani na hivyo kufanya maisha yawe ya mashakamashaka. Watu wote wanaopiga kelele za tunaonewa, hatutaki Muungano, MOU nk na hata kuiba na kuzichoma nyumba za ibada ni wapinzani sana wa Elimu Magharibi. Naomba tusifike huko unakotaka tufike.

Hapana, siko huko kabisa, siipingi elimu ya magaharibi wala mashariki, naamini kwenye elimu, yoyote ile iwayo na ndio maana naamini tuna Ubaguzi wa Ujinga, mmoja wapo ni huo wa kubagua elimu.

Siamini kama Mwaarabu alitutawala, naamini kuwa sisi ndio tulitawala nchi zenye Waarabu. Siamini kuwa Kontinenti hili linastahiki kuitwa "Africa" jina linalotokana na Kiarabu kwa maana ya "Afriti".

Unapofikiri au kuwaza hayo uliyoyaandika, nawe unakuwa kwenye kundi lilelile la Ubaguzi wa Ujinga.

Amir Andanenga nimemsoma kama ninavyomsoma Kandoro, Shaaban Robert na wengineo. Wanastahili sifa.
 
hayo maswali nalolijua ni Kuwa Vasco Da Gama alikuwa mzungu wa kwanza kupita Pwani ya Africa Mashariki akienda bara Hindi.. Sasa na wewe unaendelea Kuwa mmbaguzi wa Ujinga badala ya kutupa Elmu kuhusu hayo maswala mengine na ufafanuzi unaturingishia Kama unatoa darasa toa sio ujivuni wa kujua kitu halafu husemi, wengine sisi ni walimu na nyuzi za historia Kama hizi zinztufundisha mengi na tunapata challenges mpya za kuwapelekea wanafunzi wetu Sasa ka wewe hutoi majibu wala maelezo afu unatunanga utakuwa hujatusaidia sisi wala wanafunzi wetu. Siku zote najua Dar Es Salaam ni bandari ya salama ka sio hivyo sema ni nini? Na tupe maana ya majina ya Mikoa ili tuelimike sisi na wanafunzi wetu, ni Kama unajua kitu afu unataka ubembeleeezweee! Kufafanua huo pia ni ubaguzi wa ujinga
 
Kajipangeeee vizuriiii ndio ujeeeee no evidence, sources huelewekiii naona kama vileeee umepoteaaa jaribuu tena baadaee
 
Back
Top Bottom