Ukiacha Wanavyuo, watanzania ni waoga wa kugoma. Nikumbusheni ni lini watanzania wamegoma na kushinikiza serikali yao ikubaliane nao. Fikiria ni serikali gani inapandisha bei ya umeme kwa asilimia 40, kama si kujua kwamba hakuna chochote kitakachotokea.:canada:
Sababu sio wengi wanaojua haki zao. Jiulize ni watanzania wangapi wame wahi kuipitia katiba ya nchi. Hamna serkali wala NGO inayowapa elimu ya uraia kwa ufasaha. Ni mbinu ya serkali kuwafanya wananchi wake wakati wote wfikirie wapi watapata mlo ujao, karo ya watoto, kodi ya nyumba na fedha ya kulipia umeme ili wasiwe na muda kutafakari muelekeo na mustakbal wa nchi yao. Hii ndiyo inayowapa fursa serkali ya kufanya maamuzi kufawatana na maslahi ya walio madarakani na sio nchi kwa ujumla.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.