Watanzania hawapendi kuambiwa ukweli

Mapinduzi

JF-Expert Member
Aug 23, 2008
2,422
94
Nimesoma mada nyingi hapa, mtu akiandika mawazo yake kuhusu kiongozi anashushuliwa na kuanza kuambiwa kuwa analipwa na mafisadi.

Imefika wakati watanzania tuwe tunakubali kuambiwa ukweli hasa pale tunapokuwa tumekosea. Ukweli huu unaweza kuwa mchungu, ila kila mtu awajibike kwa yale anayoyafanya ama yawe mazuri au mabaya.

Akisemwa kiongozi hata kama kiongozi huyo ni wa juu kwa mfano Spika Sitta basi tukae chini na kujiuliza kwa nini asemwe? Hata kama kuna uhusiano na huyo anayesemwa say awe baba au mama yako, mume mke wako, mpenzi wako au jirani yako, uwe kwenye kambi yake au awe ni boss wako, inakuwa vizuri kutwanga na kupepeta ili kuhahakikisha tunatoa hoja zilizopembuliwa kiyakinifu.

Inatia woga kuona kiongozi anasema halafu badala ya kutetewa kwa hoja anatetewa kwamba anayemsema ni fisadi au habari inayomsema ina mkono wa fisadi.Tabia ya kuwaamini viongozi kwa asilimia 1000% kwamba wao hawajawahi kufanya ufisadi si mbaya pale inapokuwa na ushahidi uliokamilika kwa kuzipinga shutuma kwa vielelezo na sio kusema eti shutuma zinakuja kwa sababu ya chuki binafsi.

Tuamke, vita ni vita!
 
I like this. Inanikumbusha rafiki yangu mmoja aliyekuwa anagombea uongozi katika klub moja ya mipira wa miguu. Aliwaambia wapiga kura kuwa mkinichagua nitahakikisha kuwa tunaweka utaratibu mzuri wa kudhibiti mapato na kuhakikisha kuwa fedha hazipotei tena...kilichofuata baada ya kura ni kupata kura yake mwenyewe! Lakini yule aliyesema kuwa tutajenga uwanja wetu wenyewe ndani ya miaka miwili ijayo ndiye aliyepata kura...kilichofuata baada ya miaka miwili ni kuzidi kutafunwa pesa za klub kama shamba la bibi.
 
Pundadlimia07,
Mkuu wangu hata mimi ningemchagua anayetaka kujenga uwanja.. Huu ni mchezo wa mpira, ujenzi wa kiwanja ndio unaweza kuongeza pato la club na biashara nzima huanzia hapo.. Utathibiti fedha vipi, ikiwa club yenyewe haiwezi hata kuwa na kipato zaidi ya mgao wa shirikisho la michezo. hiyo fedha ya kuthibiti inatoka wapi?.. michango ya wanachama! si kutiana umaskini mkuu wangu.

Mimi nakubaliana na hoja hii ya kutopenda kuambiwa ukweli lakini siku zote huwezi kumshirikisha mtu kwa ufisadi kwa sababu yeye kalaani Ufisadi. tatizo la watanzania hawataki kuambiwa ukweli linatangulia na hoja ya kwanza. Tumalize kwanza kuwasafisha mafisadi waliopo kisha kesi ya Sitta itafuata kama naye ni fisadi.. Kilichotokea hapa ni kwamba Sitta analaaniwa kwa sababu he is against Mafisadi. Tunajua fika kwamba Mwakyembe na mama Kilango wote hawa wametajwa kwa mabaya yao toka wasimame dhidi ya Mafisadi.

Na ukiangalia kwa undani, report ya mafisadi Mwakyembe hakuandaa peke yake.likuwa kamati nzima leo kila neno baya anazungumzwa Mwakyembe hatujawasikia tena wajumbe wengine wakizungumzwa wala wao kufungua vinywa vyao. Ndio hadithi hizo, Mengi fisadi, Mbowe fisadi, Dr.Slaa fisadi, Zitto fisadi lakini husikii wakisema viopngozi wengine ngazi hizo hizo toka vyama vingine kwa sababu tu wamekaa kimya kuhusiana na mafisadi!

Sasa tujiulize iweje kila anayesimama against mafisadi, kesho yake tu ndio hadithi kubwa magazetini, tutaletewa Ufisadi wao hadi maisha wanayoishi na wake au waume zao...tena basi wakati mwingine huo ukweli wenyewe hauingii hata akilini..
Sitta ni mtu powerful ktk serikali yetu, ni mtu wa tatu baada ya rais..yupo juu ya PM na mawaziri wote kikatiba kwani anaweza kushika kiti cha IKULU inapobidi.. Hivyo kukodishiwa nyumba ya dollar 7,000 kwa mwezi wakati kuna nyumba za kawaida zinapangishwa kwa dollar 3000 kwa mwezi wala sioni kitu cha ajabu sana..zaidi ya kushangaa matumizi makubwa ya serikali yetu kwa ujumla wake. I mean ni kiasi gani serikali inalipa viongozi wetu wote, tazama ukubwa wake, miradi isokuwa na maslahi kabisa toka enzi za Mkapa..... bila shaka wanalipwa kuliko viongozi wa nchi tajiri duniani..
Tusishangae hilo na kuiita serikali nzima ya kifisadi bali tunachagua baadhi ya watu wanaodai kukomesha ufisadi unaoitambulika wazi..Hivi ni kiasi gani cha fedha kinatugharimu ktk kukodisha nyumba wakati serikali ilikuwa na nyumba zake! Mkapa kauza nyumba zote watu wakamshangilia sana na wanasema hana makosa, leo Sitta kakodishiwa nyumba kutokana na makosa ya Mkapa inaonekana ni ufisadi.. how about wale walionunua nyumba za thamani ya mabillioni kwa dollar 20,000, hawa sio mafisadi na tuwataje wote basi.. ndio ukweli unavyoweza kukubalika kwani hata mnunuzi anaweza kuwa fisadi hata kama ndio bei iliyotolewa na serikali...
 
Last edited:
Kama akiletwa mtu anayedhibiti wizi wa mapato, bila shaka atachukiwa hasa kama wapiga kura ndio wezi wenyewe. Hata siku moja mwizi huwa hapendi mtu anayezuia mianya ya wao kufanya kazi zao.
Mbona huyo aliesema uwanja utajengwa ndani ya miaka miwili hata msingi bado kuchimbwa, lakini inawezekana hela zilizotumika katika posho,safari na vionywaji zinaweza kujenga nusu uwanja.
 
Bongolander nadhani umenipata vizuri sana na ndugu yangu Mkandara, bado.

Mkandara, ukitaka kujenga uwanja, unaanzia wapi? kwenye maneno matupu au kuonesha jinsi gani utajenga uwezo wa kuleta maendeleo katika klub?
Hivi hujang'amua kuwa kwenye nyingi ya kampeni zetu huwa kuna ahadi hewa nyingi sana? Ni rahisi kuhoji jinsi gani mapato yatakavyodhibitiwa kulikoni maelezo ya jinsi uwanja utakavyojengwa, kwa pesa za kutokamwapi, ilihali hakuna ahadi zozote za ufadhili wa uwanja huo?

Kimsingi ahadi ya kujenga uwanja ni hewa kwani haikuwa na msingi wa utekelezaji wake na ilikuwa njia ya kuwahadaa wapiga kura. Pili, kwa vile wapiga kura ndiyo haohao makomandoo, basi UKIWAAMBIA UKWELI kuwa utadhibiti mapato, ukweli utaambulia kura yako tu.
 
Mapinduzi umenena.
Unajua jamii yetu pamoja na baadhi ya wana JF Bado wana kasumba ya zile zana.
Hivi sasa hili neno fisadi linaanza kupoteza maana kwa sababu hiyo. Tunaposema kuwa tuna haki ya kufikiri,kujieleza nk haimaanishi lazima tukubaliane kila kitu, muhimu ni nguvu ya logic. zile enzi za 'His Majesty's Voice' pamoja na zidumu fikra...... zimeyayuka na hazirudi tena.
Ndugu yangu usiogope kupewa lebal ya ufisadi eti kwa sababu unapinga kitu ambacho wenzako hawakubaliani namawazo yako.
The most important thing is having a clear conscious.
Just slog it on brother
icon7.gif
 
Back
Top Bottom