Pengo
JF-Expert Member
- Oct 15, 2009
- 579
- 10
Inasikitisha sana pale unapoona mtangazaji wa kituo cha luninga akitangaza mpira huku akielemea upande mmoja.Hii ilitokea pale juzi kati ya mechi ya watani wa jadi Simba na Yanga.Kweli nimeamini waandishi wengi wa habari wa Tz ni mbumbumbu wa taaluma,inatia aibu kumsikia mtangazaji akisemaMimi mwenyewe nimemwona Musa Mgosi akipigwa kichwa pale katika goli la Yanga wakati wengi walikuwa uwanjani na hata sisi tuliokuwa tunatazama luninga hatukuona kichwa alichopigwa Mgosi.
Angalia hata katika kuwataja wachejazi wanapochukua mpira utasikia huyo Haruna bwana anakwenda Sweden wewe Nadir wa Zanzibar utamweza?!Na mambo mengi ya kuegemea upande fulani kama afanyavyo mtangazaji maarufu wa TBC.Huo ni ujinga.
Nawashauri nyie watangazaji wa Star TV fanyeni kazi acheni ushabiki mkiwa kazini itawaharibia sifa zenu,au nanyi nendeni mkajiunge muwe viongozi wa hizo timu kama wenzenu Sendeu na Ndimbo.
Angalia hata katika kuwataja wachejazi wanapochukua mpira utasikia huyo Haruna bwana anakwenda Sweden wewe Nadir wa Zanzibar utamweza?!Na mambo mengi ya kuegemea upande fulani kama afanyavyo mtangazaji maarufu wa TBC.Huo ni ujinga.
Nawashauri nyie watangazaji wa Star TV fanyeni kazi acheni ushabiki mkiwa kazini itawaharibia sifa zenu,au nanyi nendeni mkajiunge muwe viongozi wa hizo timu kama wenzenu Sendeu na Ndimbo.