Gosbertgoodluck
JF-Expert Member
- Mar 3, 2008
- 2,855
- 401
Ndugu zangu wanaJF,
Inawezekana wengine wamefungua thread hii wakiwa wamefura kwa hasira baada ya kusoma title. Lakini ukisoma kwa umakini ninachotaka kueleza bila shaka hasira zitapungua au kutoweka kabisa.
Tangu tupate uhuru takriban miaka 50 iliyopita nchi yetu imekuwa ikiongozwa na serikali ya chama kimoja cha siasa yaani chama cha 'mapinduzi!' chini ya awamu nne tofauti. Awamu ya kwanza alikuwa Baba wa Taifa Mwl. Nyerere, awamu ya pili Alhaji Mzee Mwinyi, awamu ya tatu Mzee Mkapa na awamu ya sasa ya nne ni Kijana(?) Kikwete. Kwa ujumla, watanzania wengi hawafurahishwi na kasi ya nchi kuelekea katika neema ya maendeleo makubwa ya kiuchumi, kisiasa na kijamii. Pamoja na upatikanaji wa rasilimali nyingi ambazo ndiyo chachu ya maendeleo, lakini chini ya uongozi wa ccm nchi yetu imeendelea kuwa maskini tena maskini wa kutupwa.
Wengi wetu (ikiwa ni pamoja na Hayati Mwl. Nyerere mwenyewe) tumekuwa tukitamani sana ifike siku moja ccm iondoke madarakani ili tupate mawazo mbadala ya kuongoza nchi yetu kuelekea katika maendeleo ya dhati. Pamoja na matamanio yetu hayo ilikuwa vigumu kidogo kufikiria kwamba kweli ipo siku ccm itadondoka. Ilikuwa kama ndoto vile!Lakini chini ya uongozi wa kikwete kama rais na kama mwenyekiti wa ccm, kwa mbali naona kama ndoto inaweza kutimia.
Kwa ujumla, nchi yetu sasa ipo kwenye vuguvugu la kimapinduzi. Kwa kuangalia mwenendo wa serikali na chama tawala, sasa ni dhahiri kwamba wakati wowote kunaweza kutokea mabadiliko makubwa ya kisiasa hapa nchini. Mabadiliko hayo yataambukiza mabadiliko kwenye masuala ya kiuchumi na kijamii. Yote haya mwanzilishi wake ni kikwete na sifa zote anastahili apewe yeye.
Akiwa mwenyekiti wa ccm kikwete alimteua mzee makamba kuwa katibu mkuu wake. Alichofanya babu huyu kwenye chama wengi wetu tunafahamu. Amekigawa chama katika makundi mbalimbali yanayokinzana kila kukicha. Ni kikwete huyu huyu aliyekitelekeza chama na kuamua kutumia familia yake ishike usukani katika kampeni zake za kurejea madarakani.
Ni kikwete huyu huyu aliyeunda serikali ya kirafiki na kusababisha uongozi wa nchi kuyumba huku mafisadi wakiendelea kutamalaki. Chini ya uongozi wa kikwete watanzania wengi wameweza kuamka kutoka usingizini na kuona umuhimu wa mabadiliko ya katiba ya nchi.
Sasa jamani katika hali kama hii, kwa nini tutende dhambi ya kubeza mchango mkubwa wa kikwete wa kutupeleka kwenye ukombozi wa kweli? Tafakari.
Inawezekana wengine wamefungua thread hii wakiwa wamefura kwa hasira baada ya kusoma title. Lakini ukisoma kwa umakini ninachotaka kueleza bila shaka hasira zitapungua au kutoweka kabisa.
Tangu tupate uhuru takriban miaka 50 iliyopita nchi yetu imekuwa ikiongozwa na serikali ya chama kimoja cha siasa yaani chama cha 'mapinduzi!' chini ya awamu nne tofauti. Awamu ya kwanza alikuwa Baba wa Taifa Mwl. Nyerere, awamu ya pili Alhaji Mzee Mwinyi, awamu ya tatu Mzee Mkapa na awamu ya sasa ya nne ni Kijana(?) Kikwete. Kwa ujumla, watanzania wengi hawafurahishwi na kasi ya nchi kuelekea katika neema ya maendeleo makubwa ya kiuchumi, kisiasa na kijamii. Pamoja na upatikanaji wa rasilimali nyingi ambazo ndiyo chachu ya maendeleo, lakini chini ya uongozi wa ccm nchi yetu imeendelea kuwa maskini tena maskini wa kutupwa.
Wengi wetu (ikiwa ni pamoja na Hayati Mwl. Nyerere mwenyewe) tumekuwa tukitamani sana ifike siku moja ccm iondoke madarakani ili tupate mawazo mbadala ya kuongoza nchi yetu kuelekea katika maendeleo ya dhati. Pamoja na matamanio yetu hayo ilikuwa vigumu kidogo kufikiria kwamba kweli ipo siku ccm itadondoka. Ilikuwa kama ndoto vile!Lakini chini ya uongozi wa kikwete kama rais na kama mwenyekiti wa ccm, kwa mbali naona kama ndoto inaweza kutimia.
Kwa ujumla, nchi yetu sasa ipo kwenye vuguvugu la kimapinduzi. Kwa kuangalia mwenendo wa serikali na chama tawala, sasa ni dhahiri kwamba wakati wowote kunaweza kutokea mabadiliko makubwa ya kisiasa hapa nchini. Mabadiliko hayo yataambukiza mabadiliko kwenye masuala ya kiuchumi na kijamii. Yote haya mwanzilishi wake ni kikwete na sifa zote anastahili apewe yeye.
Akiwa mwenyekiti wa ccm kikwete alimteua mzee makamba kuwa katibu mkuu wake. Alichofanya babu huyu kwenye chama wengi wetu tunafahamu. Amekigawa chama katika makundi mbalimbali yanayokinzana kila kukicha. Ni kikwete huyu huyu aliyekitelekeza chama na kuamua kutumia familia yake ishike usukani katika kampeni zake za kurejea madarakani.
Ni kikwete huyu huyu aliyeunda serikali ya kirafiki na kusababisha uongozi wa nchi kuyumba huku mafisadi wakiendelea kutamalaki. Chini ya uongozi wa kikwete watanzania wengi wameweza kuamka kutoka usingizini na kuona umuhimu wa mabadiliko ya katiba ya nchi.
Sasa jamani katika hali kama hii, kwa nini tutende dhambi ya kubeza mchango mkubwa wa kikwete wa kutupeleka kwenye ukombozi wa kweli? Tafakari.