kilimasera
JF-Expert Member
- Dec 2, 2009
- 3,068
- 268
Msukuma mmoja alibahatika kwenda zake Uingereza, baada ya kufika alishangaa uzuri wa mji na majengo ya kushangaza.
Ili akirudi Tanzania awakonge wenzake kila alichokiona alitaka kujua kinamilikiwa na nani. Cha kwanza kuuliza kilikuwa kujua uwanja ule wa ndege unamilikiwa na nani. Alimuona Mzungu mmoja amesimama alimfuata na kumuuliza.
Eti uwanja huu wa ndege ni wa nani?
Speak English, Mzungu hakumuelewa na kumuomba azungumze Kiingereza.
Jamaa baada ya kuelezwa vile aliondoka akiamini anayemiliki ule uwanja ni Speak English. Alipoondoka pale alikwenda hoteli moja kubwa na kuulizia ile ni ya nani, aliyemuuliza kwa Kiswahili hakumuelewa alimjibu Speak English.
Kila kona alielezwa vile, basi jamaa aliporudi Tanzani aliamini Speak English ndiye tajiri mkubwa nchini Uingereza. Kila kona aliwaeleza jinsi kila kona alipouliza watu kuhusu mmiliki wa vitu vya thamani aliambiwa Speak English.
Watu walimcheka na kumueleza Speak English siyo tajiri bali walimueleza azungumze Kiingereza kwa vile walikuwa hawamuelewi akizungumza kiswahili. Mmh, hii kali kujua lugha nako raha.
Ili akirudi Tanzania awakonge wenzake kila alichokiona alitaka kujua kinamilikiwa na nani. Cha kwanza kuuliza kilikuwa kujua uwanja ule wa ndege unamilikiwa na nani. Alimuona Mzungu mmoja amesimama alimfuata na kumuuliza.
Eti uwanja huu wa ndege ni wa nani?
Speak English, Mzungu hakumuelewa na kumuomba azungumze Kiingereza.
Jamaa baada ya kuelezwa vile aliondoka akiamini anayemiliki ule uwanja ni Speak English. Alipoondoka pale alikwenda hoteli moja kubwa na kuulizia ile ni ya nani, aliyemuuliza kwa Kiswahili hakumuelewa alimjibu Speak English.
Kila kona alielezwa vile, basi jamaa aliporudi Tanzani aliamini Speak English ndiye tajiri mkubwa nchini Uingereza. Kila kona aliwaeleza jinsi kila kona alipouliza watu kuhusu mmiliki wa vitu vya thamani aliambiwa Speak English.
Watu walimcheka na kumueleza Speak English siyo tajiri bali walimueleza azungumze Kiingereza kwa vile walikuwa hawamuelewi akizungumza kiswahili. Mmh, hii kali kujua lugha nako raha.