Mtoboasiri
JF-Expert Member
- Aug 6, 2009
- 5,101
- 1,946
Waungwana;
Nimekuwa natatizwa na jinsi huduma zinavyotolewa kwenye taasisi (hasa za umma japo na za binafsi nimeona kitu kile kile). Hivi huwa tunajiuliza mantiki ya kufuata utaratibu fulani? Natoa mifano ifuatayo:
1. Kuna siku nilinyimwa huduma benki moja (niliandikiwa hundi na mwajiri wangu ambayo ni "open"), sikuwa na kitambulisho cha kazi ila nilikuwa na pasipoti. Yule mfanyakazi wa benki hakuwa tayari kunilipa kwa kutumia pasipoti yangu kwa kuwa "taratibu inasema uje na kitambulisho cha kazini kwako au shahada ya mpiga kura" (hata walipokuja "supervisor" na meneja wake wa tawi walikuwa na msimamo kama huo).
2. Nilikuwa nafanyiwa "interview" ya kazi ambayo sifa iliyotakiwa ni angalau shahada ya kwanza. Nilikuwa "disqualified" kwa kuwa sikuja na cheti cha kidato cha nne na sita pamoja na "University Degree", mimi nilikuwa na "Academic Transcript" - ambayo ukurasa wake wa nyuma unaonyesha nilichaguliwa kujiunga na chuo kikuu kwa vigezo vipi.
3. (Hii inamhusu mtu mwingine japo niliishuhudia mwenyewe) Mstaafu mmoja alikuwa ana hundi yake "open" benki. Hakuwa na kitambulisho (ukistaafu unamrudishia mwajiri kitambulisho chako) ila alikuwa na pasipoti ila imeisha muda wake wa matumizi. Hakupewa huduma kwa kuwa pasipoti yake "ime-expire".
Nawauliza waungwana; kuna uhalali wowote wa maamuzi ya namna hii?
Nimekuwa natatizwa na jinsi huduma zinavyotolewa kwenye taasisi (hasa za umma japo na za binafsi nimeona kitu kile kile). Hivi huwa tunajiuliza mantiki ya kufuata utaratibu fulani? Natoa mifano ifuatayo:
1. Kuna siku nilinyimwa huduma benki moja (niliandikiwa hundi na mwajiri wangu ambayo ni "open"), sikuwa na kitambulisho cha kazi ila nilikuwa na pasipoti. Yule mfanyakazi wa benki hakuwa tayari kunilipa kwa kutumia pasipoti yangu kwa kuwa "taratibu inasema uje na kitambulisho cha kazini kwako au shahada ya mpiga kura" (hata walipokuja "supervisor" na meneja wake wa tawi walikuwa na msimamo kama huo).
2. Nilikuwa nafanyiwa "interview" ya kazi ambayo sifa iliyotakiwa ni angalau shahada ya kwanza. Nilikuwa "disqualified" kwa kuwa sikuja na cheti cha kidato cha nne na sita pamoja na "University Degree", mimi nilikuwa na "Academic Transcript" - ambayo ukurasa wake wa nyuma unaonyesha nilichaguliwa kujiunga na chuo kikuu kwa vigezo vipi.
3. (Hii inamhusu mtu mwingine japo niliishuhudia mwenyewe) Mstaafu mmoja alikuwa ana hundi yake "open" benki. Hakuwa na kitambulisho (ukistaafu unamrudishia mwajiri kitambulisho chako) ila alikuwa na pasipoti ila imeisha muda wake wa matumizi. Hakupewa huduma kwa kuwa pasipoti yake "ime-expire".
Nawauliza waungwana; kuna uhalali wowote wa maamuzi ya namna hii?