watangazaji kuweni makini mnapotangaza!

bigcell

JF-Expert Member
Oct 6, 2010
219
60
Wakuu kwema? usiku wa kuamkia leo wakati narejea home kutoka kuwapa pole wahanga wa mabomu ya gongo la mboto,niliikuta radio inatumbuiza miziki laini,meseji za kuwaliwaza wafiwa,wahanga Walionusurika na milipuko ya mabomu ya g.mboto. Ila kitu kimoja ambacho nilishindwa kumuelewa mtangazaji wa kipindi Gadna James a.k.a King G, wakati akitafsiri au kuuelezea asili ya wimbo,nilimnukuu akisema ' kuna wakati fulani miaka ya zamani kulitokea tetemeko kubwa sana duniani,ila sikumbuki ni nchi gani na mwaka gani,ndipo walipojikusanya wanamuziki wengi na kuamua kutunga wimbo wenye urefu wa dk 7 kwa ajili kuchangia wahanga wa tetemeko la ardhi. Namaliza kumnukuu.Wimbo ukaanza ni 'We are the world' ambao ulitungwa na Michael Jackson na Lionel Richie na kuwashirikisha wanamuziki 45.Wimbo ulitungwa jan 1985 na kurekodiwa mach '85, mahususi kwa ajili ya baa la njaa lilotokea afrika kuanzia mwaka 1982-85 barani afrika ktk baadhi ya nchi esp Sudan,Ethiopia na somali.Naomba aelimishe uma wa tz.
 
hao ndio watangazaji wenu wa kibongo bongo, pumba tupu, eti mtangazaji huna uhakika na ujumbe unaotaka kuwapa wananchi na bado unawadanganya."kuna wakati fulani miaka ya zamani kulitokea tetemeko kubwa sana duniani,ila sikumbuki ni nchi gani na mwaka gani"
haya bwana, kazi kwenu
 
:laugh:

Huyo mtangazaji ameakisi tabia yetu halisi waTanzania, kuleta usanii kwenye kila jambo hata kama unapotosha...

:laugh:
 
Wakuu kwema? usiku wa kuamkia leo wakati narejea home kutoka kuwapa pole wahanga wa mabomu ya gongo la mboto,niliikuta radio inatumbuiza miziki laini,meseji za kuwaliwaza wafiwa,wahanga Walionusurika na milipuko ya mabomu ya g.mboto. Ila kitu kimoja ambacho nilishindwa kumuelewa mtangazaji wa kipindi Gadna James a.k.a King G, wakati akitafsiri au kuuelezea asili ya wimbo,nilimnukuu akisema ' kuna wakati fulani miaka ya zamani kulitokea tetemeko kubwa sana duniani,ila sikumbuki ni nchi gani na mwaka gani,ndipo walipojikusanya wanamuziki wengi na kuamua kutunga wimbo wenye urefu wa dk 7 kwa ajili kuchangia wahanga wa tetemeko la ardhi. Namaliza kumnukuu.Wimbo ukaanza ni 'We are the world' ambao ulitungwa na Michael Jackson na Lionel Richie na kuwashirikisha wanamuziki 45.Wimbo ulitungwa jan 1985 na kurekodiwa mach '85, mahususi kwa ajili ya baa la njaa lilotokea afrika kuanzia mwaka 1982-85 barani afrika ktk baadhi ya nchi esp Sudan,Ethiopia na somali.Naomba aelimishe uma wa tz.

Hapo sijui nani kajichanganya wewe , yeye au wote . KUna We r the World mbili, moja uliyo iongelea na nyingine ilikua a remake kwa ajili ya kuchangia maafa ya tetemeko la Ardhi la Haiti , sasa sijui huyu mtangazaji alipo sema "zamani" alikua na maana ya zamani ipi na labda alikua ana maana ya Haiti ila akakosa nyimbo hiyo mpya akapiga ile ya zamani au labda alielezea sema wewe hukujua kama kuna "We r the world " mpya iliyo fanyika karibuni.
 
Hapo sijui nani kajichanganya wewe , yeye au wote . KUna We r the World mbili, moja uliyo iongelea na nyingine ilikua a remake kwa ajili ya kuchangia maafa ya tetemeko la Ardhi la Haiti , sasa sijui huyu mtangazaji alipo sema "zamani" alikua na maana ya zamani ipi na labda alikua ana maana ya Haiti ila akakosa nyimbo hiyo mpya akapiga ile ya zamani au labda alielezea sema wewe hukujua kama kuna "We r the world " mpya iliyo fanyika karibuni.

We're the world ya kwanza iliwashirikisha akina Lionel Richie, Michael J, Harry Belafonte n.k. na ilikuwa mahususi kwa ajili ya Janga la njaa kule Ethiopia na jirani.
Kama Gardner anasema anakumbuka miaka 1985 ni wazi alimaanisha hii ya kwanza. Kama amemtaja Michael ni wazi alimaanisha hii ya kwanza.
We're the world ya pili ilikuwa mwaka jana baada ya tetemeko, na hii ilikuwa Remake ikiwa na Lionel Richie na vijana wengine. Micheal Jackson hakuwepo then.
Kwa jinsi ya maelezo yalivyo ni dhahiri G amejichanganya, (We're the world, Njaa, Michael Jackson,Tetemeko, Remake we're the world) haviwezi kutengeneza paragraph moja kamili bila kutofautisha.
 
Unashangaa?!!! Mi niliwahi kumsikia mtangazaji akifafanua kuwa Jasusi ni liJangili au Jambazi lililoshindikana kwenye jamii (Radio capita FM)
 
Back
Top Bottom