WASTAAFU wanapewa tena madaraka kwanini?

We acha tu. Ni tz pekee .


MMM ati ni TZ pekee...hapa hapa kwetu ugonjwa huu ni chronic....sijui nani kati ya TZ na Kenya kaambukiza mwenzake! inaudhi sana unapata secretary hapa kazini kwetu ana miaka 64 ( retirement age ni 60) mama mzima hata memory loss tayari imeingia ukitaka kitu lazima umkumbushe mara ishirini...aaaaargggggh...
 
kaka hapo umesema na kama watakuwa hawafai basi utawakuta kwenye mabodi na makamati. utakuta mtu mmoja yuko kwenye bodiya mfuko, kamati ya kuteuliwa nk na zote ziko wizara moja. nenda mawasiliano, habari, fedha, viwandank mtu mmoja yuko kwenye kamati mbili au tatu sasa unajiuliza maka sual ni ushauri mtu huyo huyo kumshauri waziri masual matatu kwanini asiteue mwingine awe na ushauri mwingi zaidi?
 
Nimefuatilia kwa muda mrefu suala la uteuzi wa viongozi katika Tanzania nikashindwa kuelewa usahihi wa mtu kustaafu, eneo moja (hasa jeshini) na kisha kupewa madaraka mengine eneo jingine.
Kwa mfano unasikia KANALI MSTAAFU ..... ameteuliwa kuwa mkuu wa mkoa fulani au wilayaa fulani.
Kuna siri gani kuhusu jammbo hili wana JF?
Siri yake ni kuwa ipo imani kubwa ndani ya system kwamba, old soldiers never die...they just fade away. Kuwaacha watu waliokuwa na siri nyingi za ulinzi bila control, inaweza kuwapa wao shida, kama waliokuwa nazo wakiamua kuzitumia vibaya.
 
Wanakuwa washazizoea hela za kifisadi(si unajua zilivyo nyingi)?!Sasa muda ukiisha akiondoka moja kwa moja bila kurudishwa tena serikalini atazipata wapi tena?!
Sharti la hela za kifisadi uzichote kisawasawa,sasa wanaona wakimuweka fisadi mtoto hatazitumia vile inavyotakiwa...!
 
Wanakuwa washazizoea hela za kifisadi(si unajua zilivyo nyingi)?!Sasa muda ukiisha akiondoka moja kwa moja bila kurudishwa tena serikalini atazipata wapi tena?!
Sharti la hela za kifisadi uzichote kisawasawa,sasa wanaona wakimuweka fisadi mtoto hatazitumia vile inavyotakiwa...!

Ee ee ee.
Hii inahitaji utafiti?
 
Mie ndugu zangu wanawambia mpaka haya mawazo mgando yawatoke hawa wanawateuwa manake kwengine mpaka unashangaa huyu si mstaafu toka tunakuwa lakini kwa siasa za bongo bado yupo sijui tunakwenda wapi kama mtu ni swahiba wako si umpatie madili yao ya ufisadi hata kama vipi awe dalali wa rada au tender za mitambo na magari ya serikali nadhani inatakiwa watanzania tupige yowee kwamba sasa inatosha mtu akishastaafu anatakiwa apumzike wengine washike nafasi sasa kama lile swali liliulizwa na yule dogo kule mwanza kwanini kiongozi wa ule mkoa kipindi kile mamvi kiranja mkuu wa mawaziri halijajibiwa manake yule mkubwa alikuwa mkuu wa mkoa alafu mbunge........sasa mpaka leo naona hakuna mabadiliko wako wastaafu na wako wenge kofia mbili jamani nadhani tanzania inaweza kubadilika kama tutapinga haya mawazo mgando
 
Bwana weh! wanaogopa watatoa siri wakikaa domant...

Huo udomant unatoka wapi wakati wanapostaafu wanapewa marupurupu kibao na pensheni juu? Wajishughulishe na shughuli za kujitegemea ili wawe mfano kwa wengine ambao hawana kazi. Sio kujidekeza na kutegemea serikali mpaka mauti ikukute. Kama bado wana nguvu basi waombe kazi kwenye private sector. Nchi zingine askari akistaafu anaenda kuomba kazi mtaani. Sio lazima serikalini tu; mnatupa mashaka na kutukatisha tamaa ya kwenda mbele. Ukistaafu chukua zako tim. Ndio maana mnatakiwa muwe mnajiandaa kwa maisha ya uzeeni. Mtu aliekwishajiandaa anapostaafu wala hang'ang'anii viposti vya upendeleo na kubebwabebwa serikalini. Anaanza zake mbele tu, na akipewa post anasema "sasa muda wangu umepita wacheni nipumzike." Kuna mambo mengi tu ya kufanywa na wastaafu: kilimo,biashara,ufugaji,kuimba kwaya,muziki,maigizo,kujitolea ktk shughuli za maendeleo sehemu wanazoishi etc. Wakati umefika sasa wa kuwa na program za kuwaandaa watumishi kwa maisha baada ya kustaafu.
 
Kwa wanajeshi ukiacha generals, wanastaafu wakiwa na umri mdogo kwa hiyo mtu kama anaelimu nzuri anaweza bado akatumika ktk shughuli nyingine. Mimi kinacho niboa ni kumpa cheo mtu ambaye hana elimu ya kutosha lakini sababu tu ikiwa ni uanajeshi wake, hili si sahihi.
 
.......maelezo ya Barubaru na Magezi kuhusu wanajeshi ni sahihi kabisa........ukiangali mfano Luteni/Kapteni/Major/Luteni kanali umri huwa wnastaafu umri ukiwa bado kabisa wa kuwa na uwezo wa kufanya kazi........la msingi ni wawe qualified kufanya kazi walizoitiwa..........

kwa kuwa system yetu ni mbovu mbovu.......watu wengi wandanganya umri wao......

........Peter Kisumo ni CCM strategist mzuri.......kama kawekwa Vodacom wala sishangai kabisa........anajua kutumia nafasi yake......na hili ni goli la kiufundi la CCM......
 
Jamani si kuna muda maalumu wa mtu kustaafu? Na hapa kwetu ni miaka mingapi? na kama upo kwa nini bado wanapeana.
 
2/3 wastaafu wa kiume hufariki baada ya kustaafu hii inatokana mfadhaiko wa kuishi bila kazi au madaraka mazoea hii inasaidia kupunguza vifo hivyo
 
Kwa wanajeshi ukiacha generals, wanastaafu wakiwa na umri mdogo kwa hiyo mtu kama anaelimu nzuri anaweza bado akatumika ktk shughuli nyingine. Mimi kinacho niboa ni kumpa cheo mtu ambaye hana elimu ya kutosha lakini sababu tu ikiwa ni uanajeshi wake, hili si sahihi.

Wanajeshi kazi yao ni ya mkataba nafikiri kila baada ya miaka 6, unajaza mkataba upya kama unataka tena 6 ingine au umechoka.

Sasa mtu akikataa mkataba anaitwa mstaafu, suala la kuteuliwa katika uongozi limekaa kiusalama zaidi ili kuwafanya waliopo jeshini watulie kwani wanajua kuwa nao one day wanaweza teuliwa. Lakini kimaendeleo na ubunifu ni kuua maendelea kwani hawa si wabunifu wa maendeleo (entrepreneurial skills hawana) wao ni wazuri kwenye ulinzi tu.

Ndiyo maana Tanzania hatuna maendeleo bali tuna amani. Wanajeshi hawafikirii kuiondoa serikali madarakani japo inaweza kuwa si kwa maslahi ya nchi. Kitu kingine watawala ni wajanja sana, wanahakikisha wanajeshi wanapata huduma zote muhimu. Yaani hapa kutulizana zaidi ya kuwajibika
 
Wanajeshi kazi yao ni ya mkataba nafikiri kila baada ya miaka 6, unajaza mkataba upya kama unataka tena 6 ingine au umechoka.

Sasa mtu akikataa mkataba anaitwa mstaafu, suala la kuteuliwa katika uongozi limekaa kiusalama zaidi ili kuwafanya waliopo jeshini watulie kwani wanajua kuwa nao one day wanaweza teuliwa. Lakini kimaendeleo na ubunifu ni kuua maendelea kwani hawa si wabunifu wa maendeleo (entrepreneurial skills hawana) wao ni wazuri kwenye ulinzi tu.

Ndiyo maana Tanzania hatuna maendeleo bali tuna amani. Wanajeshi hawafikirii kuiondoa serikali madarakani japo inaweza kuwa si kwa maslahi ya nchi. Kitu kingine watawala ni wajanja sana, wanahakikisha wanajeshi wanapata huduma zote muhimu. Yaani hapa kutulizana zaidi ya kuwajibika

Kama ndivyo,
Mbona imekaa kama hongo vile?
 
Back
Top Bottom